AIM Global, Qnet, Forever Living, One Coin, GNLD na wengine mbadili mbinu za utapeli, hii ya utajiri ndani ya siku 2 imepitwa na wakati

AIM Global, Qnet, Forever Living, One Coin, GNLD na wengine mbadili mbinu za utapeli, hii ya utajiri ndani ya siku 2 imepitwa na wakati

Nilipelekwaga office za Forever aisee wanakutamanisha balaa ila bidhaa hawakwambii bei zake hadi ujiunge nao kadri maelezo alivo zidi kuyatoa naona huu uongo wanamsifia kila yule dada Blandina...ile muda nataka kuondka nikamvuta pembeni yule jamaa nikamuomba nauli kama alistuka fulani akaongea huku anajikaganyag kanyaga tu mara sitembeagi na cash sijui nini blah blah kibao nikaona hapa hamna kitu... kuja kuulza kwa wanaofahamu ndo naambiwa ungemuuzia nani dawa ya mswaki elf 50?
Nikasema duh kweli ukiitwa kwenye fursa jua wewe ndo fursa
 
Hizo ndo akili za ngamia ! wewe una amini katika kilimo cha matikiti maji kuwa utatoboa basi komaa mkuu siku moja utanunua fuso ucjali

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu acha kujibu kwa jazba naskia nyinyi matajiri wa Qnet hamtakiwi kuwa na jazba but acheni kuwatapeli baadhi ya Watanzania kwa uelewa wao ambao may be n mdogo kuhusu hizi issue za Qnet et all,ndiyo ninaamini katika matikiti,machungwa,mananasi,pilipili hoho na pilipili za mwendo kasi,mihogo,mahindi,na vitunguu maji tena muda huu vinalipa kweli kweli hivi vitunguu maji,acheni kuumiza watu mkuu.

Sent from Nokia 7 Plus
 
Nilipelekwaga office za Forever aisee wanakutamanisha balaa ila bidhaa hawakwambii bei zake hadi ujiunge nao kadri maelezo alivo zidi kuyatoa naona huu uongo wanamsifia kila yule dada Blandina...ile muda nataka kuondka nikamvuta pembeni yule jamaa nikamuomba nauli kama alistuka fulani akaongea huku anajikaganyag kanyaga tu mara sitembeagi na cash sijui nini blah blah kibao nikaona hapa hamna kitu... kuja kuulza kwa wanaofahamu ndo naambiwa ungemuuzia nani dawa ya mswaki elf 50?
Nikasema duh kweli ukiitwa kwenye fursa jua wewe ndo fursa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] dawa ya mswaki shilling ngapi? Hata wakina MO wenye mkwanja mrefu hawawezi kuingizwa kwenye chaka hilo. Dah![emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa jamaa wanahitaji kuwa makini maana watapata laana kubwa kwa kuhangaisha binadamu wasio na hatia. Et unakuta mtu anakuambia, nilikuwa dactari, nikaacha sasa ona niko tajiri, kwa magari ya ndugu zao. Nafikiri watu wasikubari kuingia katika mitego ya namna hii pia ni vyema serikali hawa watu iwapige marufuku kabisa. Hata kama watakuwa wanalipa kodi, wasiruhusiwe kufanya utapeli huu kwa raia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amejenga nyumba mkuu within this 3 yrs ! na huko Malaysia anaenda kwa pesa zake zinazotokana na juhudi zake za network marketing.Nawafahamu hao marafiki zangu miaka mitatu ya nyuma walikuwa ktk hatua gani kimaisha na sahizi wapo wapi, mmoja kati yao kapiga hela ndefu na mwaka jana kawekeza ktk kikimo chha mihogo eka 120 huko Tanga maeneo ya Mkata, kikubwa hapa naona physical progress siyo blabla ! na wanajitoa kwelikweli kufanya kazi across the whole country,upo hapo nyonyo

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaweza kuwa kweli,waliojiunga kuwapata chambo wengine hakuna kikibwa ,wanasuffer sana mkuu..


Mimi Nina rafiki zangu wengi huko network marketing firms ,wanafanya biashara zingine ,wananunua magari na kujenga ,LAKINI SIO network MARKETING INAYOWAPA HIZO HELA....

MTU ABAKOPA GARI KUPITIA KAZINI BENKI , ALAFU ANADAI NI QNET IMEMFIKISHA HAPO .Nina ushahidi .


Waliojiunga wakwanza wanawatumia wachini .

Ni kama pyramid scheme tu.


Only 10% ya walioko huko wananufaika, wengi wanaumia ......


Kuna mwingine kajiunga mwaka sasa hata elf 50 inamshinda ya ghafla ..........

#kitendo cha kuwaambia watu ni biashara ya part time na utatengeneza billions within one year kiurahisi na wanasema NO RISK ,ndio utapeli wenyewe
 
Ninavyoelewa ni kuwa kufanikiwa au kushindwa kwenye jambo fulani ni namna mtu husika anavyopambana.Nrtwork Marketing hutegemea ni namna gani una bidii kupata mtaji kwa maana ya watu na fedha. Ila wengi wana pata shida kwa kuwa viingilio ni vikubwa sana afu kupata watu wakujoin ni issue pia kws kuwa mwisho anayefaidika ni wa juu hata kama ukifanikisha pesa na wstu.So uhalisia wa kufanikiwa ni mdogo au hakuna kabisa endapo ukikosa watu wa kukujoin. Nashauri mtu anayeanza chini asaidiwe na wa juu sio tajiri avune kwa maskini hapo ndio watu watashawishika. Wangesema mtu kujiunga na network marketing unapewa bidhaa bure kwa makuliano maalum kauze afu pasent fulani rudisha ofisini mpaka utakapojitegemea kimtaji ndipo uendelee mwenyewe hiyo ingesaidia.
 
Stupid companies. Stupid country kwa kuruhusu huu ujinga wamekaa wanaangalia tu. OneCoin walijaribu kufanya conference marekani FBI waliwawakia vibaya mno mama wa watu akakimbia kujificha na trilioni za watu hadi leo haijulikani alipo.

Hua nawaambia watu waache ujinga wa kutafuta shortcut kama huna kazi njoo nikupe nikulipe usave ufanye kazi yako nyingine. Seriously serikali yetu inafanya nini hawa matapeli wanakuja wanabeba hela za watanzania wanaondoka tumekaa tu tunachekacheka kufunga watu kama Idris kwa ujinga. Stupid country run by stupid people
 
Hahahaha hawa wajinga walini block kwenye whatsap

Eti karibu AIM BLOGAL ALLIANCE, yani ile naanza ku type kua ahsante nikastukizwa attachment imetumwa kucheki ni jamaa mmoja kanyuka suti kali halafu kashikilia mi noti ya misimba pembeni kuna gari kali

Kwa chini akaweka na ujumbe naitwa mr flani ni mshiriki wa global alliance karibu kwa maswali ya namna ya kufanya ili upate pesa

Moyoni Nikajisemea "aah inamaana akili yake imeridhika kabisa na hicho kipicha kua kinatosha kua ushahidi ili mimi niwaamini?"

Hivi nini kinachowafanya wahisi watu wote wenye mionekano kama yao ni watu wenye mafanikio ya kimaisha kwa kumilika pesa nyingi? Na kwanini wamejijengea dhana potofu kwamba muonekano wa nje wa mtu husadifu hali ya kimaisha yake?

Kwanini vazi la suti wamelipa kipaumbele sana katika kuji brand ili kuwaaminisha watu kua wako serious?

Ni mfano wa bongo movies wanavyo act kua jambazi lazima awe na sura mbaya halafu avae mikoti mirefu myeusi pamoja na glass za tinted wakati ili mradi tu kuwashawishinwatu kua jamaa ni jambazi, hapo washajijengea dhana kua akikaa mshakaji ambaye ni handsome halafu havai makoti na miwani watazamaji wanaweza kua bored wasivutiwe kua haiwezekani jambazi akawa huyo mtu wakati kila ukimuangalia huonekana innocent

Lakini ukiangalia movies za hollwood utakuta sekta ya jambazi anakaa mtu yeyote yule na anafit na movie bado ipo katika ubora wake ule ule ambao hata mtazamaji hapepesi macho pembeni ya runinga.

Tunawaona matajiri wakina billget jeffbozes, jack ma na huyu mmiliki wa facebook ambaye hadi watu walimsema kwamba anarudia rudia kuvaa shati moja kila siku yenye rangi ya kijivu. Hao wote matajiri huwezi ukakuta wamepiga picha wameshika hela kama swaga, picha ambayo unaweza bahatika kuiona unakuta ni kumbukumbu siku ambayo alitoa mabilioni ya pesa kuwasaidia wasiojiweza.

Sasa hawa wa global alliance wanadai kua campuni hiyo ilianzishwa na malegend wawili huko ufilipino ambao ni mabilionea wa kidunia, lakini huji kuwakuta wakioneaha picha za hao matajiri kuwasaidia masikini wasio jiweza wakati sera ya campuni yao ni kusaidia vijana
 
Hahahaha hawa wajinga walini block kwenye whatsap

Eti karibu AIM BLOGAL ALLIANCE, yani ile naanza ku type kua ahsante nikastukizwa attachment imetumwa kucheki ni jamaa mmoja kanyuka suti kali halafu kashikilia mi noti ya misimba pembeni kuna gari kali

Kwa chini akaweka na ujumbe naitwa mr flani ni mshiriki wa global alliance karibu kwa maswali ya namna ya kufanya ili upate pesa

Moyoni Nikajisemea "aah inamaana akili yake imeridhika kabisa na hicho kipicha kua kinatosha kua ushahidi ili mimi niwaamini?"

Hivi nini kinachowafanya wahisi watu wote wenye mionekano kama yao ni watu wenye mafanikio ya kimaisha kwa kumilika pesa nyingi? Na kwanini wamejijengea dhana potofu kwamba muonekano wa nje wa mtu husadifu hali ya kimaisha yake?

Kwanini vazi la suti wamelipa kipaumbele sana katika kuji brand ili kuwaaminisha watu kua wako serious?

Ni mfano wa bongo movies wanavyo act kua jambazi lazima awe na sura mbaya halafu avae mikoti mirefu myeusi pamoja na glass za tinted wakati ili mradi tu kuwashawishinwatu kua jamaa ni jambazi, hapo washajijengea dhana kua akikaa mshakaji ambaye ni handsome halafu havai makoti na miwani watazamaji wanaweza kua bored wasivutiwe kua haiwezekani jambazi akawa huyo mtu wakati kila ukimuangalia huonekana innocent

Lakini ukiangalia movies za hollwood utakuta sekta ya jambazi anakaa mtu yeyote yule na anafit na movie bado ipo katika ubora wake ule ule ambao hata mtazamaji hapepesi macho pembeni ya runinga.

Tunawaona matajiri wakina billget jeffbozes, jack ma na huyu mmiliki wa facebook ambaye hadi watu walimsema kwamba anarudia rudia kuvaa shati moja kila siku yenye rangi ya kijivu. Hao wote matajiri huwezi ukakuta wamepiga picha wameshika hela kama swaga, picha ambayo unaweza bahatika kuiona unakuta ni kumbukumbu siku ambayo alitoa mabilioni ya pesa kuwasaidia wasiojiweza.

Sasa hawa wa global alliance wanadai kua campuni hiyo ilianzishwa na malegend wawili huko ufilipino ambao ni mabilionea wa kidunia, lakini huji kuwakuta wakioneaha picha za hao matajiri kuwasaidia masikini wasio jiweza wakati sera ya campuni yao ni kusaidia vijana
Mkuu hawa jamaa wa AIM GLOBAL mimi nilitarajia katika kipindi hiki cha janga la covid-19 wangenunua hata ventilators mbili tu waziweke mloganzila utajiri wao upo kwenye maigizo ya kupiga picha na magari ya watu na kupost ili kutumika kama chambo kwa wengine ili wavutike na kununua bidhaa zao ambazo kimsingi ndio chanzo chao cha mapato.
 
Jamaa akaanza kunipa dondoo

Mi ni mshindi wa pili kwa ukanda huu wa afrika mashariki nimevuna milion 175 za kitanzania kupitia hii kampuni. Nadhani ujumbe katika picha umeuona.

Unachotakiwa nikutoa laki5 kwa ajili ya kutengeneza pair ambayo ndio mzunguko wa pesa yako utakapokua unafanyika. Sisi tutakupa package ambayo ndani yake ina vidonge vya asili ambavyo vinauwezo wa kutibu magonjwa mbali mbali ikiwemo vifonda vya tumbo nk.

Kwaiyo hiyo package utaamua ukauze au utumie kwa faida yako, huo utakua ni uamuzi wako maana hatuna mamlaka nayo hiyo package kwasababu ishakua mali yako.

Kwaiyo ukitoa hiyo laki 5 tunakufungulia account yako halafu tunakuwekea balance la shl. 70 kama kiasi cha kuanzia kisha tunakupa na hizo package za dawa

Utachotakiwa kufanya ni wewe uanze kutafuta watu uwashawishi wajiunge watoe hiyo laki 5 kamaili utengeneze pair uanze ku-make mkwanja.

Akanikaribisha kuuliza maswali

Mimi: hii kampuni yenu mmesema imelenga kuwasaidia watu sindiyo?

Yeye: Ndiyo hususani vijana maana ndio taifa la leo

Mimi: ok na dau la kujiunga ili kupata hiyo package ndio umedai laki tano in cash au kuna malipo ya nusunusu?

YEYE: ni cash hatupokei pesa nusu

MIMI: katika kipindi hiki cha corona shughuli zangu za utafutaji zimeathiriwa sana na hili janga, nina shauku ya kujiunga na kampuni lenu je mnanisaidiaje sina mshiko?

YEYE: kwa hapo ndugu hatuwezi kukusaidia, kwasababu hiki sio kikoba wala saccos

MIMI: swala la kusaidia si lipo katika ajenda zenu na ni moja ya policy zenu katika kuitangaza kampuni yenu?

YEYE: kama ujuavyo mashirika mbali mbali yamedhurumiwa na watu kwa kukopesa pesa, wako wapi tala saizi wanalia so hatuwezi kufanya hivyo

MIMI: yani unamiliki milion 175 halafu unaogopa kukopesa laki 5 kwa kuogopa kutapeliwa? Kama unavyodai kua mchongo huu haunaga hasara kwanini uweke possibilities za kudhurumiwa?

YEYE: Unajua katika makosa ambayo hatutakiwi kufanya katika kampuni hii ni kumuamini mtu, halafu inaendekeza uzembe kwasababu watu kama wewe watakua wanakuja kukopa kila siku

MIMI: kama kuaminiana ni swala ambalo haliwezekani Mbona wewe unanishawishi mimi nikuamini nitoe pesa yangu nikupe wewe ili nije kumiliki nyingi zaidi? Huoni kwa kauli yako unanipa wasi wsi juu ya ahafi yako ambayo umeitoa muda mfupi uliopita?

YEYE: hii ni campuni ipo duniani kote swala la wewe kudhurumiwa na sisi halipo, kizuri zaidi ni kwamba kampuni yetu ishakua registered kiserikali na malipo yetu tunayafanya kupitia bank ya NMB

MIMI: Sasa kama hiyo kampuni inatambulika kiserikali basi ndo unatakiwa ufate sheria ambazo unazitangaza huku, au hizi sheria za kusaidia hazitambuliki na serikali?

YEYE: zinatambulika na ndiyo tunakusaidia ila hatukukopeshi

MIMI: Sasa kama mtu anakuja na pesa yake hapo unakua umemsaidia nini?

YEYE: Mkuu si tunakupa package ya dawa tunakua tumekusaidia afya yako

MIMI: Anhaa kama msaada wenu ni dawa ina maana member wanaotakiwa ujiunga hapo wanatakiwa wawe wagonjwa? Na je wakija wagonjwa kujiunga hiyo package mnagawa bure kuwasaidia?

YEYE: mkuu mbona huelewi?

MIMI: Haya tufanye nimeelewa, vipi kulingana na hufuma zenu zimewalenga wagonjwa sasa kulingana na situatiin ya sasa je hizo package zenu za dawa je wagonjwa wa corona nao wanajumuishwa hapo kwenye hiyo tiba yenu au?

YEYE: typing....

Blocked
 
Mkuu hawa jamaa wa AIM GLOBAL mimi nilitarajia katika kipindi hiki cha janga la covid-19 wangenunua hata ventilators mbili tu waziweke mloganzila utajiri wao upo kwenye maigizo ya kupiga picha na magari ya watu na kupost ili kutumika kama chambo kwa wengine ili wavutike na kununua bidhaa zao ambazo kimsingi ndio chanzo chao cha mapato.
Niliwajibu hovyo sana, halafu kinachokera ni usumbufu wao.
 
Jamaa akaanza kunipa dondoo

Mi ni mshindi wa pili kwa ukanda huu wa afrika mashariki nimevuna milion 175 za kitanzania kupitia hii kampuni. Nadhani ujumbe katika picha umeuona.

Unachotakiwa nikutoa laki5 kwa ajili ya kutengeneza pair ambayo ndio mzunguko wa pesa yako utakapokua unafanyika. Sisi tutakupa package ambayo ndani yake ina vidonge vya asili ambavyo vinauwezo wa kutibu magonjwa mbali mbali ikiwemo vifonda vya tumbo nk.

Kwaiyo hiyo package utaamua ukauze au utumie kwa faida yako, huo utakua ni uamuzi wako maana hatuna mamlaka nayo hiyo package kwasababu ishakua mali yako.

Kwaiyo ukitoa hiyo laki 5 tunakufungulia account yako halafu tunakuwekea balance la shl. 70 kama kiasi cha kuanzia kisha tunakupa na hizo package za dawa

Utachotakiwa kufanya ni wewe uanze kutafuta watu uwashawishi wajiunge watoe hiyo laki 5 kamaili utengeneze pair uanze ku-make mkwanja.

Akanikaribisha kuuliza maswali

Mimi: hii kampuni yenu mmesema imelenga kuwasaidia watu sindiyo?

Yeye: Ndiyo hususani vijana maana ndio taifa la leo

Mimi: ok na dau la kujiunga ili kupata hiyo package ndio umedai laki tano in cash au kuna malipo ya nusunusu?

YEYE: ni cash hatupokei pesa nusu

MIMI: katika kipindi hiki cha corona shughuli zangu za utafutaji zimeathiriwa sana na hili janga, nina shauku ya kujiunga na kampuni lenu je mnanisaidiaje sina mshiko?

YEYE: kwa hapo ndugu hatuwezi kukusaidia, kwasababu hiki sio kikoba wala saccos

MIMI: swala la kusaidia si lipo katika ajenda zenu na ni moja ya policy zenu katika kuitangaza kampuni yenu?

YEYE: kama ujuavyo mashirika mbali mbali yamedhurumiwa na watu kwa kukopesa pesa, wako wapi tala saizi wanalia so hatuwezi kufanya hivyo

MIMI: yani unamiliki milion 175 halafu unaogopa kukopesa laki 5 kwa kuogopa kutapeliwa? Kama unavyodai kua mchongo huu haunaga hasara kwanini uweke possibilities za kudhurumiwa?

YEYE: Unajua katika makosa ambayo hatutakiwi kufanya katika kampuni hii ni kumuamini mtu, halafu inaendekeza uzembe kwasababu watu kama wewe watakua wanakuja kukopa kila siku

MIMI: kama kuaminiana ni swala ambalo haliwezekani Mbona wewe unanishawishi mimi nikuamini nitoe pesa yangu nikupe wewe ili nije kumiliki nyingi zaidi? Huoni kwa kauli yako unanipa wasi wsi juu ya ahafi yako ambayo umeitoa muda mfupi uliopita?

YEYE: hii ni campuni ipo duniani kote swala la wewe kudhurumiwa na sisi halipo, kizuri zaidi ni kwamba kampuni yetu ishakua registered kiserikali na malipo yetu tunayafanya kupitia bank ya NMB

MIMI: Sasa kama hiyo kampuni inatambulika kiserikali basi ndo unatakiwa ufate sheria ambazo unazitangaza huku, au hizi sheria za kusaidia hazitambuliki na serikali?

YEYE: zinatambulika na ndiyo tunakusaidia ila hatukukopeshi

MIMI: Sasa kama mtu anakuja na pesa yake hapo unakua umemsaidia nini?

YEYE: Mkuu si tunakupa package ya dawa tunakua tumekusaidia afya yako

MIMI: Anhaa kama msaada wenu ni dawa ina maana member wanaotakiwa ujiunga hapo wanatakiwa wawe wagonjwa? Na je wakija wagonjwa kujiunga hiyo package mnagawa bure kuwasaidia?

YEYE: mkuu mbona huelewi?

MIMI: Haya tufanye nimeelewa, vipi kulingana na hufuma zenu zimewalenga wagonjwa sasa kulingana na situatiin ya sasa je hizo package zenu za dawa je wagonjwa wa corona nao wanajumuishwa hapo kwenye hiyo tiba yenu au?

YEYE: typing....

Blocked
Mkuu ulimuliza maswali makini sana! Hongera kwa hilo.Kwa sababu kama mtu ana miliki 175M anashindwa kukukopesha 500k ili nawe uanze kufanya hiyo biashara ,basi ujue hiyo biashara ina mlolongo mrefu sana na inachukua muda sana kupata mafanikio.Ingelikuwa inaleta returns kwa haraka basi wangekua wanakopesha kama kweli lengo lao ni kudaidia vijana kuondokana na hali za kiuchumi,zaidi ya hapo Inaonekana watu ndo mtaji kwao!.
 
Amejenga nyumba mkuu within this 3 yrs ! na huko Malaysia anaenda kwa pesa zake zinazotokana na juhudi zake za network marketing.Nawafahamu hao marafiki zangu miaka mitatu ya nyuma walikuwa ktk hatua gani kimaisha na sahizi wapo wapi, mmoja kati yao kapiga hela ndefu na mwaka jana kawekeza ktk kikimo chha mihogo eka 120 huko Tanga maeneo ya Mkata, kikubwa hapa naona physical progress siyo blabla ! na wanajitoa kwelikweli kufanya kazi across the whole country,upo hapo nyonyo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nenda na wewe jiunge nao upige mipesa. Ndani ya miaka minne utupe mrejesho!
 
Afu waalim ni wengi sana katika watu wanaojiunga qnet. Walishatutambia kwamba mwaka 2020 mwezi february wanaacha kazi cha ajabu wanaulizia vipi semina za kusimamia mtihani wa Taifa wa form 6 badoooo.😂😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom