Absalom Kibanda: Namuogopa Abdurahman Kinana

WOWOWO

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2011
Posts
599
Reaction score
456
Great Thinkers,
Baada ya kuisoma makala hii ya Absalom Kibanda Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, nimejikuta napata mashaka sana na zaidi kupoteza imani na uzalendo wake. Pia nimejikuta nikiamini maneno niliyokuwa nikiyapata kijiweni kwamba Kibanda ni mmoja wa beneficieries wa Ufisadi kutoka tasnia ya Habari nchini.

My Take:
-Hapo kwenye RED naona Kibanda kajikita katika kueleza kifo tarajiwa cha upinzani kwa kumezwa na rekodi ya kinana tu bila hata kuzingatia nyakati zilizopo za kisiasa, kupwaya kwa ushindi wa JK kwneye matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na zaidi mchoko wa kimaisha walionao watanzania sasa. Kibanda amejaza mahaba binafsi kwa Kinana pasipo kuzingatia muktadha wa kisiasa uliopo nchini.

Lakini pia Kibanda amejikita katika kusisitiza hatari ya upinzani kufa kutokana na Kinana kuwa GS wa CCM bila kueleza ni kwa vipi anaweza kupambana na hoja zinazotoka kambi ya upinzani hasa CDM au ni Uluteni wake tu Jeshini ndiyo utamfanya aue upinzani.

Aidha, Kibanda anatumia Umeneja Kampeni wa Kinana kwa wagombea wa urais wa CCM bila hata kusumbua kichwa chake,kwamba kuwa meneja haina maana unakuwa incharge wa ushindi wa mgombea bali timu nzima ya kampeni ya Chama ndiyo hufanya kazi hiyo. Mathalan, utamsifu vipi Kinana kwa ushindi wa Mkapa mwaka 1995 wakati Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kivuri chake kilikuwa bado kinaishi ndani ya mioyo ya watanzania? Ni kweli hili si la kubeza lakini si la kumpa credit kubwa kiasi anachotoa Kibanda

-Kwenye Blue, Kibanda kawa kipofu kiasi kwamba kwakwe yeye tuhuma za ufisadi zinazomkabili Kinana na baadhi ya wana safu wa Sekretarieti mpya ya CCM anaziona nyepesi na zisizo na mashiko. Kwake yeye (Ufisadi ni mwepesi na si hoja kwa sasa) bali hoja ni Kinana na rekodi yake tu tena ya huko nyuma.

Tujadili kwa pamoja hii makala.

PIA, SOMA:

-
Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa
 
Muogope sana. Juzi tu katuhumiwa kusafirisha meno ya tembo kupitia kampuni yake yani ukicheza anaweza akakusafirisha na ww.
 
Ama kweli Tanzania bado tuna safari ndefu sana kufikia Ukombozi! Yaani Mwandishi wa Habari anathubutu kuandika Makala ya kuita "hoja ya Ufisadi" kuwa ni "Hoja Dhaifu"!!! Kama mpaka Tasnia ya Habari imeshafisadiwa ki-fikra kiasi hiki, tutawezaje kuutokomeza huo Ufisadi??? Tafakari!!!
 
Ama kweli CCM mtahangaika sana kufufua maiti, yaani mnapamba visivyopambika

Kibanda ameonesha sura yake halisi lakini pia napata shaka sana na uwezo wake wa uchambuzi wa mambo maana makala imekosa vitu vingi vya kumfanya afikishe hitimisho lake.
 
Kibanda ni miongoni mwa wahariri wachache ambao mimi binafsi nilishapoteza imani na makala zao, tangu pale alipoanza kumvurumishia makombora Samuel Sitta na kumsafisha Lowasa.

Kwamba kwake yeye ufisadi wa Samwel Sitta wa kununua madawa ya shilingi milioni mbili na kujenga ofisi ya spika ya sh.500 milioni jimboni kwake urambo ni zaidi ya ufisadi ambao umekuwa ukifanywa na Lowasa miaka nenda rudi na ambao kimsingi umeliingiza taifa hili katika matatizo makubwa sana ya kiuchumi na kusababisha umasikini mkubwa kwa watanzania.

Hapa tulipofika si mahali pa kuwahofia wanaccm na hasa huyo kinana, kinachomsumbua kibanda ni kuwa anaishi katika mwavuli wa historia ya kinana. Anasahau haraka kiasi kwamba ni kinana huyu huyu aliyekuwa kampeni manager wa kikwete na tukashuhudia mporomoko wa kura za kikwete kwa kiasi cha 20%, kama uwezo na mikakati ya kinana ni ya hali ya juu kwanini mwaka 2010 ameshindwa kumpa mgombea wao ushindi wa kishindo kama alivyofanya 2005 na kwa mkapa 1995 na 2000?

Kwa hali ya ccm ya sasa hawana namna yoyote ya kujinasua na anguko , hata kama watamteua nani kuwaongoza kwakuwa walipokifikisha chama chao ni beyond repair na ni muhimu kuzingatia kuwa watanzania hawa wamekuwa wakijitambua taratibu na kutodanganyika kirahsi kama ambavyo kibanda anadhani.
 
Sasa nimeanza kupata picha halisi kuwa jamaa kanunuliwa sio na mafisadi ila na fisadi PAPA lowasa
 
Kibanda ameonesha sura yake halisi lakini pia napata shaka sana na uwezo wake wa uchambuzi wa mambo maana makala imekosa vitu vingi vya kumfanya afikishe hitimisho lake.

Nadhani wengi hamumjui Kibanda, mimi hiyo Makala niliona online nilipoanza kuisoma wala sikupoteza muda wangu kuendelea kuisoma maana ni ushuzi mtupu.

Ni kweli Kibanda anamuogopa Kinana kwa sababu Kibanda ni kibaraka wa Lowasa na uwepo wa Kinana kama katibu Mkuu wa CCM si habari njema kwa kina Kibanda & co, huyu ni mtu wa ovyo sana.

Namshangaa sana Freeman Mbowe kuendelea kumvumilia Mhariri mpumbavu wa namna na kusababi Gazeti la Tanzania Daima kushuka mvuto na kupitwa na Gazeti la Mwananchi wakati mwanzo Tanzania Daima ndio lilikuwa linaongoza. Kama kuna mtu ambaye yupo karibu na Mbowe na anapenda Tanzania Daima lifanye vizuri basi huyu Kibanda afutwe kazi mara moja na nafasi yake apewe Ansbert Ngurumo.
 

Kwanza nianze kwa kusema, Great Thinker hawezi kujenga hitimisho kwa kusoma makala moja ya mwandishi ambayo ukiichunguza kwa undani inajaribu tu kueleza wasifu wa mlengwa (Kinana).

Nafikili umeisoma makala kwa jicho moja huku tayari ukiwa una mawazo hasi kwa mlengwa (Kinana), matokeo yake hata mwandishi wa makala naye utamuona ni hasi.

Huu ndiyo ukweli, Kinana kwa kiasi kikubwa ameiwezesha CCM kujikusanya wakati wa kampeni zote za marais katika mfumo wa vyama vingi nchini. Hata pale ambapo kampeni za mwisho (2010) za urais zilitawaliwa na makundi aliweza pia kuyakutanisha na kuwa kitu kimoja.

Kelele za mizengwe haziwezi kufuta ukweli. linapokuja swala la oganaizesheni, Kinana ni kinara kwa hilo.

Kazi ya Ukatibu mkuu wa chama siyo kila kukicha kupiga kelele majukwaani kama wengi wanavyoaminishwa, bali ni oganaizesheni ndani ya chama.

kumuhukumu Absalom Kibanda kwa hili na kusema ni puppet wa mafisadi ni kutomtendea haki ukilinganisha na makala zake nyingi nyingine alizoandika pamoja na kwamba kila kitu Tanzania kinawezekana.
 
Umahiri wa Kinana kiutendaji siuoni na in fact ni kosa kubwa tena sana kumpima Kinana kwa nafasi ya Kampeni Meneja wa chaguzi zetu ambazo siyo huru na haki. Sura halisi ya Kibanda sasa ipo wazi. Huyu tunayemsoma sasa ndiye Kibanda mwenyewe. Yule wa mwanzo alikuwa feki. Kibanda genuine ni huyu anayedhihaki vita dhidi ya ufisadi na bila shaka atakuwa tayari amevuta mlungula unaotokana na huo ufisadi.
 
kajichokea, najua baada ya kumaliza kuandika utumbo wake alimpelekea kinana asome kwanza ndio akatoa gazetini. njaa kitu mbaya sana.amenichefua!
 
Honesty is a very expensive GIFT. Do not expect it from cheap people.LIKE KIBANDA Nau sio Mwita Maranya?

Nimekusoma nivea lakini nikuulize kitu, una uhakika kwamba kibanda amekuwa honesty katika hii makala yake ama anamtumikia kafiri apate mradi wake. Angekuwa honesty kama angekiri tu kwamba ana maslahi na mtu/watu hao.

Ukijitahidi kuunganisha dots utaona ni kwanini kibanda anaandika makala very cheap kama hii. Tafuta uhusiano ama ukaribu/umbali wa Kinana na Lowasa ndipo ujue kilichopo nyuma ya pazia.


Hakuna namna yoyote mtu unaweza kuwa honest kwa kutetea ufisadi na mafisadi. Angekuwa honest angewashambulia wote kwakuwa hakuna fisadi mdogo wala mkubwa.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…