ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 631
- 1,577
TAARIFA KWA UMMA
BARAZA LA VYAMA VYA SIASA LIMEPOTEZA UHALALI
Kamati ya Uongozi Taifa ya Chama cha ACT Wazalendo kwenye kikao chake cha tarehe 10 Machi, 2025 imeazimia kutoshiriki vikao vya Baraza la Vyama vya Siasa kuanzia kikao cha tarehe 12 na 13 Machi, 2025 kwa sababu zifuatazo;-
1. Baraza la Vyama vya Siasa linaloratibiwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini limepoteza uhalali baada ya kushindwa kuwa jukwaa la majadiliano kati ya Serikali na Vyama vya Siasa kwa ajili ya kujenga na kukuza misingi ya demokrasia nchini ya vyama vingi nchini, ambalo lilikuwa ndiyo lengo lake kuu wakati linaanzishwa.
2. Baraza la Vyama vya Siasa limegeuzwa kuwa jukwaa la kutumika kuhalalisha na kusafisha uchafuzi na wizi katika chaguzi kama ilivyofanyika kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019, Uchaguzi Mkuu 2020 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.
3. Serikali kupuuza maazimio ya Baraza la Vyama vya Siasa ya kuboresha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024;
Kwenye Kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika tarehe 11 Oktoba 2024 Jijini Dodoma na kutanguliwa na vikao vya Kamati za Baraza na Kamati ya Uongozi ya Baraza, maazimio mbalimbali yalifikiwa kuboresha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Serikali, kupitia Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ilitoa ahadi ya kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa.
Kinyume na ahadi yake ambayo ilitolewa kimaandishi, Serikali iliyatupa mapendekezo ya Baraza la Vyama vya Siasa na kuendelea na mpango wake wa kudhulumu sauti ya wananchi kupitia wizi wa kura na uchafuzi kama ilivyoshuhudiwa nchi nzima.
WITO WETU
1. ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kama kweli inataka tulichukulie Baraza hili kuwa ni chombo makini cha sisi kushiriki shughuli zake basi iweke mezani kalenda ya utekelezaji wa mapendekezo ya kupata Tume Huru ya Uchaguzi na marekebisho mengine ya Sheria za Uchaguzi ikiwemo Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar na pia mabadiliko madogo ya Katiba yatakayopelekea kufanyika kwa Uchaguzi Huru na wa Haki.
2. Chama cha ACT Wazalendo kimewasilisha tena kwa Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye ndiye Katibu wa Baraza la Vyama vya Siasa uchambuzi wake wa kina wa masuala yanayohitaji kufanyiwa maboresho katika tasnia ya siasa ili kuhakikisha Uchaguzi Mkuu 2025 unakuwa huru, wa haki na wa kuaminika.
3. Kinyume na hapo, ACT Wazalendo hatutakubali kutumika kuhalalisha na kusafisha uchafu unaoandaliwa ili kupora mamlaka ya wananchi ya kuchagua na kuwaweka madarakani viongozi wanaowataka kama yalivyo matakwa ya Ibara ya 8 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Ibara ya 9 ya Katiba ya Zanzibar.
Imetolewa na;
Ado Shaibu
Katibu Mkuu
ACT Wazalendo
11 Machi, 2025.
Dar es Salaam.
BARAZA LA VYAMA VYA SIASA LIMEPOTEZA UHALALI
Kamati ya Uongozi Taifa ya Chama cha ACT Wazalendo kwenye kikao chake cha tarehe 10 Machi, 2025 imeazimia kutoshiriki vikao vya Baraza la Vyama vya Siasa kuanzia kikao cha tarehe 12 na 13 Machi, 2025 kwa sababu zifuatazo;-
1. Baraza la Vyama vya Siasa linaloratibiwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini limepoteza uhalali baada ya kushindwa kuwa jukwaa la majadiliano kati ya Serikali na Vyama vya Siasa kwa ajili ya kujenga na kukuza misingi ya demokrasia nchini ya vyama vingi nchini, ambalo lilikuwa ndiyo lengo lake kuu wakati linaanzishwa.
2. Baraza la Vyama vya Siasa limegeuzwa kuwa jukwaa la kutumika kuhalalisha na kusafisha uchafuzi na wizi katika chaguzi kama ilivyofanyika kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019, Uchaguzi Mkuu 2020 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.
3. Serikali kupuuza maazimio ya Baraza la Vyama vya Siasa ya kuboresha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024;
Kwenye Kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika tarehe 11 Oktoba 2024 Jijini Dodoma na kutanguliwa na vikao vya Kamati za Baraza na Kamati ya Uongozi ya Baraza, maazimio mbalimbali yalifikiwa kuboresha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Serikali, kupitia Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ilitoa ahadi ya kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa.
Kinyume na ahadi yake ambayo ilitolewa kimaandishi, Serikali iliyatupa mapendekezo ya Baraza la Vyama vya Siasa na kuendelea na mpango wake wa kudhulumu sauti ya wananchi kupitia wizi wa kura na uchafuzi kama ilivyoshuhudiwa nchi nzima.
WITO WETU
1. ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kama kweli inataka tulichukulie Baraza hili kuwa ni chombo makini cha sisi kushiriki shughuli zake basi iweke mezani kalenda ya utekelezaji wa mapendekezo ya kupata Tume Huru ya Uchaguzi na marekebisho mengine ya Sheria za Uchaguzi ikiwemo Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar na pia mabadiliko madogo ya Katiba yatakayopelekea kufanyika kwa Uchaguzi Huru na wa Haki.
2. Chama cha ACT Wazalendo kimewasilisha tena kwa Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye ndiye Katibu wa Baraza la Vyama vya Siasa uchambuzi wake wa kina wa masuala yanayohitaji kufanyiwa maboresho katika tasnia ya siasa ili kuhakikisha Uchaguzi Mkuu 2025 unakuwa huru, wa haki na wa kuaminika.
3. Kinyume na hapo, ACT Wazalendo hatutakubali kutumika kuhalalisha na kusafisha uchafu unaoandaliwa ili kupora mamlaka ya wananchi ya kuchagua na kuwaweka madarakani viongozi wanaowataka kama yalivyo matakwa ya Ibara ya 8 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Ibara ya 9 ya Katiba ya Zanzibar.
Imetolewa na;
Ado Shaibu
Katibu Mkuu
ACT Wazalendo
11 Machi, 2025.
Dar es Salaam.