Leo nilikuwa nasikiliza redio asubui (nadhani BBC) wakawa wanaongelea sober houses Tanzania wanahoji walioanzisha hiyo makitu...
Nikafikiria sana nikaona hili tatizo la unga wangejaribu njia nyingine...
Maana wengi wa walioingia humo (kwenye unga) hawatoki...wataenda sober house baada ya miaka wanarudia kutumia...eti mmoja akasema tatizo mazingira...
mtu anaacha afu anarudi alikotoka na kukutana na mateja ni raisi kurudia...
Mi naona sio isuue pia..sasa mtu ataenda kusihi wapi? Ilala meteja wapo, posta wapo, mbagala wapo...
DAWA ni kuwakinga wale ambao hawajaanza...
Itolewe elimu endelevu mashuleni kuanzia shule za msingi kuhusu madhara ya haya madawa...ukiingia hakuna njia ya kutokea...ingekuwepo kina Whitney wasingekufa...Hizo NGOs zinge focus kwa vijana ambao bado hawajalambishwa hayo makitu...hao walokwisha lamba ni kupoteza ela tu (si kuwa siwahurumii...ila hiyo ndio fact)