AIM Global, Qnet, Forever Living, One Coin, GNLD na wengine mbadili mbinu za utapeli, hii ya utajiri ndani ya siku 2 imepitwa na wakati

AIM Global, Qnet, Forever Living, One Coin, GNLD na wengine mbadili mbinu za utapeli, hii ya utajiri ndani ya siku 2 imepitwa na wakati

Uongo mtupu hawa hawa jamaa wa Qnet wanaovaa suti za kuunga unga za pale karume eti ndio wamiliki nyumba?

Wanachojua wale jamaa ni kudanganya tu ooh kuna watu wameacha kazi TRA wamejiunga QNET,nillikaona kadada ka moja kwny video huko watsap kanasema eti hii kazi ya QNET imenipa gari yangu hii aina ya Benz wkt hio gari ni bmx x5 nikasema tu hiiiiiiiii baghosha,ntombanewe.
Huyo jamaa nadhan atakuwa n member wa Qnet,so anajaribu kutetea.

Sent from Nokia 7 Plus
 
Jamaa yangu kanifuata anataka kujiunga na huko kwa hao jamaa kuna dada mmoja ndio kamshawishi na ahadi kibao za utajiri na yule dada anajisifu kuwa ana hela, nikamwambia mkuu hakuna wema kama huu mbona yule dada ana wadogo na ndugu zake kibao wamepigika balaa na hajawaunganisha huko wapige hela ili familia yake iwe tajiri, jamaa yangu akashituka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna binti mmoja classmate alinishawishi nijiunge kwenye hizo mambo nikamtolea nje, yeye alikuwa alishajiunga na kira mara nilikuwa naona anaweka status kuwa muda si mrefu atamiliki tv kali, sijui hyundai nk nk.

Hivi ninavyoandika ni beki tatu mahali na uchumi umeyumba hadi vocha anakosa.

Haya makampuni yapigwe marufuku, yanatufilisi sana sisi wanyonge.
 
Ukombozi wa kifikra ni pamoja na kufanya comprehensive business analysis before huja opt fursa unayoletewa mezani.Mkuu kama huna pesa tuliza mshono,hii dunia kiongozi ni kubwa sana na fursa za kibiashara ni nyingi pia ! sipo hapa kuku convince but we need to think out of the box na tusiwe na corrupt mind ya kujenelaizi kuwa all network marketing hapa Tz ni utapeli tu hapana mkuu.Sema tu wanaotuletea hizo fursa baadhi yao wanakuja na motivational convincing language inayowafanya watu waamini kuwa wanaweza kupata fedha kwa uharaka na pengine bila kufanya kazi hapana,everything you have to toil

Sent using Jamii Forums mobile app
Chief, network marketing za Tanzania zimejaa utapeli utapeli, watu wanarubuniwa wanaenda wanakopa maskini ya Mungu, convincing power inayotumika ni kubwa mno ila mara tu mtu akishatoa pesa anaachwa solemba, ahadi zote alizoaidiwa atasaidiwa kutafuta partiners pindi akipata pesa inaota mbawa ila anaambiwa akomae kivyovyote ndo maana unakuta hadi anaenda kukodi magari ili awadanganye watu wamwamini ili aweze kurudisha pesa zake, me huwa simung'unyi maneno kwenye hili QNET ni matapeli
 
Lack of global exposure inawasumbua wengi sana aisee,so sad yaani !

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu naona ujanielewa na umeni-quote sivyo mimi kama Akwota nasema hivi "Qnet" n matapeli wanawaumiza watu,hii kauli ya lack of Global exposure ni umavi wa kiwango cha lami na ndiyo baadhi ya kauli mnazotumia kuwarubuni watu kuingi huko kwenye utapeli.

Sent from Nokia 7 Plus
 
Hizo ndo akili za ngamia ! wewe una amini katika kilimo cha matikiti maji kuwa utatoboa basi komaa mkuu siku moja utanunua fuso ucjali
Mkuu naona ujanielewa na umeni-quote sivyo mimi kama Akwota nasema hivi "Qnet" n matapeli wanawaumiza watu,hii kauli ya lack of Global exposure ni umavi wa kiwango cha lami na ndiyo baadhi ya kauli mnazotumia kuwarubuni watu kuingi huko kwenye utapeli.

Sent from Nokia 7 Plus

Sent using Jamii Forums mobile app
 
haya na wewe kajiunge sasa uwe tajiri kama hao wenzako usiishie kwenye theories tu.
Siri ya mtu ni kichaka ndugu hiyo haina utofauti na mtu kusema biashara ya daladala inalipa kwa sababu nilimuona fulani alikuwa nayo moja mwaka jana sasa hivi anazo 3.
Na hata kama kweli wamezipata hizo pesa ni kwa sababu kuna wajinga kadhaa wamepigwa ndio ikafanikisha wao kuwa hapo kwa hiyo usigeneralize kwamba hiyo ni biashara nzuri.
Amejenga nyumba mkuu within this 3 yrs ! na huko Malaysia anaenda kwa pesa zake zinazotokana na juhudi zake za network marketing.Nawafahamu hao marafiki zangu miaka mitatu ya nyuma walikuwa ktk hatua gani kimaisha na sahizi wapo wapi, mmoja kati yao kapiga hela ndefu na mwaka jana kawekeza ktk kikimo chha mihogo eka 120 huko Tanga maeneo ya Mkata, kikubwa hapa naona physical progress siyo blabla ! na wanajitoa kwelikweli kufanya kazi across the whole country,upo hapo nyonyo

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hyo kwenda Malysia ni sifa, acheni utapeli,QNET ni matapeli kama walivyo matapeli wengine ,
Hzo nguvu mnazitumia kuwarubuni watu mngekuwa mnawahamasisha kilimo au ufugaji nchi hii ingekuwa mbali sana.
Hizo ndio gia zao qnet, kwenda malysia, ugiriki, sijui wapi. Hizo ndio gia zao za kitaahira.
 
Nimeangalia michango ya mawazo ya watu humu ndani inasikitisha kweli,kila mtu kasimulia matukio tu lakini hakuna mtu aliye kuja na simulizi la uzoefu katika moja ya hizo network marketing.Ni kweli zipo unprofessional and illegal scheme ambazo zinawahadaa watu ili kuwarubuni but siyo zote.Hiyo Qnet mnayoiponda as if ipo kwa lengo la kuwaibia watu naweza kusema ni a big NO maana nina jamaa zangu watatu wanapiga kazi sana na huu ni mwaka wa tatu nawaona wanapata exposure ya kwenda nje huko Malaysia kwaajili ya mikutano ya kupeana mbinu na uzoefu wa biashara,kikubwa hapa siyo kuingia fursa halafu unabaki unabweteka na shemejiyo nyumbani ukiamini umetapeliwa badala ya wewe nawe kufanya network marketing ili kile ulichokiwekeza kiweze kurudi na mwisho wa siku uendelee kunufaika na hiyo fursa kwa kufanya kazi.Hapa kazi tu !

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa nini weww usiungane na hao jamaa zako uuage umasikini maana wewe na familia yako, ukoo wenu mmejaa ufukara. Kwa nini usiwashawishi ndugu zako na jamaa zako wakauza kila kitu mkaungana na hao jamaa zako mkapiga hela, mkaenda Malysia, Ugiriki, Ufaransa na hata New York mkale maisha muage ufukara muwe mabilionea? Kwa nini msifanye hivyo? Huu ndio wakati wenu kuuaga umasikini.

Haina akili kua wewe uone fursa ya kuuaga umasikini usiwashirikishe na kuwaambia ndugu zako wa damu uje kujifanya unawapenda watu humu usiowajua uwaambie watumie fursa, kwani ukoo wenu hawaitaki hiyo fursa?
 
Nimeangalia michango ya mawazo ya watu humu ndani inasikitisha kweli,kila mtu kasimulia matukio tu lakini hakuna mtu aliye kuja na simulizi la uzoefu katika moja ya hizo network marketing.Ni kweli zipo unprofessional and illegal scheme ambazo zinawahadaa watu ili kuwarubuni but siyo zote.Hiyo Qnet mnayoiponda as if ipo kwa lengo la kuwaibia watu naweza kusema ni a big NO maana nina jamaa zangu watatu wanapiga kazi sana na huu ni mwaka wa tatu nawaona wanapata exposure ya kwenda nje huko Malaysia kwaajili ya mikutano ya kupeana mbinu na uzoefu wa biashara,kikubwa hapa siyo kuingia fursa halafu unabaki unabweteka na shemejiyo nyumbani ukiamini umetapeliwa badala ya wewe nawe kufanya network marketing ili kile ulichokiwekeza kiweze kurudi na mwisho wa siku uendelee kunufaika na hiyo fursa kwa kufanya kazi.Hapa kazi tu !

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu. We angalia hata katika huu uzi 99% ya wadau ni walioponea chupuchupu kuingia kwenye huu uhuni. Sijaona aliyejitokeza kusema yeye amefanikiwa na anapata hizo billioni kila mwaka. Huu ni uhuni ambao inabidi upigwe marufuku na serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi biashara za network marketing si utapeli sema ni biashara ngumu Sana sasahiv kupata watu wa kujiunga ni ngumu na bidhaa zao ni ghali hapo ndo wanakosea hawasemi kweli unadanganywa utapata faida kwa haraka kumbe inahtajika usote haswa walionufaika ni wale walioanza hizi biashara miaka ya nyuma uko

Sent using Jamii Forums mobile app
Watanzania wangapi utawauzia saa ya million 5? Yani ni kichekesho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuhusu Q-net binafsi ninaweza kusema haya....

-Ni wale wale, pyramid scheme fulani, wachache sana (wa mwanzo) wanaweza kuvuna kwa kutumia migongo ya wengine wengi (wanaofuata nyuma).

-Ukitaka uanze kuvuna chochote (kurudisha mtaji wako) kupitia Qnet inabidi ukubali kwanza kutoa (kulizwa!) milioni 5 zako kwanza na kisha uhakikishe watu wengine zaidi ya 20 hivi wanajiunga katika mnyororo unaohusiana na wewe. Sasa kimbembe sio tu kuzipata hizo milioni 5 za kujiunga, kimbembe kikubwa zaidi ni mtiti wa kushawishi watu wengine wajiunge. Unaweza kuwa kichaa, ukakonda, ukadhoofu, ukachoka au kuchukiwa hadi na ndugu, marafiki au majirani zako.

-Tofauti kubwa ya mfumo wa Qnet na network marketing zingine ni kuwa, mnyororo wa kuunganisha watu huwa ni watu wawili wawili (Binary). Muundo huo una faida na hasara pia. Mambo mengine ni yale yale tu na tofauti zilizopo hazina msingi.

-Tatizo kubwa lililopo katika biashara ya Qnet ni gharama za mwanzo za kujiunga kuwa kubwa sana (Kwa sasa ambazo ni wastani wa milioni 5) huku ukizugwa kuwa unanunua bidhaa au huduma, kitu ambacho huenda 99% ya watu waliopo Qnet hapa Tz hakikuwa kivutio chao cha awali cha kupenda kujiunga.

-Makosa makubwa yanayofanywa na member wa Qnet kiasi cha kuonekana ni biashara ya kitapeli ni kitendo chao cha kuwapa matumaini hewa ya uongo na kweli kwa kuwaaminisha watu wanaowashawishi kujiunga kuwa watakuwa mabilionea chap chap kitu ambacho sio ukweli. Na hapo huwa wanawaaminisha kuwa biashara zingine zote au kazi za kuajiriwa ni kupoteza muda na hazina manufaa. Wakati kiuhalisia ni rahisi kupiga pesa kwa kubet kuliko kuvuna hata senti tano kwa Qnet.

-Ukweli mchungu kuhusu Qnet ni kuwa pesa yoyote utakayovuna kupitia Qnet ni matokeo ya mtu mwingine kulizwa haswaa. Hivyo kama utatajirika kwa Qnet basi ujue wazi kabisa hayo ni matokeo yalitokana na kutengeneza ufukara kwa member wengine wa Qnet.

-Kuhusu salamu yao ya Good morning! Binafsi sioni tatizo. Ni kitu cha kawaida na kina maana nzuri. Kivipi? Kwanza ni utambulisho wao, hivyo wanaweza kufahamiana na kuwafahamisha wengine wao ni akina nani. Pili, kwa kuwa wanafanya biashara kutumia online platforms na wapo dunia nzima, tofauti za masaa baina ya nchi na nchi ni kubwa, hivyo kuwa na salamu inayofanana wanapowasiliana regardless ya majira ya nchi yako ni jambo zuri. Mwisho, Good morning! maana yake ni kumekucha! Tupo macho, hatuja lala, ndio kwanza tumeamka, bado mapema sana, tuna nguvu mpya, tuanze sasa kazi nk.
Hivyo hiyo ni motivation greeting kwa watu wengi duniani wanaokuwa busy katika mishe mishe zao.

Yote kwa yote simshauri mtu yoyote kujiunga katika hii biashara ya Qnet, maana uwezekano wa kulizwa ni zaidi ya 90% na kwa wale wachache waliofanikiwa au watakaofanikiwa kupitia hii biashara basi walipigika na kupambana mnoo kwa muda mrefu (ikiwemo kutumia uongo au ujanja mwingi wa maneno) pamoja na bahati kuwaangukia upande wao.
 
Acha wawapige tu. Hivi mtu unaingiwa na kirusi gani kwenye ubongo hadi unakubali kujiunga na upuuzi huu
 
Jamani miaka inasonga, ni miaka miwili tangu nigome kujiunga Qnet ila ni kama jana tu make nakumbuka kila kitu... nilivyodakwa hadi nilivyopelekwa ofsini kuseminishwa.

Ajabu huyu mwenyeji wangu aliyedai kunipenda na kunipendelea sana hadi kunishirikisha kwenye utajiri, bado namuona akisaga na rhumba tu japo alisema muda si mrefu nitajutia ubishi wangu.

Good Morning! [emoji276]
 
Back
Top Bottom