Abel na Kaini (kizazi cha Adamu na Hawa); Je, wake zao ni kizazi cha nani?

Abel na Kaini (kizazi cha Adamu na Hawa); Je, wake zao ni kizazi cha nani?

Adam alimzaa Kaini na Abili, Adam akaishi miaka mia tisa thelathini 930 ndipo akafa, katikati hapo aliwazaa watotot wengi ambao walisambaa kote duniani na hivyo ikawa raisi kumpata mtu wa kuoa, story hii iko vizuri katika kitabu cha mwanzo 5. karibu jisomee dont argue without facts.
 
Bado hujajibu swali.tufanye walioa na miaka mia nane sasa kijiji kilitokana na kinanani?itakuwa walioana kaka na Dada maana hakukua na shangazi wala mjomba ni baba mama na watoto tu na hapo kwenye miaka zamani hawakuhesabu kama leo ilivyo siku zilikuwa chache tu na dunia ilikuwa ni sehemu wanazojua wao tu.


Umeshajijibu
 
Bado hujajibu swali.tufanye walioa na miaka mia nane sasa kijiji kilitokana na kinanani?itakuwa walioana kaka na Dada maana hakukua na shangazi wala mjomba ni baba mama na watoto tu na hapo kwenye miaka zamani hawakuhesabu kama leo ilivyo siku zilikuwa chache tu na dunia ilikuwa ni sehemu wanazojua wao tu.


Umeshajijibu
 
Swali jepesi sana.iko hivi
Adam na hawa hawakuwa watu halisi kama tulivyo mimi na wewe bali yalikuwa ni majina ambayo yalitumika kuwakilisha makundi ya watu.so Adam alikuwa anawakilisha wanaume na hawa alikuwa anawakilisha wanawake.lengo la kitabu cha mwanzo ni kuonyesha historia ya binadamu so isingewezekana kuzungumziwa namna kila mtu alivyopatikana so yakachaguliwa majina mawili ili yawe vielelezo au kuwakilisha makundi hayo ya watu.ukisoma vizuri kitabu chenyewe kinajieleza mfano habari ya nyoka kuongea unaona kabisa kwamba No kitu ambacho hakileti maana.so mwandishi wa kitabu kile alitumia majina ya adamu na hawa kwa maana hizo.mfano mzuri ni hadithi za sungura na fisi ambazo hutumia majina hayo kuwakilisha watu halisi.
Huo ndio ukweli wa mambo.Nilikwishaeleza humu kitu muhimu katika vitabu vya Agano la Kale na Jipya ni Maudhui.Wapo wahusika wengine hasa katika Agano la Kale wengi ni majina ya kutungwa (kama tunavyofanya leo katika Fasihi Andishi na Simulizi) ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa.Aghalabu Agano Jipya wahusika wengi ni watu halisi.Katika Agano la Kale,vitabu vingine ni hadithi.
 
Binadamu wa kwanza kuumbwa Na Mungu ni Adam Na Hawa.Watoto waliowazaa ni Abel Na Kaini.Abeli Na Kaini walioa je Wake zao ni kizazi cha nani?
Biblia inazungumzia ukomboz wa mwanadamu ambao story inaanzia kwa adam na hawa
Ila dunian kullikuwa na watu wengne ambao hawausiki katka ukomboz wa mwanadamu
Ndio maana Mungu anamuweka kain alama ili watu wasimdhuru baada ya kumuua nduye

Binadamu wa kwanza kuumbwa Na Mungu ni Adam Na Hawa.Watoto waliowazaa ni Abel Na Kaini.Abeli Na Kaini walioa je Wake zao ni kizazi cha nani?
 
ukinipa source nyingine manake biblia haina hizi info zaidi ya story ya adam na hawa ambayo haileti maana. unakubali kwamba biblia haijitoshelezi?

Kuna vitu vingine kwa hali ya kawaida ukitaka ku-trace source of the source(fundamental origin )huwezi kufahamu walau kwa akili za kibinadamu.Kwa mfano unaweza leo kupata historia ya Babu wa Babu wa Babu wa Babu wa Babu wa Babu...wa Baba yake Bilgate au Osama au Nyerere? Ikiwa binadamu hakujiumba haiwezekani ajue mwanzo aliumbwaje au waliumbwa wangapi bila kuambiwa.Kuna Uwezekano kwamba waliumbwa watu zaidi ya wawili mwanzo kabisa katika sayari ya dunia lakini pia pengine maeneo tofauti fofauti pia.Au pia kwamba Mungu aliumba binadamu tofauti tofauti katika sayari mbalimbali ambao baadaye waliweza kuingiliana.Jambo la msingi na ambalo Biblia inalidokeza katika kitabu cha Mwanzo ni hili tu:kwamba asili ya binadamu ni kuumbwa.Jinsia ya Kike na Kiume zote chanzo chake ni kuumbwa.Waliumbwa wangapi na wapi hakuna ajuaye!
Hebu tukuchukulie leo hii: Umezaliwa Mhimbili Jengo la Watoto.Je usipoambiwa ulizaliwa huko utajuaje kama ulizaliwa Mhimbili?Na kama kusingekuwa na mtu wa kukueleza hivyo ungejuaje?Sasa chukulia hali hiyo kwa binadamu wa kwanza.Yawezekana waliambiwa waliumbwa wangapi na sehemu gani lakini hawaku-document au wali-document ila kumbukumbu zikapotea.Hakuna anayejua dunia na viumbe vyake imekuweko kwa hakika toka lini.Katika mazingira kama hayo ni vigumu kuweza kujua maisha yao yalianzaje na yalikuwa ya namna gani.
 
kwa kuwa Mungu ni master scientist, inawezekana uzao wa kwanza kabisa aliujalia genetics za tofauti ili kusiwepo na effect ya back crossing, hata kaka na dada wa tumbo moja wangeweza kuzaliana pasipo changamoto yoyote. Kwa upande wa pili mambo haya ni IMANI so ondoa LOGIC [emoji23][emoji23][emoji23]

Kwa kiasi fulani umetaka kuongelea ukweli ambao upo na watu hawauzingatii kabisa.Mungu hakuumba mtu mzima kama tunavyojiona leo. Alianza na Sperm na Ovum.Kwa hiyo kunapozungumzwa uumbaji wa watu wa kwanza kunamaanisha Mungu kutengeneza structures za Sperm na Ovum.Baadaye ndio zikakutanishwa. Alizikutanishia katika Oviduct na Uterus ya namna gani hakuna ajuaye.Ukweli huu ukitaka kuuona jaribu kuangalia viumbe vyote vya Ulimwengu.Vyote ni Auto(Vinajiendesha).Kwa hiyo kama unavyoona dunia kwa mfano baada ya kuumbwa pengine alii-start ili ianze rotation na baada ya hapo inaendelea yenyewe.Hali kadhalika Binadamu.Baada ya sperm na Ovum kuungana kila kitu baada ya hapo kikawa Auto (kinajiendesha).

Na kwa hiyo tunapozungumza juu ya kuumbwa kwa mwanadamu tunaongelea juu ya genetic programming(coding) aliyoifanya Mungu kwenye hizo single cells za Sperm na Ovum.Gene ndio code zenyewe.Gene kwa watu wa Electronics unaweza kulinganisha na Micro-Controller katika Computer au simu au kifaa chochote cha Electronics.Gene ndio imebeba uhai(information).
 
Naona wengi tunasoma Biblia kwa mistari michache na kufanya conclusions ambazo hazitusaidii kujibu maswali muhimu. Kwanza tuelewe stori ya Adam na Hawa imewekwa kwa kusudio la kumwelewesha mwanadamu na mahusiano yake na Mungu, na mtiririko wa maisha ya binadamu toka wakati huo hadi sasa. Adam na Hawa walikuwa wanadamu pekee ambao waliishi bustani ya Eden ikimaanisha kuwa wanadamu wengineo waliishi sehemu nyingine mbali mbali.


Ukisoma Mwanzo 1:26-29 wanadamu waliumbwa wengi tu na walikuwepo kila kona ya dunia kabla ya Adam na Hawa.

I don't get you. Unatumia Biblia version gani mkuu?

Genesis 1:26-29New International Version (NIV)

26 Then God said, “Let us make mankind in our image, in our likeness, so that they may rule over the fish in the sea and the birds in the sky, over the livestock and all the wild animals,[a] and over all the creatures that move along the ground.”

27 So God created mankind in his own image,
in the image of God he created them;
male and female he created them.
28 God blessed them and said to them, “Be fruitful and increase in number; fill the earth and subdue it. Rule over the fish in the sea and the birds in the sky and over every living creature that moves on the ground.”

29 Then God said, “I give you every seed-bearing plant on the face of the whole earth and every tree that has fruit with seed in it. They will be yours for food.
 
Adam alimzaa Kaini na Abili, Adam akaishi miaka mia tisa thelathini 930 ndipo akafa, katikati hapo aliwazaa watotot wengi ambao walisambaa kote duniani na hivyo ikawa raisi kumpata mtu wa kuoa, story hii iko vizuri katika kitabu cha mwanzo 5. karibu jisomee dont argue without facts.

Adam na hawa walikwepo eneo gani?

Ilikuwaje akafika America ambapo lazima uwe na boti kufika ukitokea Asia?

Alifikaje Australia? Madagascar? Na kuenea maeneo yote? Kwa sababu mabara hayajaungana.

Pia ilikuwa ni miaka gani?

Utafiti wiki iliuopita unasema jamii ya kale kufika Australia ilifika miaka ya 75,000 mpaka 100,000 kutokana na ushahidi wa mabaki ya mifupa ya kale.

Pia adam na hawa walikuwa races gani ambazo mpaka leo zipo? Na utofauti wa race ulitoka wapi kama walikuwa wapo the sama race (its impossible kusema walikuwa race moja kwa sababu eve alitoka kwenye ubavu wa Adam, its likely walikuwa the same race ).

Ilikuwa miaka gani? Na species gani? Homo sapies huyu wa sasa? Je Homo Erectus, Homo Neanderthals, na Homo ergaster hizi species ambazo zinafanana na mwanadamu lakini zina utofauti kidogo kwenye size ya fuvu, meno, na brain size zilikuwa moja ya vizazi vya Adam au ni kama wanyama wengine?

Je kwenye Biblia tunaweza kuona Stone tools zilitumika kabla ya chuma? Kama stone tools sio za wanadamu wa kale ni viumbe gani vilikuwa vina akili ya kuchonga? Na bushmens mpaka leo wanatumia mawe kuwindia. Kwenye biblia kipindi cha adam ndio hao walikuwa wanatumia mawe?

Nina haya maswali na ninagamani mwenye kujua anifahamishe zaidi maana napenda kujua hizi clues vyema.
 
Kwa kiasi fulani umetaka kuongelea ukweli ambao upo na watu hawauzingatii kabisa.Mungu hakuumba mtu mzima kama tunavyojiona leo. Alianza na Sperm na Ovum.Kwa hiyo kunapozungumzwa uumbaji wa watu wa kwanza kunamaanisha Mungu kutengeneza structures za Sperm na Ovum.Baadaye ndio zikakutanishwa. Alizikutanishia katika Oviduct na Uterus ya namna gani hakuna ajuaye.Ukweli huu ukitaka kuuona jaribu kuangalia viumbe vyote vya Ulimwengu.Vyote ni Auto(Vinajiendesha).Kwa hiyo kama unavyoona dunia kwa mfano baada ya kuumbwa pengine alii-start ili ianze rotation na baada ya hapo inaendelea yenyewe.Hali kadhalika Binadamu.Baada ya sperm na Ovum kuungana kila kitu baada ya hapo kikawa Auto (kinajiendesha).

Na kwa hiyo tunapozungumza juu ya kuumbwa kwa mwanadamu tunaongelea juu ya genetic programming(coding) aliyoifanya Mungu kwenye hizo single cells za Sperm na Ovum.Gene ndio code zenyewe.Gene kwa watu wa Electronics unaweza kulinganisha na Micro-Controller katika Computer au simu au kifaa chochote cha Electronics.Gene ndio imebeba uhai(information).

Mhhh.

[emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
 
Mkuu Apollo kila kitu umeshaweka bayana hapo kwenye mstari wa 27, "male and female he created them" ona kuwa imewekwa kwa wingi (plural) kuonyesha kuwa walikuwa wengi. Sura ya kwanza inazungumzia siku sita za kwanza katika uumbaji, wakati sura ya pili inazungumzia zaidi kuumbwa na kuwekwa kwa mwanadamu ndani ya bustani ya Eden.
Hakuna mahali popote palipoandikwa kwenye Biblia inaposema kuwa Adam ni binadamu wa kwanza duniani. Watu mbali mbali waliotajwa kwenye Biblia ni kwa ajili ya kutujuza sisi mahusiano yetu na Mungu na kutufundisha yaliyotokea kabla yetu.
 
Zamani na hata katika Biblia wanawake walikua hawahesabiwi hivyo Adam na Hawa walikua na watoto wakike na hawakuandikwa na basi waliolewa na Abel na Kain
Waktisto wanadai biblia iliandikwa kwa muongozo wa roho mtakatifu ambayo pia ni matakwa ya Mungu sasa huyu Mungu anaubaguzi? Kwahiyo aliona hakuna umuhimu wa kuwaregard wanawake? Kama ni ivo anamapungufu
 
Mkuu Apollo kila kitu umeshaweka bayana hapo kwenye mstari wa 27, "male and female he created them" ona kuwa imewekwa kwa wingi (plural) kuonyesha kuwa walikuwa wengi. Sura ya kwanza inazungumzia siku sita za kwanza katika uumbaji, wakati sura ya pili inazungumzia zaidi kuumbwa na kuwekwa kwa mwanadamu ndani ya bustani ya Eden.
Hakuna mahali popote palipoandikwa kwenye Biblia inaposema kuwa Adam ni binadamu wa kwanza duniani. Watu mbali mbali waliotajwa kwenye Biblia ni kwa ajili ya kutujuza sisi mahusiano yetu na Mungu na kutufundisha yaliyotokea kabla yetu.

Asante kwa details mkuu.

"male and female, he created them"

Sasa hapo "them" ipo kwa subject gani zaidi ya hao wawili, kwa sababu kabla ya hiyo sentensi hakuna sehemu iliposema aliumba wanadamu zaidi ya hai wawili. Katika kingereza sahihi haijaonyesha wengine kwa kufuatilia mtiririko wa story. Them inaweza pia kutumika kwa nafsi 2 na kuendelea

I think tukisema kuwa aliumba wengi na adam na hawa ni sample italeta contradictions nyingi sana than hypothesis iliyopo.

Kwa sababu tutajiuliza kwanini alitumia Adam na hawa kama sample? Mwanadamu aliumbwaje na yupi wa kwanza kuumbwa? Kama alitengeneza mtu kutoka kwenye udongo ni kwamba alitengeneza wengi? Wapi paliposema kuwa alitengeneza wengi katika process moja?

It will contradict!
 
Zamani wanawake walikuwa hawahesabiwi, pia ndugu walioana. Hivyo waliwaoa ndugu zao wa kike na uzao ukaendelea.
Nani kasema wanawake walikuwa hawaesabiwi?
Jina adamu ni jina ambalo Mara ya kwanza lilitumika kuwakilisha jinsia zote mbili soma mwanzo 1:26,mwanzo 5:1-3
Alafu ndo utajua kuwa wanawake walikuwa wanaesabiwa na jina adamu lilikuwa la Mwanamke na mwanaume.
Kwa kifupi ni kuwa jina adamu likitumika kuwakilisha jinsia zote mbili kabla na baada ya jinsia hizo kutenganishwa.
Neno hawa au eva lilianza kutumika mara baada ya kula tunda la ujuzi wa mema na mabaya tena mara moja tu na baada ya kufukuzwa eden likitumika jina la adamu na mkewe.
 

Attachments

  • 1474710299142.png
    1474710299142.png
    88.3 KB · Views: 126
Unapozungumza mambo ya hypothesis kwenye Biblia unaenda nje kidogo na matumizi yake. Biblia ni neno la Mungu lililolengwa kuwapa wanadamu busara,mwongozo,amri na ushauri kuhusu maisha yao ya duniani na baada ya dunia. Biblia imeandikwa kwa lugha ya mafumbo na sio rahisi kuelewa maana ya hayo mafumbo. Ili kuelewa inabidi uwe na upako (Roho Mtakatifu). Wasomi wa Biblia wako wa aina mbili, ukiitizama Biblia kama mtu aliyevishwa kanzu wasomi wa Biblia aina ya kwanza wanaangalia zaidi muonekano wa kanzu na kutafsiri juu juu maana ya Neno, kundi la pili la wasomi wa Biblia ni wale wanaojaribu kutambua na kujaribu kuelewa kilicho ndani ya kanzu hivyo kuelewa maana halisi ya Neno.
 
Unapozungumza mambo ya hypothesis kwenye Biblia unaenda nje kidogo na matumizi yake. Biblia ni neno la Mungu lililolengwa kuwapa wanadamu busara,mwongozo,amri na ushauri kuhusu maisha yao ya duniani na baada ya dunia. Biblia imeandikwa kwa lugha ya mafumbo na sio rahisi kuelewa maana ya hayo mafumbo. Ili kuelewa inabidi uwe na upako (Roho Mtakatifu). Wasomi wa Biblia wako wa aina mbili, ukiitizama Biblia kama mtu aliyevishwa kanzu wasomi wa Biblia aina ya kwanza wanaangalia zaidi muonekano wa kanzu na kutafsiri juu juu maana ya Neno, kundi la pili la wasomi wa Biblia ni wale wanaojaribu kutambua na kujaribu kuelewa kilicho ndani ya kanzu hivyo kuelewa maana halisi ya Neno.

Thanks kwa mawazo mazuri.

Japokuwa kwa upande wangu its hard to believe that bible inajibu kila kitu kuhusiana na maisha na tunahitaji nguvu fulani kuelewa ulimwengu na maisha. Pale mtu anapokuja kutoka nje ya biblia na kusoma Quran, Torah, Talmud, Bhavad Gitta, Tao Te Ching, Dhamma, na Kabbalah hapohapo hawezi kurudi kuitazama Biblia kama alivyoitazama mwanzo.

Kuelewe Biblia inahitaji mtu ambaye sio mtafutaji wa details nyingi, mwepesi kuamini kila kitu kirahisi na ambaye sio mpekuzi nje ya biblia. Kuna a lot of knowledge hazipo kwenye Biblia lakini zipo kwenye vitabu vingine vikuu vya elimu ya dunia na pia kuna elimu ambayo ipo kwenye biblia ambayo nayo ina umuhimu.

Barikiwa [emoji120]
 
Back
Top Bottom