ACT-Wazalendo na CHADEMA wamefanya pakubwa ila sisi Wananchi ndiyo tumewaangusha. Tusiwaingilie katika maamuzi yoyote wanayochukua baada ya Uchaguzi

ACT-Wazalendo na CHADEMA wamefanya pakubwa ila sisi Wananchi ndiyo tumewaangusha. Tusiwaingilie katika maamuzi yoyote wanayochukua baada ya Uchaguzi

M-mbabe

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2009
Posts
13,203
Reaction score
23,027
Wanaonifuatilia humu wanajua mimi ni CCM. Lakini ni ile iliyokuwa CCM ya Mwalimu (RIP mzee wetu), siyo hii CCM ya sasa iliyojaa ulaghai mtupu.

Kutokana na CCM kukengeuka, nimejikuta (siko peke yangu, tupo wengi sana) sina namna bali kuunga mkono jitihada na harakati zote zinazofanywa na vyama mbadala makini, hususani kwa sasa hivi ni ACT-Wazalendo na CHADEMA.

Sote tunakumbuka wakati wa kampeni kuelekea uchaguzi wa October 28, mikutano ya Maalim Seif kule visiwani ilikuwa inajaza nyomi ya kufa mtu. Halkadhalika huku bara, Tundu Lissu nyomi zake zilikuwa kwa mamilioni.

Watanzania wengi tunaamini, na dunia nzima pia inaamini uchaguzi wa mwaka huu Tundu Lissu alishinda kwa kura halali na Maalim Seif naye vivyo hivyo.

Baada ya uchaguzi kuporwa na CCM, wito kutoka kwa Tundu Lissu na Maalim Seif ulikuwa watu wote tuingie barabarani. Ni wito ambao ulikuwa pia ukisisitiziwa sana na viongozi hawa wakati wa kampeni.

Cha ajabu sasa, zile nyomi zilizokuwa zinakuja kwenye mikutano ya kampeni haijulikani zimepotelea wapi, hata ambapo viongozi wakuu wa vyama walipoanza kuwa persecuted na dola, sisi wananchi KIMYAA!

Wenzetu Kenya wana moja ya mifumo mizuri sana ya demokrasia nchini mwao, ni ya kupigiwa mfano si barani Africa pekee bali dunia nzima. Hii imetokana na kuwepo kwa katiba mpya ambayo ililazimika kupatikana baada ya kambi ya upinzani kudhulumiwa uchaguzi. Sote tunajua kilichotokea baada ya hapo.

Pointi yangu ni kwamba hakuna mahali popote chini ya jua mtu anapewa haki yake kwenye kishaza cha dhahabu. Hakuna, hakuna na hakuna!

Viongozi wa ACT-Wazelendo na CHADEMA wamejitahidi sana kwa kadri ya uwezo wao kufanya mass mobilization ili ku replicate zile jitihada za Kenya, lakini matokeo yake ni uthibitisho wa kauli chungu ya mzee Jomo Kenyatta aliyomtamkia Mwalimu Nyerere kuwa "wewe huko Tanzania unaongoza makondoo" (not the exact quote but no mistake about the content).

Sasa, sasa.... kwa vile sisi Watanzania tumeshindwa kuwa wafuasi wazuri wa hawa viongozi wa hivi vyama viwili mbadala, basi tusiviingilie hata kidogo katika maamuzi yoyote watakayoona yanafaa now and going forward kwa ajili ya mustakabali wa vyama vyao.

Kuna mijadala inaendelea kwenye media kutoka kwa wafuasi na wasio wafuasi wa ACT/CHADEMA kuhusu eti wafanye au wasifanye nini baada ya kuporwa uchaguzi na dola, ilihali wananchi hao wameshindwa kufanya kile vyama hivi kiliwaomba kufanya (yaani mass revolt) in the first place. Huu ni unafiki mkubwa wa Watanzania (makondoo a la mzee Jomo) na tabia zetu za kupenda vya kutelezea!

Annoyed,
Mwalimu M-mbabe.
 
Uwingi wa watu kwenye kampeni sio uhalisia wa kura,mimi nimehudhuria Mara nne hiyo mikutano ya kibaraka wa wazungu Lissu tena katika mikoa tofauti si kweli kwamba nilikuwa mfuasi wake Bali nilikuwa nam-zoom tu.

Kitu kingine ambacho wanaharaka kama akina Lissu na Lema hawajui ni kuwa wananchi hawako tayari kuchafua amani ya nchi yao kwa manufaa ya mtu ambaye hata urai wake haujulikani kwa sasa, sijui ni Mbeligiji au Mtanzania.
 
Kuna mijadala inaendelea kwenye media kutoka kwa wafuasi na wasio wafuasi wa ACT/Chadema kuhusu eti wafanye au wasifanye nini
Mwalimu M-mbabe.
Pole sana Mwalimu Mbabe

Waliovipa kura hivyo vyama sio wanachama wao pekee bali ni wananchi!.

Hivyo wananchi wana right ya kuvishauri vyama vyao baada ya kushindwa, lazima vifanye the right thing.

Viongozi wa baadhi vyama hawako kwenye the right thinking capacity, they don't think right, kuchanganyikiwa kushindwa kumewafanya kuwa na hali inayotwa preudo insanity, hivyo wanaweza kufanya rational decisions za ajabu.

Wale viongozi na wanachama wenye cool minds muwasaidie viongozi wa vyama vyenu kufanya maamuzi sahihi yenye public interest.

P
 
Sikutegemea jambo la ajabu kutoka kwa wafuasi wanaosubiri rais akosee kuongea kiingereza wambeze.

Watu wanasema mlitarajia yaote mahindi eneo mlilopanda changarawe.
 
Niliwahi kumpigia mpinzani kura mara moja tu na Dr.Slaa baada ya hapo huwa nampigia kura Dr.JPM
Wewe baki na CCM yako tu, mambo ya wapinzani tuwachie wapinzani
 
Hata huyo Dr. Slaa angekwambia uingie barabarani usingeingia.

Watanzania ni wanafki.

Slaa alimponza Josephina mkewe akapasuliwa na FFU nayeye binafsi akiwa mstari wa mbele, unadhani ni uthubutu kiasi gani huyo mtu amewaonyesha wafuasi wake?
 
Unasema Tundu Lissu alishinda kwa Kura halali? Kura zipi ? Au Kura za Twitter na JF! Hivi nyie mbona mnaota Sana CHADEMA! Tena ashukuru Sana hata kupata Kura hizo M1, hivi mlitegemea TL atafikisha Kura 6M kama alizopata lowassa 2015?

Kubalini Uchaguzi mmeshashi dwa ! Kelele hizi tulizitegemea Sana! Na Tatizo lenu hamkubali kuambiwa ukweli.
 
Kimsingi Tu wananchi hawapo aware kabisa na maandamano , ukitaka ukosane na mtanzania mwambie issue za fujo, mtanzania ni mtu wa bata na Amani zaidi ya hapo humpati.

Kuhusu kuibiwa kura mi nakataa, kuna wabunge kweli kura zao zimechakachuliwa ila kwenye uraisi Lissu kapigwa peupeee, na maraia wanajua ndo mana wanaona issue ya maandamano ni ngoma isiyochezeka, wanajua walichomfanyia Lissu kwenye sanduku, in short Tu wananchi ni wajumbe waliochangamka.

Na hii ya kuannounce maandamano ilikuwa ndo the greatest test Kwa Lissu kama kwel anakubalika mioyoni mwa watu na issue imeburst na kuonyesha kuwa most Tanzanian adult people hawamuelewi.
 
Unasema Tundu lissu alishinda kwa Kura halali? Kura zipi ? Au Kura za Twitter na JF! Hivi nyie mbona mnaota Sana CHADEMA! Tena ashukuru Sana hata kupata Kura hizo M1 ,hivi mlitegemea TL atafikisha Kura 6M kama alizopata lowassa 2015? .Kubalini Uchaguzi mmeshashi dwa ! Kelele hizi tulizitegemea Sana! Na Tatizo lenu hamkubali kuambiwa ukweli .
Usijitoe akili.

Hakukuwa na ushindani. Unaujua ushindani wewe? Ushindani unaongozwa na kusimamiwa na kanuni za ushindani. Pale kulikuwa na uhuni uliosimamiwa na NEC na Vyombo vya Dola.

Kwa Ushindani CCM haina ubavu wa Kushindana na CDM.
 
Uchaguzi ulikuwa huru na haki na msipolikubali hili vyama vyenu ndio vinakufa maana hamtaweza kutatua tatizo ambalo hamlijui.

Ukweli ni kwamba wananchi wa kawaida hawakupiga kura na hao ndio wanaowapigiaga kura wapinzani.

Kama uchaguzi hu ungekuwa sio wa haki basi sa hizi kungekuwa na kesi nyingi mahakamani za kupinga matokeo ya udiwani maana diwani ni rahisi kulinda kura zake na huwa wanaweka mawakala katika kila kituo.

Sasa kama madiwani wenu wamekubali kuwa wameshindwa kihalali hizo kura za wabunge na raisi mtazitoa wapi.
 
Tz bado kabisa kujitambua itachukua miaka 100. Hutakiwi ku risk maisha yako kwa sababu sabubu yao. Akili za kikoloni bado zipo kwa wengi. Imagine msomi anakwambia anatamani Magufuli aongezewe muda. Kwa hiyo kati ya watanzania wote anaaminika mwenye uwezo ni mmoja tu.
 
Back
Top Bottom