Afande Sele: Tozo zimekuwa nyingi na hazionekani zinafanya kazi gani

Afande Sele: Tozo zimekuwa nyingi na hazionekani zinafanya kazi gani

Tozo hazionekani zinafanya nini wakati zimesajili wachezaji wa Singida au haoni?
 
Watu wote huenda kwenye ziara za mh Rais wetu mpendwa kwa hiari na upendo mkubwa Sana Tulio nao kwa mh Rais wetu, maana tunajuwa kuwa Rais wetu Ni kiongozi wa kazi muda wote, hivyo tunakuwa tunakwenda kumsikiliza kwa hamu kubwa Sana, Rais wetu Ni mtumishi wa watu anayetutumikia kwa upendo na unyenyekevu mkubwa Sana, Tunampenda na tunaendelea kuwa na Imani na matumaini naye

Nchi hii rais kupata watu kwenye ziara zake kulianza toka enzi za Nyerere,na mbinu za kuwakusanya watu tunafahamu ni kushinikiza kwa nguvu za dola, vitisho na burudani mbalimbali ili watu wajae kutengeneza Hadaa kuwa wanakubalika sana.

Cha muhimu ili tutenge hizi propaganda zenu na ukweli, tengeneza jedwali kuonyesha aina ya mradi, thamani yake, chanzo cha fedha kwenye mradi husika, mkoa, wilaya na kata. Hapa tutakata mzizi wa fitina. Hizo siasa za kuongopea wananchi pelekeeni ile mifugo inayojitokeza kushangilia bila uwezo wa kuhoji chochote.
 
Mwigulu anatakiwa kutuambia tozo anazokusanya kila mwezi ni shilingi ngapi na zinapelekwa kwenye matumizi yapi, ili tupime matumizi ya tozo tunazokatwa kama yanaendana na thamani ya hiyo miradi, anavyokaa kimya maana yake anatuibia.
Kumbuka Singida Big Stars sio yake! Hahahaa
 
Usijifanye kama vile umepata uraia wa Tanzania leo,ulijiuliza kwanini 'MKUU aliwaambia kua NAJUA MNAKULA KWENYE MAENEO YENU' akawasihi wasivimbiwe,ulijiuliza kua mtu anaweza akavimbiwa mshahara?
Hukujiuliza alivyowaambia WAJIPIMIE,hivi mshahara WAAJIRIWA wanajipangia?
Acha kudharau kichwa chako bhana,kipe kichwa chako heshima ya kuchanganua sentensi.
Pep Kuna watu wanadharau vichwa vyao[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Tozo zimeondoa " Ile yakulipa kwa Dpp" waliita.proo bargaini
 
Msipende kuupotosha huu msemo wa kula kwa urefu wa kamba yako....kwani Kuna tatizo kula kulingana na urefu wa kamba yangu?kamba yangu ni kipato changu NI mshahara wangu,urefu wake NI laki 6 kwa mwezi ,lazima NIISHIE hapo,maana huo ndio urefu wa kamba yangu...SASA MNATAKA NILE KWA UREFU WA KAMBA YA MWENZANGU?(HIYO NDIYO RUSHWA SASA,NDIYO MATUMIZ MABAYA YA MADARAKA YAKO)
We nae kichwa boga kweli kwa hiyo mkuu wa refu za kamba alimanisha walamba asali wanavimbiwa mishahara heeee .sehemu.siriaz usilete maneno maneno ya khanga bhana ee
 
Pole sana mkuu😀😅
Siwezi kupoa kirahisirahisi hivyo,huku kwa akili zangu timamu,nashuhudia watu wenye akili kama zangu,wakila keki ya nchi,mimi nikiwa nje ya mfumo,zinakuja fursa mfano za ajira za ualimu,dogo wa 2021,2020,2019 anaajiriwa,na kasoma masomo yaleyale niliyosoma mimi hadi kuhitimu 2016,mimi nipo nje tu ya mfumo,hadi familia yangu inaniwazia vibaya kua labda nilishafeli nikawaficha,ndiyomaana siajiriwi,wanaajiriwa wengine.It pains much,basi tu,nagikisha miaka thelathini na kitu,nipo gheto,naishi kitotokitoto,hadi najiuliza kwanini nilisoma,si ningeishiaga hata form four tu,kuliko kusoma hadi chuo kikuu hata sensa nakosa,inauma sana.
 
Siwezi kupoa kirahisirahisi hivyo,huku kwa akili zangu timamu,nashuhudia watu wenye akili kama zangu,wakila keki ya nchi,mimi nikiwa nje ya mfumo,zinakuja fursa mfano za ajira za ualimu,dogo wa 2021,2020,2019 anaajiriwa,na kasoma masomo yaleyale niliyosoma mimi hadi kuhitimu 2016,mimi nipo nje tu ya mfumo,hadi familia yangu inaniwazia vibaya kua labda nilishafeli nikawaficha,ndiyomaana siajiriwi,wanaajiriwa wengine.It pains much,basi tu,nagikisha miaka thelathini na kitu,nipo gheto,naishi kitotokitoto,hadi najiuliza kwanini nilisoma,si ningeishiaga hata form four tu,kuliko kusoma hadi chuo kikuu hata sensa nakosa,inauma sana.
So sad aiseee, hata sensa umekosa?😧😠.
 
Watu wote huenda kwenye ziara za mh Rais wetu mpendwa kwa hiari na upendo mkubwa Sana Tulio nao kwa mh Rais wetu, maana tunajuwa kuwa Rais wetu Ni kiongozi wa kazi muda wote, hivyo tunakuwa tunakwenda kumsikiliza kwa hamu kubwa Sana, Rais wetu Ni mtumishi wa watu anayetutumikia kwa upendo na unyenyekevu mkubwa Sana, Tunampenda na tunaendelea kuwa na Imani na matumaini naye
Mkuu inaonekana una mapenzi makubwa na mama!, Oya umempenda Kwa sababu ya mitindi yake nini?

Meaning no offense!
 
Matusi gani sasa? Kwani hana mitindi?😀😂
Kwani wewe huna mzazi mwanamke au mama yako ambaye hata Mimi naweza mwita mama yangu kiheshima japo Ni wako, je Hivyo ndivyo huwa unaweza kumwelezea kwa watu, au haujawahi kulelewa na mama yako mzazi, hata Kama hukulelewa Naye, je aliyekulea unamwita Nani, uwe na adabu na hekima hata kwa wale unaotofautiana nao, labda Kama umeandika huku akili ikiwa haipo sawa maana naweza nikawa nakuelimisha kumbe Kuna tatizo kubwa unalotakiwa kupewa kimatibabu
 
Kwani wewe huna mzazi wa mwanamke au mama yako ambaye hata Mimi naweza mwita mama yangu kiheshima kapo Ni wako, he Hivyo ndivyo huwa unaweza kumwelezea kwa watu, au haujawahi kulelewa na mama yako mzazi, hata Kama hukulelewa Naye, je aliyelea unamwita Nani, uwe na adabu na hekima hata kwa wale unaotofautiana nao, labda Kama umeandika huku akili ikiwa haipo sawa maana naweza nikawa nakuelimisha kumbe Kuna tatizo kubwa unalotakiwa kupewa kimatibabu
Nilijua tu utamtetea bi mkubwa wako!, haya hongereni na tozo zenu😐😠.
 
Mbona mnalalamika wakati juzijuzi zimefadhili mkutano wa caf na mashindano ya cecafa vilabu
 
Mwigulu anatakiwa kutuambia tozo anazokusanya kila mwezi ni shilingi ngapi na zinapelekwa kwenye matumizi yapi, ili tupime matumizi ya tozo tunazokatwa kama yanaendana na thamani ya hiyo miradi, anavyokaa kimya maana yake anatuibia.
Kwani umeona timu ya Singida Big Stars ikishindwa kufanya usajili? Au wale wachezaji wana changamoto ya mishahara?
 
Back
Top Bottom