Pre GE2025 ACT waongea baada ya Nondo kupatikana, wasema alipigwa sana na alikuwa kwenye kitisho cha kifo

Pre GE2025 ACT waongea baada ya Nondo kupatikana, wasema alipigwa sana na alikuwa kwenye kitisho cha kifo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Wakuu,


Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Isihaka Mchinjita amesema kuwa Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa chama hicho Abdul Nondo amepigwa sana na kuumizwa sana pia kwa hali aliyonayo hawezi kuzungumza vizuri.

Mchinjita ameyasema hayo usiku huu (2:15 Disemba 02, 2024) baada ya kufika katika hospitali ya Aga Khan alipolazwa Nondo na kueleza kuwa baada ya kutekwa kwa Nondo alifungwa kitambaa cheusi na kupigwa sana huku akitishiwa kifo.

Pia soma:
Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

“maelezo yake ni kwamba alipotolewa pale stendi ya Magufuli alifungwa kitambaa kwa hiyo hakuwa anaona baada ya hapo amekuwa akipigwa muda mrefu baadae walisitisha kwenye eneo ambalo halifahamu baadae alitupwa pale Coco Beach ambapo walimfungua kitambaa na pingu na alibaini kwamba yupo Coco Beach na akaomba msaada”.

Soma pia: Taarifa ya Polisi kuhusu kutekwa kwa Abdul Nondo sijaielewa

Kuhusu kitu ambacho Nondo alikuwa anaambiwa na watekaji Mchinjita amesema “maelezo anaytoa (Abdul Nondo) ni kwamba alipigwa na alikuwa kwenye kitisho cha kifo na yeye alipopelekwa pale Coco Beach na pale baharini alijua ni hatma yake kwa sababu alikuwa amefungwa na wakamuacha kwenye lile eneo lakini baadae akatishwa tu kwamba akikamatwa tena basi hawatomuachia”.
 
Mhhhh.....
Mbona tena maelezo ya mwenyekiti hayaeleweki..🤔

Wakati anapigwa alikua anaambiwa nini??

Alipo tupwa coco, aliomba msaada kwa nani??

Kidogo inafikirisha usiku wa saa nne/tano unapo omba msaada eneo kama koko nani atakuamini na kubeba msala huku akiona muhusika anahali mbaya??
Au ndio tuhitimishe kama wahenga walivyosema mganga karudisha kuku...😜
 
Mhhhh.....
Mbona tena maelezo ya mwenyekiti hayaeleweki..🤔

Wakati anapigwa alikua anaambiwa nini??

Alipo tupwa coco, aliomba msaada kwa nani??

Kidogo inafikirisha usiku wa saa nne/tano unapo omba msaada eneo kama koko nani atakuamini na kubeba msala huku akiona muhusika anahali mbaya??
Au ndio tuhitimishe kama wahenga walivyosema mganga karudisha kuku...😜
Inaonekana Kuna ukweli unaujua.ebu tuambie tusije kuwapa lawama polisi bure
 
D
Mhhhh.....
Mbona tena maelezo ya mwenyekiti hayaeleweki..🤔

Wakati anapigwa alikua anaambiwa nini??

Alipo tupwa coco, aliomba msaada kwa nani??

Kidogo inafikirisha usiku wa saa nne/tano unapo omba msaada eneo kama koko nani atakuamini na kubeba msala huku akiona muhusika anahali mbaya??
Au ndio tuhitimishe kama wahenga walivyosema mganga karudisha kuku...😜
Uh! Umeshangaza sana. Yaani mtu akiwa kwenye hali mbaya sana, watu hawawezi kumsaidia!! Wakati kwa watu wenye akili timamu, unachokisema ni kinyume chake. Kwa mwenye akili timamu, mtu aliyepo kwenye hali mbaya sana ndiye watu humsaidia kwa haraka.

Mara 3 nimewahi kuwachukua watu waliogongwa na magari, na kuwakimbiza haraka hospitali, wakiwa hawajitambhi, na sijui kama walipona au la, ila mimi nilitekeleza wajibu wangu wa kiutu.

Polisi walinishukuru sana na kusema kuna watu wa ajabu, wakiona mtu amegongwa na gari, wanamkimbia huyo majeruhi, huku wakieneza maneno ya uwongo, kuwa eti ukimsaidia aliyegongwa na gari, unageuziwa kesi kuwa ni wewe uliyemgonga. Labda hao ndiyo wenye mawazo kama hayo ya kwako.

Mimi katika hizo mara zote 3, polisi walinishukuru, na hakuna hata mmoja aliyewahi kunisumbua kwa lolote, zaidi ya kuombwa tu details zangu.
 
Rais yupo upande wa watekaji au upande wa wanaotekwa?
Km jeshi lake la polisi au usalama hawahusiki na huu utekaji yeye anajitengaje na huu utekaji?
Lini katoa onyo kwa watekaji?
Wazee wastaafu wa rank ya juu hawasikii hawaoni yanayoendelea?
Wao wako upande upi?
Wameshindwa kumshauri rais juu ya haya yanayoendelea au kwa sababu wanaotekwa si wanaccm?
 
D

Uh! Umeshangaza sana. Yaani mtu akiwa kwenye hali mbaya sana, watu hawawezi kumsaidia!! Wakati kwa watu wenye akili timamu, unachokisema ni kinyume chake. Kwa mwenye akili timamu, mtu aliyepo kwenye hali mbaya sana ndiye watu humsaidia kwa haraka.

Mara 3 nimewahi kuwachukua watu waliogongwa na magari, na kuwakimbiza haraka hospitali, wakiwa hawajitambhi, na sijui kama walipona au la, ila mimi nilitekeleza wajibu wangu wa kiutu.

Polisi walinishukuru sana na kusema kuna watu wa ajabu, wakiona mtu amegongwa na gari, wanamkimbia huyo majeruhi, huku wakieneza maneno ya uwongo, kuwa eti ukimsaidia aliyegongwa na gari, unageuziwa kesi kuwa ni wewe uliyemgonga. Labda hao ndiyo wenye mawazo kama hayo ya kwako.

Mimi katika hizo mara zote 3, polisi walinishukuru, na hakuna hata mmoja aliyewahi kunisumbua kwa lolote, zaidi ya kuombwa tu details zangu.
Una bahati sana ya kusaidia watu watatu mahututi.
 
Mhhhh.....
Mbona tena maelezo ya mwenyekiti hayaeleweki..🤔

Wakati anapigwa alikua anaambiwa nini??

Alipo tupwa coco, aliomba msaada kwa nani??

Kidogo inafikirisha usiku wa saa nne/tano unapo omba msaada eneo kama koko nani atakuamini na kubeba msala huku akiona muhusika anahali mbaya??
Au ndio tuhitimishe kama wahenga walivyosema mganga karudisha kuku...😜
Na wanadai alikuwa hawezi kuongea. Vipi huo msaada aliombaje??
 
Rais yupo upande wa watekaji au upande wa wanaotekwa?
Km jeshi lake la polisi au usalama hawahusiki na huu utekaji yeye anajitengaje na huu utekaji?
Lini katoa onyo kwa watekaji?
Wazee wastaafu wa rank ya juu hawasikii hawaoni yanayoendelea?
Wao wako upande upi?
Wameshindwa kumshauri rais juu ya haya yanayoendelea au kwa sababu wanaotekwa si wanaccm?
Taifa letu linaelekea mahali pabaya sana san!
 
Mhhhh.....
Mbona tena maelezo ya mwenyekiti hayaeleweki..🤔

Wakati anapigwa alikua anaambiwa nini??

Alipo tupwa coco, aliomba msaada kwa nani??

Kidogo inafikirisha usiku wa saa nne/tano unapo omba msaada eneo kama koko nani atakuamini na kubeba msala huku akiona muhusika anahali mbaya??
Au ndio tuhitimishe kama wahenga walivyosema mganga karudisha kuku...😜
Mimi nasisitiza kuwa maswali yako yannikumbusha mbali namna nilivyodanganya alafu kujibu maswali magumu siwezi
 
Mhhhh.....
Mbona tena maelezo ya mwenyekiti hayaeleweki..🤔

Wakati anapigwa alikua anaambiwa nini??

Alipo tupwa coco, aliomba msaada kwa nani??

Kidogo inafikirisha usiku wa saa nne/tano unapo omba msaada eneo kama koko nani atakuamini na kubeba msala huku akiona muhusika anahali mbaya??
Au ndio tuhitimishe kama wahenga walivyosema mganga karudisha kuku...😜
cha msingi wanajua watanzania ni waelewa ndiyo maana hata zile sarakasi za utekwaji wa moh'd dewji ziliisha kwa namna hii, na wakiona jamii inahoji sana wanaachia connection ya mtu na ndiyo kazi ya spin doctors.
 
Kujuliza maswali sio vibaya ni katika kutafuta ukweli.

Eneo la coco Beach lilivyo kwa usiku watu hawapitipiti labda,kama alitupwa kando ya barabara eneo la coco beach. Ikiwa walimtupa ndani ufukweni au kule kwenye machaka kwenye mawemawe au kando kabisa ya ufukwe katika mchanga ni vigumu kwa usiku mwingi ule Nondo kuonekana na angeonekana asubuhi na wale wanaoenda ufukweni kuufanya nazoezi.

Haya maelezo tuliyoambiwa hadi sasa yanatia shaka mtu asiyejiweza kutokana na kuumizwa aliwezaje kuomba msaada je alinyanyuka akasogea hadi barabarani akaomba msaada?
 
Kujuliza maswali sio vibaya ni katika kutafuta ukweli.

Eneo la coco Beach lilivyo kwa usiku watu hawapitipiti labda,kama alitupwa kando ya barabara eneo la coco beach. Ikiwa walimtupa ndani ufukweni au kule kwenye machaka kwenye mawemawe au kando kabisa ya ufukwe katika mchanga ni vigumu kwa usiku mwingi ule Nondo kuonekana na angeonekana asubuhi na wale wanaoenda ufukweni kuufanya nazoezi.

Haya maelezo tuliyoambiwa hadi sasa yanatia shaka mtu asiyejiweza kutokana na kuumizwa aliwezaje kuomba msaada je alinyanyuka akasogea hadi barabarani akaomba msaada?
Je,umejiuliza pia ni vipi kama waliosaidia nao ni waliopo kwenye mpango wa utekeji ili alieteswa asikate moto ikaleta kelele.

Ni dhahania tu kama hiyo mliyonayo maana unaweza kutekwa ukaachwa eneo lisilopitika na watu lakini msaada ukapata kwa hao hao watekaji wakasimama kama watoa msaada ili kuacha maswali ya namna hii.

Kumbuka hii ni mara yake ya pili,ile ya kwanza wanasema hadi perfume alikuwa kajipulizia.
 
Back
Top Bottom