TANZIA Agnes Gerald ‘Masogange’ afariki dunia Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge, Dar

TANZIA Agnes Gerald ‘Masogange’ afariki dunia Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge, Dar

Naomba nielimishwe kidogo maana sijaelewa. Huyo Masogange sijawahi muona hata movie moja au kuhudhuria vikao vya bongo movie ilaa kwanini kina Steve Nyerere wameuchukua msiba wake na kuuweka upande wao?

anataka kupiga rambi rambi huyo
 
siku zote ukifa na ilhali maarufu ambae umaarufu wako ulitokana na jambo ambalo wengi walikuwa wanalifanya kama wewe basi tambua huna safari ya utajo wa milele au wa muda mrefu.

Kanumba kafa mda sana lakini kile ambacho alikuwa anakifanya kuna ambae alifikia ubora wake?

lakini ni mtu anatajwa mpaka leo na kazi zake zinafahamika.

Lakini tukija kwako wewe ambae umekufa na ilhali ulikuwa na skendo chafu ambazo zimethibitika ni kweli mpaka ikafika hatua kushtakiwa na kulipa dhamana kwa kosa ambalo wengi katika watu wanaumia na kuteseka watoto wao basi jua huna utajo mwema wa muda mrefu.

hakuna kitu kibaya kama madawa ya kulevya ambayo tunapoteza watu na vijana kwa sababu hii moja wapo na tanzania tumeona madhara yake japo yana pesa.

neno langu ni kwamba wauza unga wote mfano wa dada masogange vifo vyao haitakuja kudumu kabisa na watasahaulika kama kuna watu walikuwa wao kutokana na kufa katika umaarufu ambao wakati hajafa wwngi walikuwa wanaufanya..

sina bifu na mtu lakini tambueni tu muuza unga yeyote atakufa kifo cha kufedhehesha na kusahaulika mara moja kutokana na kufanya ufisadi wake wa unga na kuharibu jamii ya watu wengi.

povu ruksa
 
Tabia mbaya kumsema marehemu
wewe ndo mwenye tabia mbaya mkuu.

utamteteaje muuza unga ambae kaharibu watoto wa watu na nguvu kazi ya taifa eti kwa kuwa tu atoboe kimaisha huku anadhuru wengine?

au unadhani wanatoa unga tz wanapeleka nje?

ule unga unatoka nje unaletwa tz ili mtoto wako na wangu watumie waathirike huku wao wanapiga pesa.

.lakini note kwamba vifo vya wauza unga ni vya kidhalili
 
Kafa na umbo lake kweli maisha mafupi

Apumzike kwa amani
After this life ni vile ulivyoyaandaa! RIP prayers zingekuwa ni kweli, zingewapeleka wengi kwenye hiyo peace maana mnajitahidi sana kuwaombea!
Mungu hadhihakiwi, unachopanda ndicho utakachovuna (Wagalatia 6:7~8). Haitatokea kamwe (irrespective your prayers~sijui RIP), uishi duniani maisha yasiyompendeza Mungu halafu baada ya kufa ukarithi eternal peace kwa maombi ya RIP!
 
siku zote ukifa na ilhali maarufu ambae umaarufu wako ulitokana na jambo ambalo wengi walikuwa wanalifanya kama wewe basi tambua huna safari ya utajo wa milele au wa muda mrefu.

Kanumba kafa mda sana lakini kile ambacho alikuwa anakifanya kuna ambae alifikia ubora wake?

lakini ni mtu anatajwa mpaka leo na kazi zake zinafahamika.

Lakini tukija kwako wewe ambae umekufa na ilhali ulikuwa na skendo chafu ambazo zimethibitika ni kweli mpaka ikafika hatua kushtakiwa na kulipa dhamana kwa kosa ambalo wengi katika watu wanaumia na kuteseka watoto wao basi jua huna utajo mwema wa muda mrefu.

hakuna kitu kibaya kama madawa ya kulevya ambayo tunapoteza watu na vijana kwa sababu hii moja wapo na tanzania tumeona madhara yake japo yana pesa.

neno langu ni kwamba wauza unga wote mfano wa dada masogange vifo vyao haitakuja kudumu kabisa na watasahaulika kama kuna watu walikuwa wao kutokana na kufa katika umaarufu ambao wakati hajafa wwngi walikuwa wanaufanya..

sina bifu na mtu lakini tambueni tu muuza unga yeyote atakufa kifo cha kufedhehesha na kusahaulika mara moja kutokana na kufanya ufisadi wake wa unga na kuharibu jamii ya watu wengi.

povu ruksa
Naona unajishuku mwenyewe bila kuambiwa
 
Una uhakika amekufa kwa ukimwi.
Maana yangu tusipende kujaji vifo vya watu na magonjwa yao.
NANI MZIMA?
Mi uhakika nautoa wapi, wakati wewe ndio umeongea habari za ukimwi! Kwani mpaka leo kifo cha ukimwi kinakutatiza?
 
ushaambiwa alikuwa anaumwa sasa unatka chanzo gani tena wakati taarifa tayari
Hakuna taarifa sahihi,kila mtu anasema lake.
1.Homa ya Matumbo(Typhoid)
2.Pumu.
3.Upungufu wa damu.
4.Pneomonia(homa ya mapafu)
5."KIFUA"
?????? Which is which???
 
  • Thanks
Reactions: ABJ
Back
Top Bottom