KERO Abiria wa Mwendokasi tuliotakiwa kutoka Kivukoni kwenda Kimara, Dereva katupeleka Morocco kisha akaturudisha Kivukoni

KERO Abiria wa Mwendokasi tuliotakiwa kutoka Kivukoni kwenda Kimara, Dereva katupeleka Morocco kisha akaturudisha Kivukoni

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Jana Machi 26, 2024 nikiwa kwenye Kituo cha Mwendokasi cha Kivukoni, kulikuwa na nyomi la hatari mida ya jioni, mabasi mengi yalikuwa yamepaki pembeni na machache yaliyokuja hayakukidhi haja ya huduma iliyotakiwa kutolewa.

Watu walikuwa wengi na wengine wakionekana wanataka kuwahi kwenda kupata futari.

Tukiwa katika hali hiyo, Saa 1:00 Usiku likaja basi kushusha abiria Namba zake za usajili T 591 DWR, baada ya kumaliza kala halijaanza utaratibu wa kuja pale tulipokuwa tumepanga foleni ya kwenda Kimara, Dereva wa Basi hilo akaanza kupandisha Wafanyakazi wenzake na baadhi ya Walemavu.

Wakati akifanya hivyo idadi ya aliokuwa akiwapandisha ni kubwa, ikabidhi watu waanze kuvamia nao waingie bila kufuata utaratibu, nami nikachoma ndani.

Dereva akatutaka tushuke, watu tukakaza, kaona sasa atukomeshe, badala ya Kwenda Kimara akatupeleka Morocco, huko napo watu wakakaza kushuka, eti alitaka tushuke pale.

Baada ya ubishi wa muda mrefu akachoma mafuta akaturudisha Kivukoni, huko napo abiria wakakaza, akaja Msimamizi wake, naye badala atumie busara, akaanz kutuambia “Nyie si mnajifanya vichaa, sasa sisi vicha zaidi yenu, leo mtalala hapohapo.”

Kulikuwa na vijana na madogo kibao wanafunzi wakaanza kuimba nyimbo kama vile wanaandamana.

Ndipo kuna mtu mzima mmoja nikaona ameshika simu akampigia Waziri Mohammed Mchengerwa, akamweleza kinachoendelea, kwanza Waziri hakuamini, akamwambia apige picha au arekodi video amtumie, yule mdingi akafanya hivyo.

Ndipo baadaye nasikia huyu bosi mpya wa Mwendokasi naye akapiga simu na kusema anakuja eneo la tukio, kusikia hivyo yule supervisor na dereva wake wakasepa, wakaona msala huo.

Tukapata dereva mwingine safari ya kuondoka Kivukoni ikaanza Saa 3:25 Usiku, tukafika Kimara almost saa Nne usiku.

Imagine tumekata tiketi Saa 12 Jioni kisha tunafika Kimara Saa Usiku.

Hawa madereva wa Mwendokasi nadhani wanatakiwa kuangaliwa saikolojia ya akili yao, pia huduma kwa ujumla za Mwendokasi ni janga.

Serikali ina kazi kubwa ya kufanya katika huu mradi.

Majibu ya DART - DART kuchukua hatua dhidi ya Dereva na Wasimamizi wa Mwendokasi waliowapeleka Abiria Morocco badala ya Kimara
yaani basi zima mpo zaidi 100 supavaiza na dereva wanawazunguusha mnawaangalia tu! na kuwalamba makofi? nyie nae ni wa hovyo hovyo tu mxsiuu!
 
Yaan umasikin unakusumbua...mi ningeshuka kuliko kupoteza masaa yote hayo...hivi ninyi muda kwenu huwa unasimama eeh....jaman hakuna serikali itayo hudumia familia yako...yaani mmekaa kama mazombi masaa zaid ya manne sa si bora hata mngeshusha kipondo kwa huyo dereva...unakuja lia lia jamii forum huku....mla kasa mkubwa wewe..
mwenyewe nimemwambia mkuu.. yaani wapo zaidi ya 100 wanazunguushwa na watu 2 tu? kamata dereva na huyo supavaiza chapa makofi yanguvu.. shuwain kbs!
 
Sasa na nyie ndugu zangu watanzania ni wajinga kiasi fulani.
Mtu anapakia walemavu na staff wengine,nyie kiliwawasha nini kuvamia mkapande wakati hamuhusiki? Ingekua mwendokasi inaendeshwa na Jeshi ingetakiwa walau mkashushiwe lugalo walau na bakora mbili mbili za matako.
Jifunzeni ustaarabu
we utakuwa unaishi kule ngulyati bariadi kwa wachawi na ww ni mwanga tu.. umeambiwa hayo mabasi ni spesho kwa hao unaowasema? wanahusika wao tu? hovyooo!
 
Jana Machi 26, 2024 nikiwa kwenye Kituo cha Mwendokasi cha Kivukoni, kulikuwa na nyomi la hatari mida ya jioni, mabasi mengi yalikuwa yamepaki pembeni na machache yaliyokuja hayakukidhi haja ya huduma iliyotakiwa kutolewa.

Watu walikuwa wengi na wengine wakionekana wanataka kuwahi kwenda kupata futari.

Tukiwa katika hali hiyo, Saa 1:00 Usiku likaja basi kushusha abiria Namba zake za usajili T 591 DWR, baada ya kumaliza kala halijaanza utaratibu wa kuja pale tulipokuwa tumepanga foleni ya kwenda Kimara, Dereva wa Basi hilo akaanza kupandisha Wafanyakazi wenzake na baadhi ya Walemavu.

Wakati akifanya hivyo idadi ya aliokuwa akiwapandisha ni kubwa, ikabidhi watu waanze kuvamia nao waingie bila kufuata utaratibu, nami nikachoma ndani.

Dereva akatutaka tushuke, watu tukakaza, kaona sasa atukomeshe, badala ya Kwenda Kimara akatupeleka Morocco, huko napo watu wakakaza kushuka, eti alitaka tushuke pale.

Baada ya ubishi wa muda mrefu akachoma mafuta akaturudisha Kivukoni, huko napo abiria wakakaza, akaja Msimamizi wake, naye badala atumie busara, akaanz kutuambia “Nyie si mnajifanya vichaa, sasa sisi vicha zaidi yenu, leo mtalala hapohapo.”

Kulikuwa na vijana na madogo kibao wanafunzi wakaanza kuimba nyimbo kama vile wanaandamana.

Ndipo kuna mtu mzima mmoja nikaona ameshika simu akampigia Waziri Mohammed Mchengerwa, akamweleza kinachoendelea, kwanza Waziri hakuamini, akamwambia apige picha au arekodi video amtumie, yule mdingi akafanya hivyo.

Ndipo baadaye nasikia huyu bosi mpya wa Mwendokasi naye akapiga simu na kusema anakuja eneo la tukio, kusikia hivyo yule supervisor na dereva wake wakasepa, wakaona msala huo.

Tukapata dereva mwingine safari ya kuondoka Kivukoni ikaanza Saa 3:25 Usiku, tukafika Kimara almost saa Nne usiku.

Imagine tumekata tiketi Saa 12 Jioni kisha tunafika Kimara Saa Usiku.

Hawa madereva wa Mwendokasi nadhani wanatakiwa kuangaliwa saikolojia ya akili yao, pia huduma kwa ujumla za Mwendokasi ni janga.

Serikali ina kazi kubwa ya kufanya katika huu mradi.

Majibu ya DART - DART kuchukua hatua dhidi ya Dereva na Wasimamizi wa Mwendokasi waliowapeleka Abiria Morocco badala ya Kimara
MLIVAA JEZJ ZA MAMELODY AMA AL AHLY MAANA HAO WANATAFUTWA NA PASSPORT MPAKA SASAA AISEE SHETANI GA. KAWAINGIA MWENDO...
 
Uzi kama huu ulitakiwa uandike tukampiga dereva ndio wakatupeleka.
 
Dereva alipiga gongo la soko la samaki linalopikwa kwa samaki waliooza.
 
Huu mradi ni wa kipumbavu sana.umekula Kodi zetu na faida sifuri.bora Huu mradi uvunjwe na gari zote zianze kupita kwenye Barabara za mwendokasi
Hawa dereva na msimamizi wachukuliwa hatua ya kinidhamu na washtakiwe kwa kosa la kutia hasara shirika. Iwe ni fundisho kwa watendaji wengine.
 
Wale Dereva mnawaonea bure, usimamiz ndio tatizo mabasi ni machache hivyo dereva analazimika kufanya kaz ya ziada au kujiongeza ili awaokoe watu wenye uhitaji zaid, sasa tatizo abiria wa Dar hawaelewi hiyo changamoto yeye akishakata Tiket tu basi anajiona ana haki ya kuondoka muda huo huo bila kuwazingatia Walemavu, wazee na watoto.

Mimi ningewapeleka Kibaha mrudi kwa Mguu.
 
Ndiyo maana anataka kupewa mwekezaji aendeshe hayo mabasi.

Waliopo wameshindwa.
Hivi wa kina Simon Msena wale walinunua UDA si ndo walipewa huo mradi kama wawekezaji au najichanganya. All in all anaeendesha anahisi anatia huduma na amesahau kama Ile ni biashara kama zilivyo biashara nyingine.
 
Tunajitoa TU akili.ila kiukweli hao madereva na mfumo mzima wa hayo mabasi,hawataki uwekezaji,hiyo ni meseji,nikama mgomo baridi

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Inasemekana wengi wa madereva wa mabasi ya mwendokasi walitolewa jeshini kupunguza gharama za uendeshaji. Sasa mwana jeshi na kuhudumia raia ni wapi na wapi?
 
Hivi wa kina Simon Msena wale walinunua UDA si ndo walipewa huo mradi kama wawekezaji au najichanganya. All in all anaeendesha anahisi anatia huduma na amesahau kama Ile ni biashara kama zilivyo biashara nyingine.
Siwafahamu wawekezaji wa sasa.
 
Sasa na nyie ndugu zangu watanzania ni wajinga kiasi fulani.
Mtu anapakia walemavu na staff wengine,nyie kiliwawasha nini kuvamia mkapande wakati hamuhusiki? Ingekua mwendokasi inaendeshwa na Jeshi ingetakiwa walau mkashushiwe lugalo walau na bakora mbili mbili za matako.
Jifunzeni ustaarabu
Si ndo hapo. Yeye kakili walemavu na staff wamepandishwa. Walijua anakoenda? Haya,kawambia washuke,bado hawataki. Angewasaidiaje sasa! Kama mabasi mengine yamepaki,ina maana hakuwa kazini hata yeye. Kimara angeenda kufanya nini kama hakupangiwa? Aliepiga simu,nae wale wale tu. Mara mia angepiga simu kwa niaba ya wote waliokosa usafili. Sasa dereva kawakimbia,na leo yupo kazini. Mmefaidi nini sasa
 
Huo mradi umekuwa na utotot mwingi sana
 
Back
Top Bottom