Adui mkubwa wa Mtanzania ni Mtanzania mwenyewe!

na ndiyo maana Mh. Mbowe kaamua ku- reconcile na Dola ili kuangalia namna bora ya kudai haki kwa mazungumzo sababu kaona hakuna njia nyingine zozote ambazo nchi zingine walifanya wakafanikiwa kwetu zimedunda zote.

Kwa mfano watanzania mnapanga maandamano kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu kesho unajikuta peke yako mtaani na bango lako...unakula mkongoto wa haja unakwenda kuuza majeraha kwa pesa yako na kesi juu.
 
Aisee ulipotelea wapi?
 
Haya mambo tunayapigia lip service, lakini kiukweli wengi tumepandishiwa tu.

1. Elimu ya darasani.
2. Demokrasia ya kiliberali.
3. Fikra za kisayansi.
4. Maendeleo ya uchumi wa kisasa.
5.Research and Development.
6. Heshima kwa utu wa kila mtu na ushirikishwaji wa umma.
7. Fikra tunduizi na dhahania.
8. Fikra hojaji.
9. Ukweli.
10. Haki.

Hivyo, nchi zinazodharau umuhimu wa haya, kuendelea ni vigumu.
 
Njoo uandamane, sio unaandika uko chini ya uvungu.

Halafu wewe ndio ulikuwa mshabiki mkubwa wa Jiwe alivyokuwa akikandamiza watu na kuteka, kisa ni msukuma mwenzio.

Sasa Leo wewe uliyeunga mkono ukandamizaji unahoji kwanini waliokandamizwa hawakuandamana
 
Inakatisha tamaa kweli!

Hivi unakumbuka yake maandamano ya Tahrir Square kule Misri?

Kitu kama hicho hapa Tanzania hakiwezekani.
 

Mbona mikutano haikufanyika miaka Saba Sasa na Bado Deni limeongezeka mpaka Trilioni 92?. Mfumuko wa Bei, mgao wa umeme , na maji, Hali ngumu ya Maisha.

Halafu yeye kaongelea siasa, wewe waweza ongelea uchumi.
 
Ulichosema ni sahihi sana

Naweza kuongezea kidogo, watanzania nashindwa namna nzuri ya kuongea lakini ni aina ya watu ambao wanaamini ukishakua kwenye madaraka basi umefanikiwa kimaisha wao hawatamani kuongoza ili walete mabadiliko chanya lakini wao wanatamani waongoze wajiletee mabadiliko chanya kwao ( ubinafsi wa hali ya juu)
Kila anayeingia kwenye nafasi yeyote hata mtendaji wa kijiji anawaza namna gani aile keki ya taifa hawazi namna gani anaweza kuilinda au aongeze keki zingine


Pili sisi ni watu wa mizaha na masihara sana Kila mtanzania ni mtu wa hivyo ni wepesi wa kuongea na si vitendo hili na uhakika nalo asilimia Mia mtanzania yeyote yule ni mtu wa aman aisee tuna extremists wachache sana nchini na sijui kwann hili limetokea wengi ni wanyonge wasio na sauti lakini wacheshi na wenye furaha basi maisha yanaenda haka ni kama ka immune flani hivi kanazuia mengi sana kwa haya mambo ya ccm watu wangekua washauana sana lakini tunaishi

Tatu na mwisho hili ntatoa kwa mfano then utaona mwenyewe watanzania ni watu wa namna gani mfano, 1.utakuta wanamshukuru raisi kuruhusu mikutano ya kisiasa
2. Wanamshukuru raisi kuwajengea let's say barabara
3. Vifurushi vikipandishwa vikashushwa na rais watamshukuru raisi

Kila jambo wao wanaona ni hisani so Unaweza kufikiria mwenyewe hawa watu ni wa namna gani si wasomi na ambao hawajasoma wote huwa wana behave hivi

Nini haswa kifanyike ngoja ninywe maji nirudi.!.
 
Kama katiba iliyopo inakiukwa na hatufanyi kitu, hiyo mpya ikikiukwa tutafanya nini?

Sisi ni watu wa ajabu sana.
elimu yetu yenyewe bado haisaidii kujitambua ndo kwanza inazidisha ujinga na uoga, vijana wanaomaliza vyuo kila siku wanajiunga kwenye mapambio na kuendeleza uchawa wakati tulitegemea hawa waje kuwa mabalozi wazuri kwa wananchi wengine kaujitambua ili kupingana na udhulumati.

Unakuta muda mwingine bora hata wazee ambao hawana elimu za vyuo vikuu wanatambua haki zao ipasavyo kuliko vijana wa sasa wenye degree.
 
maisha ya janja janja ya kutotaka kufata sheria na utaratibu ndio yametufikisha hapa,unakuta magari yana issue nyingi sana kiasi kwamba ukifatwa utaratibu basi hela itakayotolewa ni kubwa bila kujali kwamba hata hizo buku mbili mbili angeweza kuclear issue zote zisingekuwa zimtoka sasa kinachofanyika madereva wanaepusha shari na kuamua kulipa buku mbili ili mambo yaende kuliko kufanya kitu ambacho sheria itamlinda na hatopata usumbufu....janja janja tunaipenda sana na ndio tunaiishi kwa kujiaminisha kwamba ni nafuu
 

Wengi wa wanaopewa vyeo huko kwenye vyombo vya dola, aidha wana uwezo mdogo,na pia huongozwa na ubinafsi. Hivyo mtu anajua akitaka mwanasiasa afuate sheria atamtoa kwenye hicho cheo, na kumuweka mwingine kisha yeye binafsi atakosa mshahara mnono na posho kedekede.
 
Iko sababu ya kimaadili na elimu.

WaTanzania wengi hawana maadili mazuri, ujanja ujanja, majizi, unafiki, rushwa, siyo watu wa kupenda haki.

Hili tatizo ni kubwa sana hata kwa mtu mmoja mmoja kila akipata nafasi atataka akuibie, achukue rushwa hii hata ukienda ofisi tu za uma za kawaida utakutana nayo.
Wengine wanafikia hatua kusema maisha hayawezi kwenda bila kufanya hayo, wanaona fahari.

Sasa watu wa hivi wasiojua na kufahamu misingi ya haki na uadilifu hawawezi kuhoji haki zao zikivunjwa wanajionea sawa tu.

Sababu hata wenyewe wako vilevile, yani mwizi anamkemea mwizi hii ni ngumu sana.

Elimu inayotolewa huko mashuleni kuanzia msingi hadi vyuoni haina ubora.

Hili ni janga la kitaifa.

Inawadumaza tu wengi yani bila juhudi binafsi ya mtu kutafuta maarifa sahihi ataondoka na vyeti vina A lakini kichwani mtupu.

Hata wasomi vyuo vikuu hawawezi hata kuhoji, wamekua majuha tu sababu wamefundishwa kwa mazingira kama hayo siyo rahisi kuuliza maswali kwa uhuru kwa lecturer atakufelisha Tanzania, ataona unampinga.

Kwa hivyo hatokuja kuweza kudai haki zake au kuhoji mamlaka, kuwadhibiti walio kwenye mamlaka wanapovunja sheria na katiba.

Watanzania kukosa maadili na Elimu duni.
 
Prof. Lumumba aliwahi kusema kuwa;
Demokrasia ya Marekani haiwezi kuwa sawa na demokrasia ya Afrika/ Tanzania, wala hatulazimiki kufuata demokrasia za mataifa ya ulaya.

Sisi kama watanzania tuna aina yetu ya demokrasia iliyo ambatana na desturi zetu sisi.
usituletee mambo ya waamarekani ambao wao hata ushoga kwao ni haki!! na wala hawaoni aibu kudai haki hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…