Ahukumiwa miaka 20 jela kwa kumiliki fisi kinyume cha sheria

Ahukumiwa miaka 20 jela kwa kumiliki fisi kinyume cha sheria

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
1741779220977.png
Emmanuel John (31), Chifu mkazi wa Kijiji cha Kilulu wilaya ya Bariadi kwenda jela miaka 20 na kuchapwa viboko 12 baada ya kupatikana na hatia ya kumiliki fisi kinyume cha sheria.

Hukumu hiyo imetolewa leo Jumatano, Machi 12, 2025 katika Mahakama ya Wilaya ya Bariadi na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Caroline Kiliwa baada ya mshtakiwa kukutwa na hatia.

Mshtakiwa huyo ambaye pia ni mganga wa kienyeji, alipewa adhabu hiyo katika kesi iliyokuwa inamkabili kwenye mahakama hiyo baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka.

Awali akisoma kosa la mshtakiwa, Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mashtaka Mkoa, Lupiana Mahenge alielezea mahakama kuwa Chifu alikutwa na nyara ya Serikali ambayo ni fisi akiwa hai akimfuga nyumbani kwake kinyume cha sheria.
 
Chezea mnyama yoyote lakini usimchezee "Hyena Hyena . . . nambari wani."
Mhhh! Hahahaa. Hutaki achezewe Ni kwa sababu huyo ni Crocuta crocuta na ww ni lycaon pictus(Mbwa mwitu)mpo jirani kwa makazi ya huko kwenu porini?(kwa Utani lakini).
Mi navyojua ni usijaribu kuchezea Twiga. Kwa Tanzania, Twiga ni mnyama mtakatifu -haguswi hovyo.
Huku Umasaini ndani ndani huku fisi wanatumalizia mbuzi aisee.
 
Back
Top Bottom