Abdulla Ali Mwinyi: Ninagombea nafasi ya Naibu Spika, tuziache mamlaka husika zitimize taratibu kisha Wabunge wapige kura

Abdulla Ali Mwinyi: Ninagombea nafasi ya Naibu Spika, tuziache mamlaka husika zitimize taratibu kisha Wabunge wapige kura

Mgombea wa nafasi ya Naibu Spika mh Abdulla Ali Mwinyi amesema yeye hana maneno mengi zaidi ya kumwachia Mungu mwingi wa rehema aweze kumvusha.

Mwinyi amewataka waandishi wa habari waziache mamlaka husika ndani ya chama zitimize majukumu yake na kisha wabunge wakamilishe mchakato kwa kupiga kura.

Source: ITV habari
Weka na kapicha mkuu
 
Hii nchi Mamwinyi wapo tukubali! Hakuna cha demokrasia!
Ndiyo maana Baba Spika mama DED,
Kaka balozi mdogo mtu DAS,

Ukichunguza Sana wawezakuta kelele za Humphrey, huenda ni kukosa. Kila akipeleka majina ya wanafamilia, hakuna uteuzi unaowakuta!
Ukweli mtupu kwa 100%.
 
Hii nchi Mamwinyi wapo tukubali! Hakuna cha demokrasia!
Ndiyo maana Baba Spika mama DED,
Kaka balozi mdogo mtu DAS,

Ukichunguza Sana wawezakuta kelele za Humphrey, huenda ni kukosa. Kila akipeleka majina ya wanafamilia, hakuna uteuzi unaowakuta!
😄😄 Watoto wanne wa Mwinyi Ni wabunge huko zenji,mtoto wa chief hangaya nae Ni mbunge Zenji.

Yaani Ni uroda mtupu.
 
Tunaelekea kuwa na tawala za kifalme.
 
Nchi ya Kimfalme hii, kwani nje ya familia za kifalme hakuna mtu anayefaa
 
Yaani watu watatu watoto wa baba mmoja washike nafasi za juu kwa wakati mmoja!
ndio mana yake.maji hufuata mkondo tazama kwenu utajua kaz ya ukoo wako.anza na babu yake mzaa babu yako kisha baba yako utajua kaz ya nature yenu.
mbona Uk hawasem kila kitu cha UK ni mali ya malkia. bata wa mto Thames ni mali yote ya malikia kamata mmoja uone

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi teuzi ni kama zinakuwa na macho vile, labda tukibadili mfumo wa kupata wateuliwa ndo uwezo binafsi utatumika kuliko kujuana........
 
Enzi za utoto tulikuwa tukiona mtu ana kademu tulikuwa tunasema jamaa
ANAWEKEKELEA KANYAU YULE DEMU
Sasa huu ukoo unatuwekelea KANYAU watanganyika kwa AJILI ya mizahazaha na ROHO mbaya za Wana Lumumba kuchafua watanganyika wenzao
 
Inaonekana the elites na watoto wao hawawezi kujiajiri kabisa,eeh? Ila wakiwa mbele ya mic wanawaambia watoto wa wasakatonge waliosoma kwa kuuza mashamba,mifugo,malimao,uji wa ulezi,makande ya nazi,n.k wakajiajiri baada ya kuhitimu elimu ya juu. Sawa, Mungu anawaona.
 
Hii Tweet ya Maria Sarungi imenifikirisha mara mbili mbili, Hapa kuna shida kubwa sana na sikutemea mchakato huu uanze namna hii, Mh. Mwinyi huenda kashauriwa vibaya au ana overconfidence kupitiliza aliyopewa toka juu kuja kuzalisha drama zote hizi.

6F6DDA8A-32BB-4B67-B3FA-1559B7CDDEA3.jpeg


Kiukweli mchakato huu unahitaji utulivu sana wa akili na CCM waangalie atleast vitu kama hivi visijeonyesha credibility ya chama kuwa poor hasa kwa wapinzani kuona tunajikaanga sisi wenyewe. Natumaini watatuletea Naibu spika asiye na makando kando wala viulizo vya aina yoyote kwa faida ya Taifa lote kiujumla.

Nawatakia mchakato mwema watu wote waliochukua fomu na kuendelea kusubiri + kuamini kauli ya mwisho ya chama chetu.
 
Back
Top Bottom