Ahsante Rais Samia, hatimaye baada ya miaka 7 kazini mwezi huu nimepanda daraja

Ahsante Rais Samia, hatimaye baada ya miaka 7 kazini mwezi huu nimepanda daraja

Achana naye! Ana stress za hali ngumu ya kiuchumi. Hajui wapi ataingiza kipato halafu anaona post ya mtu kapandishwa daraja.
Mtu mwenye uhakika wa "kula", akisikia jirani yake "anakula" wala hapati tabu.
Ila ambaye hana uhakika wa "kula", hata akisikia halufu ya chakula kutoka kwa jirani, atakikosoa chakula asichokiona!
Amepata maumivu!
 
Mimi hata wanipandishe huo mwezi ujao baada ya kunipotezea mwezi huu, nikiwa na watumishi wenzangu wengi tu!
Bado sina sababu ya kumshukuru!

Kwa sababu kupanda daraja, kuongezewa mshahara, kufanya kazi katika mazingira mazuri, nk hayo yote ni haki yangu kutoka kwa Mwajiri na wala siyo fadhila.
jiwe aliwasiginia mpini hadharani na hamkufurukuta!
kuweni na soni
 
Tutegemee bei ya vitu kupanda mara dufu

Hii ndo inayofanya increment imezwe

Mfano Tu mwaka Jana maharagwe mbeya mwezi wa tatu wa nne yalikuwa 20,000 lkn mwaka huu hayajashuka 27,000 Kwa debe
Kwan tangu 2016 vitu havijapanda bei?
Hii ni kauli aliyokuwa a natumia magu kuficha utapeli wake...
2015 cement ilikuwa 10500...mwaka 2020 ni 14000.
Kikwete alia ha sukari 1800kg yeye kaa ha 3500.
Ni ujuha kusema salary ikiongezeka bei ya vitu inapanda
 
Mimi hata wanipandishe huo mwezi ujao baada ya kunipotezea mwezi huu, nikiwa na watumishi wenzangu wengi tu!
Bado sina sababu ya kumshukuru!

Kwa sababu kupanda daraja, kuongezewa mshahara, kufanya kazi katika mazingira mazuri, nk hayo yote ni haki yangu kutoka kwa Mwajiri na wala siyo fadhila.
Sure maumivu ni makubwa sana maana unawaza labda kitasaidia kwa namna moja sasa haukipati hata kwa wakati, tuanze kuandikia salary arrears

Sent from my Infinix X652 using JamiiForums mobile app
 
jiwe aliwasiginia mpini hadharani na hamkufurukuta!
kuweni na soni
Una uhakika hatukufurukuta? Umejiunga lini JF? Ungekuwepo humu kitambo, usingeandika huu ugoro wako.

Kwa taarifa yako tulimpa makavu live humu mara zote alipotoa kauli zake zenye utata! Na hata huyu mama kama hatatenda haki, bado tutamkosoa tu. Na huu ndiyo uhuru halisi wa kuongea.
 
Wewe sikujui Ila utakua ni mwalimu tuuu !!! Akili za kijinga hivi mnazo nyie!!! Sijui hao watoto watafaulu vipi aisee

Haukua na sababu ya kutukana.

Kama haikuhusu ungeachana nayo.
Wote Hatuwezi kuwa kama wewe.

Kama Mungu kakujaalia kipato usidharau wengine.
 
Sina Mengi Mungu akubariki Sana mama ambaye umeona na kuthamini mchango wa wafanyakazi nchini.

Wewe uliyeona kuwa wafanyakazi nao ni watu wenye mahitaji, familia na changamoto kama Binadamu wengine.

Tofauti kabisa na mtangulizi ambaye aliamini wafanyakazi ni maroboti na wanatakiwa kufanya Kazi TU bila kuongezewa maslahi yoyote.

Naamini mama atarudi katika kanuni na taratibu za Utumishi wa uma ikiwemo Kutoa nyongeza ya kawaida kila mwaka kwa mujibu wa sheria na kupandisha madaraja KWA wakati.

Hongera mama

Kama vipi uongezewe Muda utake usitake!

Mazuri mengi yaja ,siku 100 mama kaupiga mwingi ,kazi iendelee MIKUMI tena kwa Mh SSH.
 
Mimi hata wanipandishe huo mwezi ujao baada ya kunipotezea mwezi huu, nikiwa na watumishi wenzangu wengi tu!
Bado sina sababu ya kumshukuru!

Kwa sababu kupanda daraja, kuongezewa mshahara, kufanya kazi katika mazingira mazuri, nk hayo yote ni haki yangu kutoka kwa Mwajiri na wala siyo fadhila.

Mwezi huu ambao umekwama utalipwa hiyo fedha yako japo kuna muda inaweza kuchelewa mimi mara ya mwisho wenzangu walipanda mimi nimebadilishwa miezi minne baadaye nilikuja kulipwa hilo gap lake lote. Hivyo usiumie utalipwa haki yako
 
Una uhakika hatukufurukuta? Umejiunga lini JF? Ungekuwepo humu kitambo, usingeandika huu ugoro wako.

Kwa taarifa yako tulimpa makavu live humu mara zote alipotoa kauli zake zenye utata! Na hata huyu mama kama hatatenda haki, bado tutamkosoa tu. Na huu ndiyo uhuru halisi wa kuongea.
dogo mimi ni mkongwe JF mpaka mitaani
pia huenda mimi ni baba yako jiangalie
 
Una uhakika hatukufurukuta? Umejiunga lini JF? Ungekuwepo humu kitambo, usingeandika huu ugoro wako.

Kwa taarifa yako tulimpa makavu live humu mara zote alipotoa kauli zake zenye utata! Na hata huyu mama kama hatatenda haki, bado tutamkosoa tu. Na huu ndiyo uhuru halisi wa kuongea.
toto limeifahamu jf 2019
aseee ama kweli hii ni heshima ya kambare
baba ndevu mama ndevu
 
Anashukuru kupitakiasi bila kujua hiyo n haki yake!!! Pia waliopanda possibly it us 40% wengi ni vilio
Wabongo kushukuru ni utamaduni tu.

Hata ukienda dukani kununua chumvi, unatoa pesa halafu unamwambia muuzaji naomba chumvi na akikupa unashukuru.

Binafsi naona ni uungwana tu
 
toto limeifahamu jf 2019
aseee ama kweli hii ni heshima ya kambare
baba ndevu mama ndevu
Una akili fupi sana wewe! Uliza nimekuwepo JF tangu lini na nimetumia ID ngapi kabla ya hii! halafu nitakuambia.
 
Back
Top Bottom