Adui mkubwa wa Mtanzania ni Mtanzania mwenyewe!

Adui mkubwa wa Mtanzania ni Mtanzania mwenyewe!

Mimi nilidhani mleta mada unakuja na hoja inayogusa jamii ya wananchi kwa ujumla wake kumbe ni maslahi ya kisiasa na vyama vya siasa.

Kwa hio kama hao viongozi wasingezuia hio mikutano ya kisiasa wasingekua na ubaya wowote.

Hivo mikutano ya kisiasa ilikuwepo kipindi kile cha uongozi wa Kikwete mbona faida yake haionekani katika jamii.

Kwamba kuruhusiwa hio mikutano ya kisiasa ndio mwanzo wa taifa na wananchi kwa ujumla wataondokana na umaskini na kadhia zote zilizo kati yetu?

Kwa hiyo unashauri sheria zifuatwe kwakuwa hata zikifuatwa matatizo yetu hayataisha?!
 
Prof. Lumumba aliwahi kusema kuwa;
Demokrasia ya Marekani haiwezi kuwa sawa na demokrasia ya Afrika/ Tanzania, wala hatulazimiki kufuata demokrasia za mataifa ya ulaya.

Sisi kama watanzania tuna aina yetu ya demokrasia iliyo ambatana na desturi zetu sisi.
usituletee mambo ya waamarekani ambao wao hata ushoga kwao ni haki!! na wala hawaoni aibu kudai haki hiyo.

Kwahiyo katiba yetu ina sheria za demokrasia ya Marekani?
 
Naomba nizungumzie kiujumla, licha ya kwamba kati yetu binafsi, wapo ambao wako tofauti na walio wengi.

Watanzania wengi ni wajinga [wasiozijua haki zao] na ni waoga sana.

Mchanganyiko wa hizo sifa mbili ni kikwazo kikubwa sana katika maendeleo ya jamii.

Huwezi kupata maendeleo yoyote yale ya maana endapo idadi kubwa ya watu kwenye hiyo jamii wana hizo sifa za ujinga na uoga.

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu, pale mtu asiye na mamlaka ya kukupora haki zako anapokupora, na wewe humpingi huyo mporaji kwa nguvu na uwezo wako wote, ni kitu gani kingine utakachoweza kukipigania kwa hali na mali?

Watanzania tumeshuhudia kuporwa baadhi ya haki zetu kwa miaka ya hivi karibuni kuanzia takriban 2016 mpaka hivi sasa. Na tumekuwa wapole na wanyonge mno.

Alianza Rais Magufuli kukiuka katiba na kuvikataza vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa, kikubwa kikiwa ni mikutano ya kisiasa.

Magufuli kaondoka, kaja Rais Samia naye akaendeleza huo uvunjaji wa katiba.

Wote hawa wawili wamevunja katiba waziwazi kabisa. Na sisi wananchi wenye nchi hakuna lolote la maana tulilolifanya kuwapinga hao wawili!

Tunaburuzwa buruzwa tu. Juzi hapa Samia eti katoa ruhusa ya vyama vya siasa kuanza kufanya mikutano ya kisiasa!

Hiyo ruhusa kaitoa kwa msingi gani wa mamlaka aliyonayo kisheria na kikatiba?

Sisi ni banana republic. Hatuongozwi na sheria wala katiba. Tunaongozwa na hisia, hisani, na matakwa ya mtu ambaye kimsingi ni mtumishi wetu, lakini kiuhalisia ni kama vile sisi ndo tunamtumikia yeye na si vinginevyo.

Kuna wakati kule Marekani, kipindi ambacho Donald Trump alikuwa Rais, kulikuwa na mjadala kuwa endapo angetoa agizo kwa jeshi la nchi hiyo, agizo lililo haramu kisheria na kikatiba, viongozi wa jeshi walikuwa wako tayari kabisa kulikaidi hilo agizo. Hawakuwa tayari kutekeleza agizo lolote linaloenda kinyume na sheria na katiba yao.

Hao ni watu wanaojitambua. Ni watu wasio waoga. Ni werevu na ni majasiri pia.

Hapa kwetu jambo kama hilo bado sijaona kama linawezekana.

Magufuli na Samia walipaswa kupingwa vikali sana.

Maagizo yao haramu ya kuzuia mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani yalipaswa kukaidiwa na watekelezaji wa sheria.

Mtu kama kweli unajitambua, si mjinga wala muoga, kwa nini utekeleze amri ambayo si halali?

Kwani ukikataa kutekeleza amri ambayo si halali, nini kitakutokea?

Ije katiba mpya au isije, hii tuliyonayo sasa hivi inayotupatia haki tulizonazo sasa hivi, inakiukwa waziwazi kabisa na hatufanyi chochote kulinda hizo haki zetu, hiyo mpya tunayoitaka tutailinda kweli?

Kwa sasa nimeshahitimisha kuwa tatizo letu kubwa wala siyo katiba mpya. Tatizo ni sisi wenyewe. Bado tupo wajinga sana, wapole sana, na waoga sana.

Kwa hizi sifa, hata ije katiba mpya, hakutokuwa na tofauti yoyote ile. Tutaendelea kuburuzwa tu hadi pale tutapobadilika.

Na kwa kizazi hiki kilichopo, sitegemei tubadilike.

Adui wetu mkubwa ni sisi wenyewe!

Rais Samia hastahili pongezi yoyote ile kwa ‘kuruhusu’ vyama vya siasa kufanya mikutano ya kisiasa.

Hakuwa na haki ya kukataza hiyo mikutano. Hivyo hana haki ya kuruhusu mikutano hiyo.

Hastahili kabisa pongezi.

Anachopaswa kufanya ni kuomba radhi. Aombe radhi kwa kukiuka katiba.

Akiomba radhi kwa hilo, mimi nitakuwa wa kwanza kumpongeza kwa kuona kosa lake na kuamua kujirudi.

Nje ya hapo, siwezi kumpongeza mporaji aliyeamua kunirudishia kilicho changu.
Pole sana nyanu ngabu Ile Layer yako yoote ya Sgang kwisha habari. Naona sasa akili zimekurudi
 
Naomba nizungumzie kiujumla, licha ya kwamba kati yetu binafsi, wapo ambao wako tofauti na walio wengi.

Watanzania wengi ni wajinga [wasiozijua haki zao] na ni waoga sana.

Mchanganyiko wa hizo sifa mbili ni kikwazo kikubwa sana katika maendeleo ya jamii.

Huwezi kupata maendeleo yoyote yale ya maana endapo idadi kubwa ya watu kwenye hiyo jamii wana hizo sifa za ujinga na uoga.

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu, pale mtu asiye na mamlaka ya kukupora haki zako anapokupora, na wewe humpingi huyo mporaji kwa nguvu na uwezo wako wote, ni kitu gani kingine utakachoweza kukipigania kwa hali na mali?

Watanzania tumeshuhudia kuporwa baadhi ya haki zetu kwa miaka ya hivi karibuni kuanzia takriban 2016 mpaka hivi sasa. Na tumekuwa wapole na wanyonge mno.

Alianza Rais Magufuli kukiuka katiba na kuvikataza vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa, kikubwa kikiwa ni mikutano ya kisiasa.

Magufuli kaondoka, kaja Rais Samia naye akaendeleza huo uvunjaji wa katiba.

Wote hawa wawili wamevunja katiba waziwazi kabisa. Na sisi wananchi wenye nchi hakuna lolote la maana tulilolifanya kuwapinga hao wawili!

Tunaburuzwa buruzwa tu. Juzi hapa Samia eti katoa ruhusa ya vyama vya siasa kuanza kufanya mikutano ya kisiasa!

Hiyo ruhusa kaitoa kwa msingi gani wa mamlaka aliyonayo kisheria na kikatiba?

Sisi ni banana republic. Hatuongozwi na sheria wala katiba. Tunaongozwa na hisia, hisani, na matakwa ya mtu ambaye kimsingi ni mtumishi wetu, lakini kiuhalisia ni kama vile sisi ndo tunamtumikia yeye na si vinginevyo.

Kuna wakati kule Marekani, kipindi ambacho Donald Trump alikuwa Rais, kulikuwa na mjadala kuwa endapo angetoa agizo kwa jeshi la nchi hiyo, agizo lililo haramu kisheria na kikatiba, viongozi wa jeshi walikuwa wako tayari kabisa kulikaidi hilo agizo. Hawakuwa tayari kutekeleza agizo lolote linaloenda kinyume na sheria na katiba yao.

Hao ni watu wanaojitambua. Ni watu wasio waoga. Ni werevu na ni majasiri pia.

Hapa kwetu jambo kama hilo bado sijaona kama linawezekana.

Magufuli na Samia walipaswa kupingwa vikali sana.

Maagizo yao haramu ya kuzuia mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani yalipaswa kukaidiwa na watekelezaji wa sheria.

Mtu kama kweli unajitambua, si mjinga wala muoga, kwa nini utekeleze amri ambayo si halali?

Kwani ukikataa kutekeleza amri ambayo si halali, nini kitakutokea?

Ije katiba mpya au isije, hii tuliyonayo sasa hivi inayotupatia haki tulizonazo sasa hivi, inakiukwa waziwazi kabisa na hatufanyi chochote kulinda hizo haki zetu, hiyo mpya tunayoitaka tutailinda kweli?

Kwa sasa nimeshahitimisha kuwa tatizo letu kubwa wala siyo katiba mpya. Tatizo ni sisi wenyewe. Bado tupo wajinga sana, wapole sana, na waoga sana.

Kwa hizi sifa, hata ije katiba mpya, hakutokuwa na tofauti yoyote ile. Tutaendelea kuburuzwa tu hadi pale tutapobadilika.

Na kwa kizazi hiki kilichopo, sitegemei tubadilike.

Adui wetu mkubwa ni sisi wenyewe!

Rais Samia hastahili pongezi yoyote ile kwa ‘kuruhusu’ vyama vya siasa kufanya mikutano ya kisiasa.

Hakuwa na haki ya kukataza hiyo mikutano. Hivyo hana haki ya kuruhusu mikutano hiyo.

Hastahili kabisa pongezi.

Anachopaswa kufanya ni kuomba radhi. Aombe radhi kwa kukiuka katiba.

Akiomba radhi kwa hilo, mimi nitakuwa wa kwanza kumpongeza kwa kuona kosa lake na kuamua kujirudi.

Nje ya hapo, siwezi kumpongeza mporaji aliyeamua kunirudishia kilicho changu.
Mkuu mimi siyo mbobezi wa mambo ya katiba na sheria, ila natambua kutokana na katiba yetu, tamko ama agizo la Rais, "presidential decree", huweza kuondolewa na kupitia tamko lingine la Rais mwenyewe, endapo hakutawepo mchakato wowote ule wa kisheria kulipinga tamko hilo.

Kwa kudesa katika nyaraka za kimtandao tunaona;

A decree of that nature is a legal proclamation issued by the president of a republic, according to certain procedures (usually established in a constitution). It has the force of law. The particular term used for this concept may vary from country to country. The executive orders are decrees (although a decree is not exactly an order).

Kwa hiyo kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, pale tu JPM alipotoa agizo hilo, vyombo vya dola vikalichukulia kama katazo rasmi, na yeyote ambaye angekwenda kinyume chake angepambana na nguvu ya vyombo hivyo. Kwa hiyo pasipo kujali uharamu wake, Rais SSH ametumia vyema nafasi yake kulikondoa katazo hilo kwa hekima.
 
Kweli sisi ni mazuzu,na hatujuwi mpaka leo tunataka nini?

Eti sahvi dk slaa anaponda katazo la kuzuiwa mikutano ya kisiasa,wakati yeye alipokuwa balozi hakuwahi kuhoji

Ova
 

Nilishangazwa sana na viongozi wa vyama vya upinzani kusimama na kumpigia makofi Rais Samia.

Unampongeza mtu kwa kuwa ametangaza kuacha kuvunja sheria? Huku ndiko nchi yetu ilipofikia, ni aibu mno.
 

Nilishangazwa sana na viongozi wa vyama vya upinzani kusimama na kumpigia makofi Rais Samia.

Unampongeza mtu kwa kuwa ametangaza kuacha kuvunja sheria? Huku ndiko nchi yetu ilipofikia, ni aibu mno.
Lazima wapige makofi maana hyo ndiyo atawapa ruzuku za vyama

Ova
 
Katiba mpya ni mwanzo mzuri.

Kama rais yuko juu ya sheria, hakuna chombo chochote kitakachothubutu kuwa kinyume naye….Iwe jeshi, polisi au mahakama.
 
Ndio maana mimi najiuliza mara nyingi, kama kwa katiba hii hata haki za kikatiba tunashindwa kuzidai ni nini katiba mpya itafanya?

Kwanza isambazwe elimu ya uraia ili tujitambue walau kwa haki za msingi zilizopo. Bila hivyo katiba mpya itakuwa mvinyo mpya kwenye kiriba kikuu.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Katiba mpya ni mwanzo mzuri.

Kama rais yuko juu ya sheria, hakuna chombo chochote kitakachothubutu kuwa kinyume naye….Iwe jeshi, polisi au mahakama.
Ni kweli kwamba Watanzania wengi hawaitumii kikamilifu hata hii katiba iliyopo, hawaijui vizuri, hili ni tatizo.

Kuna mzee mmoja aliulizwa na Tume ya Warioba anataka nini katika katiba mpya, akasema anataka haki ya kuoa wake wengi, kitu ambacho kinaruhusiwa kikatiba tayari.

Tunahitaji utamaduni wa kuheshimu na kuitumia katiba.

Lakini hii si sababu ya kuacha kudai katiba mpya, kwa maana, hata mazungumzo ya, na mchakato wa kudai katiba mpya tu, vinawafungua macho Watanzania wengi kuhusu si tu umuhinu wa katiba mpya, bali hata utamaduni wa kuheshimu katiba na ukatiba, pamoja na kuitumia vizuri hata katiba ya sasa.
 
Katiba mpya ni mwanzo mzuri.

Kama rais yuko juu ya sheria, hakuna chombo chochote kitakachothubutu kuwa kinyume naye….Iwe jeshi, polisi au mahakama.
Rais hayuko juu ya sheria, hata kwa hii katiba ya sasa.

Ni ujinga na uoga wetu sisi Watanzania ndo unaowapa uthubutu hao watawala wa kupora haki za watu.
 
Ndio maana mimi najiuliza mara nyingi, kama kwa katiba hii hata haki za kikatiba tunashindwa kuzidai ni nini katiba mpya itafanya?

Kwanza isambazwe elimu ya uraia ili tujitambue walau kwa haki za msingi zilizopo. Bila hivyo katiba mpya itakuwa mvinyo mpya kwenye kiriba kikuu.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
Hapo ndo unapoona kuwa matatizo yetu ni zaidi ya katiba [mpya].
 

Nilishangazwa sana na viongozi wa vyama vya upinzani kusimama na kumpigia makofi Rais Samia.

Unampongeza mtu kwa kuwa ametangaza kuacha kuvunja sheria? Huku ndiko nchi yetu ilipofikia, ni aibu mno.
Mimi bado nashangaa!
 
05 January 2023

Askofu - Siwezi kumsifia kwa kuchelewa kuondoa amri haramu ya rais aliyepita, alitakiwa siku ya kwanza alipoingia madarakani angeiondoa amri hii haramu ya mtangulizi wake ...

 
Naomba nizungumzie kiujumla, licha ya kwamba kati yetu binafsi, wapo ambao wako tofauti na walio wengi.

Watanzania wengi ni wajinga [wasiozijua haki zao] na ni waoga sana.

Mchanganyiko wa hizo sifa mbili ni kikwazo kikubwa sana katika maendeleo ya jamii.

Huwezi kupata maendeleo yoyote yale ya maana endapo idadi kubwa ya watu kwenye hiyo jamii wana hizo sifa za ujinga na uoga.

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu, pale mtu asiye na mamlaka ya kukupora haki zako anapokupora, na wewe humpingi huyo mporaji kwa nguvu na uwezo wako wote, ni kitu gani kingine utakachoweza kukipigania kwa hali na mali?

Watanzania tumeshuhudia kuporwa baadhi ya haki zetu kwa miaka ya hivi karibuni kuanzia takriban 2016 mpaka hivi sasa. Na tumekuwa wapole na wanyonge mno.

Alianza Rais Magufuli kukiuka katiba na kuvikataza vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa, kikubwa kikiwa ni mikutano ya kisiasa.

Magufuli kaondoka, kaja Rais Samia naye akaendeleza huo uvunjaji wa katiba.

Wote hawa wawili wamevunja katiba waziwazi kabisa. Na sisi wananchi wenye nchi hakuna lolote la maana tulilolifanya kuwapinga hao wawili!

Tunaburuzwa buruzwa tu. Juzi hapa Samia eti katoa ruhusa ya vyama vya siasa kuanza kufanya mikutano ya kisiasa!

Hiyo ruhusa kaitoa kwa msingi gani wa mamlaka aliyonayo kisheria na kikatiba?

Sisi ni banana republic. Hatuongozwi na sheria wala katiba. Tunaongozwa na hisia, hisani, na matakwa ya mtu ambaye kimsingi ni mtumishi wetu, lakini kiuhalisia ni kama vile sisi ndo tunamtumikia yeye na si vinginevyo.

Kuna wakati kule Marekani, kipindi ambacho Donald Trump alikuwa Rais, kulikuwa na mjadala kuwa endapo angetoa agizo kwa jeshi la nchi hiyo, agizo lililo haramu kisheria na kikatiba, viongozi wa jeshi walikuwa wako tayari kabisa kulikaidi hilo agizo. Hawakuwa tayari kutekeleza agizo lolote linaloenda kinyume na sheria na katiba yao.

Hao ni watu wanaojitambua. Ni watu wasio waoga. Ni werevu na ni majasiri pia.

Hapa kwetu jambo kama hilo bado sijaona kama linawezekana.

Magufuli na Samia walipaswa kupingwa vikali sana.

Maagizo yao haramu ya kuzuia mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani yalipaswa kukaidiwa na watekelezaji wa sheria.

Mtu kama kweli unajitambua, si mjinga wala muoga, kwa nini utekeleze amri ambayo si halali?

Kwani ukikataa kutekeleza amri ambayo si halali, nini kitakutokea?

Ije katiba mpya au isije, hii tuliyonayo sasa hivi inayotupatia haki tulizonazo sasa hivi, inakiukwa waziwazi kabisa na hatufanyi chochote kulinda hizo haki zetu, hiyo mpya tunayoitaka tutailinda kweli?

Kwa sasa nimeshahitimisha kuwa tatizo letu kubwa wala siyo katiba mpya. Tatizo ni sisi wenyewe. Bado tupo wajinga sana, wapole sana, na waoga sana.

Kwa hizi sifa, hata ije katiba mpya, hakutokuwa na tofauti yoyote ile. Tutaendelea kuburuzwa tu hadi pale tutapobadilika.

Na kwa kizazi hiki kilichopo, sitegemei tubadilike.

Adui wetu mkubwa ni sisi wenyewe!

Rais Samia hastahili pongezi yoyote ile kwa ‘kuruhusu’ vyama vya siasa kufanya mikutano ya kisiasa.

Hakuwa na haki ya kukataza hiyo mikutano. Hivyo hana haki ya kuruhusu mikutano hiyo.

Hastahili kabisa pongezi.

Anachopaswa kufanya ni kuomba radhi. Aombe radhi kwa kukiuka katiba.

Akiomba radhi kwa hilo, mimi nitakuwa wa kwanza kumpongeza kwa kuona kosa lake na kuamua kujirudi.

Nje ya hapo, siwezi kumpongeza mporaji aliyeamua kunirudishia kilicho changu.
Unalinganisha Bongo na Marekani?
Sie wenzetu ni Kenya,Uganda,wabongo sio wajinga kiasi hicho,waliwahi kumpinga Nyerere,na wengine walipoteza maisha!wakati wa Maghu,wengi walimpinga,na walilipa kwa kupoteza maisha yao!!
Wewe unayesema wabongo ni wajinga,hujawahi hata kulala lockup!!
Umekaa sehemu unaandika makala nyuma ya keyboard hutaki hata kujulikana!
 
Naunga mkono..

Tumekuwa watu wakuomba wakati mwingine ni wajibu na hali yetu kupata...
Tumeshazowea kuomba ! Hata dukani tunasemaga naomba kiberiti huku nampa pesa Mangi au Mgosi. !
 
Back
Top Bottom