Ahmed Ali bado sana kumfikia Haji Manara ingawa Haji kashaanza ingiwa na hofu

Ahmed Ali bado sana kumfikia Haji Manara ingawa Haji kashaanza ingiwa na hofu

Cvez

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2018
Posts
4,405
Reaction score
13,411
Katika moja ya Interview ya Haji Manara wakati akiwa ni msemaji wa Simba, alishawahi kusema "Mimi sitadumu Simba milele ipo siku nitaondoka na atakuja mtu mwingine. Haji amefanya mengi sana na sidhani kama itakua fair kumjudge msemaji ajae kwa kumfananisha na Haji viatu vyangu ni vikubwa ila tukimpa support atafanya atakapo weza". Kipindi hicho Haji alikua kipenzi cha Wanasimba na alikua na confidence ya kutosha sana. Katu hakua na shaka na ukubwa wake.

"Mimi hapa mmoja ni sawa na wale wote kule Utopolo (Bumbuli na Nugaz), Haji mtu mkubwa bwana" Hayo yalikua maneno ya Haji kudhihirisha ukubwa wake. Siku zikapita Haji akang'atuka Simba kwa style iliyofanya kila Mwanasimba kusahau yote aliyoyatenda, mwamba akawa mkosoaji mkuu wa Simba.

Baadae Simba wakamtambulisha Ahmed Ally kama Manager wa mawasiliano na habari. Katika Interview akiwa Clouds Fm aliulizwa unahizi unaweza kuvaa viatu vya mtangulizi wako ambae alifanya makubwa sana ndani ya Simba na alikua kipenzi cha mashabiki. "Kuhusu mtangulizi alifanya makubwa sana ndani ya Simba ingawa kwa namna alivyoondoka ameifanya kazi yangu iwe nyepesi zaidi. Wanasimba walikua wanahitaji mtu wa kuwasemea baada ya kuachwa na mtangulizi wangu, hivyo hakuna uzito wowote".

Kitu alichotegemea Haji kingekua mlima kwa mrithi wake imekuja kua tambalale sababu ya namna alivyoondoka. Na uzuri ni kua mtu aliyekuja ameingia na kuanza kufanya kazi yake na ikaonekana kwa namna tofauti na ile ya mtangulizi wake. Ingawa ni ukweli usiopingika Ahmed bado sana kumfikia HAJI ila jamaa kashaingiwa na wasiwasi kuona ile legacy aliyodhani itakua mlima ishaanza kufutika ndani ya miezi mitatu. Hata zile kauli zake za kusema yeye ni mkubwa huliko wote sasa hivi ameacha na ameanza kuona mbali ya makubwa mtu anayoweza kufanya, ukishawapatia watu sababu ya kukusahau wanafanya hivyo.​
 
Haji ndio nani ,picha kidogo mkuu
Huyu hapa

FB_IMG_1650454933885.jpg
 
unamfananisha Ally msemaji mwenye weledi msomi na huyo manara mzee wa midundiko, ambaye anaongea bila weledi, huyo (hajui kama hajui) anachokiongelea vibaya leo kesho anaenda kukifanya mwenyewe na anakisifia: huyo ni kama myama nguruwe hajui anye wapi ili abakize sehemu salama ya kulala, mwenyewe anachafua kote tu! anajali kuvimbisha tumbo kwa leo hajui kesho inakuwaje, hana future, rubbish......
 
unamfananisha Ally msemaji mwenye weledi msomi na huyo manara mzee wa midundiko, ambaye anaongea bila weledi, huyo (hajui kama hajui) anachokiongelea vibaya leo kesho anaenda kukifanya mwenyewe na anakisifia: huyo ni kama myama nguruwe hajui anye wapi ili abakize sehemu salama ya kulala, mwenyewe anachafua kote tu! anajali kuvimbisha tumbo kwa leo hajui kesho inakuwaje, hana future, rubbish......
Hivi msomi ni mtu mwenye elimu ya kiwango gani?
 
Kumfikia kivipi. Siku hizi kuna kujivunia kumfikia mtu kwa upunguani,uzuzu,uropokaji,majivuni?!

Ungeniambia Ahmed amfikie Masao Bwire au Thobias Kifaru Lugalambwike ningekuelewa kwa sababu wale ni watu timamu. Kumfikia Manara ni kuufikia upunguani,kudhalilisha na kukashfu wengine.

Ahmed usimfikie Manara, huna kitu cha kujifunza kwa Manara,nenda kachote madini kwa Masao Bwire na Kifaru.
 
Ahmedy ni mtu Smart, mtazame hata anapoongea.

ukitaka kujua huyo mzungu pori ana shida huwa hakawii kupopoana na waandishi. Busara kwake ni ndogo sana.
 
unamfananisha Ally msemaji mwenye weledi msomi na huyo manara mzee wa midundiko, ambaye anaongea bila weledi, huyo (hajui kama hajui) anachokiongelea vibaya leo kesho anaenda kukifanya mwenyewe na anakisifia: huyo ni kama myama nguruwe hajui anye wapi ili abakize sehemu salama ya kulala, mwenyewe anachafua kote tu! anajali kuvimbisha tumbo kwa leo hajui kesho inakuwaje, hana future, rubbish......
Kwa taarifa yako msomi hawwzi kuleta hamasa na msisimko kwa mashabiki kama anavyoweza kufanya kayumba flani.
Kazi ya usemaji inahitaji kujitoa ufahamu kama afanyavyo Manara.
Nachelea kusema unanwona Haji hafai sasa baada ya kujiondoa timu yako.
 
Kwa taarifa yako msomi hawwzi kuleta hamasa na msisimko kwa mashabiki kama anavyoweza kufanya kayumba flani.
Kazi ya usemaji inahitaji kujitoa ufahamu kama afanyavyo Manara.
Nachelea kusema unanwona Haji hafai sasa baada ya kujiondoa timu yako.
Kwanza nna wasiwasi hata na wanaomtetea huyu mzungu wa bigwa naona kama na wao ni mazwazwa,
Mzungu pori hana alijualo,hajui inachokisemea na impact yake,
Kwa domo lake alisema kule yanga wenye akili ni wawili tu, yaani KIKWETE na BABA YAKE,alafu leo na yeye anaenda hukohuko[emoji86] kwanza hana TIN NUMBER.


AHMED ALLY ni msemaji mwenye weredi wa kujua kile anachokisemea kwa kuangalia mbele zaidi,
Na anayo TIN NUMBER

Sent from my PBBM00 using JamiiForums mobile app
 
Kumfikia kivipi. Siku hizi kuna kujivunia kumfikia mtu kwa upunguani,uzuzu,uropokaji,majivuni?!

Ungeniambia Ahmed amfikie Masao Bwire au Thobias Kifaru Lugalambwike ningekuelewa kwa sababu wale ni watu timamu. Kumfikia Manara ni kuufikia upunguani,kudhalilisha na kukashfu wengine.

Ahmed usimfikie Manara, huna kitu cha kujifunza kwa Manara,nenda kachote madini kwa Masao Bwire na Kifaru.
Wengi hawajui Manara, na wengi wamemjuwa akiwa Simba, ila wangepata nafasi ya kumjuwa akiwa ccm msingesumbuka akili.

Hata hapo Yanga ni GSM ndio wamemchukuwa, na hizi timu huwezi kushindana na mwenye pesa ndio maana kuna watu wa Yanga wanajilazimisha kumpenda, lakini binafsi sijawahi kumkubali Haji akiwa ccm kwa matusi yake mazito yasiyokuwa na staha kwa wakubwa hasa Maalim Seif, sijawahi kumkubali akiwa Simba na wala sasa kuletwa kwake Yanga ni kitu binafsi sikubaliani nacho lakini Yanga ya sasa ni GSM hakuna kuleta fyoko.
 
Kwanza nna wasiwasi hata na wanaomtetea huyu mzungu wa bigwa naona kama na wao ni mazwazwa,
Mzungu pori hana alijualo,hajui inachokisemea na impact yake,
Kwa domo lake alisema kule yanga wenye akili ni wawili tu, yaani KIKWETE na BABA YAKE,alafu leo na yeye anaenda hukohuko[emoji86] kwanza hana TIN NUMBER.


AHMED ALLY ni msemaji mwenye weredi wa kujua kile anachokisemea kwa kuangalia mbele zaidi,
Na anayo TIN NUMBER

Sent from my PBBM00 using JamiiForums mobile app
TIN NUMBER si kila mwenye driving license anayo? au wewe kwako kuna maajabu gani kwenye tin number?
 
Back
Top Bottom