Africa Cup of Nations (AFCON) 2015 updates

Africa Cup of Nations (AFCON) 2015 updates

Hawa watunisi wanaweza lala na viatu manake hawa jamaa wa visiwani cape verde wamekasirika haswa!!
 
Maana yake? Nimejaribu Google translator ina'respond' "Filipino detected", lakini inashindwa kutafsiri.

Asante Mzee, usiku mwaka (usiku mwema), ngoja nikatengeneze watoto (mambo ya kiutu uzima).

Ni hayo tu Mkuu.
 
Cape verde wanakosa nafasi ya wazi, dak ya 29 tuniasia 0-0 cape verde
 
Huyu mchezaji alie vaa jezi namba 10 (HELDON) wa cape verde anachezea klabu gani mbona mtamu!!! Anafanya vitu vya kufurahisha sana.
 
Hata kule hawapo. Wako vilabuni na kwenye vijiwe wakisakata gongo na disco wakishangilia ushindi wa jana.

Kwa kuwa wewe unatumia basi unadhani kila mtu ni mteja. Unajua sana nani anayeongoza kunywa bia hasa za 'Zungusha kikwetu kwetu'.
Mliopata milioni 5 mkashindwa hata kunywa bia tunaelewa mnatumia kinywaji gani cha bei chee, usichokoze nyuki....
 
Huyu mchezaji alie vaa jezi namba 10 (HELDON) wa cape verde anachezea klabu gani mbona mtamu!!! Anafanya vitu vya kufurahisha sana.

Heldon Ramos anachezea Sporting ya Portugal. Mkuu
 
Haya Cape verde si tulishawahi wafunga mbona sisi tunarudi nyuma wao wanasonga tu
 
Tena wengine hawapatikani humu mpaka wasikie simba imeshinda, hebu angalieni mpira wa watu wanaojua sio kila siku kelele kwa kumsifia mkude wakati hata hajawahi kupata offer ya kwenda kufanya majaribio hata fc leopard au tp mazembe???? acha akina Bolasie wafanye mambo ninyi bakini na sserunkuma wenu.

Acha makelele mkuu mbona tukiwepo humu mnafyata mkia makalioni? Kuna wengine humu walikuwa wanachungulia jukwaa na kutoka hata likes hatukuziona. Baadaya wazee wa kazi kuhamia majukwaa mengine wakarudi na visingizio ooohhh nilikuwa ibada, kwa hiyo wengine hatukuenda ibada?
Jaribu kupitia majukwaa mengine humo uone tulivyotibua sio unasema bila utafiti.

Kama haitoshi kuna mipira mingine yenye akili watu tulikuwa tunafuatilia pia. Man city 0 Arsenal 2.
 
Haya Cape verde si tulishawahi wafunga mbona sisi tunarudi nyuma wao wanasonga tu

Mliwafunga lini au unaizungumzia cape verde ya mwaka 1970 kabla hawajapata uhuru kutoka kwa wa-portugal!!! soka linaloonesha na hawa jamaa wa visiwani si mchezo watz mkitia mguu mnaweza kupigwa hata wiki.
 
Mliwafunga lini au unaizungumzia cape verde ya mwaka 1970 kabla hawajapata uhuru kutoka kwa wa-potugal!!! soka linaloonesha na hawa jamaa wa visiwani si mchezo watz mkitia mguu mnaweza kupigwa hata wiki.

Kipindi cha maximo nakumbuka tuliwahi wapiga goli hawa jamaa
 
Ningekuwa wewe ningekuwa more concerned na fowadi yenu butu inayopata
nafasi 10 na kushindwa kufunga hata kagoli kamoja.Tambwe alijaribu kufunga kwa mkono akapewa kadi ya njano.

Tambwe ametoka kuwa mfungaji bora sasa anaongoza kwa ukosaji magoli bora.
 
Back
Top Bottom