Adui hatari nambari wani wa taifa letu Tanzania ni CCM, je unaafiki?

Adui hatari nambari wani wa taifa letu Tanzania ni CCM, je unaafiki?

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592
Nakiri kuwa sijawahi kuishabikia CCM hata kwa bahati mbaya. CCM ni chafu na inanuka. Siwezi kuishi kwenye nyumba inayonuka, nikijifunika blanketi moja na wanaonuka, nikikesha na wenzangu wanaonuka halafu nidanganye umma kwamba sinuki. Kuwa mwanachama wa CCM maana yake ni kwamba huo uvundo haukusumbui, unauona kama marashi ya Pemba.

Kuwa mwanachama wa CCM ni hatua ya kwanza katika kulisaliti taifa kwa kukubaliana na tulipokuwa, tulipo na tunakoelekea. Hata mwenyekiti muasisi wa CCM, Baba wa Taifa, alishindwa kuvumilia huo uvundo na kutishia kujitoa kama juhudi za makusudi hazikufanyika kukisafisha chama kilichoonekana wazi kabisa kukosa dira lakini masikini, hata yeye akapotezwa?

Niliipinga CCM kabla ya mfumo wa vyama vingi, nikaendelea kuipinga baada ya mfumo mpya na nitaendelea kuipinga hadi itoke madarakani. Hii ni kwa sababu ninaamini kwa dhati kabisa kwamba chama ambacho kwa muda zaidi ya nusu karne haikuweza kutuopoa katika lindi la ujinga, maradhi na umasikini, imechoka, imezeeka na haina uhalali wowote wa kubaki madarakani.

CCM inaamini katika kuhodhi kila kitu…kuhodhi uhai, kuhodhi nchi, kuhodhi uraia, kuhodhi Katiba, kuhodhi utawala, kuhodhi haki (mahakama), kuhodhi madaraka, kuhodhi fikra, kuhodhi hoja (bunge), kuhodhi akili na kuhodhi hata ujinga! Naam, ukianza kuhodhi kila kitu, umekuwa sawa na kokoro na si ajabu kuhodhi hadi ujinga! Angalia ilipofikia CCM imehodhi hadi ulevi wa madaraka!

Mwinyi aliingia na yake, Mkapa akaingia na yake, Kikwete akaingia na yake, Magufuli akaingia na yake na sasa Mama naye kaingia na yake lakini washiriki bado ni wale wale na nyumba inayonuka bado ni ile ile. Baada ya kupoteza mvuto kwa wananchi, ikaamua kung'ang'ania madaraka kwa ulaghai na matumizi ya nguvu, hata hivyo la kuvunda halina ubani na mwisho wake hauko mbali.
 
Hata sijasoma japo nimesoma kichwa cha habari.

Adui ni wewe mwenye mawazo mgando, vyama havisaidii chochote kwa mahala popote,adui ni mtu mvivu anaye chagua cha kufanya
 
Mwinyi aliingia na yake, Mkapa akaingia na yake, Kikwete akaingia na yake, Magufuli kaingia na yake na sasa Mama naye kaingia na yake lakini washiriki bado ni wale wale na nyumba inayonuka bado ni ile ile. Baada ya kupoteza mvuto kwa wananchi, ikaamua kung'ang'ania madaraka kwa ulaghai na matumizi ya nguvu...hata hivyo la kuvunda halina ubani!

IMG-20210902-WA0012.jpg


Sent from my Infinix X692 using JamiiForums mobile app
 
Mag3 Unalosema ni kweli, tatizo ni wananchi ambao wengi ni zao la uongozi mbovu wa ccm.

CCM imewanyang'anya watanzania uwezo wa kujua haki zao na pia imewapora na kuficha nguvu za wananchi walizo nazo kisheria za kujua na kudai maslahi yao.
 
Mwinyi aliingia na yake, Mkapa akaingia na yake, Kikwete akaingia na yake, Magufuli kaingia na yake na sasa Mama naye kaingia na yake lakini washiriki bado ni wale wale na nyumba inayonuka bado ni ile ile. Baada ya kupoteza mvuto kwa wananchi, ikaamua kung'ang'ania madaraka kwa ulaghai na matumizi ya nguvu...hata hivyo la kuvunda halina ubani!View attachment 1920398

Sent from my Infinix X692 using JamiiForums mobile app
Mwenyeji wa galilaya na sio Galilaya, aliyetembea njia ile ya yesu na mkewe na sio Yesu
 
Nakiri kuwa sijawahi kuishabikia CCM hata kwa bahati mbaya. CCM ni chafu na inanuka. Siwezi kuishi kwenye nyumba inayonuka, nikijifunika blanketi moja na wanaonuka, nikikesha na wenzangu wanaonuka halafu nidanganye watu kwamba sinuki. Kuwa mwanachama wa CCM maana yake ni kwamba huo uvundo haukusumbui...unauona kama marashi ya Pemba.

Kuwa mwanachama wa CCM ni hatua ya kwanza katika kulisaliti taifa kwa kukubaliana na tulipokuwa, tulipo na tunakoelekea. Hata mwenyekiti muasisi wa CCM, Baba wa Taifa, alishindwa kuvumilia huo uvundo na kutishia kujitoa kama juhudi za makusudi hazikufanyika kukisafisha chama kilichoonekana wazi kabisa kukosa dira lakini masikini, hata yeye akapotezwa!

Niliipinga CCM kabla ya mfumo wa vyama vingi, nikaendelea kuipinga baada ya mfumo mpya na nitaendelea kuipinga hadi itoke madarakani. Hii ni kwa sababu ninaamini kwa dhati kwamba chama ambacho kwa muda zaidi ya nusu karne haikuweza kutuopoa katika lindi la ujinga, maradhi na umasikini, imekosa kabisa uhalali wowote wa kubaki madarakani.

CCM inaamini katika kuhodhi kila kitu...kuhodhi nchi, kuhodhi uraia, kuhodhi Katiba, kuhodhi utawala, kuhodhi haki, kuhodhi madaraka, kuhodhi fikra, kuhodhi hoja, kuhodhi akili, kuhodhi mawazo na kwa sasa kuhodhi hata ujinga! Naam, ukianza kuhodhi kila kitu, umekuwa sawa na kokoro utahodhi hadi ujinga! Angalia ilipofikia CCM na utaelewa gharama zake

Mwinyi aliingia na yake, Mkapa akaingia na yake, Kikwete akaingia na yake, Magufuli kaingia na yake na sasa Mama naye kaingia na yake lakini washiriki bado ni wale wale na nyumba inayonuka bado ni ile ile. Baada ya kupoteza mvuto kwa wananchi, ikaamua kung'ang'ania madaraka kwa ulaghai na matumizi ya nguvu...hata hivyo la kuvunda halina ubani mwisho wake hauko mbali!

.

Haswaaa
 
Siyo Magufuli tena?

Mimi nilifikiri mbaya wetu hii nchi ni Magufuli, na hata zile shangwe za wana chadema baada ya kifo chake nilifikiri sasa mtajiona mko Newyork!

Mmakwama wapi mabavicha?
 
Siyo Magufuli tena?

Mimi nilifikiri mbaya wetu hii nchi ni Magufuli, na hata zile shangwe za wana chadema baada ya kifo chake nilifikiri sasa mtajiona mko Newyork!

Mmakwama wapi mabavicha?
Magufuli kaacha misukule yake inatafuna taifa
 
Tuanzishe basi operation adui

Hii itasaidia sana kuongeza awareness kwa wananchi
 
Mwinyi aliingia na yake, Mkapa akaingia na yake, Kikwete akaingia na yake, Magufuli kaingia na yake na sasa Mama naye kaingia na yake lakini washiriki bado ni wale wale na nyumba inayonuka bado ni ile ile. Baada ya kupoteza mvuto kwa wananchi, ikaamua kung'ang'ania madaraka kwa ulaghai na matumizi ya nguvu...hata hivyo la kuvunda halina ubani!View attachment 1920398

Sent from my Infinix X692 using JamiiForums mobile app
Aibu sn kwa taifa letu
 
Back
Top Bottom