Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Deadbody umenichekesha sana na uandishi wako hasa ukizingatia nilikuwa nakumbuka matukio ya advance. Kwa kweli ile level ya elimu kwa masomo ya sayansi ni ngumu kupita hata masomo ya digrii ya kwanza (sijui kuhusu ya pili).
Old moshi hiyo,tulikuwa tunafundishwa na mwalimu (aka Pdiddy) ana sauti ndogo halafu ana aibu sana hivyo anaishia kusema na ubao tu. Mifano yake ubaoni mnaelewa vizuri tu sema sasa akiacha maswali unaona kama haukuwamo darasani vile.
Prep ya physics nikifanikiwa swali moja tu kutoka kwenye UP,siku imeisha maana nakuwa nimetumia si chini ya masaa 3-4 kupata ufumbuzi ukijumlisha na baridi la moshi ndio hamu ya kulalal inakuja haraka.
Nakumbuka tulikuwa na mshikaji wangu tukakubaliana kuuza godoro moja (tuwe tunatumia moja kwa zamu) ili kupunguza muda wa kulala ili fiziksi isitushinde lakini mwisho wa hakuna cha maana tulichopata.
Nadhani sitamshauri mwana familia wangu yeyote kusoma advance, ni kupoteza muda tu.
Usinikumbushe P. Diddy yule faza ni katili wa MECHANICS sijapata ona
 
Hahaha Daaah physics ni balaa Kuna T.O mmoja hivi alimaliza 2006 alikuja Kutufundisha sisi tukiwa form 6 tukajiona Vilaza Wote.. vitabu vya Chand...Roger. vyote tuliona Tumemaliza na Hakuna Swali Gumu.. Jamaa Halafu alikuwa ana dharau balaa na Chuo alifukuzwa Kisa Dharau kwa Maprofesa kwahiyo akabak anapiga Tuition mtaani tu na Sifa Kibao na Kuwaona Watanzania wote hawana Akili ila Yeye peke yake

Ila Nakumbuka Siku ya Mtihani wa Physics Nilipiga msuli Usiku halafu kesho yake Pepa Asubuhi Na Nikasolve Maswali Kama matatu hivi ya Chand kwenye Pepa Yamekuja Vile vile Nikasema Nashukuru Mungu Ndalichako kaniona

Ila Yote tisa nitarudi Shule Zote ila Siyo Advance
Atakua T.O Martin Chegere huyo. Ndio najua ali wai kupata mshike mshike chuo kati yake na lectures...
 
Hahaha Daaah physics ni balaa Kuna T.O mmoja hivi alimaliza 2006 alikuja Kutufundisha sisi tukiwa form 6 tukajiona Vilaza Wote.. vitabu vya Chand...Roger. vyote tuliona Tumemaliza na Hakuna Swali Gumu.. Jamaa Halafu alikuwa ana dharau balaa na Chuo alifukuzwa Kisa Dharau kwa Maprofesa kwahiyo akabak anapiga Tuition mtaani tu na Sifa Kibao na Kuwaona Watanzania wote hawana Akili ila Yeye peke yake

Ila Nakumbuka Siku ya Mtihani wa Physics Nilipiga msuli Usiku halafu kesho yake Pepa Asubuhi Na Nikasolve Maswali Kama matatu hivi ya Chand kwenye Pepa Yamekuja Vile vile Nikasema Nashukuru Mungu Ndalichako kaniona

Ila Yote tisa nitarudi Shule Zote ila Siyo Advance
Huyo dogo hakufukuzwa chuo kwa dharau ila alidisco kwa kushindwa ku manage time...
 
Physics advance ni Nouma,Unahitaji mkono mwepesi kusolve bila kuremba,Pia Unahitaji kufall in love naturally katika hisabati,
 
Ugumu wa Physics unategemea na Mwl ,sisi tulipata bahati miaka hy kufundishwa na Wamarekani (volunteers) yaani wako very simple na wana tactics nyingi na simple huwezi amini National exam kwa PCB , Physics na Biology watu ndio walifaulu mostly ,nilichojifunza walimu wa kibongo wana complicate sana mambo .
 
MAANA YA SHULE NI ADVANCED PHYSICS ILIKUWA INAFIKA WAKATI NAJIULIZA HILI SOMO MTAALA UMEKOSEWA NINI

MAANA KUNA ZILE PRAC ZA HEAT UNATAKIWA UFANYE VITU VINGI SANA KWA WAKATI MMOJA SIJUI USOME STOP WATCH WAKATI HUO HUO THERMOMETER WAKATI HUO HUO UFANYE COOLING WAKATI HUO HUO URECORD DATA



DAH JAMANI JAMANI PHYSICS ADVANCE AISEE

OLD MOSHI PALE KULIKUWA NA KATILI WA MECHANICS P. DIDDY
P. Diddy sijui atakuwa wapi sasa hivi ,Kinunda ,Mzee Maganga ,Kirumbuyo nk
 
Physics itabaki kuwa Story kwa wengi but ma TO wengi hutokea kombi ya pcm kwani ni rahisi kutransfer knowledge ya physics kwenda hesabu na chemistry.
 
Nimesoma Advanced Physics hivyo nakumbuka vizuri mziki wake, tena enzi hizo ukifika unapewa UP kama reference book pia kulikuwa na Nelkon 6th edition.

Physics noma sana. Ukitaka ujue Physics sio mchezo tembelea kwenye vyuo vikuu ulizia waosoma Physics kwa level zote iwe BSc, MSc na PhD yaani wa kutafuta. Nakumbuka kuna rafiki yangu alikuwa kwenye darasa la BSc (Education) waliokuwa wanasoma Physics na Maths ni wawili tu. Hao jamaa walikuwa hawalali jinsi Physics ilivyokuwa inawasumbua.
 
Back
Top Bottom