Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Taliban wako kwenye operesheni ya kuwatafuta watu waliofanya kazi kwa vikosi vya Nato au serikali ya zamani ya Afghanistan, waraka wa Umoja wa Mataifa umeeleza.
Usema wapiganaji hao wamekuwa wakienda nyumba kwa nyumba kuwatafuta wanaowalenga na kuzitishia familia zao.
Kundi hilo lenye msimamo mkali wa Kiislamu limejaribu kuwahakikishia Waafghan tangu kutwaa madaraka, na kuahidi hakutakuwa na "kisasi".
Lakini kuna hofu kwamba Taliban wamebadilika kidogo tangu miaka ya ukatili ya 1990.
Onyo ambalo limetolewa kuhusu kundi hilo linalowalenga "washirika" lililetwa katika hati ya siri na Kituo cha RHIPTO cha Norway cha Uchambuzi ambacho hutoa usaidizi wa masuala ya ujasusi kwa UN.
"Kuna idadi kubwa ya watu ambao kwa sasa wanalengwa na Taliban na tishio liko wazi," Christian Nellemann, ambaye anaongoza jopo la walioandaa ripoti hiyo, aliiambia BBC.
"Ik kwenye maandishi kuwa wasipojisalimisha Taliban watakawamata na kuwashtaki, na kuwaadhibu wanafamilia kwa niaba ya watu hao."
Alionya kuwa mtu yeyote kwenye orodha ya Taliban yuko katika hatari kubwa, na kwamba kunaweza kuwa na mauaji ya watu wengi.