Agizo: Wasafiri watakaoingia nchini watakaa karantini siku 14 kwa gharama zao

Agizo: Wasafiri watakaoingia nchini watakaa karantini siku 14 kwa gharama zao

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Serikali ya Tanzania hii leo imetoa mwongozo mpya kuhusu ugonjwa wa corona ambapo wasafiri watakaokuwa wanatoka katika nchi zenye maambukizo ya virusi vipya vya corona watatakiwa kukaa karantini kwa siku 14.

Mwongozo huo uliosainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ya nchi hiyo Profesa Abel Makubi utaanza kufanyiwa kazi rasmi kesho Mei 4 2021, unaeleza kuwa karantini hiyo itawahusu wasafiri ambao ni wakaazi na wageni.

Kabla ya kwenda karantini kwanza watafanyiwa vipimo vya lazima vya corona.

Kwa wageni watatakiwa kukaa karantini kwa gharama zao "watachagua eneo moja katika orodha itakayotolewa na serikali."

Wasafiri ambao ni wakaazi wa Tanzania wataruhiswa kujitenga kwa siku 14 katika nyumba zao wenyewe.

Hatua hizo zitawahusu pia wasafiri ambao safari zao zilipitia katika nchi hizo walau katika siku 14 zilizopita.

Mwezi mei mwaka jana Tanzania iliondoa karantini ya lazima kwa wasafiri kutaka nje ya nchi hiyo na badala yake wakatangaza kuwa kutafanyika vipimo vya ugonjwa huo.

Wizara ya Afya ya Tanzania imeeleza kuwa nchi hizo zenye virusi vipya vya corona zitatambuliwa kupitia taarifa zinazotolewa kila siku na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Kwa sasa virusi vipya vinavyogonga vichwa vya habari zaidi ni vya India na Brazili.

Nchini India hali ni mbaya zaidi ambapo zaidi ya watu 300,000 kila siku hukutwa na maambukizi ya corona.

Wataalamu wanatahadharisha kuwa idadi ya maambukizi inaweza ikawa kubwa zaidi ya hiyo.

1620059664445.png

1620059692791.png

1620059751830.png
 
Serikali ya Tanzania hii leo imetoa mwongozo mpya kuhusu ugonjwa wa corona ambapo wasafiri watakaokuwa wanatoka katika nchi zenye maambukizo ya virusi vipya vya corona watatakiwa kukaa karantini kwa siku 14.

Mwongozo huo uliosainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ya nchi hiyo Profesa Abel Makubi utaanza kufanyiwa kazi rasmi kesho Mei 4 2021, unaeleza kuwa karantini hiyo itawahusu wasafiri ambao ni wakaazi na wageni.
Kabla ya kwenda karantini kwanza watafanyiwa vipimo vya lazima vya corona.

Kwa wageni watatakiwa kukaa karantini kwa gharama zao "watachagua eneo moja katika orodha itakayotolewa na serikali.

Wasafiri ambao ni wakaazi wa Tanzania wataruhiswa kujitenga kwa siku 14 katika nyumba zao wenyewe.

Hatua hizo zitawahusu pia wasafiri ambao safari zao zilipitia katika nchi hizo walau katika siku 14 zilizopita.

Mwezi mei mwaka jana Tanzania iliondoa karantini ya lazima kwa wasafiri kutaka nje ya nchi hiyo na badala yake wakatangaza kuwa kutafanyika vipimo vya ugonjwa huo.

Wizara ya Afya ya Tanzania imeeleza kuwa nchi hizo zenye virusi vipya vya corona zitatambuliwa kupitia taarifa zinazotolewa kila siku na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Kwa sasa virusi vipya vinavyogonga vichwa vya habari zaidi ni vya India na Brazili.

Nchini India hali ni mbaya zaidi ambapo zaidi ya watu 300,000 kila siku hukutwa na maambukizi ya corona.

Wataalamu wanatahadharisha kuwa idadi ya maambukizi inaweza ikawa kubwa zaidi ya hiyo.
Source: BBC Swahili
 
Kuna kitu nyuma ya Pazia kimeanza kutokota

Ili kikiwaka vizuri waseme hatua zilichukuliwa

Lakini mambo bado hayajaharibika sana

Kwa jinsi India kilivyoumana na Hawa wenzetu lazima Itakuwa kuna ndugu zao huko wanasepa kuja Bongo kujificha

India wana hali tete sana sana

All in all, Sijajua kwanini hawa virusi wanawavamia sana ngozi nyeupe

Au wanakula sana Burger, Pizza na vile vitu laini laini kama biscuits na choklate
 
Serikali ya Tanzania hii leo imetoa mwongozo mpya kuhusu ugonjwa wa corona ambapo wasafiri watakaokuwa wanatoka katika nchi zenye maambukizo ya virusi vipya vya corona watatakiwa kukaa karantini kwa siku 14.
Mwongozo huo uliosainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ya nchi hiyo Profesa Abel Makubi utaanza kufanyiwa kazi rasmi kesho Mei 4 2021, unaeleza kuwa karantini hiyo itawahusu wasafiri ambao ni wakaazi na wageni.
Kabla ya kwenda karantini kwanza watafanyiwa vipimo vya lazima vya corona.
Kwa wageni watatakiwa kukaa karantini kwa gharama zao "watachagua eneo moja katika orodha itakayotolewa na serikali.

Wasafiri ambao ni wakaazi wa Tanzania wataruhiswa kujitenga kwa siku 14 katika nyumba zao wenyewe.
Hatua hizo zitawahusu pia wasafiri ambao safari zao zilipitia katika nchi hizo walau katika siku 14 zilizopita.

Mwezi mei mwaka jana Tanzania iliondoa karantini ya lazima kwa wasafiri kutaka nje ya nchi hiyo na badala yake wakatangaza kuwa kutafanyika vipimo vya ugonjwa huo.
Wizara ya Afya ya Tanzania imeeleza kuwa nchi hizo zenye virusi vipya vya corona zitatambuliwa kupitia taarifa zinazotolewa kila siku na Shirika la Afya Duniani (WHO).
Kwa sasa virusi vipya vinavyogonga vichwa vya habari zaidi ni vya India na Brazili.
Nchini India hali ni mbaya zaidi ambapo zaidi ya watu 300,000 kila siku hukutwa na maambukizi ya corona.
Wataalamu wanatahadharisha kuwa idadi ya maambukizi inaweza ikawa kubwa zaidi ya hiyo.
Source: BBC Swahili

Kwamba wanajitenga wenyewe makwao kwa ridhaa zao tu.

Hivi wale waliokuwa wizara ya afya awamu ile bado wako ofisini?
 
Niliwahi kutoa uzi hapo awali kuhusu wave MPYA ya corona kali toka India ambako kuna taarifa kundi la wahindi waliokuepo India linarudi Tanzania kukimbia janga jipya la corona cha ajabu serikali yetu ipo kimya bado tumetia pamba masikioni, usafiri na India Uko pale pale huku nchi nyingi zikifuta Safari za kwenda na kutoka India.
 
Niliwahi kutoa uzi hapo awali kuhusu wave MPYA ya corona kali toka India ambako kuna taarifa kundi la wahindi waliokuepo india linarudi tanzania kukimbia janga jipya la corona cha ajabu serikali yetu ipo kimya bado tumetia pamba masikioni, usafiri na India Uko pale pale huku nchi nyingi zikifuta Safari za kwenda na kutoka India.
Leo wamekurupuka na kusema watu wanaotoka nchi zenye virus wakali wakae karantiini siku 14. Hili sidhani kama linatosha kwa wasafiri kutoka India. Wangesitisha safari kwanza. Virus wakienea Tanzania inaweza kuleta maafa.
 
Huu ni mtazamo wa kiuchumi kuliko kiafya.
Kwahiyo wageni ndio wana possibilty kubwa ya kuambukiza corona kuliko wenyeji?Kwanini wwnyeji wanaruhusiwa kujitenga nyumbani?

Hivi serikali mnachotafuta kwenye hii janga ni nini,kwanini hamko makini?

Mwaka jana tuliwaambia hamkusikia.
Mwaka huu tunawaambia tena,chukueni hatua za kudhibiti mwingiliano na mataifa yaliyoathirika kama India mapema.

Mnabeba dhamana ya afya zetu sote,nchi si yenu peke yenu,BE STRICT on this issue kwa ajili yetu watu milioni 60!

ACHENI KUJIVUTAVUTA!BE STRICT!😡
 
Wizara ya afya Tanzania imesema kuanzia kesho wasafiri wote kutoka nchi zenye maambukizi ya Corona watakaa karantini ya siku14.

Watanzania wanaorudi nyumbani watakaa karantini majumbani mwao.

Source BBC Dira ya Dunia
 
Kuna mtanzania amefariki juzi, leo hii kuna taarifa za muambata kufariki. Hawa wawili labda na wengi wengineo watahudumiwa kuja kuhifadhiwa na ATCL ambayo muda huu niandikapo iko hewani inaelekea Mumbai.

Kenya kuna sauti zinazopinga ndege iliyobeba abiria kutoka India isitue JKIA. Kuzuia ndege za Tanzania zisifanye kazi iliyokusudiwa kwa ajili ya woga wa COVID19 si busara hasa ukizingatia kuwa kifo ni kitu cha uhakika kwa asilimia mia.

Tuchukue tahadhari zote kujikinga na maradhi yote yanayosambaa kwa njia ya hewa... Vinginevyo kazi iendelee.
 
Tanzania kwa wananchi waliopo ndani watangazieni watumie barakoa hali sio shwari na iwe lazima hiyo rapid test kazungura iliwachanganya mtu huyo huyo mmoja asubuhi akipima ana corona jioni hana tena ile wave two wakati imekomaa wakaacha kupima wakawa wanabaki kusoma majibu ya kipimo cha UTH Lusaka..inatakiwa kusitisha safari za ndege kutoka na kuingia India au Brazil kama zipo...
Matumizi ya sanitizer au kunawa na kupunguza misongamano isiyo ya lazima..
Kila ofisi au duka iwekwe sanitizer au maji ya kunawa na sabuni..
Kupunguza misongamano kwenye vyombo vya usafiri wa ndani..
Kupunguza misongamano huko polisi..
Watu waache kusalimiana kwa kushikana mikono...
Mechi ya Simba vs Yanga washabiki waruhusiwe wachache tuu..
Kuhamasisha matumizi ya barakoa kuwa ya lazima..
 
Back
Top Bottom