Ahsante kufuatilia Bajeti ya Wizara ya Jamii 2024/24

Ahsante kufuatilia Bajeti ya Wizara ya Jamii 2024/24

Mambo ni mengi sana naona kuna vitu umefumbia macho kukemea mnaufyata kwa wafadhili, maisha ni kimya kimya tusubiri kizazi cha mashangazi siku za usoni
 
wanaona kama vile wao siyo watu wa kukutwa na msongo wa mawazo kwa kuwa hiyo ni dalili ya udhaifu na udhaifu ni ishara ya wanawake. SAIKOLOJIA. Hii ndiyo shida.....
Wanaume wabishi wameongezeka sana, wanapigwa vitasa na wake zao Ila hawatafuti msaada kwa sababu ni wabishi.

Fanya maarifa hao wanaume wasaidiwe
 
Hongera sana Dr Gwajima, watoto wa kiume nao ni muhimu sana kuwaweka katika mipango ya serikali, Kwa maana tunaona mmeegemea sana Kwa mtoto wa kike pekee.
 
Mambo ni mengi sana naona kuna vitu umefumbia macho kukemea mnaufyata kwa wafadhili, maisha ni kimya kimya tusubiri kizazi cha mashangazi siku za usoni
Naweza kusema tu kuwa, ufuatiliaji wako kuhusu kazi nafanya nadhani siyo wa Kila siku kwa Kila content. Ndiyo maana kuna kazi zangu zingine hukuzipata. Ingia google andika Dorothy Gwajima Shinyanga, kisha chagua video halafu tafuta video moja ina dakika 3.19 ya tarehe 5 Disemba 2022 kisha uje utoe maoni tafadhali. Shukrani kwa muda wako. Ukiona tatizo kinyume na sheria ukawa huna msaada nitumie sms tuunganishe nguvu kwenye 0765345777 nakala 0734124191, mpe na mwingine, kazi iendelee
 
Hongera sana Dr Gwajima, watoto wa kiume nao ni muhimu sana kuwaweka katika mipango ya serikali, Kwa maana tunaona mmeegemea sana Kwa mtoto wa kike pekee.
Ahsante Sana kwa maoni. Nami niruhusu nielimishe kwamba; ni uelewa tu, kwa kuwa, idara ya watoto inashughulika na watoto wote wa kike na kiume kupitia program ya malezi na makuzi, lakini madawati ya ulinzi wa watoto shule za msingi na Sekondari ni wote, kwenye madawati ya Jinsia na watoto Polisi ni wote, kwenye mabaraza ya watoto ni wote, mabaraza ya Wazee ni jinsia zote, kwenye program ya vijana balehe ni wote. Changamoto Iko kwa watu wazima wanaume ambao wakiwa kwenye migogoro ya mahusiano hawaji kwa aibu zao tu na siyo kwamba hawapokelewi. Mbona mimi nawapokea na nawaunganisha na mifumo? Na wanapata huduma?
 
Hivi kuna bunge linaendelea hapa dodoma? Npo hapahapa dodoma na sjui kama kuna mjadala wa bunge la budget....maana humo kila ktu tunamshukuru rais as if mpo mle kwa lengo kuwa wasemaji wa rais na kutetea ccm ndo maana watz weng hatuna muda wa kupoteza kuwaskiliza.
 
Wasaalam.

Nawashukuru watanzania wote kwa ufuatiliaji wa wasilisho la bajeti ya wizara ya jamii 2024/25.

Namshukuru Mungu kwamba, mjadala mkubwa wakati wa uwasilishaji, ni ishara ya elimu kuifikia jamii kwa kina kuhusu kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kudhibiti mmomonyoko wa maadili unaosababisha vitendo mbalimbali viovu.

Kuzinduliwa kwa mpango wa pili wa kutokomeza ukatili huu na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla, utaipeleka ajenda hii hadi ngazi ya mtaa, kijiji, kata, halmashauri, vikao vya mabaraza ya madiwani, baraza la madiwani, baraza la maendeleo la wilaya na mkoa kwa kina zaidi. Na hapo ndiyo tutakuwa tumeungana wote kama taifa kwenye vita hivi kupitia ugatuaji madaraka na kuyasogeza karibu na jamii (DxD).

Tuendelee kushirikiana kwa upya kabisa, inawezekana kutunza maadili.

Elimu zaidi kuhusu bajeti yetu, Sera mpya ya jinsia na maendeleo ya wanawake na mpango mkakati wa pili wa MTAKUWWA tuliozindua 15 Mei, 2024: tukutane wiki ijayo Jamii Forums online na Twitter space pia na space zingine. Ratiba inakuja. Kisha kutoka online kwenda halmashauri kwa halmashauri.

Asubuhi njema🙏🏽

View attachment 2992948

Unaweza kuisoma yote hapa: Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka 2024/25
Hongera
 
Wasaalam.

Nawashukuru watanzania wote kwa ufuatiliaji wa wasilisho la bajeti ya wizara ya jamii 2024/25.

Namshukuru Mungu kwamba, mjadala mkubwa wakati wa uwasilishaji, ni ishara ya elimu kuifikia jamii kwa kina kuhusu kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kudhibiti mmomonyoko wa maadili unaosababisha vitendo mbalimbali viovu.

Kuzinduliwa kwa mpango wa pili wa kutokomeza ukatili huu na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla, utaipeleka ajenda hii hadi ngazi ya mtaa, kijiji, kata, halmashauri, vikao vya mabaraza ya madiwani, baraza la madiwani, baraza la maendeleo la wilaya na mkoa kwa kina zaidi. Na hapo ndiyo tutakuwa tumeungana wote kama taifa kwenye vita hivi kupitia ugatuaji madaraka na kuyasogeza karibu na jamii (DxD).

Tuendelee kushirikiana kwa upya kabisa, inawezekana kutunza maadili.

Elimu zaidi kuhusu bajeti yetu, Sera mpya ya jinsia na maendeleo ya wanawake na mpango mkakati wa pili wa MTAKUWWA tuliozindua 15 Mei, 2024: tukutane wiki ijayo Jamii Forums online na Twitter space pia na space zingine. Ratiba inakuja. Kisha kutoka online kwenda halmashauri kwa halmashauri.

Asubuhi njema🙏🏽

View attachment 2992948

Unaweza kuisoma yote hapa: Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka 2024/25
Hongera Mhe. Gwajima.

Ila mbunge wa Iringa mjini Msambatavangu ana hoja ya msingi, asikilizwe..


View: https://youtu.be/AyJYIuH8O9Q?si=hfjntscyOLeFAW_O
 
Hongera Dkt. Gwajima D , sikujua kama wewe ni mdau hapa, nimefurahi kuona uzi wako hapa.

Kuna wimbi kubwa sana la watoto kulawitiana wenyewe kwa wenyewe na wengine na ndugu wa familia kwenye shule za msingi serekali, naomba iundwe tume ya kupita kwenye shule zote utashangaa.

Natolea mfano shule za Bagamoyo, kwa uchunguzi wangu mwaka huu pekee kumekuwa na visa zaidi ya vitano kwa shule tatu tofauti za hapa mjini.

Mbaya zaidi mambo haya yamekuwa yalimalizwa juu kwa juu lakini bado watoto wanabaki na adhari za kisaikolojia.
 
Hongera sana mama kwa uchapaji wako kazi mimi ni moja kati ya mashabiki wako wakubwa sana na ninakukubali sana mama kwa utendaji wako uliotukuka.kazi iendelee

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kwanza nikupongeze mama kwa kazi nzuri unayoifanya kwenye hii wizara. Kiukweli hii wizara ina mtu.

Kuna huu mpango wa marekebisho ya tabia kwa watoto waliokinzana na sheria. Ni moja ya mipango mizuri sana inayosimamiwa na ofisi za ustawi wa jamii. Nikuombe mama ukae na wataalamu wako uone ni namna gani ya kuendeleza mpango huu uendelee kuwa na ufanisi kama ilivyokuwa huko nyuma. Mpango umewasaidia sana watoto ambao wanajihusisha na vitendo vya uhalifu, ni matumaini yangu ukiboreshwa, utaendelea kuwasaidia sasa wahalifu watoto ili wasiendelee na vitendo vya uhalifu.
 
Wasaalam.

Nawashukuru watanzania wote kwa ufuatiliaji wa wasilisho la bajeti ya wizara ya jamii 2024/25.

Namshukuru Mungu kwamba, mjadala mkubwa wakati wa uwasilishaji, ni ishara ya elimu kuifikia jamii kwa kina kuhusu kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kudhibiti mmomonyoko wa maadili unaosababisha vitendo mbalimbali viovu.

Kuzinduliwa kwa mpango wa pili wa kutokomeza ukatili huu na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla, utaipeleka ajenda hii hadi ngazi ya mtaa, kijiji, kata, halmashauri, vikao vya mabaraza ya madiwani, baraza la madiwani, baraza la maendeleo la wilaya na mkoa kwa kina zaidi. Na hapo ndiyo tutakuwa tumeungana wote kama taifa kwenye vita hivi kupitia ugatuaji madaraka na kuyasogeza karibu na jamii (DxD).

Tuendelee kushirikiana kwa upya kabisa, inawezekana kutunza maadili.

Elimu zaidi kuhusu bajeti yetu, Sera mpya ya jinsia na maendeleo ya wanawake na mpango mkakati wa pili wa MTAKUWWA tuliozindua 15 Mei, 2024: tukutane wiki ijayo Jamii Forums online na Twitter space pia na space zingine. Ratiba inakuja. Kisha kutoka online kwenda halmashauri kwa halmashauri.

Asubuhi njema🙏🏽

View attachment 2992948

Unaweza kuisoma yote hapa: Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka 2024/25
You are the best da Dr Dorice
 
Ahsante Sana kwa maoni. Wanaume wengi hawajakubali kuwa, binadamu wote Wana udhaifu wakati fulani fulani na udhaifu siyo ulemavu bali inaweza kuwa ni kiwango cha hekima fulani katika kuepusha madhara. Sasa tuna mikakati ya kuelimisha jamii ya wanaume tangu wadogo, vijana na hata watu wazima. Tunashirikiana na vyama vya wanaume pia. Mwaka huu wengi wataijua zaidi hii wizara na tutaenda pamoja.

Hata hivyo, mimi binafsi nimepokea na kuwaunganisha na mifumo ya Dawati la jinsia wanaume wengi tu. Nimeshauri Hadi kuundwa kwa vyama vya wanaume, na Sasa tunavyo. Tunaelekea sasa kwenye Kampeni kubwa ya "male champion, he for she".

Mambo yaja ndugu zangu, wizara ina miaka 2 tu na hata nusu bado.
Mhe. Waziri, hauko sahihi katika jambo hili.

Lazima ujaribu kupunguza kuamini unayoyaamini ili uitendee haki nafasi yako. Nafasi yako kumbuka ni (Managerial Post siyo technical post). Kusikiliza na kusoma kuwe kwingi ili baadaye utoe majumuisho jumuishi.

Kiuhalisia, mwanaume ana hatua muhimu tatu katika kuishi kwake duniani:-
1. Ni hatua ambayo anakuwa ni Mkuu wa Kaya na neno lake ni Amri. Katika hatua hii, akinamama, hujitahidi kuvumilia na kukubali kuwa chini ya mwanaume. Hapa ndipo Wanawake hunyanyasika (Wizara yako kwa wakati huu Wanawake wanaitegemea sana). Ukweli wa mambo ni hapa mwanaume anakuwa ni hodari kitandani. Lakini kadri miaka inavyokwenda na kusema za ukweli mwanaume akawa goigoi kitandani, mwanamke huanza kuchukua hatamu kidogo kidogo kwa kuhakikisha anamrudisha chini mwanaume. Katika hatua hii, watoto bado ni wadogo.
2. Ni hatua ambayo mwanamke anakuwa ni Mkuu wa Kaya, mwanaume anapokea amri kutoka kwa mke wake. Hii hali huanza hasa baada ya Tezi dume kuchachamaa na mwanaume kutoweza kitandani. Hapa ndipo Mbunge wa Iringa jana (
View: https://www.youtube.com/watch?v=fcKfgmE-zkc) alikuwa anakueleza kuwa umewasahau wanaume katika budget yako. Hapa Mwanamke huwa analipiza kwa yale ya hatua ya kwanza. Jinsi inavyoanza, ni mwanamke anakuwa na commands nyingi kiasi mwanaume anakubali ili yaishe ili kupunguza kero. Watoto wanakuwa wamemaliza vyuo na wanaanza kujitegemea. Mzazi anakuwa amestaafu, pension imekata.
3. Ni hatua ambapo wote wawili (Mwanaume na Mwanamke) wanatawaliwa na watoto. Watoto ndiyo wanatoa amri na pengine wazazi wanaishi nao. Baada ya hapo ni kusubiri wakati wao.

Ukizijua hatua hizi tatu muhimu, utagundua kuwa Mwanaume ana uhitaji wa huduma za Wizara yako nyeti. Wengi huangalia

Nawasilisha
 
Mama wewe Wakutengee hata bilioni 100.Wizara yako Ndio inabeba afya ya jamii na sura yake.
 
Back
Top Bottom