Prof Griff
JF-Expert Member
- Aug 29, 2008
- 6,772
- 5,258
Old ass nigga…you already know whenever me and you cross paths, it’s on-site.Afrika, na hususan Tanzania siyo Marekani wewe hayawani. Wewe na werevu na ujasiri wako, ulikuwa wapi kupinga hilo katazo wakati wa utawala wa JPM? Mnasubiri jambo litokee halafu mnakuja kuonyesha unafiki wenu. Siasa waachieni Wanasiasa: mikutano ya kisiasa nje ya chaguzi ni watu wachache sana wanahudhuria.
DuhOld ass nigga…you already know whenever me and you cross paths, it’s on-site.
I’ll fold you like a pretzel and dunk you in some Sweet Baby Ray’s Hickory & Brown Sugar barbecue sauce.
Watch your Twitter fingers.
Tutashitakiwa MIGA ~~~~~ LisuWe.nae punguwani kweli.
Unaaminije mambo ya kijinga namna hiyo?
Kama katiba hii inamruhusu rais kuwa dikteta, basi tambuwa dikteta huwa juu ya sheria.Rais hayuko juu ya sheria, hata kwa hii katiba ya sasa.
Ni ujinga na uoga wetu sisi Watanzania ndo unaowapa uthubutu hao watawala wa kupora haki za watu.
Most Tanzanians are lazy and sloppy, let's face the facts.Naomba nizungumzie kiujumla, licha ya kwamba kati yetu binafsi, wapo ambao wako tofauti na walio wengi.
Watanzania wengi ni wajinga [wasiozijua haki zao] na ni waoga sana.
Mchanganyiko wa hizo sifa mbili ni kikwazo kikubwa sana katika maendeleo ya jamii.
Huwezi kupata maendeleo yoyote yale ya maana endapo idadi kubwa ya watu kwenye hiyo jamii wana hizo sifa za ujinga na uoga.
Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu, pale mtu asiye na mamlaka ya kukupora haki zako anapokupora, na wewe humpingi huyo mporaji kwa nguvu na uwezo wako wote, ni kitu gani kingine utakachoweza kukipigania kwa hali na mali?
Watanzania tumeshuhudia kuporwa baadhi ya haki zetu kwa miaka ya hivi karibuni kuanzia takriban 2016 mpaka hivi sasa. Na tumekuwa wapole na wanyonge mno.
Alianza Rais Magufuli kukiuka katiba na kuvikataza vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa, kikubwa kikiwa ni mikutano ya kisiasa.
Magufuli kaondoka, kaja Rais Samia naye akaendeleza huo uvunjaji wa katiba.
Wote hawa wawili wamevunja katiba waziwazi kabisa. Na sisi wananchi wenye nchi hakuna lolote la maana tulilolifanya kuwapinga hao wawili!
Tunaburuzwa buruzwa tu. Juzi hapa Samia eti katoa ruhusa ya vyama vya siasa kuanza kufanya mikutano ya kisiasa!
Hiyo ruhusa kaitoa kwa msingi gani wa mamlaka aliyonayo kisheria na kikatiba?
Sisi ni banana republic. Hatuongozwi na sheria wala katiba. Tunaongozwa na hisia, hisani, na matakwa ya mtu ambaye kimsingi ni mtumishi wetu, lakini kiuhalisia ni kama vile sisi ndo tunamtumikia yeye na si vinginevyo.
Kuna wakati kule Marekani, kipindi ambacho Donald Trump alikuwa Rais, kulikuwa na mjadala kuwa endapo angetoa agizo kwa jeshi la nchi hiyo, agizo lililo haramu kisheria na kikatiba, viongozi wa jeshi walikuwa wako tayari kabisa kulikaidi hilo agizo. Hawakuwa tayari kutekeleza agizo lolote linaloenda kinyume na sheria na katiba yao.
Hao ni watu wanaojitambua. Ni watu wasio waoga. Ni werevu na ni majasiri pia.
Hapa kwetu jambo kama hilo bado sijaona kama linawezekana.
Magufuli na Samia walipaswa kupingwa vikali sana.
Maagizo yao haramu ya kuzuia mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani yalipaswa kukaidiwa na watekelezaji wa sheria.
Mtu kama kweli unajitambua, si mjinga wala muoga, kwa nini utekeleze amri ambayo si halali?
Kwani ukikataa kutekeleza amri ambayo si halali, nini kitakutokea?
Ije katiba mpya au isije, hii tuliyonayo sasa hivi inayotupatia haki tulizonazo sasa hivi, inakiukwa waziwazi kabisa na hatufanyi chochote kulinda hizo haki zetu, hiyo mpya tunayoitaka tutailinda kweli?
Kwa sasa nimeshahitimisha kuwa tatizo letu kubwa wala siyo katiba mpya. Tatizo ni sisi wenyewe. Bado tupo wajinga sana, wapole sana, na waoga sana.
Kwa hizi sifa, hata ije katiba mpya, hakutokuwa na tofauti yoyote ile. Tutaendelea kuburuzwa tu hadi pale tutapobadilika.
Na kwa kizazi hiki kilichopo, sitegemei tubadilike.
Adui wetu mkubwa ni sisi wenyewe!
Rais Samia hastahili pongezi yoyote ile kwa ‘kuruhusu’ vyama vya siasa kufanya mikutano ya kisiasa.
Hakuwa na haki ya kukataza hiyo mikutano. Hivyo hana haki ya kuruhusu mikutano hiyo.
Hastahili kabisa pongezi.
Anachopaswa kufanya ni kuomba radhi. Aombe radhi kwa kukiuka katiba.
Akiomba radhi kwa hilo, mimi nitakuwa wa kwanza kumpongeza kwa kuona kosa lake na kuamua kujirudi.
Nje ya hapo, siwezi kumpongeza mporaji aliyeamua kunirudishia kilicho changu.
Actually sidhani kama katiba hii inamruhusu Rais kuwa dikteta.Kama katiba hii inamruhusu rais kuwa dikteta, basi tambuwa dikteta huwa juu ya sheria.
Kama sikosei, the late mwalimu Nyerere alilisema hili.
Rais ambaye hawezi kushitakiwa popote na yeyote akiwa madarakani na hata baada ya kustaafu, anaweza kupingwa na nani? Kumbuka dola yote iko mikononi mwake. Siyo jeshi, polisi wala usalama tu. Hadi mahakama hakuna mwenye uwezo wala uthubutu wa kwenda kinyume na rais.Actually sidhani kama katiba hii inamruhusu Rais kuwa dikteta.
Kinachompa fursa Rais kuwa dikteta ni ujinga na uoga wa wananchi.
Magufuli na Samia walitumia kipengele gani cha katiba hii kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa?
Kwa comment hii, nimemwamini Nyami Ngabu.Mimi nilidhani mleta mada unakuja na hoja inayogusa jamii ya wananchi kwa ujumla wake kumbe ni maslahi ya kisiasa na vyama vya siasa.
Kwa hio kama hao viongozi wasingezuia hio mikutano ya kisiasa wasingekua na ubaya wowote.
Hivo mikutano ya kisiasa ilikuwepo kipindi kile cha uongozi wa Kikwete mbona faida yake haionekani katika jamii.
Kwamba kuruhusiwa hio mikutano ya kisiasa ndio mwanzo wa taifa na wananchi kwa ujumla wataondokana na umaskini na kadhia zote zilizo kati yetu?
Nimezungumzia ujinga wa Watanzania na kutolea mfano majenerali wa Marekani walivyokuwa tayari kukaidi amri haramu toka kwa Trump.Rais ambaye hawezi kushitakiwa popote na yeyote akiwa madarakani na hata baada ya kustaafu, anaweza kupingwa na nani? Kumbuka dola yote iko mikononi mwake. Siyo jeshi, polisi wala usalama tu. Hadi mahakama hakuna mwenye uwezo wala uthubutu wa kwenda kinyume na rais.
Wakati maandamano yalipotaka kufanyika sijui yale ya “ukuta”, rais alituma jeshi la wananchi mtaani.
Rais akilalamika juu yako huna lako. Usipopotezwa unaweza kufia jela kwa kesi ya kupewa.
Pesa yako halafu unasema unaomba😂Tumeshazowea kuomba ! Hata dukani tunasemaga naomba kiberiti huku nampa pesa Mangi au Mgosi. !
Eti wewe pia ni Great Thinker!Prof. Lumumba aliwahi kusema kuwa;
Demokrasia ya Marekani haiwezi kuwa sawa na demokrasia ya Afrika/ Tanzania, wala hatulazimiki kufuata demokrasia za mataifa ya ulaya.
Sisi kama watanzania tuna aina yetu ya demokrasia iliyo ambatana na desturi zetu sisi.
usituletee mambo ya waamarekani ambao wao hata ushoga kwao ni haki!! na wala hawaoni aibu kudai haki hiyo.
Unataka kusema mkuu watanzania hawana rekodi za kuandamana huko nyuma na kupata misukosuko ya polisi katika nchi hii?na ndiyo maana Mh. Mbowe kaamua ku- reconcile na Dola ili kuangalia namna bora ya kudai haki kwa mazungumzo sababu kaona hakuna njia nyingine zozote ambazo nchi zingine walifanya wakafanikiwa kwetu zimedunda zote.
Kwa mfano watanzania mnapanga maandamano kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu kesho unajikuta peke yako mtaani na bango lako...unakula mkongoto wa haja unakwenda kuuza majeraha kwa pesa yako na kesi juu.
Labda wewe ndiyo umeshindwa kuilewa point yangu.Nimezungumzia ujinga wa Watanzania na kutolea mfano majenerali wa Marekani walivyokuwa tayari kukaidi amri haramu toka kwa Trump.
Ukiwa mjinga na muoga utakubali kutekeleza amri zilizo haramu.
Ukiwa mjinga na muoga, hata katiba ikiruhusu Rais kushitakiwa mahakamani, huko mahakamani utakutana na majaji wajinga na walio waoga, hivyo hayo mashitaka dhidi ya Rais hayatakuwa na maana yoyote ile maana hakuna atayethubutu kumkuta na hatia Rais.
Inaonekana point yangu umeshindwa kuielewa.