ACT Wazalendo Kunani? Membe aonekana uwanja wa ndege JKNIA, akimbia kampeni?

Maji ya shingo...ahahah
 
hyu sie yule aliesema niguse ninuke, hivi majuzi nimemsikia tena akisema hatorudi nyuma wala hatajitoa kwenye ligi
anyway, muda ni hakimu
 
Lakini,huenda kapata dharura hivyo tusimuhukumu moja kwa moja bali tujipe muda ingawa dharura hiyo haipaswi kufanywa siri kama kweli kapata dharura.
hana pesa,hana watu,kampeni sio lelemama
 
Kuonekana kwa mgombea urais wa JMT mh Membe JNIA akikwea pipa kuelekea kusikojulikana kumezua sintofahamu ikiwemo furaha kubwa kwa makamanda wa Chadema na makada wa CCM.

Hadi sasa ACT wazalendo hawajatoa taarifa yoyote kuhusu taarifa za safari ya Membe zilizoenea mitandaoni.

Ndio najiuliza Membe kamkimbia nani mbona CCM na Chadema wote wanashangilia.

Maendeleo hayana vyama!
 
Hakuna mwanaccm aliyeshangilia mkuu..... Maccm yamenuna balaa maana kura zote kwa Tundu Lissu hata wakiiba vipi bado Lissu atashinda tu
 
Tusikubali kabisa Membe kumuunga mkono Lisu ni hatari kubwa. Huko ACT mpinzani wa kweli ni Maalim Seif na Wapemba wenzake. Lakini hawa wakina Zito ni kukaa nao kwa akili.
Hivi kuunga mkono kunasababishwa na muungaji au muungwaji ?

Kama mtu anasema ninakubaliana na wewe na uchofanya wewe utasema hapana haukubaliani au sikubaliani na wewe ?

Kama hakuna Quid Pro Qou who cares? Tatizo hizi siasa watu wanazifanya kama imani ya Dini au Ushabiki wa mpira ambao no matter what nyekundu haiwezi kuwa njano....
 
Ila wabongo wana mamidimo aiseee, they talk about anything anything aisee.

Kwa akili yawezekana CCM likatawala hata miska 500 tuna kizazi cha ovyo sana, na hatujui hata tunataka nini
 
Unaweza ukawa sahihi
Shida hata Mkuu wa chama ana muda hajasema jambo
Hope sivyo navyofikiri
 
Nimefuatilia na kuziangalia picha ambazo Mh. Membe - Mgombea urais kupitia ACT amepigwa akiwa JNIA zinaleta maswali mengi kuliko majbiu.
1. Nani alimpiga hizo picha?
2. Kwa nini apigwe picha bila hata ridhaa yake?
3. Kwa nini ziwekwe kwenye mitandao ya kijamii na wengine hasa viongozi wa kisiasa kuzitolea matamko?

Ni kweli watu hupiga picha wakiwa Airport lakini ukiangalia makini na hasa picha ya pili, inaonesha kabisa ni CCTV camera ya Airport ndiyo ilitumika.
Sasa swali nani aliruhusu zitoke/downloaded kutoka harddisk au server ya Security System ya Airport na kwa minajili gani?
Huyo aliyeruhusu zitoke sio mtu mdogo lazima atakuwa na mamlaka pale Uwanjani, je hili si kosa kisheria?

Kuna jambo hapo la kufikirika hapo!



 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…