Aibu: Vyombo vya Habari nchini kwa makusudi vyapotosha alichokisema Dkt. Slaa kwenye Mkutano wake na Waandishi wa Habari

Aibu: Vyombo vya Habari nchini kwa makusudi vyapotosha alichokisema Dkt. Slaa kwenye Mkutano wake na Waandishi wa Habari

A
Who is Dr. Slaa currently, ameongea na vyombo vya habari kama nani?
Acha maswali ya kipuuzi mkuu, Kila mtanzania ana haki ya kutoa maoni yake kwa mujibu WA Sheria na katiba isitoshe haswa kwenye rasilimali za nchi,
Huyo ni msomi balozi na kiongozi mzalendo so hatakama angekuwa Hana hivyo vyote uraia wake wa nchi unatosha kutoa maoni
So wakati mwingine uache foolish question
 
Kuna sehemu nilisoma, nikarudia kucheki clip chache ,daaa ndugu zangu , watanzania ni watu wa hovyo Sana .
 
A

Acha maswali ya kipuuzi mkuu, Kila mtanzania ana haki ya kutoa maoni yake kwa mujibu WA Sheria na katiba isitoshe haswa kwenye rasilimali za nchi,
Huyo ni msomi balozi na kiongozi mzalendo so hatakama angekuwa Hana hivyo vyote uraia wake wa nchi unatosha kutoa maoni
So wakati mwingine uache foolish question
Achana nae Hawa ni moja ya species za hovyo Sana kwenye nchi hii.
 
Katika mkutano wake na vyombo vya habari uliofanyika leo, Dr Slaa ameongea kiuzalendo na kuonyesha ubaya wa miataba tuliokuwa nao. Lakini cha ajabu vyombo vya habari nchini kinyume na maadili ya ukma vimepotosha kwa makusudi kauli na mantiki na dhima ya alichokizungumza.

Ili kuwachanganya wananchi, vyombo hivyo vimetia kichwa cha habari tata ili kuwachanganya wananchi.

Huu ni ushahidi wa wazi kuwa Media yetu ina shida, ina tatizo, na tatizo siyo dogo.

Kama media inaweza kutengeneza habari, kwa makusudi ya kuhadaa umma, kuupa umma taarifa feki kwa kufanya ommission makusudi.Basi kiufupi, ndugu zangu muone tuna jamii ya namna gani.

Pengine waliokuwa wanasema kuwa kuna baadhi ya Wamiliki na waandishi wa habari wapo katika Payroll ya kupigia debe uuzwaji wa nchi ni kweli. Otherwise niambieni ni chombo gani cha habari chenye heshima kinachoweza kutoa taarifa ya kupika namna hii.

Kwa kweli media ya Tanzania inatia aibu, tena ibu kubwa.

Upotoshaji huu unathibitisha kuwa hili dili la kuuza bandari yetu ni dili chafu, otherwise kwa nini nguvu kubwa inatumika kuhadaa umma?

Tumemsikiliza Dr Slaa alichosema. Kaita azimio la bunge ni la kihuni, na kaita mkataba ule kuwa ni uuzwaji wa nchi. Sasa hivi vyombo vya habari inakuwaje vinatumia vichwa tata ili kupotosha kauli ya Dr Slaa?

Cheki vichwa vya habari vya hivi vyombo, bila shaka vimekubaliana kupotosha kwa makusudi.


View attachment 2656443
Kati ya watu wa hovyo kabisa hapa nchini, baada ya wabunge hawa bandia ni waandishi wa habari wa hapa nchini.

Wengi wao ni watu wenye akili ndogo, uelewa duni, maadili zero, vipato vya ubangaizaji, wanaohongeka hata kwa elfu hamsini.

Kuna wakati waziri alikuja kwenye kampuni yetu, na hao waandishi njaa walikuwa wametoka kwenye vyombo 6 tofauti tofauti. Baada ya kikao, msaidizi wangu akaja, akaniambia kuwa kuna mwandishi mmoja wa habari alimwendea na kumweleza kuwa anawawakilisha wenzake, na kwamba idadi yao wapo 14, wanaomba angalao chochote ili kuwawezesha wakaiandike vizuri kampuni. Kauli hiyo ilinikera sana, nikamwambia yule msaidizi wangu kuwa, kama wana njaa wangeomba tu kuwa wana hali mbaya, wanaomba chochote, lakini kuniambia eti wakaiandike vizuri kampuni, ina maana kampuni ina mabaya gani hayo ninayotakiwa kuyafunika kwa fedha?

Niliwakatalia, wakaandika walivyotaka. Toka wakati huo nikaelewa kuwa hiyo tabia chafu haiwezekani kuwa alianzia kwangu, ina maana ndiyo tabia yao ya kila siku. Nikawapuuza toka hiyo siku.

Hivyo haya waliyomfanyia Dr. Slaa siwezi kushangaa maana naamini Dr. Slaa hawezi kumhonga mtu.
 
Hizo walipewa hivyo hivyo bila wao kufanya chochote cha ziada.
Waandishi wetu ni wajinga, sawa tu akina Musukuma. Wanachopewa na serikali wana-copy na kupaste. Wanafanya kazi kama tarishi wa serikali..
 
Lazima wapotoshe kwasababu hata nao wameshindwa kuripoti ukweli.
 
Hakuna upotoshaji hapo.Yote hayo aliongea.Alisema mkataba ni wa hovyo.Akashauri uangaliwe upya na wananchi waelemishwe.Pia alisistiza kuwa yeye hapingi uwekezaji bandarini.
 
Magazeti na wahariri wake siku hadi siku mnazidi kujipotezea imani yenu kwa wananchi kama muhimili wa nne kulisaidia taifa

Hakika upotoshaji dhidi ya Dr Slaa na mengineyo mengi mmejiharibia sana

Waziri wa habari na serikali kwa ujumla inawashibisha vya haramu,iko siku yenu mtajibu kwa huu upuuzi wenu,hasa kwenye critical issues zinazohusu maslahi ya taifa kama bandari na mengineyo yajayo
 
Mkuu, ungetumia muda huo kusahihisha ^upotoshaji^ wa Dkt Slaa, badala ya kuzungumza na ^hewa!^
 
Mkuu, ungetumia muda huo kusahihisha ^upotoshaji^ wa Dkt Slaa, badala ya kuzungumza na ^hewa!^
Balozi Dkt. Willibrod Slaa anazungumza na Wanahabari katika Hoteli ya Regency Jijini Dar es Salaam, leo Juni 13 2023 kuhusu hati ya makubaliano yaliyoingiwa kati ya Tanzania na DP World.

=======

Dkt. Slaa: Hadi kufikia hatua ya azimio hili kuridhiwa na Bunge, ikumbukwe makubaliano ya awali yalifanyika tarehe 28 February, kampuni ya DP World na bandari waliingia kwenye makubaliano yalitokana na shughuli iliyofanyika Dubai expo 2022, hatujaambiwa ni tathmini gani au utafiti gani ulifanyika

Kwenye expo, kwenye maonesho kama yale ya sabasaba Dar es Salaam watu wanaingia kwenye mkataba mkubwa wa kulifunga Taifa, nadhani mnaelewa hiyo maana yake ni nini!

Hadi wakati huu Taifa na watanzania walikuwa hawajapewa taarifa yoyote ile inayohusu mkataba mkubwa wa aina hiyo.

Naomba kuwakumbusha pia kuwa pamoja na mkataba huu, katika Dubai 2020 Serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Rais mwenyewe kulisainiwa mikataba 17, nani kati yenu hadi leo hii anaifahamu mikataba 17 inahusu nini, ni usiri mtupu, ni nchi inaingizwa kwenye giza, Rais wa Nchi amehudhuria lakini mambo hayo yote yako ndani ya giza.

Waliohudhuria maonesho ni viongozi wa Serikali, wamesafiri, wamelala hoteli, wamekula chakula kwa kodi ya watanzania, ni Tanzania pekee ambako Serikali haiwajibiki kwa wananchi wake, jambo ambalo katika hatua hii, jambo ambalo linalazimisha kuwakumbusha uhitaji wa haraka wa katiba mpya na bora.

Hii taarifa tunayozungumzia hatukuipata Serikalini, tumepata taarifa iliyovuja. Ni nchi gani duniani tunasubiri taarifa ivuje tuanze kuizungumzia. Siku siku 30 zilizotajwa kwenye mkataba na Bunge, kwa maneno mengine umeridhiwa ndani ya siku 30 lakini umekuja kuridhiwa baada ya miezi takribani 8, kwa hali hiyo tuna uhakika gani Tanzania ina uwezo wa kutimiza mkataba huu kama mwanzo tayari ni mbaya na hakuna anayeeleza uchelewashaji huo unatokana na nini.

Dkt. Slaa ametoa hoja zifuatazo

1. Dkt. Slaa: Nchi inayojulikana kisheria ni United Arab Emirates, Je Dubai ni Serikali? Dubai ni mji unaojiongoza, sisi ni nchi ya Jamhuri ambayo maamuzi yetu yanafanyika kwa kutumia Bunge. Bunge lilitangaza wanataka maoni ya wananchi tarehe 5 Juni wanaotoka maeneo mbalimbali wawe wamefika bungeni tarehe 6. Kwa saa 24 mtanzania gani anafika Dodoma na kutoa maoni yake. Ni dhahiri kuliwa na hila na Serikali haikuwa na nia ya kushirikisha wananchi wake. Hatukushirikishwa na imepelekwa bungeni na mjadala ulivyokuwa bungeni ulikuwa ni mjadala wa ki-mangimushi
2. Aidha ikumbukwe Serikali iliyopo ina legitimacy ya wasiwasi kutokana na uchaguzi wa 2019 na 2020. Simung'unyi maneno, uchaguzi wa 2019 na 2020 inaweza kuwa na legitimacy lakini sina hakika kama uchaguzi huo ulikuwa sahihi, najua ulivurugwa kwa makusudi na chama cha mapinduzi na vyombo vyake. Mwenye macho haitaji kuambiwa kuhusu hilo na wananchi wote ni mashahidi.
3. Kwa mujibu wa kifungu cha nne cha IGA kinatamka wazi rasilimali zote zilizotajwa zinakabidhiwa kwa Serikali ya kigeni. Rasilimali hizo ni bandari zote za nchi nzima(bahari, maziwa, mito, zitakazokuwepo hata kwenye mabwawa) yale yote yaliyokuwepo leo na hata yatakayokuja. Huu ni uuzaji wa nchi, hakuna mtanzania mwenye akili atakaekubali jambo hilo bila uhakika wa rasilimali zake hizo.
4. Serikali ya awamu ya nne wakati inataka kutaifisha mashirika muhimu ikiwemo bandari, aliyetupa taarifa alifukuzwa kazi. Alitupa taarifa ya kutokubali kuyataifisha kutokana umuhimu wake kwa usalama wa Taifa.
Dkt. Slaa ameongelea mfano wa mbia katika kampuni ya mafuta wakati wa vita ya Uganda ambapo Tanzania ilikuwa inamiliki 51% katika kampuni hiyo huku mbia akiwa na 49% lakini aliweka ngumu kwasababu alidai mtu tunayepigana nae ni mbia wake pia hivyo. Slaa amedai kwa siku 5 vifaa havikuweza kuondoka kwasababu ya mafuta wakati nchi inaendelea kupigwa.
5. Slaa pia ametoa mfano wa 'Entebbe Raid' ambapo amesema ndege ya Air France ilitekwa nyara na wapiganaji wa Palastine wakishinikiza mambo yao ya kisiasa ndani ikiwa na waisraiel ilitua uwanja wa Entebbe. Slaa amedai Waisrael iliwachukua chini ya dakika 90 kuwakomboa watu wao na amedai iliwezekana kwasababu wao ndio waliojenga uwanja na ramani zote walikuwa nazo ikiwepo sehemu ya kuingilia na kutokea.
6. Slaa amesema sababu hapo juu pia ilisababisha Serikali ya awamu ya tano itumie wajenzi wa ndani kujenga Ikulu lakini sasa bandari zote zinakabidhiwa kwa mgeni.
7. Dkt. Slaa: Mkataba unaotoa 'exclusive rights' daima uogope, inatoa pia kifungu baadae yatakayojadiliwa kwenye mikataba midogo midogo, unatoa kwanza mali yako, unajuaje wakifika kwenye hiyo mikataba midogo midogo wakikutalia! Una nguvu gani, ulishasain 'exclusive rights'
8. Utekelezaji wa DP World sio kwamba unaanza Tanzania, katika Afrika peke yake tuna migogoro mingi. Nenda nchi za Ulaya, Brussels ni ya Ulaya lakini wako mahakamani, karibu kote kunakogombaniwa ni rushwa, kuna wabungwe walipelekwa, wakalishwa, wakapewa posho ya dola 2000 yote hiyo ni rushwa. Kama ingekuwa nchi nyingine, hizo zinatosha kufuta mkataba huu na kapeleka hata hiyo kampuni mahakamani.
9. Sijawahi kuona mkataba(IGA) Marekani na Ulaya ambao una lugha kama hii ya kwetu, waathirika tumewaandaaje mfano ujenzi wa reli bandarini mpaka airport. Tumeona barabara ya Kibaha watu walivyolia Kimara. Mikataba hii lazima iwe ya tahadhari sana.
10. Tunayasema haya kwa nia njema lakini tunashangazwa na kutishwa na propaganda ambayo Serikali inafanya, jambo jema huwa haliendeshwi kwa propaganda, ukiona mtu anafanya propaganda ikiwa ni pamoja na kwenda kwenye madhehebu ya dini anza kuweka mashaka, kuna maslahi gani nyuma ya makubaliano hayo!

Dkt. Slaa: Niseme yafatayo

11. Kwa lugha rahisi, taarifa hii haina lengo la kupinga. Hoja ya msingi ni kukosekana kwa uwazi katika namna ya kushughulia rasimali ya nchi yetu

12. Vifungu vingi vinavyotia mashaka vinahitaji kuangaliwa upya hata kama mkataba ni mzuri au mbaya, unaweza kuboreshwa kwa kushauriana na wananchi wake. Mkataba wowote hata kama ni mbaya, mzuri unaweza kuboreshwa. Mkataba huu utazamwe upya ili vipengele vyote vyenye utata viondolewe.

Mfano tunaona mkataba huu wanasema ni nchi nzima, bandari zote. Kwanini tusiseme bandari ya Dar es Salaam, mengine yote tutaingia wakati tumeridhika.

Mkataba hauweki muda maalum, kwanini tusiseme tutakuwa na mkataba wa bandari kwa miaka 10, tena kuna kifungu kinazungumza hatutaweza kuondoa. Halafu kuna masharti kama tunataka kuondoa tufanye nini, unaweka masharti. Haya masharti yote wanajua ni ya kutupiga, hata mkienda kwenye mahakama ya malalamiko tumeshapigwa tayari. Hata Serikali ikibadilika hatuwezi kuondoa mkataba huu.

13. Bandari inazungumzia upande mmoja wa Tanzania, nimeshangaa na watu hawakosei. Wanasema Rais ni kutoka upande mmoja wa muungano, waziri wake ni kutoka upande huo huo wa muungano. Tafsiri za watu huwezi kuzifungia kwenye sanduku, huwezi kuzuia watanzania wasifikiri kwasababu Rais anatoka upande huu, waziri wake ndio maana wameuza bandari zetu, mbona zile hazikuuzwa.

Slaa amesema suala la bandari ni la muungano lakini ameshangazwa kwa Zanzibar kuwa na sheria ya bandari yao. Slaa ameshangazwa na nchi moja kuwa na bandari mbili ilhali sheria ni moja.

Dkt: Slaa: Mbona hawalielezi hata bungeni hilo, kumbe kuna mambo mengi hata bunge limefichwa na bunge letu jinsi lilivyo la hovyo, naomba radhi sana na waniite kwa hilo, kilichofanyika juzi ni uhuni.

Dkt. Slaa: Natoa wito kwa watanzania wote kwa pamoja tusikubali kupokea upotoshwaji aina yoyote katika mambo yanayotuhusu sisi wenyewe na vizazi vyetu vijavyo. Mkataba huu ujadiliwe upya, uangaliwe upya tuweze kukubaliana vitu gani vifanyike.
 
Back
Top Bottom