Afikishwa Mahakamani kwa wizi wa Mita za Maji - Kinondoni

Afikishwa Mahakamani kwa wizi wa Mita za Maji - Kinondoni

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mfanyabiashara na mkazi wa Kinondoni, Daud George (28) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kuiba mita za maji na kuisababishia hasara ya Sh904,277. Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (Dawasa).

George amefikishwa Mahakamani hapo leo, Jumatano Januari 8, 2025 na kusomewa kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka matatu.

Mshtakiwa huyo amesomewa mashtaka yake na wakili wa Serikali, Erick Kamala, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki.

Hakimu Nyaki ameahirisha kesi hiyo hadi Januari 21, 2025 itakapotajwa na mshtakiwa amerudishwa rumande.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma ~ Ruvuma: Huu utaratibu wa mteja kulipia mita za maji zilizoibwa upoje? Au mnaiba wenyewe ili tuwaongezee mapato?
 
Mfanyabiashara na mkazi wa Kinondoni, Daud George (28) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kuiba mita za maji na kuisababishia hasara ya Sh904,277. Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (Dawasa).

George amefikishwa Mahakamani hapo leo, Jumatano Januari 8, 2025 na kusomewa kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka matatu.

Mshtakiwa huyo amesomewa mashtaka yake na wakili wa Serikali, Erick Kamala, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki.

Hakimu Nyaki ameahirisha kesi hiyo hadi Januari 21, 2025 itakapotajwa na mshtakiwa amerudishwa rumande.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma ~ Ruvuma: Huu utaratibu wa mteja kulipia mita za maji zilizoibwa upoje? Au mnaiba wenyewe ili tuwaongezee mapato?
Hii haijakaa sawa. Kuna uzembe mwingi watoa huduma ya maji. Mita imening'inia naiweka ndani pale napafunga ili maji yasipotee, na mita kuibiwa. Kosa langu ni lipi hapa
 
Hawa wa idara ya maji ni wazembe mno, hapa kuna mita ambayo walikuja wenyewe na kujifanya wanaiweka juu ,

Kazi iliwsshinda, sasa ni mwaka unapita, mita ipo mguu upande,

Wakipita ni ahadi nyingi ambazo hazitekelezeki.

Hata huyo dogo hiyo kesi itakuwa ya uonevu.

Watu wa maji badilikeni
 
Back
Top Bottom