Adhabu ya kunyongwa hadi kufa ndio Siri ya uchumi mkubwa duniani

Adhabu ya kunyongwa hadi kufa ndio Siri ya uchumi mkubwa duniani

Sasa hivi tunaandika humu kama mchezo lakini hakika maandishi yetu haya yatakuja kutafutwa kwenye archives ili yasomwe Na wajukuu wetu kama hatua mojawapo ya ukombozi wa taifa kiuchumi.

Ni heri ya anaetafuta wawekezaji kuliko anayetafuta misaada, hakuna cha bure ndugu zangu tuambine ukweli. Vya bure vina madhara, vina ndoana nyingi sana ambazo zitalinasa taifa kooni huko mbele ya safari, ni heri watoto Na wajukuu wetu wakute msululu wa orodha ndefu za majina ya watanzania wenzetu tuliowanyonga sisi wenyewe kwa makosa ya ufisadi, rushwa Na uzembe wa kuingia mikataba mibovu kuliko kukuta msululu wa watu Na mataifa wanaotudai. Watatudharau sana kama tunavyowabeza Leo akina Chief Mangungo wa Msovero dhidi ya akina Karl Peters.
 
Mataifa ambayo uchumi wao uko juu sana duniani wana adhabu katili sana kwa watu wao wanaobainika kuhujumu uchumi kunakosababisha mtu afikirie mara mbili kabla ya kuiba Mali ya umma. Hapa kwetu adhabu ya kumtia mimba mtoto wa shule ni kubwa kuliko aliyeiba hela za umma kwa mabilioni. Nani katuroga?

Hapa kwetu eti Rais hata akituibia kiasi gani Cha fedha eti hashitakiwi Wala kuguswa, ni nani ameturoga?

Adhabu zetu hizo ndio maana mtumishi wa TRA au Bandari haoni ni kwanini asijizolee pesa kabla hajaondolewa kwenye nafasi na kabla ya uzee haujamkuta, maana adhabu zenyewe zinavumilika kabisa.

ya Uchina, Marekani, Asia na Ulaya kuiba mali ya umma hakuna kinga kwa yeyoye yule. Sisi hapa hatukao serious, hata anaeonekana kufoka sana kuhusu ufisadi anaigiza tu.
Unapokuwa na adhabu kubwa kama ya kunyonga ni lazima uwe na penal codes makini za support , ili usinyonge watu kwa petty crimes
Uhujumu uchumi kwetu ni neno pana sana ikiwemo kuharibu mali ya umma , yani unaweza ukaigonga nguzo ya waya ya Tanesco na hapo hapo ikaunekana unataka kuhujumu uchumi
 
Unapokuwa na adhabu kubwa kama ya kunyonga ni lazima uwe na penal codes makini za support , ili usinyonge watu kwa petty crimes
Uhujumu uchumi kwetu ni neno pana sana ikiwemo kuharibu mali ya umma , yani unaweza ukaigonga nguzo ya waya ya Tanesco na hapo hapo ikaunekana unataka kuhujumu uchumi
Ni heri ukosee kuchukua hatua kuliko kuacha kuchukua hatua. Wazungu wamefika huko kwa kuchukua hatua makosa madogo ya kudhaniwa Na kusingiziwa tu. Ndio maana hata vitabu vya dini viliandika kuwa dhambi ni dhambi hakuna dhambi ndogo. Wazungu wanapopigana vita wanaweza kupiga Bomu hata hospitali, nia yao ni kuacha uzembe wa kufikiria kuwa adui hawezi kujificha kwenye hospitali, kanisani, msikitini, shuleni au kwenye msafara wa maharusi.

Watoto wangu wote wamesoma kwakuwa nilikuwa sipuuzii taarifa hata kama walisingiziwa tu kuhusu tabia zao mbaya zisizoendana Na shule. Mimi nilitoa adhabu stahili bila kusema nikweli au sio kweli kafanya. Ukianza kutenga makosa utashindwa tu.
 
Mafisadi wanyongwe Hadharani...

Tena kama wale hasa walio liingiza taifa kwenye mikataba Mibovu kama ile ya Gass ya Mtwara asee...



Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Tunawasifu wachina wanachapa Kazi Na uchumi wao unapaa, aisei, hali hiyo haikutokea tu, IPO machinery inayosukuma hayo yatokee. Sisi hapa tunashindwa kumsogeza machinga atoke kwenye njia zinazotumiwa na watanzania wenzao kupea ajali za magari. Eti kumwambia machinga sogea kuepusha ajali kwa wenzako nako kunahitaji mjadala mrefu, kumnyonga MTU aliyeiba twiga mzima mchana kweupe na kumpakia kwenye ndege kupeleka uarabuni tutaweza?
 
Tunawasifu wachina wanachapa Kazi Na uchumi wao unapaa, aisei, hali hiyo haikutokea tu, IPO machinery inayosukuma hayo yatokee. Sisi hapa tunashindwa kumsogeza machinga atoke kwenye njia zinazotumiwa na watanzania wenzao kupea ajali za magari. Eti kumwambia machinga sogea kuepusha ajali kwa wenzako nako kunahitaji mjadala mrefu, kumnyonga MTU aliyeiba twiga mzima mchana kweupe na kumpakia kwenye ndege kupeleka uarabuni tutaweza?
Wapeane wao tuu najua akija mwamba mmoja atatutengeneza tuu vyema
 
Kwavyovyote vile raia lazima tuache kuishi kwa mazoea. Viongozi wetu wanapata maisha ambayo hayana maelezo ya kutosheleza zaidi ya wizi wa mali zetu kwa kutumia dhamana tunazowapa. Kuandika Katiba inayolinda Mali zetu sio ombi Wala hisani, na kuhakikisha tunaongozwa na kutendewa kwa mujibu wa Katiba hiyo sio ombi wala hisani. Elimu yetu mashuleni lazima iwaambie hivyo watoto wetu.

Hata kama sio Leo lakini siku ifike task force ya kitaifa iundwe kupitia Mali za kila kiongozi tangu nchi hii ipate Uhuru kuona ana nini Na kakipataje. Miaka 60 ya Uhuru Kazi kama hii ya kuwatathimini viongozi namna walivyotuongoza Na hasara Na faida waliyoliletea taifa ndiyo ingekuwa miongoni kwa mambo muhumu ya kujitathimini. Maana wako viongozi ambao wameliingiza taifa hasara na faida, na waliotuibia pia Na waliotenda mambo mema kwetu. Wote hawa tulipaswa tuwatambue kwenye miaka 60 hii ya Uhuru.

Unaposema kwa miaka 60 tumejenga shule 2000 haitoshi, lazima tuseme pia tulipaswa kujenga shule ngapi Na kwanini hazikujengwa hizo na Nani hakufanya nini au kafanya nini .

Mfano mzuri Rais wetu Samia ameshaianzisha tathimini ya aina hii. Wakati anazindua ukamilishaji wa ujenzi wa magati 1-7 bandari ya DSM aliwatimua wenyeviti wa Bodi kwa ubadhilifu alisema kuwa wizi huo haukutokea kwenye awamu yake bali kwenye awamu za nyuma, hivyo asipakwe matope na kunyooshewa kidole yeye. Na amesema hatakubali kupakwa matope. Hiuu ni ushahidi kuwa taarifa zote za nani alifanya nini zipo, ni muda ufike pachimbike. Hii ya Rais Samia kuzinyooshea kidole awamu zilizopita ni fursa mpya ya kuliponya taifa kwa kumulika kila awamu ilituibia nini kwa kiasi gani badala ya kusema jumlajumla tu bila takwimu.
Hata hiyo fafanuzi uliyo toa MAZUZU BADO AWAJAKUELEWA
 
Huyu Mama anataka kuwaonyesha wanaume walichokuwa wakikosea kwa miaka 60 mfululizo. Shida yetu wananchi ilikuwa kuwachagua watu maskini sana kwenye ukoo kuwa viongozi. Mtu maskini anafikiria na kutenda kimaskini hata ofisini. Anafikiria matumbo ya watu Badala ya tumbo kubwa la nchi.
 
Mataifa ambayo uchumi wao uko juu sana duniani wana adhabu katili sana kwa watu wao wanaobainika kuhujumu uchumi kunakosababisha mtu afikirie mara mbili kabla ya kuiba Mali ya umma. Hapa kwetu adhabu ya kumtia mimba mtoto wa shule ni kubwa kuliko aliyeiba hela za umma kwa mabilioni. Nani katuroga?

Hapa kwetu eti Rais hata akituibia kiasi gani Cha fedha eti hashitakiwi Wala kuguswa, ni nani ameturoga?

Adhabu zetu hizo ndio maana mtumishi wa TRA au Bandari haoni ni kwanini asijizolee pesa kabla hajaondolewa kwenye nafasi na kabla ya uzee haujamkuta, maana adhabu zenyewe zinavumilika kabisa.

Mataifa ya Uchina, Marekani, Asia na Ulaya kuiba mali ya umma hakuna kinga kwa yeyoye yule. Sisi hapa hatuko serious, hata anaeonekana kufoka sana kuhusu ufisadi anaigiza tu.
Na maandiko matakatifu yanasema hivi,
"Shetani hawezi kumfukuza shetani mwenzake"
 
Na maandiko matakatifu yanasema hivi,
"Shetani hawezi kumfukuza shetani mwenzake"
Lakini, dawa ya moto ni moto, na mwizi anakamatwa na mwizi mwenzie, mchawi mpe mwanao a Lee.
 
Lakini, dawa ya moto ni moto, na mwizi anakamatwa na mwizi mwenzie, mchawi mpe mwanao a Lee.
Kwa misemo hii ni rahisi kuingia choo cha jinsia tofauti.

Sijawahi kuona gari ya zimamito ikibeba moto kwenda kuzima moto ila maji.
 
Kwa misemo hii ni rahisi kuingia choo cha jinsia tofauti.

Sijawahi kuona gari ya zimamito ikibeba moto kwenda kuzima moto ila maji.
Shida iko hivi, maji ni mbabe wa moto na moto ni mbabe kwa maji , yaani hakuna mbabe kati ya maji na moto. Yaani moto unayakausha maji na kutobakiza hata tone na maji yanauzima moto na kutobakiza hata cheche moja.
 
Mkuu na siku zote ukiona mtu anazungumzia Kinga ujue ni muovu
Unahubiri kufungua makama nyingi za mafisi ili wahukumiwe haraka sana lakini wakati huohuo unajiongezea mwenyewe na rafiki zako kinga ya kutokushitakiwa kwenye mahakama hizo, na wanyonge wanageuka mazuzu wanashangilia mkombozi wa wanyonge kaletwa na Mungu. Kweli wajinga hawaishi hata siku ya kiyama watakuwepo tu!!
 
Umenena vyema Tza fisadi afungwi ulipa faini mbuzi kibaka ufungwa sababu hana pesa ya kumuhonga hakimu.
 
Hii nchi inatafunwa hatari tunaopiga kelele ni sisi tusiopata nafasi
 
Nyerere ndipo alipokosea, alikuwa na uchumi kama wa China lakini akaacha mambo muhimu kuhusu uchumi wa China. Wachina wanamnyonga mwizi wa Mali za umma, lakini Mwl Nyerere alicheka na wezi wa Mali za umma. Eti aliwapiga viboko 12 matakoni wakawaoneshe wake zao. Hii nayo ni adhabu inayomfanya mtu asiibe mabilioni?

Watanzania tunafurahia kupewa misaada na wachina lakini hatupendi kujua wachina wanalindaje mali zao.
Pia Nyerere alikuwa akiwahamisha wizara wezi eti ndo adhabu mtu kaiba anahamishwa.
 
Nyerere ndipo alipokosea, alikuwa na uchumi kama wa China lakini akaacha mambo muhimu kuhusu uchumi wa China. Wachina wanamnyonga mwizi wa Mali za umma, lakini Mwl Nyerere alicheka na wezi wa Mali za umma. Eti aliwapiga viboko 12 matakoni wakawaoneshe wake zao. Hii nayo ni adhabu inayomfanya mtu asiibe mabilioni?

Watanzania tunafurahia kupewa misaada na wachina lakini hatupendi kujua wachina wanalindaje mali zao.
Sasa tunaanza kuongea vitu vya maana , kongole kwa wote watakaounga mkono hoja hii !!
 
Back
Top Bottom