Adhabu ya kunyongwa hadi kufa ndio Siri ya uchumi mkubwa duniani

Adhabu ya kunyongwa hadi kufa ndio Siri ya uchumi mkubwa duniani

Sio katiba mkuu, ni uzalendo mtakuja kugundua mzizi wa yote ni ukosefu wa uzalendo unaochagizwa na katiba mbovu.

Uzalendo unapelekea usimamizi thabiti na usimamizi thabiti unapelekea kufuata katiba kwa ukamilifu!

Mihimili mitatu yote ifanye kazi bila kuwa na muingiliano na Head of State. Ili kuwe na uwezekano wa kumuwajibisha head of state bila kuogopa kwamba ndio mwenyekiti wa chama ama atawafutia uanachama.

Pia head of state asiwe mwenyekiti wa chama wala kuwa na influence yeyote kwa wanachama. Hii itasaidia sana chama kiwe stand alone entity.

Separate body ya kuwawajibisha wanachama iwepo kulingana na katiba na asie tekeleza jukumu lake la kumuwajibisha mkosefu kwa mujibu wa katiba aidha kwa upendeleo au kwa namna yeyote ile aachie ngazi straight away anakuwa amejifukuzisha kazi within stated days!
Mtoto anajifunza kukomba mboga kutoka kwa mzazi wake, huwezi kuwa mzalendo kama viongozi sio wazalendo. Mimi huwa naangalia tamthilia ya Ertugul pale Azam two kila SAA 4 usiku. Wale jamaa wanaigiza historia ya kweli kuhusu Ottoman empire. Ertugul bay ndio viongozi wao, lakini anaishi maisha yanayofanana Na watu anaowaongoza, wezi Na wasaliti wanachinjwa baada ya kujiridhisha kuwa kweli wana makosa. Maisha kama Yale ndiyo waliyoyapitia watu weupe tangu enzi hizo hadi Leo hii, kila MTU anafahamu kitakachompata kama atatenda kosa lolote LA kiuhujumu Na makosa mengine. Hawana huruma wanachinja baada ya kuthibitika pasipo shaka kuwa umetenda kosa.

Hapa kwetu wanaotuibia na kuuza madawa ya kulevya tunayo orodha yao vifuani mwetu, wanafahamika lakini watanzania wanashindwa kuwaondoa wala kuwaadhibu. Hali hii ni mpaka lini?
 
Nitajibu hilo la "viongozi"
Linaanzia kwa wananchi, kuwachagua viongozi wanaoamini wanaweza kushughulikia swala hilo kwa umakini mkubwa. Utaona hapa, tena tunarudi kwa "tatizo ni wananchi" wanaochagua viongozi wabovu

Laiti kama pangejitokeza na kiongozi mwenye msimamo thabiti, na mwenye uwezo wa kuwashawishi wananchi waelewe wajibu wao wa kuchagua viongozi imara, hapa tungekuwa tumeanza hatua muhimu.

Ngoja nikwambie jambo.
Pamoja na ubovu wote aliokuwa nao Magufuli, lakini katika swala la rushwa na mambo ya aina hiyo, watu waliweza kumwelewa (hata kama alikuwa akiwahadaa).
Basi atokee Magufuli mwingine, asiyekuwa na matabia mengine ya hovyo hovyo kama aliyokuwa nayo Magufuli, lakini akajitoa mhanga kabisa kusimamia sheria zinazobana jambo hili. Watu watamwelewa sana, na utaona hali inabadilika sana kuliko ilivyo sasa.

Hatuwezi kuacha kujishughulisha na tatizo eti kwa vile ni "tatizo la enzi na enzi". Si unaona utumwa ulikomeshwa? Kwa nini tusifanye tunayoweza kufanya kwa sasa kwa kufikiri tu kwamba ni tatizo la enzi na enzi?
Ndugu yangu kwanza uelewe kuwa biashara ya utumwa ilikomeshwa na wazungu na weusi waliokuwa utumwani waliokuwa na dhamiri ya kuthamini ubinadamu wengine kiasi cha kujitoa mhanga kama Benjamin Lay, Olaudah Equiano, Benjamin Rush, Elizabeth Freeman, Abraham Lincoln, nk.

Viongozi wa Afrika wa wakati huo hawakutaka biashara hiyo ikomeshwe. Walipigana kulinda biashara hiyo iendelee pale walipozuiwa kuifanya. Tena ajabu wengine tunawaita mashujaa.

Pili sidhani kama una ushahidi kwamba Magufuli alipambana kwa dhati dhidi ya rushwa na ufisadi. Alijitoa mhanga? Kivipi? Alipiga kelele sana majukwaani lakini kipindi chake wizi na matumizi mabaya serikalini viliendelea kwa kiwango kikubwa sana (ripoti za CAG). Na alizuia habari za ufisadi serikalini kuandikwa/kutangazwa kwenye vyombo vya habari.

Tatu nina hakika hata wewe unajua jinsi serikali ya Magufuli ilivyovuruga chaguzi za 2019 na 2020 na kunyima wananchi fursa ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Rais wa sasa akiwa mgombea mwenza 2020 akihutubia katika kampeni kanda ya Ziwa aliwaambia wananchi wasipoteze kura zao kwa kupigia upande mwingine. Itakuwa kama kuunga kijiko cha sukari ziwani kwani hata wakipigia kura upande mwingine CCM ndiyo itakayounda serikali.

Wananchi wanachaguaje viongozi bora katika mazingira ya aina hiyo?
 
Pili sidhani kama una ushahidi kwamba Magufuli alipambana kwa dhati dhidi ya rushwa na ufisadi. Alijitoa mhanga? Kivipi? Alipiga kelele sana majukwaani lakini kipindi chake wizi na matumizi mabaya serikalini viliendelea kwa kiwango kikubwa sana (ripoti za CAG). Na alizuia habari za ufisadi serikalini kuandikwa/kutangazwa kwenye vyombo vya habari.
Mkuu, unaweza kunionyesha popote katika niliyoandika panapoonyesha nikisema "kwamba Magufuli alipambana kwa dhati dhidi ya rushwa na ufisadi..."?
Ndugu yangu kwanza uelewe kuwa biashara ya utumwa ilikomeshwa na wazungu na weusi waliokuwa utumwani waliokuwa na dhamiri ya kuthamini ubinadamu wengine kiasi cha kujitoa mhanga kama Benjamin Lay, Olaudah Equiano, Benjamin Rush, Elizabeth Freeman, Abraham Lincoln, nk.

Viongozi wa Afrika wa wakati huo hawakutaka biashara hiyo ikomeshwe. Walipigana kulinda biashara hiyo iendelee pale walipozuiwa kuifanya. Tena ajabu wengine tunawaita mashujaa.

Pili sidhani kama una ushahidi kwamba Magufuli alipambana kwa dhati dhidi ya rushwa na ufisadi. Alijitoa mhanga? Kivipi? Alipiga kelele sana majukwaani lakini kipindi chake wizi na matumizi mabaya serikalini viliendelea kwa kiwango kikubwa sana (ripoti za CAG). Na alizuia habari za ufisadi serikalini kuandikwa/kutangazwa kwenye vyombo vya habari.

Tatu nina hakika hata wewe unajua jinsi serikali ya Magufuli ilivyovuruga chaguzi za 2019 na 2020 na kunyima wananchi fursa ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Rais wa sasa akiwa mgombea mwenza 2020 akihutubia katika kampeni kanda ya Ziwa aliwaambia wananchi wasipoteze kura zao kwa kupigia upande mwingine. Itakuwa kama kuunga kijiko cha sukari ziwani kwani hata wakipigia kura upande mwingine CCM ndiyo itakayounda serikali.

Wananchi wanachaguaje viongozi bora katika mazingira ya aina hiyo?
Ninashangaa sana kwa andiko lako hili.
Ni kama hukusoma kabisa niliyoandika mimi, lakini ukaona ni lazima unihusishe na hayo unayoyaweka hapa, hata kama ni kinyume kabisa na niliyoandika.
 
Ni kweli kabisa, na adhabu ya kifo ikitiliwa mkazo, CCM karibia wote ni marehemu...
 
Mkuu, unaweza kunionyesha popote katika niliyoandika panapoonyesha nikisema "kwamba Magufuli alipambana kwa dhati dhidi ya rushwa na ufisadi..."?

Ninashangaa sana kwa andiko lako hili.
Ni kama hukusoma kabisa niliyoandika mimi, lakini ukaona ni lazima unihusishe na hayo unayoyaweka hapa, hata kama ni kinyume kabisa na niliyoandika.
Kwangu mimi ukimpa Magufuli sifa ya kusimamia sheria that’s a red line. Alikuwa mlaghai aliyeaminiwa na watu wenye ufahamu haba na uwezo mdogo wa kupambanua kati ya propaganda na uhalisia.

Si aina ya kiongozi wa kutajwa kama mfano kwa chochote tunapotafuta viongozi bora.
 
Kwangu mimi ukimpa Magufuli sifa ya kusimamia sheria that’s a red line.
Mkuu, naona unapiga kivyako tu bila lengo.

Unarukia mtu ambaye ungejiongeza kidogo tu usingehangaika na kupoteza muda huu wote unaopoteza kueleza mambo yasiyomhusu unayemweleza mambo hayo.

Nadhani unajaribu ku'project' mawazo yako yawe yangu, halafu uyatafutie jibu unalotaka wewe.
Si aina ya kiongozi wa kutajwa kama mfano kwa chochote tunapotafuta viongozi bora.
Inawezekana ukawa na tatizo la kuelewa unachokisoma, au unarukia tu kujibu bila ya kutafakari na kuelewa kilichoelezwa.
 
Umenena vyema Tza fisadi afungwi ulipa faini mbuzi kibaka ufungwa sababu hana pesa ya kumuhonga hakimu.
Tutaendelea na hivi hadi lini? Nani aje kuibadili hii hali kwa niaba yetu?
 
Bila kuweka sheria watawala wa kiafrica kuishia jela tusitegemee maendeleo
 
Kwangu mimi ukimpa Magufuli sifa ya kusimamia sheria that’s a red line. Alikuwa mlaghai aliyeaminiwa na watu wenye ufahamu haba na uwezo mdogo wa kupambanua kati ya propaganda na uhalisia.

Si aina ya kiongozi wa kutajwa kama mfano kwa chochote tunapotafuta viongozi bora.
AAA, yule Mzee wacha tu apunzike kwa amani, alipaswa kuwa Mchungaji kanisani badala ya kuwa rais, maana muda wote alikuwa akimtaja Mungu, Malaika Na shetani. Ni njia ya kuwapumbaza watu sawa Na wakoloni walivyotupumbaza Na makanisa Na misikiti wakati wanatuibia Mali zetu. Wakoloni walikuwa walikuwa wakibatizwa Na kusali makanisani bila ya maaskofu kuwanyooshea vidole kuhusu wizi wa Mali za waafrika Na hata biashara mbaya ya utumwa. Wakoloni walikuwa wanaiba Mali zetu Na kuuza watumwa Na kutoa sadaka kwenye nyumba za ibada wanakosali.

Magufuli alikuwa anatupa false hopes Na mazuzu walikuwa wanapiga vigelegele. Mimi Nina uhakika kuwa mama Samia hakukuta kitu hazina, ila hasemi tu. Tuliaminishwa kuwa tz ni tajiri lakini tunaomba tujengewe shule chato, tujengewe msikiti, uwanja wa mpira Na kukopa kwa sana. Deni LA taifa likaonhezeka ghafla bin vuu. Alituamisha kuwa safari za nje ni uhuni usiokubalika akasababisha nchi kudumaa kifikra Na kiuchumi.
 
Viongozi wetu eti wanaogopa kutia saini muuaji aliyethibitika kuua wenzie anyongwe, eti wanaona ni sifa njema hiyo, lakini kila siku kiguu na njia kwenda kuomba misaada kwa nchi zinazonyonga watu wao kwa uhujumu uchumi na madawa ya kulevya
 
Bwashee, una maana sasa hivi akina Jakaya Mrisho Kikwete na Edward Ngoyai Lowassa wangeshakuwa historia tayari?
 
Mkuu rasrimali ya kwanza katika uchumi ni mtu. So ukimtia mimba mtoto wa shule umechangia kumfanya asifikie malengo na huenda huyu ndo angekuja kuwa muinua uchumi so mtia mimba nadhani anakuwa kahujumu uchumi. Adhabu kwa watia mimba wanafunzi iongezeke
 
Hatukusanyi kodi na tunakwepa kodi, hata hiyo kidogo tunayokusanya inaibwa na wajanja wenzetu tunaowafahamu kwa majina, sura, jinsia, kabila, dini na cheo. Wakati mwingine wanaiba na kwenda kuficha kwa wazungu wanaotukopetesha hela zetu hizohizo na kutudai riba kubwa.
 
Back
Top Bottom