Pre GE2025 ACT waongea baada ya Nondo kupatikana, wasema alipigwa sana na alikuwa kwenye kitisho cha kifo

Pre GE2025 ACT waongea baada ya Nondo kupatikana, wasema alipigwa sana na alikuwa kwenye kitisho cha kifo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
D

Uh! Umeshangaza sana. Yaani mtu akiwa kwenye hali mbaya sana, watu hawawezi kumsaidia!! Wakati kwa watu wenye akili timamu, unachokisema ni kinyume chake. Kwa mwenye akili timamu, mtu aliyepo kwenye hali mbaya sana ndiye watu humsaidia kwa haraka.

Mara 3 nimewahi kuwachukua watu waliogongwa na magari, na kuwakimbiza haraka hospitali, wakiwa hawajitambhi, na sijui kama walipona au la, ila mimi nilitekeleza wajibu wangu wa kiutu.

Polisi walinishukuru sana na kusema kuna watu wa ajabu, wakiona mtu amegongwa na gari, wanamkimbia huyo majeruhi, huku wakieneza maneno ya uwongo, kuwa eti ukimsaidia aliyegongwa na gari, unageuziwa kesi kuwa ni wewe uliyemgonga. Labda hao ndiyo wenye mawazo kama hayo ya kwako.

Mimi katika hizo mara zote 3, polisi walinishukuru, na hakuna hata mmoja aliyewahi kunisumbua kwa lolote, zaidi ya kuombwa tu details zangu.
Mkuu 'Bams', nadhani hukuelewa alicho lenga aliye uliza maswali (Ushman).
Huo utu wema kama ulio uonyesha wewe ndiyo inayo takiwa hiyo. Hukuwa na hofu yoyote na usalama wako ulipo kuwa unafanya wema huo. Maeneo ya hapo ulipo toa msaada hukuwa na mashaka nayo; na pengine ilikuwa ni mchana.

Hapo 'Coco beach' pana sifa yake; na wakati wenyewe ni usiku!
Huyo/hao wasamaria wema pengine walikuwa ni watu zaidi ya mmoja. Siyo rahisi kwa mtu mmoja kusimama maeneo hayo usiku
Sasa, huyu /hawa wasamaria wema walombwa na majeruhi awahishwe kwenye ofisi za chama; au hospitalini, au hata katika mikono ya polisi kwa usalama? Ni nani hawa/huyu msamaria mwema?
Wewe polisi wali kushukuru; kwa sababu ulifuata taratibu za kujitambulisha kwao, au siyo?
 
Inawezekana unatoka kwenye "ujinga" ukielekea kwenye upumbavu. Sina njia ya kukusaidia hilo lisitokee.
Bora Mimi kuliko wewe uliyejaza matope kichwani hata Mimi Sina msaada wa kukusaidia
 
Kujuliza maswali sio vibaya ni katika kutafuta ukweli.

Eneo la coco Beach lilivyo kwa usiku watu hawapitipiti labda,kama alitupwa kando ya barabara eneo la coco beach. Ikiwa walimtupa ndani ufukweni au kule kwenye machaka kwenye mawemawe au kando kabisa ya ufukwe katika mchanga ni vigumu kwa usiku mwingi ule Nondo kuonekana na angeonekana asubuhi na wale wanaoenda ufukweni kuufanya nazoezi.

Haya maelezo tuliyoambiwa hadi sasa yanatia shaka mtu asiyejiweza kutokana na kuumizwa aliwezaje kuomba msaada je alinyanyuka akasogea hadi barabarani akaomba msaada?
Tanzania ujuaji mwingi ndio maana tunaendelea kutekwa. Yaani mnahoji Kana kwamba ACT wanadanganya au kwamba Nondo alijiteka? Kwamba Serikali haihusiki? Yaani mtu aje na AK 47 mchana kweupe na asidakwe?

Tuendelee tu kutekwa na kuuwawa labda wakifa kama Soka au Kibao ndio tutaaamini
 
Huna ubora wowote, tokana na uchafu mwingi unao toka akilini mwako.
Wee ni mpumbavu.unaweza kutuambia nondo alifikaje coco beach kutoka stend ya magufuli?
Tumia akili japo kidogo basi
 
Wee ni mpumbavu.unaweza kutuambia nondo alifikaje coco beach kutoka stend ya magufuli?
Tumia akili japo kidogo basi
hayo ume yasoma wapi?
Hii hali yako mpya "upumbavu" naona bado hujaizoea vizuri. Tulizana kidogo uanze kuizoea hali hiyo kwanza.
 
hayo ume yasoma wapi?
Hii hali yako mpya "upumbavu" naona bado hujaizoea vizuri. Tulizana kidogo uanze kuizoea hali hiyo kwanza.
🤣🤣🤣.ebu meza kwanza dawa zako.maana hata haujui kinachoendelea kumbe.naona unadandia magari kwa mbele tu.kwa heri
 
🤣🤣🤣.ebu meza kwanza dawa zako.maana hata haujui kinachoendelea kumbe.naona unadandia magari kwa mbele tu.kwa heri
Inabidi nicheke tu, kwa jinsi ulivyo na upungufu mkubwa wa uelewa.
 
Rais yupo upande wa watekaji au upande wa wanaotekwa?
Km jeshi lake la polisi au usalama hawahusiki na huu utekaji yeye anajitengaje na huu utekaji?
Lini katoa onyo kwa watekaji?
Wazee wastaafu wa rank ya juu hawasikii hawaoni yanayoendelea?
Wao wako upande upi?
Wameshindwa kumshauri rais juu ya haya yanayoendelea au kwa sababu wanaotekwa si wanaccm?
Huwezi juwa, huenda yeye mwenyewe (Rais) ni mateka!
Ingawa nina mashaka makubwa na wazo hili.
 
Mimi yote najiuliza na nimeshajiuliza.

All in all kwa upande wangu naamini alitekwa.
Kutekwa ni kweli kabisa alitekwa. Lakini hapo pa kunusurika kifo(Kuuawa) ni kwa kudra ya Mwenyezi Mungu tuu na wala sio kwa ujanja wake.
 
Wakuu,


Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Isihaka Mchinjita amesema kuwa Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa chama hicho Abdul Nondo amepigwa sana na kuumizwa sana pia kwa hali aliyonayo hawezi kuzungumza vizuri.

Mchinjita ameyasema hayo usiku huu (2:15 Disemba 02, 2024) baada ya kufika katika hospitali ya Aga Khan alipolazwa Nondo na kueleza kuwa baada ya kutekwa kwa Nondo alifungwa kitambaa cheusi na kupigwa sana huku akitishiwa kifo.

Pia soma: Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

“maelezo yake ni kwamba alipotolewa pale stendi ya Magufuli alifungwa kitambaa kwa hiyo hakuwa anaona baada ya hapo amekuwa akipigwa muda mrefu baadae walisitisha kwenye eneo ambalo halifahamu baadae alitupwa pale Coco Beach ambapo walimfungua kitambaa na pingu na alibaini kwamba yupo Coco Beach na akaomba msaada”.

Soma pia: Taarifa ya Polisi kuhusu kutekwa kwa Abdul Nondo sijaielewa

Kuhusu kitu ambacho Nondo alikuwa anaambiwa na watekaji Mchinjita amesema “maelezo anaytoa (Abdul Nondo) ni kwamba alipigwa na alikuwa kwenye kitisho cha kifo na yeye alipopelekwa pale Coco Beach na pale baharini alijua ni hatma yake kwa sababu alikuwa amefungwa na wakamuacha kwenye lile eneo lakini baadae akatishwa tu kwamba akikamatwa tena basi hawatomuachia”.
Naona kama tumepigwa vile.

Haya maelezo ni kama soap opera
 
Huwezi juwa, huenda yeye mwenyewe (Rais) ni mateka!
Ingawa nina mashaka makubwa na wazo hili.
Sidhani kama ni mateka, kifo cha Mzee Kibao wakati akihutubia maafisa wa polisi asingekipuuzia na kusema kifo ni kifo tu, halafu akawashukia mataifa ya nje yaliyokuwa yakikosoa
 
Sidhani kama ni mateka, kifo cha Mzee Kibao wakati akihutubia maafisa wa polisi asingekipuuzia na kusema kifo ni kifo tu, halafu akawashukia mataifa ya nje yaliyokuwa yakikosoa
EEeeeeenHEEeeee!

Hilo la "kuwashukia mataifa ya nje..." ilikuwa ni igizo ambalo hata mtoto mdogo asinge kubali kuwa igizo lime fana.

Unajuwa, kujivimbisha huko mbele za jeshi la polisi na wananchi, ni njia nzuri ya kuwahakikishia watekaji kuwa mtu wao yupo kwenye mstari?
Hawezi kujitokeza mbele za wananchi na kujionyesha yeye siyo 'in-charge', hata kama yupo chini ya amri za watekaji.
Kwa hiyo hapo usiweke tafsiri hiyo ikufanye kuamini kwamba yeye siyo mateka.
Sasa ninayo mashaka makubwa juu ya huyu mama; kama kweli anaongoza nchi kwa utashi wake.
 
EEeeeeenHEEeeee!

Hilo la "kuwashukia mataifa ya nje..." ilikuwa ni igizo ambalo hata mtoto mdogo asinge kubali kuwa igizo lime fana.

Unajuwa, kujivimbisha huko mbele za jeshi la polisi na wananchi, ni njia nzuri ya kuwahakikishia watekaji kuwa mtu wao yupo kwenye mstari?
Hawezi kujitokeza mbele za wananchi na kujionyesha yeye siyo 'in-charge', hata kama yupo chini ya amri za watekaji.
Kwa hiyo hapo usiweke tafsiri hiyo ikufanye kuamini kwamba yeye siyo mateka.
Sasa ninayo mashaka makubwa juu ya huyu mama; kama kweli anaongoza nchi kwa utashi wake.
Wise Man Kalamu unataka kusema ni mateka kivipi?
 
Wise Man Kalamu unataka kusema ni mateka kivipi?
Kwamba kuna kundi linalo mshikilia na kumtisha kwamba asipo fanya mambo kadhaa wataondoa ushirikiano wao kwake; au kundi linalo mdanganya kwamba asipo fanya haya ya kutisha watu hataendelea kwenye uongozi.

Ukiangalia historia yake tokea ameshika wadhifa huo, amekuwa ni mtu wa kuyumba yumba sana. Kwanza alitaka kuwafurahisha lile kundi la marehemu Magufuli, kwa "Kazi iendelee"; na Mbowe angali jela kwa ugaidi wa kutungwa na yeye raisi kakandamiza zaidi kwa kubainisha kuwa magaidi wengine walio shirikiana na Mbowe tayari walikuwa jela!

Lakini wakati huo huo akitamani pia aonekane na mataifa ya nje na wafadhiri kuwa yeye ni tofauti na yule aliye mrithi . hapo ukaona maswala ya "Mazungumzo ya Maridhiano".

Pengine makundi tunayo kisia kumteka, ni hayo hayo yanayo sababisha kuyumba yumba sana katika maamuzi yake.
Unaweza pia kupata picha ya kutokuwa imara kwake hata katika teuzi anazo fanya mara kwa mara. Ni kama anaamrishwa na mtu pembeni - mtoe Palamagamba na Lukuvi; mlete Bashite pale; na kabla hawajatulia, walete ndani ya serikali wakusaidie kuendelea na madaraka 2025!

Mambo yote haya hayafanywi na mtu mwenye msimamo, anaye juwa anacho fanya yeye mwenyewe.

Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo yanaweza kuchangia dhana ya "Rais kuwa Mateka". Yapo mengi ukiyatafakari vizuri.
 
Kuhusu kitu ambacho Nondo alikuwa anaambiwa na watekaji Mchinjita amesema “maelezo anaytoa (Abdul Nondo) ni kwamba alipigwa na alikuwa kwenye kitisho cha kifo na yeye alipopelekwa pale Coco Beach na
Pole Ndugu Nondo.
===
Maelezo hayajakamilika. Walikuwa wanamueleza nini ya kwa nini wanamtishia kifo?
 
tuliyoambiwa hadi sasa yanatia shaka mtu asiyejiweza kutokana na kuumizwa aliwezaje kuomba msaada je alinyanyuka akasogea hadi barabarani akaomba msaada?
Tena amefungwa kitambaa usoni!
 
Wana balance utekaji hakuna lolote.......maigizo tu CDM ndio walemgwa sio ACT...period
 
Je,umejiuliza pia ni vipi kama waliosaidia nao ni waliopo kwenye mpango wa utekeji ili alieteswa asikate moto ikaleta kelele.

Ni dhahania tu kama hiyo mliyonayo maana unaweza kutekwa ukaachwa eneo lisilopitika na watu lakini msaada ukapata kwa hao hao watekaji wakasimama kama watoa msaada ili kuacha maswali ya namna hii.

Kumbuka hii ni mara yake ya pili,ile ya kwanza wanasema hadi perfume alikuwa kajipulizia.
Hii nadharia ina sound sana na ni very logic. Kama walivyofanya Mo Dewji... Baada ya kupigiwa kelele sana juu ya utekaji na mauaji mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea wakatafuta mtu maarufu/tycon ili kutengeneza drama na lengo lilikuwa sio kumdhuru wala kupata chochote kutoka kwake(pesa) ila tu kutengeneza drama ku cover up uhuni wao.
 
Back
Top Bottom