Adhabu ya kunyongwa hadi kufa ndio Siri ya uchumi mkubwa duniani

Adhabu ya kunyongwa hadi kufa ndio Siri ya uchumi mkubwa duniani

Tunahitaji Katiba na muundo wa utawala wenye kuupa uwekezaji na biashara binafsi imani hadi ya miaka 50 mbele, tunahitaji mfumo wa uongozi unaotabirika sio matamko mapya kila kukicha, tunahitaji mfumo wa uongozi unaojitahidi kupunguza regulations, red tapes na kodi sio unaojitahidi na kujisifia kuongeza vitu hivyo.

Mfumo huo wa uongozi unahitaji kusimikwa juu ya katiba mpya iliyo thabiti na kuelekeza kwamba sisi ni taifa la kibepari. Bila hivyo mawazo ya Ujamaa na hodhi ya dola kwa chama kimoja vitaendelea kutufanya mafukara tunaoenda kwa mwendo wa Kobe.
Katiba yetu imejengwa kwenye misingi ya kikaburu na udikiteta. Yaani ni katiba inayotegemea maadili mema, huruma, utashi na ucha Mungu wa kiongozi Mkuu. Mkipata kiongozi kichaa, kaburu, dikteta na shoga wananchi hawana la kufanya wala cha kufanya kumzuia na kumuondoa zaidi tu ya kuinua mikono yao juu kumuomba Mungu amuondoe mwenyewe kiongozi huyo kwa njia yoyote inayoifahamu yeye.

Katiba hii inamfanya Kiongozi awaone wananchi kama wanyonge na sio mabosi wake anaopaswa kuwasikiliza wanachotaka.
 
Wachina ni wezi kweli kweli wakija Afrika lakini awathubutu kuiba China ni kifo Hakuna mchezo na kodi za watu.
 
Wizi, Utapeli na uongo upo kwenye damu tangu kuzaliwa

Imagine mtoto anaanza kuiba kalamu darasani
Na waalimu wanakula sandwitch za watoto kwa kuwaibia
Sasa hapo unategemea nini
 
Na hakika wachina ni wezi kweli, si unaona wanavyohangaika wanapokuja huku? Lakini kwao hawathubutu!

Naunga mkono kabisa mada, kwamba inabidi sasa pawe na mabadiliko ya kuukabili ufisadi ndani ya Tanzania. Njia hizi zilizopo hazisaidii chochote.

Unaona watu wanateuliwa, jambo la kwanza ni kupanga safu ya upigaji..., hii haileti maana kabisa. Tena hawa watu wanapoteuliwa unasikia vigelegele vya kuwachochea wakazoe mali za waTanzania. Hapo bandarini kwa mfano, ni kama tatizo la wizi ni kidonda kisichopona kiasi kwamba kila anayeteuliwa kwenda pale ni lazima ajihusishe na njama za kuliibia taifa. Ni kama wafanyakazi mahali pale, kazi yao kubwa ni kupanga njama za wizi tu!

Tabia hizi za ukwapuzi wa mali za taifa hili ni lazima zikomeshwe kwa njia zozote ziwezekanazo, hata kunyongwa hadi kufa kwa wanaothibitika kufanya hivyo.
Hii ikitokea, akili zitawaingia kichwani wahusika.
Nani amfunge PAKA,tunapiga kelele sababu ya njaa.
We umeoona waunga juhudi baada ya kukaribishwa mezani wameendelea kubweka? Bweka ufe njaa.
Wenzetu weupe wao utengeneza maisha ya Jamii nzima ifaidike ikiwemo na kizazi chao.Wakoloni weusi wao utengeneza maisha ya watoto wao at the wanaoishia kufaidi ni watoto wao na wajukuu zao wanarudi tena kwenye poverty circle ile ile ya Jamii nzima.
 
Tunahitaji Katiba na muundo wa utawala wenye kuupa uwekezaji na biashara binafsi imani hadi ya miaka 50 mbele, tunahitaji mfumo wa uongozi unaotabirika sio matamko mapya kila kukicha, tunahitaji mfumo wa uongozi unaojitahidi kupunguza regulations, red tapes na kodi sio unaojitahidi na kujisifia kuongeza vitu hivyo.

Mfumo huo wa uongozi unahitaji kusimikwa juu ya katiba mpya iliyo thabiti na kuelekeza kwamba sisi ni taifa la kibepari. Bila hivyo mawazo ya Ujamaa na hodhi ya dola kwa chama kimoja vitaendelea kutufanya mafukara tunaoenda kwa mwendo wa Kobe.
Bila hukumu Kali kwa wezi wa Mali ya umma yote hiyo itakuwa ni kazi bure, take my word, Wachina plus others hawakuwa wajinga kuweka sheria Kali kuhusu Mali za Umma !!
 
Nani amfunge PAKA,tunapiga kelele sababu ya njaa.
We umeoona waunga juhudi baada ya kukaribishwa mezani wameendelea kubweka? Bweka ufe njaa.
Wenzetu weupe wao utengeneza maisha ya Jamii nzima ifaidike ikiwemo na kizazi chao.Wakoloni weusi wao utengeneza maisha ya watoto wao at the wanaoishia kufaidi ni watoto wao na wajukuu zao wanarudi tena kwenye poverty circle ile ile ya Jamii nzima.
Kwahiyo tukubaliane na hiyo hali ?
 
Wizi, Utapeli na uongo upo kwenye damu tangu kuzaliwa

Imagine mtoto anaanza kuiba kalamu darasani
Na waalimu wanakula sandwitch za watoto kwa kuwaibia
Sasa hapo unategemea nini
Unategemea Viongozi wezi, Baba anaiba Kazini anampa mama mama nae anamuibia baba kwa kupiga hela ya chakula anawalisha watoto viporo Ili apeleke kwao dada wa Kazi nae anaiba kwa boss apeleke kwao.
 
Sasa tunaanza kuongea vitu vya maana , kongole kwa wote watakaounga mkono hoja hii !!
Kaka Tanzania hakuna wanyonge wanaopaswa kuangaliwa kwa jicho la huruma kama viongozi wetu wanavyotaka ifahamike. Tanzania hatujafika hatua ya kuwa na watu wanyonge maana fursa bado hazijakwisha, nafasi bado ziko kwenye kilimo, ufugaji, uvuvi, uchimbaji, viwanda, usafirishaji na biashara. Shida yetu ni mipango mibovu na wizi wa rasilimali zetu na adhabu laini sana kwa wezi wakubwa kama Rais, Jaji Mkuu, na Spika. Rais hahojiwi kokote na yeyoye labda mbinguni tu hata kama atalitumbukiza taifa kwenye hasara kubwa namna gani.

Katiba ya hivi ndiyo aliyotuachia mzee wetu Nyerere kimakosa, baada ya kuona alikosea kuondoka madarakani na kuiacha katiba ya aina hiyo alitaka kurekebisha kwa kushinikiza kuanzishwa kwa vyama vingi vya kisiasa ambavyo vitawakawakosoa watawala walioko madarakani hata baada yeye kufa. Bahati mbaya Mzee hakujuwa kuwa watawala wangevitia korokoroni vyama hivyo visiwabwekee.
 
Unategemea Viongozi wezi, Baba anaiba Kazini anampa mama mama nae anamuibia baba kwa kupiga hela ya chakula anawalisha watoto viporo Ili apeleke kwao dada wa Kazi nae anaiba kwa boss apeleke kwao.
Hata huko kwa wenzetu ilikuwa ni hivyo hivyo ndio maana wakaja na hizo sheria na hukumu Kali ukiiba Mali ya umma,
 
Kaka Tanzania hakuna wanyonge wanaopaswa kuangaliwa kwa jicho la huruma kama viongozi wetu wanavyotaka ifahamike. Tanzania hatujafika hatua ya kuwa na watu wanyonge maana fursa bado hazijakwisha, nafasi bado ziko kwenye kilimo, ufugaji, uvuvi, uchimbaji, viwanda, usafirishaji na biashara. Shida yetu ni mipango mibovu na wizi wa rasilimali zetu na adhabu laini sana kwa wezi wakubwa kama Rais, Jaji Mkuu, na Spika. Rais hahojiwi kokote na yeyoye labda mbinguni tu hata kama atalitumbukiza taifa kwenye hasara kubwa namna gani.

Katiba ya hivi ndiyo aliyotuachia mzee wetu Nyerere kimakosa, baada ya kuona alikosea kuondoka madarakani na kuiacha katiba ya aina hiyo alitaka kurekebisha kwa kushinikiza kuanzishwa kwa vyama vingi vya kisiasa ambavyo vitawakawakosoa watawala walioko madarakani hata baada yeye kufa. Bahati mbaya Mzee hakujuwa kuwa watawala wangevitia korokoroni vyama hivyo visiwabwekee.
Duh ! Iko kazi !!
 
Unategemea Viongozi wezi, Baba anaiba Kazini anampa mama mama nae anamuibia baba kwa kupiga hela ya chakula anawalisha watoto viporo Ili apeleke kwao dada wa Kazi nae anaiba kwa boss apeleke kwao.

Sio cycle of life bali cycle of thieves [emoji23][emoji23][emoji23]
Kama kunyongwa waanze na watoto ili wazaliwe waoga
 
Bila kuwafunga viongozi Hakuna maendeleo
tumeaminishwa kuwa sisi ni wanyonge na tumekubali. mtu akiingia marakani anavomoa pesa bila kuhojiwa na mtu. anaweza kununua jogoo kwa laki 5 na watu wanapiga makofi badala ya kuhoji hela zAO KUPEWA MTU MMOJA KWA KUUZA JOGOO MMOJA.
 
tumeaminishwa kuwa sisi ni wanyonge na tumekubali. mtu akiingia marakani anavomoa pesa bila kuhojiwa na mtu. anaweza kununua jogoo kwa laki 5 na watu wanapiga makofi badala ya kuhoji hela zAO KUPEWA MTU MMOJA KWA KUUZA JOGOO MMOJA.
Wameua elimu Ili wazidi kuwepo madarakani
 
Sio cycle of life bali cycle of thieves [emoji23][emoji23][emoji23]
Kama kunyongwa waanze na watoto ili wazaliwe waoga
Wajukuu urudi kwenye umasikini sababu baada ya baba kufa wamerithi mali watoto haziwezi ongezeka wajukuu ubakia kwenye umasikini
 
Nani amfunge PAKA,tunapiga kelele sababu ya njaa.
We umeoona waunga juhudi baada ya kukaribishwa mezani wameendelea kubweka? Bweka ufe njaa.
Wenzetu weupe wao utengeneza maisha ya Jamii nzima ifaidike ikiwemo na kizazi chao.Wakoloni weusi wao utengeneza maisha ya watoto wao at the wanaoishia kufaidi ni watoto wao na wajukuu zao wanarudi tena kwenye poverty circle ile ile ya Jamii nzima.
Mkuu 'Kalunya',

Kwa hiyo tufanyeje, tuikubali tu hali hiyo kuwa ndiyo kawaida?

Kwanza sikubaliani kabisa na mawazo yako haya. Wewe unasema "Wenzetu weupe wao utengeneza maisha ya Jamii nzima ifaidike..."
Unao uhakika kwamba huko nako hakuna majizi? Bila shaka hata hao wachina, mfano tunaoutumia hapa, nao unawaweka kwenye "wenzetu weupe", sasa huoni kwamba inawalazimu kuweka adhabu hizo za kifo katika taratibu zao kwa kujuwa kwamba wanalo tatizo kubwa upande huo?

Hao "wenzetu weupe" unaowasema, hata kama una maana ya wazungu, unaelewa sheria zao zinazobana mafisadi na wezi zilivyo nchini mwao; na zinatekelezwa?

Jibu lako ni aina ya majibu yale yale yanayotolewa humu jamvini na kwingineko, ni jibu la kivivu kabisa ambalo hukuchukuwa muda kufikiri juu yake.

Mimi ninaamini kwa dhati kabisa, kwamba inawezekana sana hata hapa kwetu kuondoa au hata kupunguza tatizo la ufisadi na wizi kama viongozi watakuwa na nia ya kuliondoa tatizo hilo.
Tatizo linalelewa na viongozi wenyewe waliomo serikalini. Hawa ndio tatizo.
 
Watawala wa kiafrica huwa hawana heshima duniani.Check mtu kama mugabe aliitumia elimu yake kuibomoa nchi yake,means elimu yake haimkusaidia.
 
Tatizo la nchi ni Katiba, Marekani na Ulaya yote haina na haijwahi kuwa na adhabu ya kifo kwa mafisadi ila ndio mataifa yalioendelea zaidi duniani.
Sio katiba mkuu, ni uzalendo mtakuja kugundua mzizi wa yote ni ukosefu wa uzalendo unaochagizwa na katiba mbovu.

Uzalendo unapelekea usimamizi thabiti na usimamizi thabiti unapelekea kufuata katiba kwa ukamilifu!

Mihimili mitatu yote ifanye kazi bila kuwa na muingiliano na Head of State. Ili kuwe na uwezekano wa kumuwajibisha head of state bila kuogopa kwamba ndio mwenyekiti wa chama ama atawafutia uanachama.

Pia head of state asiwe mwenyekiti wa chama wala kuwa na influence yeyote kwa wanachama. Hii itasaidia sana chama kiwe stand alone entity.

Separate body ya kuwawajibisha wanachama iwepo kulingana na katiba na asie tekeleza jukumu lake la kumuwajibisha mkosefu kwa mujibu wa katiba aidha kwa upendeleo au kwa namna yeyote ile aachie ngazi straight away anakuwa amejifukuzisha kazi within stated days!
 
Kuna hekima kwenye utungaji sheria mkuu.Unapowaza sheria itungwe,fikiri na the negative side,hasa matumizi mabaya ya sheria hiyo.
Hii ni Africa,sio China.
 
Back
Top Bottom