Afungwa miaka 30 kwa kosa la kuingilia kinyume na maumbile

Afungwa miaka 30 kwa kosa la kuingilia kinyume na maumbile

Kitendo cha kumuingilia mtoto mdogo bila ridhaa yake tena kinyume na maumbile, ilipaswaa apewe adhabu kulingana na kosa lake.

Poleee zao kwa Wahanga.
 
ina maana wewe kwa umri huo huwezi kuandika neno mbwa

Inategemea nimezaliwa wapi na nimekulia wapi, afterall kutojua kuandika hivyo hakujanipunguzia chochote, na wewe hakujakuongezea chochote umbwa wewe.
 
Mahakama ya Mkoa wa Vuga, leo tarehe 31/10/2023 imemhukumu mshtakiwa MOH'D ALI HASSAN (35) Mkazi wa Jumbi Uwandani Unguja kutumikia kifungo cha miaka 30 Chuo cha Mafunzo (jela) kwa kosa la Kuingilia kinyume na maumbile.

Awali mshtakiwa huyo alimuingilia kinyume na maumbile mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 06 jambo ambalo ni kosa, kinyume na kifungu cha sheria 133 (a) cha sheria ya adhabu namba 6/2018 Sheria ya Zanzibar.

Akisoma maelezo ya hukumu hiyo, Hakimu wa mahakama hiyo Mhe. TAKI ABDALLAH amesema Mahakama imejiridhisha na ushahidi uliotolewa mbele ya mahakama ambao haukuwa na chembe ya shaka ambapo umemtia hatiani mtuhumiwa kwa makosa hayo.

Jumla ya mashahidi watano (05) walitoa ushahidi mahakamani hapo.

Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakamani tarehe 21/08/2023 ambapo ilipewa kesi namba 127/2023.
Hii jamii ina shida sana aisee. Kijana wa miaka 35 unaenda kufungwa kwa miaka yote hiyo kwa sababu ya ujinga wa kuendekeza hisia za ngono.

Kwa wakati huu ambao maisha yake yanamsubiri ayapambanie, yeye anaenda kufanya ujinga kwa mtoto wa watu na kumharibia historia yake.

Mjinga kabisa huyu jamaa, kiukweli hakupaswa kuishi hata huko jela anakokwenda kuwekwa kwa miaka 30.

Ova
 
Ingekuwa Ulaya mzazi angetaifishwa huyo mtoto, na labda kushitakiwa. Mtoto wa miaka 6 kuachwa peke yake na hilo li monster ni criminal neglect. Bahati mbaya sana hapa hatutajua the details, jamii yetu hii vichwa vyetu haviwezi ku process detail kwa hiyo hatujali kujua. Wakristo watabaki wanatukanana na Faiza Foxy makurasa 20 halafu yameisha, on to the next victim.
 
Naona baadhi ya wachangiaji wanafurahia kifungo hicho, hawajui kwamba hata wao ni wafungwa watarajiwa, nakosa ya kisheria na binaadam yanaweza kuhalalisha na ukafungwa ukiwa unaona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inauma sana, mtoto wa miaka SITA. Amaeshamuua tayari kisaikolojia hata kuwa sawa
 
Hii jamii ina shida sana aisee. Kijana wa miaka 35 unaenda kufungwa kwa miaka yote hiyo kwa sababu ya ujinga wa kuendekeza hisia za ngono.

Kwa wakati huu ambao maisha yake yanamsubiri ayapambanie, yeye anaenda kufanya ujinga kwa mtoto wa watu na kumharibia historia yake.

Mjinga kabisa huyu jamaa, kiukweli hakupaswa kuishi hata huko jela anakokwenda kuwekwa kwa miaka 30.

Ova
alikuwa amekata tamaa ya maisha

Ukishakuwa na majukumu au malengo flani kwenye maisha,kuna baadhi vitu hauwezi hata kuvifikiria achalia mbali kuvitenda
 
Mahakama ya Mkoa wa Vuga, leo tarehe 31/10/2023 imemhukumu mshtakiwa MOH'D ALI HASSAN (35) Mkazi wa Jumbi Uwandani Unguja kutumikia kifungo cha miaka 30 Chuo cha Mafunzo (jela) kwa kosa la Kuingilia kinyume na maumbile.

Awali mshtakiwa huyo alimuingilia kinyume na maumbile mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 06 jambo ambalo ni kosa, kinyume na kifungu cha sheria 133 (a) cha sheria ya adhabu namba 6/2018 Sheria ya Zanzibar.

Akisoma maelezo ya hukumu hiyo, Hakimu wa mahakama hiyo Mhe. TAKI ABDALLAH amesema Mahakama imejiridhisha na ushahidi uliotolewa mbele ya mahakama ambao haukuwa na chembe ya shaka ambapo umemtia hatiani mtuhumiwa kwa makosa hayo.

Jumla ya mashahidi watano (05) walitoa ushahidi mahakamani hapo.

Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakamani tarehe 21/08/2023 ambapo ilipewa kesi namba 127/2023.
Kama ni hko hao jamaa kesi zao nyingi za kubambikiana nashangaa wanashinda msikitini 24/7 inasikitisha sana.
 
Back
Top Bottom