ACT Wazalendo Kunani? Membe aonekana uwanja wa ndege JKNIA, akimbia kampeni?

ACT Wazalendo Kunani? Membe aonekana uwanja wa ndege JKNIA, akimbia kampeni?

Simu hizo mkuu .watakuwa abiria hao.Simu zimebadili kila kitu

Kama umeenda uwanja mpya, hakuna ghorofa kwa juu ambalo unaweza kumuona mtu wa chini kama hiyo picha ya pili, that's means ni cctv camera
 
Kuna mahala nimemsikia akijiapiza kwamba hatajitoa ng'o, yeye ni mbele kwa mbele...
Membe kama mgombea uraisi katuangusha,japo kasema tarehe 15 utakuwa muziki mzito wa vyombo vya ala .
Zitto labda amemkorofisha japo sina uhakika.
 
Kuonekana kwa mgombea urais wa JMT mh Membe JNIA akikwea pipa kuelekea kusikojulikana kumezua sintofahamu ikiwemo furaha kubwa kwa makamanda wa Chadema na makada wa CCM.

Hadi sasa ACT wazalendo hawajatoa taarifa yoyote kuhusu taarifa za safari ya Membe zilizoenea mitandaoni.

Ndio najiuliza Membe kamkimbia nani mbona CCM na Chadema wote wanashangilia.

Maendeleo hayana vyama!
Kaka mkubwa kampa stop.Labda hasira, ndio kaamua kwenda ughaibuni.
Lakini kama bado yumo sioni upenyo wa kuleta furaha ACT-WAZALENDO
 
Si nasikia na Zito nae kapanda Bombadear kwenda Kigoma, yeye kapitia airport gani kwani?.
 
Karata ni moja ya michezo inayopendwa na majasusi.

Ila kuna majasusi wanaweza kuaminiwa kuja kuwa maraisi wa nchi, Putin wa Russia akiwa ni mfano.

Ila Bernard Membe maadili yanamzuia kwa kila idara.

Haiwezekani yeye kuwa raisi wa nchi hii.
 
Membe kama mgombea uraisi katuangusha,japo kasema tarehe 15 utakuwa muziki mzito wa vyombo vya ala .
Zitto labda amemkorofisha japo sina uhakika.

Wabongo bwana, kwani mnajua anaenda wapi? Hahaha kama anaenda kenya hapo
 
Kweli hapo panafikirisha

Picha kama ni za CCTV zimetokaje na kwanini. Afu kiongozi wa chama anazitafsir picha , kwa maana ni dhahiri walilipanga hili.

Nawapongeza mliofanikisha kuikwepa hii plan B ya hasimu

Inanikumbusha picha ya Lipumba 2015 ile ya Rwanda ilivyovuja..
 
Back
Top Bottom