Afghanistan: Taliban 'wafanya msako wa nyumba kwa nyumba' Umoja wa Mataifa umeeleza

Afghanistan: Taliban 'wafanya msako wa nyumba kwa nyumba' Umoja wa Mataifa umeeleza

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Taliban

Taliban wako kwenye operesheni ya kuwatafuta watu waliofanya kazi kwa vikosi vya Nato au serikali ya zamani ya Afghanistan, waraka wa Umoja wa Mataifa umeeleza.

Usema wapiganaji hao wamekuwa wakienda nyumba kwa nyumba kuwatafuta wanaowalenga na kuzitishia familia zao.

Kundi hilo lenye msimamo mkali wa Kiislamu limejaribu kuwahakikishia Waafghan tangu kutwaa madaraka, na kuahidi hakutakuwa na "kisasi".

Lakini kuna hofu kwamba Taliban wamebadilika kidogo tangu miaka ya ukatili ya 1990.

Onyo ambalo limetolewa kuhusu kundi hilo linalowalenga "washirika" lililetwa katika hati ya siri na Kituo cha RHIPTO cha Norway cha Uchambuzi ambacho hutoa usaidizi wa masuala ya ujasusi kwa UN.

"Kuna idadi kubwa ya watu ambao kwa sasa wanalengwa na Taliban na tishio liko wazi," Christian Nellemann, ambaye anaongoza jopo la walioandaa ripoti hiyo, aliiambia BBC.

"Ik kwenye maandishi kuwa wasipojisalimisha Taliban watakawamata na kuwashtaki, na kuwaadhibu wanafamilia kwa niaba ya watu hao."

Alionya kuwa mtu yeyote kwenye orodha ya Taliban yuko katika hatari kubwa, na kwamba kunaweza kuwa na mauaji ya watu wengi.
 
Wanamgambo wa Taliban wameanza msako wa nyumba hadi nyumba dhidi ya wafanyakazi waliohusika kusaidia Jeshi la Marekani na NATO wakati walipokuwa wakihudumu nchini Afghanistan.

Shirika la Habari la AFP limeripoti kuwa wanamgambo hao wameandaa “Orodha Maalum” ya watu wanaotakiwa kukamatwa na kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria za kidini (sharia).

Hatua hii ya Taliban inakuja siku chache baada ya wanamgambo hao kuahidi kutolipiza kisasi dhidi ya waliohusika kusaidia Majeshi na Mashirika ya Kimataifa nchini humo.

Wanaolengwa na upekuzi huo ni pamoja na wanajeshi wa Jeshi la Afghanistan, Polisi na Vikosi vya Upelelezi, kwa mujibu wa taarifa ya uchambuzi ya Umoja wa Mataifa. Wanamgambo hao wamekamata pia familia za walengwa, huku wakiweka vizuizi vya upekuzi barabarani kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kabul.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa Wataliban wameanza mchakato wa kuwaajiri vijana watakaowapa taarifa.

Katika barua moja iliyochapishwa Agosti 16, Wanamgambo hao walitishia kukamata familia ya Afisa wa Serikali aliyefanya kazi Kitengo cha Kupambana na Ugaidi ikiwa atashindwa kuripoti kwa Maafisa wa Taliban.

Wanamgambo wa Taliban wanafahamika kwa kuweka sheria za kidini zenye adhabu kali ikiwamo kupigwa mawe kwa kosa la kuzini, wakati wa utawala wao wa kati ya mwaka 1996 na 2001 nchini Afghanistan.

Chanzo: AFP

1629443145033.png
 
Wamalizane tu misukule hao wameganda kwenye dini ambayo kila siku inawasababishia maafa badala ya amani na upendo, yaani waachwe hivyo hivyo wachinjane na kulipuana kwa kwenda mbele labda ipo siku watatia akili.
 
Yani na wewe bado unakubali hizo propaganda za mzungu baada ya kusanda anaamua kuleta uongo ili dunia iwachukie wataliban, Marekani alitegemea akiondoka yeye basi pale vita itatokea, kasahau hadi hao wanajeshi wa serikali wengi wao Taliban
 
Hiyo barua iko wapi?

Hii habari ni ya kuichukulia kaa tahadhali, imekaa kipropaganda sana. Tatizo la hizi western security agency, huwa zinakosa ulaji pale vikundi kama hivi vinapokuwa vimetulia. They always need an enemy either real or perceived!
 
Tembo na nyangumi ndio viumbe wakubwa wanaoonekana ukitizama hiyo picha watu wamekamata mikwaju ya nguvu yaani pana wana sayansi wameumiza vichwa kutengeneza silaha hizo kwa ajili ya binadamu wenzao huu ni wehu au ujaha wa kiwango cha juu.
 
Back
Top Bottom