Achana na UTT, unazijua "Mutual Funds" za sekta binafsi?

Achana na UTT, unazijua "Mutual Funds" za sekta binafsi?

Nmechek mkuu hao TIMIZA FUND speed yao ya upandaji wa vipande vyao ni hatari sana yani thamani ya kipande kinapanda kwa 0.04 kwa siku sio zile fursa kweli kikaja kilio.

Maana yake mtu ukiwa na 2,000,000 una wastani wa kupata 80,000 kwa siku
Mmmh ngoja wataalamu waje
Mkuu greater than mbona hukutupitisha humu.
Boss piga hesabu zako vizuri.
Inayopanda ni bei ya kipande accumulatively na sio ""each shilling""

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Na wapi wanaweza hizo pesa ni utata pia,
Hapana sio utata.
Kabla hujawekeza unatakiwa kusoma Financial books zao.
private funds nyingi hawasemi ukweli,
Ukweli unapatikana kwenye Financial books.
Mimi pesa yangu Kwa bongo ni bond za serikali tuu, hao default ni almost zero na 25 year bond ni kama 16%, very good money kama hutaki usumbufu, tatizo ni inflation tuu
Kila fund agent ana utamu wake kwa kile ukitakacho.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Inaweza ikawa poa shida inakuja pale ukitaka kuchukua chako mchakato hausumbui ? Au haichukui muda mrefu?
Ni Open ended, kuchukua fedha hawasumbui.
Unauza vipande, unasubiri siku 3 basi unaikuta pesa yako kwenye account.
Ni hekima kuwekeza sehemu ambapo utapata pesa zako kwa urahisi pale utapozihitaji...

RE: 👇👇
Financial market ya bongo inajikongoja, ila kwenye hili takwa lako IPI VIZURI.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Atalia Mtu Muda Wowote Kuanzia Sasa
Tafuta elimu ni bure.
Punguza Upimbi.

Mimi nipo FAIDA FUND, na lengo langu ni kukuza mtaji ili ninunue aset fulani ya kutumika dukani.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Sijajua kulitokea nini ila kuna mtu alikwenda huko kimyakimya baada ya mwaka mmoja akarudi na mikono kichwani
Kakudanganya.
Mikono kichwani specifically hasa, KWENYE NINI??

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Mutual fund zoteee duniani ni wawekezaji.
Wanachofanya, wanachukua/wanakusanya hela kwa wananchi halafu ile hela wanawekeza sehemu mbalimbali kama Hisa, Fixed, na Governmnet bonds.
Na kiwango cha mgao wako inategemea na bei ya kipande kwa hiyo siku.

Utofauti upo kwenye Kiwango cha kuingilia kwenye mfuko na "minimum amount" ya kununulia hivyo vipande (kuendelea kuwekeza).

Mfano; FAIDA FUND wao unaingilia na 10,000 na kuwekeza kila mara ni 5,000

Kwenye asilimia za faida, Mutual fund zotee TZ riba kwa mwaka hua ni 10% - 13%
Hii ni kutokana na kwamba bado Mutual fund bongo ni jambo geni.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
Sasa kama faida inalingana kwanini nihame UTT ambako ni salama niende kwa hao wapya?
 
Tafuta elimu ni bure.
Punguza Upimbi.

Mimi nipo FAIDA FUND, na lengo langu ni kukuza mtaji ili ninunue aset fulani ya kutumika dukani.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
Unajua we jamaa mie nakuheshimu sana, alafu mwana Liverpool mwenzangu, ila kwa hili suala sijui kwanini unanikwaza. Sio mara ya kwanza unaongelea Faida Fund, lakini unaishia kuitaja tu. Tukikuuliza ina nini cha ziada kuliko UTT sijawahi kukuona ukijibu. Huu uzi nilijua una madini,lakini umeishia kutaja tu hizo mutual funds, ikiwa ni jambo zuri kuweka awareness huoni kama ingefaa zaidi awareness creation ikifuatana na elimu ya suala husika?
 
INTRODUCTION:-
Mpo raia wotee hasa chama langu la KATAA NDOA??
Mmejiandaaje na 23/09 THE REVOLUTION DAY??

BODY:-
Anyway; turudi kwenye mada.

Ukitoa hizi harakati za ""KATAA NDOA"" mimi bana ni msomi, sijui nijiite hivyo??

Ila kifupi nina elimu ya Finance, Economics, and Investment niliyoipatia kwenye Degree na Masters.

Ilikuwa kidogoo niende kusoma PhD duniani huko ila nilighairi na kuamua ""Kutafuta hela kwenye biashara"".
Nakiri wazi ""Napenda hela balaaaa""

Sasa hapa naongea na wale wanaona wao kwao biashara ni risk na kuamua kukimbilia kwenye Passive income.
Ila ndugu zangu hata Active income ""You can make money while sleeping..!!!""
Hivyo msikimbie sanaa biashara.
SCENARIO.
Humu ndani raia huwa wanaongelea sanaa Mutual Fund, ila huongelea mutual fund za taasisi mbili tu
1. 98% Wanaongelea UTT chini ya Wizara ya Fedha
2. 2% Wanaongelea FAIDA FUND chini ya Wizara ya Utumishi kupitia kwa Watumishi Housing.
ila je mnajua kuwa zipo Mutual Fund za Sekta binafsi??

Hizi hapa....
1. Government.
UTT Amins Funds
 Faida Fund

2. Private.
Timiza Fund
Sanlam Investment Fund
 Alpha Halal Fund
Inuka Money Market Fund

CONCLUSION.
Kwanini uwekeze tu kwenye UTT hizi nyengine umezisoma ukazielewa au UNAZIJUA HATA??

Siku zotee kabla hujaamua kufanya jambo, lisome kwanza halafu lielewe, halafu ndio ufanye maamuzi SAHIHI.
Karibuni kwa maswali kuhusu MUTUAL FUND.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
Mkuu umesahau ungetoa na tofauti zake na UTT ambao ndio umeshika hatam.. kwa research ndogo ya haraka nilioifanya kuna Mutual Funds ambazo ni private nyingi na nyingine ndio zimeanza maana yake hazina hata 5 yeas sokoni na wana ofa mfuko mmoja tu sio kama UTT ina mifuko tofauti kutokana na malengo yako

Mfano faida fund ndo wameanza hawana mfuko wa gawio wao ni unakuza mtaji hawa pia ni serikali

Wale halal hawa ndio wapya sana, nafikiri ni kampuni ya Audit wameamua kuja na package moya ya mutual fund sokoni.. Sanlam pia nao kenya wana Mutual Fund kubwa tu, hapa bongo hawajaweka nguvu sana tena sasa hivi sanlam kaamua kuingia ubia na Voda ndio wamekuja na M wekeza
Kwa kifupi uko sahihi kuna MF nyingine sio UTT peke yake.

Kimachofanya watu wakimbilie UTT. Moja ni kuwa kwa miaka Ya karibuni wamekuwa agressive kwenye kujitangaza tofauti na hizo private.. pili wana mtaji wa kuwa na miaka mingi sokoni maana yake mtu anashawishika kirahisi akiangalia history ya mfuko kwa miaka 20 iliopita..

tatu sababu ni serikali maana yake wanapata ensorsement kirahis kutoka serikalini na hata viongoz wakubwa waliopo na wastaafu wako humo mfano Sumaye yuko UTT toka inaanza huko 2004, pengine ana mabilion ya shilingi sasa hivi

Nne custodian wa mfuko nae ni bank ambayo imejipambanua kuwa na faida kubwa miaka Ya karibuni (CRDB) na wao inaonekana wako karibu na serikali sasa hivi kuliko hata NMB wenyewe

Mpaka wamehost infrastructure Bond wakaipa na jina la mheshimiwa na viongoz kibao wa serikalin wananunua

private ila bado hazijashika soko ndio wameanza na wengi hawana mifuko mmoja au miwili na hawatoi gawio la mwezi so kwa anayetaka magawio ya mwez hapata mfaa ila anaetaka kukuza mtaji patamfaa

Pia private hawajitangazi sana yaan kama hujabahatika kuingia kwenye website zao hutowaona popote

Walau hata Faida fund ambao nao ni serikali walipozindua walifanya promo
 
Back
Top Bottom