Afrika ina Asilimia 3 tu ya magari yote duniani

Afrika ina Asilimia 3 tu ya magari yote duniani

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Jioni hii BBC Dira wamesema Afrika ina asilimia 3 ya magari yote duniani.

Ikabidi nichimbe nikakutana na hii.

Kufikia mwisho wa robo ya kwanza ya 2022, kulikuwa na takriban magari bilioni 1.45 ulimwenguni, ambayo karibu bilioni 1.1 ni magari ya abiria.

Hiyo ina maana kwamba kuna gari kwa kila watu 7.18 kwenye sayari dunia.

Bara la Antaktika hadi wakati huo lilikuwa na magari 50 tu na mengi ya hayo hayatumii magurudumu.

Kwa mujibu wa Hedges & Company, karibu theluthi moja ya magari yote yako katika eneo la Asia-Pasifiki, eneo la dunia ambalo lina magari milioni 531.

Hii ni pamoja na magari milioni 21 yaliyosajiliwa nchini Australia, kulingana na data ya ABS.

Ulaya ni bara la pili kwa wingi wa magari baada ya Asia, likiwa na magari milioni 405.3 (asilimia 28) yaliyoenea katika nchi za EU na zisizo za EU.

Amerika Kaskazini - ambayo inajumuisha Kanada na Mexico - inamiliki magari milioni 351 (asilimia 24), ambayo milioni 290.8 yako Marekani.

Baada ya hapo kuna mabara yenye magari machache mno kama vile bara la AFRIKA lenye magari ASILIMIA 3 tu.

Mengi ya hayo magari ya Afrika ni mkono wa pili.

Amerika ya Kusini ina magari milioni 83

Mashariki ya Kati ina magari milioni 49.

Afrika katika uchache ina magari milioni 26 tu.

Antaktika ina magari 50 tu.

MY TAKE
• Tupunguze kodi ya magari ili kuongeza idadi ya magari hasa commercial vehicles. Magari hasa ya abiria ya kibiashara/umma ni kichocheo cha uchumi

• Tuhamasishe investors kuanzisha car assembly factories

• Tujenge miundombinu ya barabara zitakazovutia watu na taasisi kuleta magari zaidi.

MAGARI NI MUHIMU SANA KATIKA KUUKIMBIZA UCHUMI. KILA KUNAPOKUCHA MAGARI NDIYO YANAUBEBA UCHUMI WETU.

AFRIKA HOIYEE, TANZANIA HOIYEE
images.jpeg-10.jpg
 
sehemu kubwa ya magari ni chuma na aluminium. Africa kwanza ijitosheleze kwenye hizi metali mbili ndipo itaweza kuunda magari. Hata muwekezaji wa kuassembly magari atahitaji walau bodi ziweze kuzalishwa kwenye nchi husika kwa bei rahisi. Siyo kila kitu aimport
 
sehemu kubwa ya magari ni chuma na aluminium. Africa kwanza ijitosheleze kwenye hizi metali mbili ndipo itaweza kuunda magari. Hata muwekezaji wa kuassembly magari atahitaji walau bodi ziweze kuzalishwa kwenye nchi husika kwa bei rahisi. Siyo kila kitu aimport
Njoo Ruangwa aluminium ya kumwaga
 
sehemu kubwa ya magari ni chuma na aluminium. Africa kwanza ijitosheleze kwenye hizi metali mbili ndipo itaweza kuunda magari. Hata muwekezaji wa kuassembly magari atahitaji walau bodi ziweze kuzalishwa kwenye nchi husika kwa bei rahisi. Siyo kila kitu aimport
Hivi Tanzania tuna aluminium!?
 
Jioni hii BBC Dira wamesema Afrika ina asilimia 3 ya magari yote duniani.

Ikabidi nichimbe nikakutana na hii...
Hakuna haja ya kuwa na magari mengi ili kudhibiti hewa ukaa, Africa ndilo bara ambalo hewa yake haijachafuliwa (haijanajisiwa) na Carbodioxides na carbonmonoxides kuoka kwenye mioshi ya magari, kumbuka raha nayo haikosi karaha.
 
Hakuna haja ya kuwa na magari mengi ili kudhibiti hewa ukaa, Africa ndilo bara ambalo hewa yake haijachafuliwa (haijanajisiwa) na Carbodioxides na carbonmonoxides kuoka kwenye mioshi ya magari, kumbuka raha nayo haikosi karaha.
Kwa hiyo tusakate rumba tu na tz 11 au sio na mizigo tutumie punda au mikokoteni au sio
 
Kwa hiyo tusakate rumba tu na tz 11 au sio na mizigo tutumie punda au mikokoteni au sio


Chagua kufa kwa maradhi yatokanayo na moshi wa magari au kusafiri kwa punda.--- NB: magari YA MTUMBA yaliyopo Africa yanatosha.
 
Back
Top Bottom