Ahadi za uongo za marafiki

Ahadi za uongo za marafiki

Mkuu pole nakushauri usitegemee watu sana kwenye shida watakuvunja moyo,
PIli hamna mtu yoyote mwenye wajibu kukusaidia isipokuwa wewe na huwezi jua labda alishasaidia ila msaada wake ukageuka mwiba kwake.
Tatu ni nzuri hajakusaidia inauma lakini na wewe ingekubidi ulipe fadhila.
Na mwisho Mungu analeta watu wa namna hiyo ili ufumbue macho ujue ni watu wa namna gani.
Nashukuru sana,ila bado tunaishi ngoja tuone mbele,kukwama kupo tu,kuna mahesabu nilikosea ndio nikaingia uhitaji,sasa jamaa nimezoea hata yeye aliwahi kupata shida na nilimpa kiasi kikamuinua,kwangu yamenipata amepiga tukio,lakini najua atakuja kwa shida.
 
Tangu nazaliwa mpaka namaliza chuo yaani mpaka leo sijawai kuomba msaada wa fedha kwa rafiki wala kumkopa,Nina marafiki wengi ila naona ni watu ninao fahamiana nao sio kama unavyochulia ...

Mi nimejitegenezea formular nikikosa basi mmekula kwangu basi hustling zangu sio za kitoto ...kwa imani yangu kuomba omba ni laana na sio vizuri ni aibu kabisa ... kuhusu kulala njaa nishalala sana kwangu sio kesi haswa kipind nipo advance nategemea wazazi wakikosa ndo basi ila sijui niombe mshkaji, dada, kaka, shangazi,mjomba ,ba mkubwa au mdogo siwezi kabisa .
Asante mkuu,umeongea mema Sana🙏
 
Tangu nazaliwa mpaka namaliza chuo yaani mpaka leo sijawai kuomba msaada wa fedha kwa rafiki wala kumkopa,Nina marafiki wengi ila naona ni watu ninao fahamiana nao sio kama unavyochulia ...

Mi nimejitegenezea formular nikikosa basi mmekula kwangu basi hustling zangu sio za kitoto ...kwa imani yangu kuomba omba ni laana na sio vizuri ni aibu kabisa ... kuhusu kulala njaa nishalala sana kwangu sio kesi haswa kipind nipo advance nategemea wazazi wakikosa ndo basi ila sijui niombe mshkaji, dada, kaka, shangazi,mjomba ,ba mkubwa au mdogo siwezi kabisa .
siku ukipitia hali niliyopitia,haya uliyoandika hapa utarudi kusema yabatilishwe.

nashukuru kwa mchango wako,ila kukopa si laana,kumbuka sijaomba hivyo nitarudisha.
 
Binaadamu wengi Huwa wanadhani Wana marafiki wa karibu na ndugu wanaowapenda sana lakini Hilo hubainika kuwa wadhaniavyo ndivyo sivyo mpaka pale siku Moja watakapo fikwa na shida/matatizo
 
Kila mtu na maswaibu yake mwamba kuna wengine hawajui kukataa .Mi kuna Uncle wangu ukimwambie niazime elf 20 utasikia sawa badae kidogo uncle ,milioni 5 nayo ni hivyo hivyo utasikia nipe muda hii niweke kwenye account yako au.Lakini hatumi hata 100.
Nina hili tatizo [emoji848]
 
Na wewe mpotezee unafikiria kuendelea kumtafuta wa Nini kwani mzazi wako huyo?
Hebu endelea kutafuta Hela achana na hiyo mbuzi kwanza anakudharau anajua haumwongezei chochote hata akikupoteza.
 
Kujitegemea kunaleta heshima sana,sema TU bas Kuna muda mambo yanakaba[emoji26]

Huenda hajapata mkuu,sema inatakiwa akujulishe Ili uangalie njia nyingine
Umenikumbusha mbali Sana!!
 
Una macho lakin huoni ,ifike hatua muwe na akili basi ,ukiona hivo jiongeze maana yake kakwama hawezi kukusaidia ,na sio wote wenye uwezo wa kuja kukuambia kuwa kakwama hawezi kukusaidia ......

Huko shuleni mlienda kusomea ujinga ,vitu vingine vinaonekana ila unakuta mtu kakaza fuvu ,et mpaka aambiwe ....acha kulalama tafuta Hela ...
 
toka lini rafiki akawa msaada wako?
marafiki ni watu Wa kubadili stori na kuishi nao kuwepo kwa wakati wa raha zako
usitegemee rafiki sio business partner huyo wengine hawawez kusema siwez saidia ila matendo yataonyesha kuwa hawez kukusaidia
 
yaani mkuu alikuwa hadi ameniambia muda wa kutuma na nimpe account number,basi baada ya hapo akaacha kupokea simu,ila status zake yuko sherehe tu anaweka,na hata hilo tatizo nilimuambia,sasa kama ameona amebadili mawazo si angesema hanipi tu nikawa na amani.

nakumbuka niliwahi kumsaidia kiasi aanzishe biashara yake,na hakinilipa chote,ila nilichukulia kama rafiki na ndio kwanza alikuwa ameoa.
relax mkuu
mi kuna jamaa ni rafiki kichizi,nimemshika mkono sanaa

siku nikawa na shida ya laki moja nikamwomba msaada majibu yake ni nakutumia (najua ana fedha maana kuna mishe tunafanya na yake iliwahi kutiki kabla yangu) nikamwibukia kwake nakuta anakarabati nyumba akanihaidi atanipa siku iyo ila wapiii

baada ya wiki 2 inshu yangu ikatiki pia akaniomba laki 3 hahahaha akipiga simu huwa napokea kwa kiitikio cha `wewe wa kuninyima laki" alafu nauchuna

huyu bwana nimemuweka kwenye orodha ya jamaa zangu watakao kumbana na vikwazo vya kiuchumi miaka yote. pia nimemwondoa kwenye orodha ya watakao fahamu kipato changu
 
Kila mtu na maswaibu yake mwamba kuna wengine hawajui kukataa .Mi kuna Uncle wangu ukimwambie niazime elf 20 utasikia sawa badae kidogo uncle ,milioni 5 nayo ni hivyo hivyo utasikia nipe muda hii niweke kwenye account yako au.Lakini hatumi hata 100.
[emoji1787][emoji1787]Nina kaka angu nayeye hajui kukataa ila hutapata hata 100..Kuna siku nlimuuliza sababu akadai hapendi kumkatisha mtu tamaa!
 
relax mkuu
mi kuna jamaa ni rafiki kichizi,nimemshika mkono sanaa

siku nikawa na shida ya laki moja nikamwomba msaada majibu yake ni nakutumia (najua ana fedha maana kuna mishe tunafanya na yake iliwahi kutiki kabla yangu) nikamwibukia kwake nakuta anakarabati nyumba akanihaidi atanipa siku iyo ila wapiii

baada ya wiki 2 inshu yangu ikatiki pia akaniomba laki 3 hahahaha akipiga simu huwa napokea kwa kiitikio cha `wewe wa kuninyima laki" alafu nauchuna

huyu bwana nimemuweka kwenye orodha ya jamaa zangu watakao kumbana na vikwazo vya kiuchumi miaka yote. pia nimemwondoa kwenye orodha ya watakao fahamu kipato changu
Na hiyo ndio dawa ya rafiki mnafiki. Siku yakimkuta na ww unamkanyagia tu.
 
yaani mkuu alikuwa hadi ameniambia muda wa kutuma na nimpe account number,basi baada ya hapo akaacha kupokea simu,ila status zake yuko sherehe tu anaweka,na hata hilo tatizo nilimuambia,sasa kama ameona amebadili mawazo si angesema hanipi tu nikawa na amani.

nakumbuka niliwahi kumsaidia kiasi aanzishe biashara yake,na hakinilipa chote,ila nilichukulia kama rafiki na ndio kwanza alikuwa ameoa.
Meet nae face to face
 
siku ukipitia hali niliyopitia,haya uliyoandika hapa utarudi kusema yabatilishwe.

nashukuru kwa mchango wako,ila kukopa si laana,kumbuka sijaomba hivyo nitarudisha.
Hapana nimepitia mengi tu siwezi kukuambia hapa..Ninachotaka kukuambia kwamba usilaumu ndo washaamua hao marafiki
 
Nashukuru sana,ila bado tunaishi ngoja tuone mbele,kukwama kupo tu,kuna mahesabu nilikosea ndio nikaingia uhitaji,sasa jamaa nimezoea hata yeye aliwahi kupata shida na nilimpa kiasi kikamuinua,kwangu yamenipata amepiga tukio,lakini najua atakuja kwa shida.
Akija msaidie itamuuma zaidi kuliko ukilipa kisasi cha kutokumsaidia.
 
Back
Top Bottom