Absalom Kibanda akamatwa!


Kama nilivyoeleza hapa: JOHN MNYIKA: Mwigamba apata dhamana; tuepuke dola ya kipolisi taratibu watawala wetu wanatupeleka kuwa na dola ya kipolisi. Mwaka 2008 walivamiwa Kubenea, Ndimara na Ofisi ya Mwanahalisi nilisema kwamba lile lilikuwa na shambulio dhidi ya uhuru wa kikatiba na haki za msingi wa kutoa na kupata habari. Matukio ya kukamatwa kwa Mwigamba na sasa Kibanda kutokana na makala ni kamata kamata ya vyombo vya dola dhidi ya uhuru wa kutoa maoni na kuwasiliana.

Ni dalili mbaya wakati huu ambapo kuna sheria mbovu kama ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2011 yenye kifungu chenye kutoa adhabu ya kifungo cha hadi miaka 7 au faini ya hadi milioni 15 kwa makosa ya kukusanya maoni au kutoa elimu juu ya mabadiliko ya katiba kinyume cha sheria husika.

Kama kuandika makala tu kuhusu polisi kwa masuala ambayo hayana mwelekeo wa uchochezi au uhaini kama inavyodaiwa tayari vyombo vya dola vimeanza kamata kamata hatma ya mchakato wa katiba na masuala mengine ya kitaifa iko mashakani. Awali ilikuwa ni wananchi wa kawaida, wanasiasa wakiwemo wabunge, sasa wanahabari na hali hii itaendelea kwa wengine katika jamii kama tusipoungana pamoja kuidhibiti.


JJ
 
mwenye ile makala please aniwekee hapa nijue woga wote huu kwa CCM na serikali yake unatokana na nini?

Usiwe mvivu wa kusoma mkuu. Kabla ya kureply walau pitia page mbili tatu ili ujue kinachoendelea kabla ya kupost!! Ni Ushauri tu tena wa Bure!!!

 
Safi Kubenea,ila ukisoma ile makala ktk Tanzania Daima ilistahili Polisi wote wa vyeo vya chini wajitokeze kumdhamini kwani makala ile iliwazindua kutoka ktk fikra mfu
 

Mkuu Mnyika,

Wewe ndiye uliyesign yale makubaliano kati ya Serikali na CDM. Kwa kuwa inasemekana kuwa serikali imekwenda kinyume na makubaliano yenu, je unaweza kutupa dondoo za hayo makubaliano??

Binafsi mpaka sasa sielewi kwa nini mlikubali kusign!!
 
Ni lini mhariri wa UHURU atakamatwa kwa uchochezi?
 
Mwigamba hana kesi. Makala ni nzuri na ya kuelimisha. Hakuna uchochezi hapo. Kukamatwa kwake kunaashiria kufilisika kifikra kwa serikali ya magamba.
 
Btn now na 2015 watakamatwa watu wengi sana wenye kuipinga ccm na utawala wake... ndo dalili za sikio la kufa
 
i definetely agree with the article Good Job Samson.
 
Safi Kubenea,ila ukisoma ile makala ktk Tanzania Daima ilistahili Polisi wote wa vyeo vya chini wajitokeze kumdhamini kwani makala ile iliwazindua kutoka ktk fikra mfu

Hivi hamuwezi weka hapa ili tujikumbushe tu.
 
Mimi ninavyoona kinachoendelea hapo kwenye story ya Mwigamba ni kuhusu maisha yake kwa ufupi na alichojifunza kuhusu dola ya CCM na anatoa fundisho kwa wengine.

Kwa mfano alichokifanya huko chuo cha magereza hakuna tofauti na kile tulichokifanya wengi wetu tuliopiti jeshini enzi hizo (JKT). Ndiyo maana huwa nasemaga kuwa hiki kizazi cha JKT ndiyo Tatizo kubwa kwa mabadiliko Bongo!!!
 

kachochea kitu gani?
 

Mr. Zero,

Nilichosaini ni "Taarifa kwa Vyombo vya Habari" ambayo ilitoa kwa umma masuala mawili ambayo tulikubaliana. Hatukukubaliana Rais asaini ile sheria, kwa kuwa suala la kusaini au kutokusaini ni kwa kadiri mamlaka yake ya katiba ibara ya 97 na ibara ya 37 inatamka bayana kwamba Rais halazimiki kufuata ushauri wa mtu yoyote.

Na sababu moja wapo ya kumueleza Rais asisaini kati ya nyingi ambazo zilielezwa kwa kina kwenye waraka kwa Rais ni hilo la kuwepo kwa kifungu cha kifungo cha hadi miaka saba au faini ya hadi milioni 15 au vyote kwa kukusanya maoni au kutoa elimu kuhusu mabadiliko ya katiba kwa kile kilichoelezwa kuwa kinyume na sheria husika.

Baadhi ya masuala ambayo umeyauliza tayari nilishayatolea majibu kwenye mkutano na wanahabari baada ya Rais kusaini sheria husika unaweza ukaingia www.chadema.tv utapata sehemu ya majibu.



JJ
 
Kwa kufuata taaluma na maadili ya uandishi katika vyombo vya habari mhariri ametoka nje ya uringo wake kwa kuruhusu makala au barua kama hii ichapishwe kwenye gazeti lake. Mhariri ana mamlaka ya kukubali au kukataa makala au habari ambayo kwa haki alizo nazo pamoja na busara yake kulinda chombo chake cha habari.

Mhariri alikuwa na haki ya kuihariri kama kuna kitu ambacho kinaonyesha kuhamasihsa kinyume cha sheria. Na kama mleta mada alikataa angeweza kuiweka kapuini, ila kwa uamuzi wake wa kuichapa alijua nini kitatokea na ndicho kilichotokea.

Kwa habari hii kama ilivyotokea kwenye gazeti lake vigumu kumtetea, kwani siku zote kutanguliza busara ni kinga kwa kazi na wajibu.
 

Mkuu sijaona tatizo lolote katika makala/barua aliyoruhusu mhariri kutolewa katika gazeti. real sijaona, zaidi naona wazi uoga wa wakubwa wa polisi tu. Askari wadogo wananyimwa hata haki zao za msingi mfano mafao wanapohamishwa,lkn hawatakiwi kuhoji cause of dhana ya kutii mamlaka ya wakubwa,but kimsingi wananyanyasika
 
“your blood,yet more my blood shall irrigate victory“
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…