Pre GE2025 ACT waongea baada ya Nondo kupatikana, wasema alipigwa sana na alikuwa kwenye kitisho cha kifo

Pre GE2025 ACT waongea baada ya Nondo kupatikana, wasema alipigwa sana na alikuwa kwenye kitisho cha kifo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wakuu,


Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Isihaka Mchinjita amesema kuwa Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa chama hicho Abdul Nondo amepigwa sana na kuumizwa sana pia kwa hali aliyonayo hawezi kuzungumza vizuri.

Mchinjita ameyasema hayo usiku huu (2:15 Disemba 02, 2024) baada ya kufika katika hospitali ya Aga Khan alipolazwa Nondo na kueleza kuwa baada ya kutekwa kwa Nondo alifungwa kitambaa cheusi na kupigwa sana huku akitishiwa kifo.

“maelezo yake ni kwamba alipotolewa pale stendi ya Magufuli alifungwa kitambaa kwa hiyo hakuwa anaona baada ya hapo amekuwa akipigwa muda mrefu baadae walisitisha kwenye eneo ambalo halifahamu baadae alitupwa pale Coco Beach ambapo walimfungua kitambaa na pingu na alibaini kwamba yupo Coco Beach na akaomba msaada”.

Kuhusu kitu ambacho Nondo alikuwa anaambiwa na watekaji Mchinjita amesema “maelezo anaytoa (Abdul Nondo) ni kwamba alipigwa na alikuwa kwenye kitisho cha kifo na yeye alipopelekwa pale Coco Beach na pale baharini alijua ni hatma yake kwa sababu alikuwa amefungwa na wakamuacha kwenye lile eneo lakini baadae akatishwa tu kwamba akikamatwa tena basi hawatomuachia”.
Hii nchi kupaza sauti tu hakutoshi bali ni kuchukua hatua. Haiwezekani watu tukaaminishwa kuwa tuko huru na wakati tunanyimwa hata tu uhuru wa kuongea. Ifike wakati tuseme sasa basi. Ila kama tutaendelea kulialia hivi hata wao wahusika wa matukio hayo watajiona wameweza. Matukio haya yanaumiza sana ila kama hayajakugusa moja kwa moja yawezekana usinielewe.
 
D

Uh! Umeshangaza sana. Yaani mtu akiwa kwenye hali mbaya sana, watu hawawezi kumsaidia!! Wakati kwa watu wenye akili timamu, unachokisema ni kinyume chake. Kwa mwenye akili timamu, mtu aliyepo kwenye hali mbaya sana ndiye watu humsaidia kwa haraka.

Mara 3 nimewahi kuwachukua watu waliogongwa na magari, na kuwakimbiza haraka hospitali, wakiwa hawajitambhi, na sijui kama walipona au la, ila mimi nilitekeleza wajibu wangu wa kiutu.

Polisi walinishukuru sana na kusema kuna watu wa ajabu, wakiona mtu amegongwa na gari, wanamkimbia huyo majeruhi, huku wakieneza maneno ya uwongo, kuwa eti ukimsaidia aliyegongwa na gari, unageuziwa kesi kuwa ni wewe uliyemgonga. Labda hao ndiyo wenye mawazo kama hayo ya kwako.

Mimi katika hizo mara zote 3, polisi walinishukuru, na hakuna hata mmoja aliyewahi kunisumbua kwa lolote, zaidi ya kuombwa tu details zangu.
Huu ndio utu kuna watu hawana utu kabisa!! Eti msalaba! Jamani!!
 
Wakuu,


Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Isihaka Mchinjita amesema kuwa Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa chama hicho Abdul Nondo amepigwa sana na kuumizwa sana pia kwa hali aliyonayo hawezi kuzungumza vizuri.

Mchinjita ameyasema hayo usiku huu (2:15 Disemba 02, 2024) baada ya kufika katika hospitali ya Aga Khan alipolazwa Nondo na kueleza kuwa baada ya kutekwa kwa Nondo alifungwa kitambaa cheusi na kupigwa sana huku akitishiwa kifo.

Pia soma: Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

“maelezo yake ni kwamba alipotolewa pale stendi ya Magufuli alifungwa kitambaa kwa hiyo hakuwa anaona baada ya hapo amekuwa akipigwa muda mrefu baadae walisitisha kwenye eneo ambalo halifahamu baadae alitupwa pale Coco Beach ambapo walimfungua kitambaa na pingu na alibaini kwamba yupo Coco Beach na akaomba msaada”.

Soma pia: Taarifa ya Polisi kuhusu kutekwa kwa Abdul Nondo sijaielewa

Kuhusu kitu ambacho Nondo alikuwa anaambiwa na watekaji Mchinjita amesema “maelezo anaytoa (Abdul Nondo) ni kwamba alipigwa na alikuwa kwenye kitisho cha kifo na yeye alipopelekwa pale Coco Beach na pale baharini alijua ni hatma yake kwa sababu alikuwa amefungwa na wakamuacha kwenye lile eneo lakini baadae akatishwa tu kwamba akikamatwa tena basi hawatomuachia”.
Ushrikiano uliokuwepo kwenye hii kadhia kati ya viongozi ACT na polisi ni kama ule wa yule mwandishi aliotekeshwa na wanaosemekana ni wafanyabiashara wenzake. Nasubiri pongezi kwa jeshi la polisi kutuka ACT
 
Isipokuwa tuwe wakweli ACT wamepambana sana kwa uharaka mkubwa na kufanikisha kumpatia. CDM wao hawako makini kwa mfano akina Soka na wengineo
 
Isipokuwa tuwe wakweli ACT wamepambana sana kwa uharaka mkubwa na kufanikisha kumpatia. CDM wao hawako makini kwa mfano akina Soka na wengineo
Hawakua na nia ya kummaliza, Mzee Kibao mbona taarifa zilitoka mapema sana na CDM walipiga kelele sana, Akina Soka CDM pia walipambana na walipaza sana Sauti mpaka mwenyekiti akaitisha waandishi wa habari akaweka wazi mchoro wa tukio la akina Soka, Ulitaka wapambaneje?

Vipi Kuhusu Kombo Wa Tanga CDM walipaza Sauti kwa Mwezi Mzima ndo Polisi wakaja kusema wanae, Unataka CDM wapambaneje waunde jeshi?

Huu mkumbo wa kusifia eti ACT wamepambana naona ndo Ajenda yenyewe, Huu utekwaji wa Nondo unaanza kutia Mashaka kwa hizi sifa yawezakua hii ilikua drama
 
Je,umejiuliza pia ni vipi kama waliosaidia nao ni waliopo kwenye mpango wa utekeji ili alieteswa asikate moto ikaleta kelele.

Ni dhahania tu kama hiyo mliyonayo maana unaweza kutekwa ukaachwa eneo lisilopitika na watu lakini msaada ukapata kwa hao hao watekaji wakasimama kama watoa msaada ili kuacha maswali ya namna hii.

Kumbuka hii ni mara yake ya pili,ile ya kwanza wanasema hadi perfume alikuwa kajipulizia.
Je, na wewe uimejiuliza Sativa alinusurikaje?
Je, wanaosema ni Kudra ya mwenyezi Mungu huwa chanzo ni nini hadi watamke hivyo?
 
Point ya msingi na weledi haijaguswa, Je Nondo alipewa maelekezo gani hata kupelekea kutishiwa kifo endapo angekamatwa mara ya pili? Na maelekezo hayo alipewa kwa masilahi ya nani?
 
Tumuombe Yesu, aondoe viongozi wasio Linda wananchi wake.
Hii 👆 👆 inafikirisha sana. Kumbuka kwamba Viongozi waliopo madarakani tumewaweka uongozini ss wenyewe (mimi na wewe)tena kwa Hiari ya Utashi wetu(Free Will) na hatukumshirikisha huyo Yesu. Sasa iweje leo unataka umsumbue Yesu?? Mbona unataka kumwonea Yesu?
 
Wakuu,


Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Isihaka Mchinjita amesema kuwa Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa chama hicho Abdul Nondo amepigwa sana na kuumizwa sana pia kwa hali aliyonayo hawezi kuzungumza vizuri.

Mchinjita ameyasema hayo usiku huu (2:15 Disemba 02, 2024) baada ya kufika katika hospitali ya Aga Khan alipolazwa Nondo na kueleza kuwa baada ya kutekwa kwa Nondo alifungwa kitambaa cheusi na kupigwa sana huku akitishiwa kifo.

Pia soma: Dar: Abdul Nondo amechukuliwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

“maelezo yake ni kwamba alipotolewa pale stendi ya Magufuli alifungwa kitambaa kwa hiyo hakuwa anaona baada ya hapo amekuwa akipigwa muda mrefu baadae walisitisha kwenye eneo ambalo halifahamu baadae alitupwa pale Coco Beach ambapo walimfungua kitambaa na pingu na alibaini kwamba yupo Coco Beach na akaomba msaada”.

Soma pia: Taarifa ya Polisi kuhusu kutekwa kwa Abdul Nondo sijaielewa

Kuhusu kitu ambacho Nondo alikuwa anaambiwa na watekaji Mchinjita amesema “maelezo anaytoa (Abdul Nondo) ni kwamba alipigwa na alikuwa kwenye kitisho cha kifo na yeye alipopelekwa pale Coco Beach na pale baharini alijua ni hatma yake kwa sababu alikuwa amefungwa na wakamuacha kwenye lile eneo lakini baadae akatishwa tu kwamba akikamatwa tena basi hawatomuachia”.
waliokuwa wanampiga walitaka nini kwake? au walikuwa wakimuulia nini? hawezi kupigwa bila sababu hata kama ni ya kijinga
 
waliokuwa wanampiga walitaka nini kwake? au walikuwa wakimuulia nini? hawezi kupigwa bila sababu hata kama ni ya kijinga
Tumwombe Mungu amjalie wepesi wa kupona halafu atakuja kusema yy mwenyewe kwa kinywa chake. Kwa sasa ni mgonjwa amelazwa Hospitali.
 
Mhhhh.....
Mbona tena maelezo ya mwenyekiti hayaeleweki..🤔

Wakati anapigwa alikua anaambiwa nini??

Alipo tupwa coco, aliomba msaada kwa nani??

Kidogo inafikirisha usiku wa saa nne/tano unapo omba msaada eneo kama koko nani atakuamini na kubeba msala huku akiona muhusika anahali mbaya??
Au ndio tuhitimishe kama wahenga walivyosema mganga karudisha kuku...😜
Nawaonea huruma vijana wanasiasa wa Tanzania, mnapoteza muda bure tu kuwapigania hao mnaowapigania, wenzenu hawana time na nyie na wanawadhiaki,


Achaneni na siasa za upinzani Vijana kina Nondo na wengine,pambanieni maisha yenu na familia yenu, Mnaona wenzenu kina Kafulila, Kina joshua Nasary,petrobas Katambi,na wengineo wapo serikalini wanakula maisha,

Mna hatarisha uhai wenu kutetea vibwengo.
Tanzania itaendelea kuwepo hata ikiliwa vipi,

Unganeni na wengine mle mema ya nchi.
 
D

Uh! Umeshangaza sana. Yaani mtu akiwa kwenye hali mbaya sana, watu hawawezi kumsaidia!! Wakati kwa watu wenye akili timamu, unachokisema ni kinyume chake. Kwa mwenye akili timamu, mtu aliyepo kwenye hali mbaya sana ndiye watu humsaidia kwa haraka.

Mara 3 nimewahi kuwachukua watu waliogongwa na magari, na kuwakimbiza haraka hospitali, wakiwa hawajitambhi, na sijui kama walipona au la, ila mimi nilitekeleza wajibu wangu wa kiutu.

Polisi walinishukuru sana na kusema kuna watu wa ajabu, wakiona mtu amegongwa na gari, wanamkimbia huyo majeruhi, huku wakieneza maneno ya uwongo, kuwa eti ukimsaidia aliyegongwa na gari, unageuziwa kesi kuwa ni wewe uliyemgonga. Labda hao ndiyo wenye mawazo kama hayo ya kwako.

Mimi katika hizo mara zote 3, polisi walinishukuru, na hakuna hata mmoja aliyewahi kunisumbua kwa lolote, zaidi ya kuombwa tu details zangu.
Umeeleza vizuri uliwakimbiza Hospital sasa kweli unamuokota mtu usiku kaumia sana unampeleka kwenye ofisi ya chama??? mhhh hebu tunyoshe maelezo hapa.
 
Hii nchi kupaza sauti tu hakutoshi bali ni kuchukua hatua. Haiwezekani watu tukaaminishwa kuwa tuko huru na wakati tunanyimwa hata tu uhuru wa kuongea. Ifike wakati tuseme sasa basi. Ila kama tutaendelea kulialia hivi hata wao wahusika wa matukio hayo watajiona wameweza. Matukio haya yanaumiza sana ila kama hayajakugusa moja kwa moja yawezekana usinielewe.
anza mkuu toka tu barabarani sisi nyuma yako
 
Mhhhh.....
Mbona tena maelezo ya mwenyekiti hayaeleweki..🤔

Wakati anapigwa alikua anaambiwa nini??

Alipo tupwa coco, aliomba msaada kwa nani??

Kidogo inafikirisha usiku wa saa nne/tano unapo omba msaada eneo kama koko nani atakuamini na kubeba msala huku akiona muhusika anahali mbaya??
Au ndio tuhitimishe kama wahenga walivyosema mganga karudisha kuku...😜
Una shida gani Kwani!?
 
Back
Top Bottom