Afande Kagame: Wanajeshi huwa hawalalamiki?

Afande Kagame: Wanajeshi huwa hawalalamiki?

Mzee walikujia wale makachero wa kawaida,au wale wanajiita special force????.Ni kawaida yao kutowaamini Watanzania mkuu.
Wanapekua hadi hotelini! Hoteli zao zote zimejaa viwavi! Mimi nilikuwa naweka mitego ya kufa mtu nakuta hadi begi limepekuliwa ( ila kwa akili sana). Hawaamini mtu wale ...

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Afande Kagame siku nyingine najua unapitia pitia mitandao ya kijamii ya Watanzania iliyoandikwa kwa lugha za Kiswahili ama Kingereza kama Jamii Forums na kadhalika.

Afande najua hupendi kuulizwa maswali ila mimi ngoja nikuulize swali, mbona unakuwa muoga wa kurudi frontline kupambana na haya makundi FDLR, RLA, PRA, RUF,PDR na mengine mengi ambayo sijayataja hapa wakati wewe ndio uliwafukuza madarakani tokea 1994?

Unadhani watakaa Congo DRC, Tanzania, Kenya, South Sudan, Burundi, Uganda, USA, Canada na Australia mpaka lini kwenye hali ngumu kimaisha na kiukimbizi wakati Rwanda ni nchi yao pia?

Wengi wa wanajeshi uliowapindua wameshakufa vimebaki vizazi vipya ambavyo dhumuni lao kubwa ni kurudi Rwanda iwe kwa nguvu au kwa demokrasia. Wewe mwenyewe ulikaa Uganda na Tanzania miaka mingapi kama mkimbizi mpaka mjomba Museveni alipokupa mipango ya kurudi Rwanda au umesahau?

Usiogope kupambana afande Kagame, sababu anayeua kwa upanga lazima atauawa kwa upanga. Au umesahau kuwa dunia nayo ilikuwa inaona jinsi RPF ilivyokuwa inaua Wahutu na Wakongomani ndani ya Rwanda na ndani ya Congo DRC majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini kulipiza kisasi cha genocide ya Watusi ya mwaka 1994 iliyofanywa na serikali ya Habriymana?

Sawa ipo wazi kuwa Habyrimana alikua mbaguzi, katili, mkabila na asiyependa demokrasia hilo linajulikana, ila na wewe toka uchukue madaraka kutoka kwenye kivuli cha Bizimungu umekua kama yeye, hakuna tofauti!

Sasa usiogope kurudi frontline kupambana na ukumbuke kuwa Rwanda hakuna uchaguzi huru toka Mbeligiji aondoke, bali mtutu wa bunduki ndio unaamua mtawala.

Mchawi wala sio Wakongomani au Watanzania au Warundi au Waganda bali mchawi ni wewe mwenyewe uliyevuruga mambo kwa kuukumbatia ukabila na ulevi wa madaraka kama role model wako mjomba Museveni.

Sasa Afande Kagame acha kulalamika kama sio mwanajeshi mbobezi, bali usiogope kurudi uwanja wa mapambano kushika bunduki na kuongoza vikosi na ipo siku usiyotegemea watu watasogea Kigali.

Yaliyomkuta Kanali Doe pale Monrovia na wewe yanaweza kukukuta siku watu wakisogea Kigali na wewe ukiwa haujaondoka ikulu. Au umesahau Mobotu alivyoponea uchupu chupu kule Gabolite alipogoma kuondoka Zaire ya zamani mwaka 1997?

Acha uoga afande, wewe uliingia madarakani kwa mtutu wa bunduki, basi na watu wakitaka kukutoa madarakani kwa mtutu wa bunduki "Usilalamike".
Kwani amelalamika nini tena?
 
Nimesoma nimebaki natetemeka

Hapo mhanga siyo Afande Kagame. Mhanga ni mwananchi wa Rwanda.

Kagame ashauriwe kukaa meza ya mazungumzo kwa sababu mema aliyoifanyia Rwanda ni kwa faida ya wananchi wa Rwanda. Kushikiana mtutu ni dalili ya kupalilia uharibifu.

Tusiwaonee wivu wanyarwanda bali tuangalie namna ya kuwapatanisha kwa sababu ni wilaya ya Afrika inayopiga hatua kubwa kiuchumi.

Tusifikie huko jamani.
Vita ni adui wa ustawi
Kwahiyo anavyoua watu mashariki ya Congo wewe unaona sawa sio? Wacongo sio watu?
 
Hilo dili ungenipa mimi 🤣🤣🤣Nina apartment,s kibao tu hazina watu.
Daah nipe mawasiliano WhatsApp still watu wanakuja kufata bidhaa na kama upo maeneo kufikika ni kwa urahisi jiunge na BNB wale jamaa Wamarekani unapata wageni vizuri na unapata hela yako kupitia wao wao wanakata mteja akiomba na mteja hata hajui mmiliki ni nani anafika kwa address tuu ila vyumba viwe na vitu vyote yeye ni kuja kulala tu na uzingatie usafi kama upo daslm wageni wa Nyerere Park wapo wengi na Mikumi wanapeleka Rhino pia utapata wageni wasiotaka kwenda Ngorongoro kuangalia Rhino...
 
Afande Kagame siku nyingine najua unapitia pitia mitandao ya kijamii ya Watanzania iliyoandikwa kwa lugha za Kiswahili ama Kingereza kama Jamii Forums na kadhalika.

Afande najua hupendi kuulizwa maswali ila mimi ngoja nikuulize swali, mbona unakuwa muoga wa kurudi frontline kupambana na haya makundi FDLR, RLA, PRA, RUF,PDR na mengine mengi ambayo sijayataja hapa wakati wewe ndio uliwafukuza madarakani tokea 1994?

Unadhani watakaa Congo DRC, Tanzania, Kenya, South Sudan, Burundi, Uganda, USA, Canada na Australia mpaka lini kwenye hali ngumu kimaisha na kiukimbizi wakati Rwanda ni nchi yao pia?

Wengi wa wanajeshi uliowapindua wameshakufa vimebaki vizazi vipya ambavyo dhumuni lao kubwa ni kurudi Rwanda iwe kwa nguvu au kwa demokrasia. Wewe mwenyewe ulikaa Uganda na Tanzania miaka mingapi kama mkimbizi mpaka mjomba Museveni alipokupa mipango ya kurudi Rwanda au umesahau?

Usiogope kupambana afande Kagame, sababu anayeua kwa upanga lazima atauawa kwa upanga. Au umesahau kuwa dunia nayo ilikuwa inaona jinsi RPF ilivyokuwa inaua Wahutu na Wakongomani ndani ya Rwanda na ndani ya Congo DRC majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini kulipiza kisasi cha genocide ya Watusi ya mwaka 1994 iliyofanywa na serikali ya Habriymana?

Sawa ipo wazi kuwa Habyrimana alikua mbaguzi, katili, mkabila na asiyependa demokrasia hilo linajulikana, ila na wewe toka uchukue madaraka kutoka kwenye kivuli cha Bizimungu umekua kama yeye, hakuna tofauti!

Sasa usiogope kurudi frontline kupambana na ukumbuke kuwa Rwanda hakuna uchaguzi huru toka Mbeligiji aondoke, bali mtutu wa bunduki ndio unaamua mtawala.

Mchawi wala sio Wakongomani au Watanzania au Warundi au Waganda bali mchawi ni wewe mwenyewe uliyevuruga mambo kwa kuukumbatia ukabila na ulevi wa madaraka kama role model wako mjomba Museveni.

Sasa Afande Kagame acha kulalamika kama sio mwanajeshi mbobezi, bali usiogope kurudi uwanja wa mapambano kushika bunduki na kuongoza vikosi na ipo siku usiyotegemea watu watasogea Kigali.

Yaliyomkuta Kanali Doe pale Monrovia na wewe yanaweza kukukuta siku watu wakisogea Kigali na wewe ukiwa haujaondoka ikulu. Au umesahau Mobotu alivyoponea uchupu chupu kule Gabolite alipogoma kuondoka Zaire ya zamani mwaka 1997?

Acha uoga afande, wewe uliingia madarakani kwa mtutu wa bunduki, basi na watu wakitaka kukutoa madarakani kwa mtutu wa bunduki "Usilalamike".
Interahamwe na ex-FAR walishajua kiswahili na Kingeleza wakiingia tu wanaandika na kupenyeza chuka zao za ubaguzi, hakuna Mtanzania ana mda wa kuandika huu upuuzi.
Kagame aliwatandika na kuwakimbiza myaka hiyo baada ya mauaji sasa Rwanda ya leo unahisi mtaiweza?sahau!
Bora mkarudi kugenga taifa lenu tu.
na kama ulifanya mauaji ujue gereza lipo kwa ajili yako.
 
Interahamwe na ex-FAR walishajua kiswahili na Kingeleza wakiingia tu wanaandika na kupenyeza chuka zao za ubaguzi, hakuna Mtanzania ana mda wa kuandika huu upuuzi.
Kagame aliwatandika na kuwakimbiza myaka hiyo baada ya mauaji sasa Rwanda ya leo unahisi mtaiweza?sahau!
Bora mkarudi kugenga taifa lenu tu.
na kama ulifanya mauaji ujue gereza lipo kwa ajili yako.
Myaka hiyo ndio lugha na wewe mnyarwanda ?
 
Daah nipe mawasiliano WhatsApp still watu wanakuja kufata bidhaa na kama upo maeneo kufikika ni kwa urahisi jiunge na BNB wale jamaa Wamarekani unapata wageni vizuri na unapata hela yako kupitia wao wao wanakata mteja akiomba na mteja hata hajui mmiliki ni nani anafika kwa address tuu ila vyumba viwe na vitu vyote yeye ni kuja kulala tu na uzingatie usafi kama upo daslm wageni wa Nyerere Park wapo wengi na Mikumi wanapeleka Rhino pia utapata wageni wasiotaka kwenda Ngorongoro kuangalia Rhino...
Nakuchek mkuu tufanye ujasiriamali.
 
Myaka hiyo ndio lugha na wewe mnyarwanda ?
Afande PS a.k.a Mgomba mrefu mjomba wangu yule hana shida,ila namkumbusha asiogope frontline wakurugwa wa FDR,,PDR,LPR,DDR, na wengineo wakilianzisha asianze kulalamika kama Habriymana.Analalamika sana utadhani sio mwanajeshi.Kuhusu kuua wote RPA na FAR walihusikana ile genocide ila mshindi kwenye vita ndio waga anaandika historia.Tumechoka kupokea wakimbizi,lazima warudi nchi yao ya asili iwe kwa demokrasia ya sanduku la kupigia kura au kwa mtutu wa bunduki
 
Back
Top Bottom