Afrika Kusini yapendekeza Sheria kwa Mwanamke kuwa na Mume zaidi ya mmoja

Ngumu sana Mungu fundi mwanamme atabaki kuwa mwanamme, Ni kitu kisichowezekana
 
Huo ni mtazamo wako, kila mtu anamtazamo wake ktk kufasiri jambo, mimi nitabaki na mtazamo wangu (sihukumu) kuhusu mwanamke msamaria nikiwa na maana ya kuwa huyu mwanamke alikuwa na viashiria vyote vya kikahaba maana alimshawishi Yesu aamini kuwa yeye ni single mother 😁

Bahati mbaya Yesu alikuwa hatafuti demu hivyo alimpiga gospel hadi huyo mama akastaajabu kisha akaenda kueneza habari za Yesu kwa wengine
 
... nakubaliana na wewe; tukienda kwa hisia (mtazamo binafsi/subjectivity) badala uhalisia (objectivity) huyo mwanamke anaweza kupewa kila aina ya sifa mbaya. Pale ambapo jambo halina uhakika ni bora kuwa wakweli badala ya mitazamo binafsi.
 
Nimeshangazwa sana leo hii nikisikiza Vyombo vya habari (Redio fulani TZ ) wakisema kuwa Bunge la South linafikiria kupitisha sheria inayowaruhusu wanawake kuolewa na zaidi ya Mwanamume mmoja.
Je wadau Hiimunaionaje?
Haya si ndiyo yale ya Safia Kawawa ya Miaka ya 80? iliyosababisha maandamano makubwa Zanzibar.? na watu kadhaa kujeruhiwa na wengine kuuwawa na Polisi.

Karibuni kwa maoni
 
Kwa mujibu wa tafiti wanawake ndio wako wengi zaidi ya wanaume duniani, sasa hicho wanachotaka kufanya hao sikielewi.
 
Siku zote sheria huzingatia changamoto ya eneo/nchi husika na kabla ya kutungwa wataalam hufanya utafiti ili kuweza kubaini ukubwa wa tatizo.

Inaweza kuwa sheria sahihi kwa mazingira ya S.A lakini si sahihi kwa Tanzania.
 
Hiv huko SA siwameisha pitisha sheria ya kutambua ndoa za jinsia moja? Kama ni "ndiyo" Bas Wapo sahh maana wanahis watu wao watakimbilia usagaji na ushoga kwaiyo wanatafta balance,
Usisahau kuwa wameruhusu na kwa mwanaume kuwa na mwanamke zaid ya mmoja kisheria.
 
Haka kaishu ndiyo form two tulifundishwa types of marriage mojawapo ndiyo hii, Polyandry.

Tukamuomba mwalimu mfano hai alishindwa kuutoa angalau miezi kadhaa mbele akiulizwa swali la mfano hai halitomsumbua.
 
mambo ya ndoa na uzazi sheria yake si ya wanadamu maana wanadamu hawajazuka tu kama mizimu bali wameumbwa na kuwekewa utaratibu mzuri wa kuishi.....kwa hivyo ni jambo la kiutawala wa muumbaji kuwawekea watu sheria ya kuoa na kuolewa wala si pendekezo la kikatiba hilo na ndio maana maumbile yetu yanasadifu utaratibu aliouweka....upuuzi unaofanywa na wanadamu kujaribu kuzifanyia editing sheria za muumba wao mwisho wake sio mwema hata kama sio leo lakini siku yao itafika..
 
binadamu ndivyo walivyo kujaribu kila jambo. Mungu alimpa Adamu mke MMOJA, Kaini akaoa wawili, kule sodoma wakaoana wanaume kwa wanaume,Sasa Afrika Kusini nayo imevumbua ndoa mpya mwanamke mmoja wanaume wawili. Ifuatayo sijui itakuwa ipi?
 
binadamu ndivyo walivyo kujaribu kila jambo. Mungu alimpa Adamu mke MMOJA, Kaini akaoa wawili, kule sodoma wakaoana wanaume kwa wanaume,Sasa Afrika Kusini nayo imevumbua ndoa mpya mwanamke mmoja wanaume wawili. Ifuatayo sijui itakuwa ipi?
mbona umemsahau Mfalme Suleiman mkuu?
 
Kwa staili hii wacha waolewe na mume zaidi ya mmoja.
Hawa ni kama Daladala tuu.kila mtu anapanda.
Unaowa leo kesho unaacha.
 
Hatari ya magonjwa ya kuambukizana lakini mtoto akizaliwa babake atakuwa ni nani??

Dini sahihi kwa maisha ya mwanadamu ni uislmau., ndio dini pekee iliyokuja muongozo sahihi kwenye jambo hili.,
Itabidi hao Wanaume wapeane zamu ya kutunga mimba.
 
Kwa staili hii wacha waolewe na mume zaidi ya mmoja.
Hawa ni kama Daladala tuu.kila mtu anapanda.
Unaowa leo kesho unaacha.
Sisi huku ndio tunaona maajabu kuona mtu yupo nyonyo nje lakin kwao hawana unafiki linapokuja swala la kuvaa kiasili wanavaa kama Bibi zao walivyokuwa wanavaa kabla ya ujio wa wazungu. Nenda Swaziland, Lesotho hayo ni mambo ya kawaida sana hasa kwenye matamasha yao ya kitamaduni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…