Aina gani ya Nyumba inayofaa Kuchukulia Mkopo Bank?

Aina gani ya Nyumba inayofaa Kuchukulia Mkopo Bank?

Hiyo milioni 30 umeitoa wapi wakati hawajaja kukufanyia tathimini?.Haupewi mkopo kwa kiasi unavyotaka wewe.Maafisa mikopo wanakuja kwako wanatathimini mali unayoiweka kama dhamana na uwezo wa marejesho kupitia biashara mara muda wakurejesha mkopo na riba yake ndo wanakufanyia tathimini ya kiasi utakachoweza kupata.Sio lazima nyumba iliyokamilika kwasababu ata kiwanja chenye hati kuna bank zinapokea.
Mil.30 nimeitolea bank, sikuwa najua naweza pewa hicho kiasi wao ndio waliniambia kutokana na mzunguko wangu wa biashara kupitia account yangu wanaweza nipa up to 30m.

Wakaniambia tu nahitajika dhamana, ila si kwamba mimi niliwambia nataka 30m ni wao baada ya kuwaeleza nia yangu wakaniambia wanahitaji kuangalia mzunguko wa pesa kwa account yangu ndio wakanipa majibu hayo.

Flat Plot Hamna BANK wanapokea hata kama kina HATI ilikuwa ni zamani sasa hivi kiwanja lazima uwe umekiendeleza kwa kukifanyia chochote kile. Otherwise hiyo Plot unayotaka chukulia mkopo iwe Center kweli kweli (napo sina hakika kama watakubali kulingana na policy za mabank za sasa) labda unyooshe mkono.

Na maswala ya kugawa hela kwa maafisa, hela yenyewe nakopa halafu naanza igawa tena naonaga mikosi inaanziaga humo.
 
Hio 30M unahitaji ndani ya muda gani?maana hio process unayopitia naona ni ndefu
30m in 6 month ndani ya miezi 6 nina uhakika itakuwa imenizalishia faida ya kutosha na kunitunishia Mtaji wangu.

Nitawarudishia pesa yao nitabaki na biashara yangu iliyo stable tena kama mwanzo.
 
Huo ni mkopo direct wa ujenzi na kiwanja ndio dhamana na marejesho yake ni ya muda mrefu.. Hapa mara nyingi unaingia ubia na bank na marejesho huanza baada ya jengo kukamilika na kuanza biashara
Kwa kifupi pesa yote inakuwa controlled na bank, kwakuwa ujenzi kama huo hupewa mkandarasi aliyesajiliwa na kuidhinishwa na bodi ya wakandarasi
Wewe kazi yako ni kusaini tu ili jamaa alipwe na bank.. Na ukianza biashara pesa inapitia kwenye account ya bank husika

Mikopo ninayozungumzia yenye gundu ni pale biashara zinaenda vema, na una maokoto ya kutosha tu halafu unataka kupanua biashara zako bila hasa kuwa specific utautumiaje huo mkopo.. Hizo pesa huitwa mlango wazi kwakuwa ukishaitia mkononi huibuka dili ya faida ya haraka nawe bila kuwaza unajitumbukiza humo

Unakumbuka ile simulizi hapa JF ya jamaa aliyekopa 4B na sasa ni kapuku?

Sent using Jamii Forums mobile app
ID ya Mshana imevamiwa anatoa madini huu uzi. Tofauti na mada za kufikirika anazopenda
 
Ukiwa mtafutaji anza na kukopa kwenye vikundi vidogo vya kuweka na kukopa. Kule mnakutana watu like minded mnaojuana na wenye vyanzo vya mapato. Huko gharama za kukopa ni ndogo na mlolongo ni mfupi na riba sio kubwa. Na mikopo hii ina faida kubwa kuliko ya mabenki. Kisha ukizoea kulipa hiyo, biashara yako ikakuwa na ukawa na vyanzo vingi na assets nyingi ndio ukope benki mkopo mkubwa kidogo.

Mambo ya kuanza na benki waachie waajiriwa wa serikali
 
Ukiwa mtafutaji anza na kukopa kwenye vikundi vidogo vya kuweka na kukopa. Kule mnakutana watu like minded mnaojuana na wenye vyanzo vya mapato. Uko gharama za kukopa ni ndogo na mlolongo ni mfupi na riba sio kubwa. Na mikopo hii ina faida kubwa kuliko ya mabenki. Kisha ukizoea kulipa hiyo, biashara yako ikakua na ukawa na vyanzo vingi na assets nyingi ndio ukope benki mkopo mkubwa kidogo.

Mambo ya kuanza na benki waachie waajiriwa wa serikali
Mkuu bank hawana RIBA kubwa, wenye riba kubwa ni hizi microfinace zingine zingine ila amini nakwambia BANK wana riba nafuu mno tofauti na hela wanayoitoa, shida tu ni hela zao hazipatikani kirahisi.
 
ID ya Mshana imevamiwa anatoa madini huu uzi. Tofauti na mada za kufikirika anazopenda
8ca9b48fa33a3c0bb9082fcd03996df9.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bila hati Hatua pati pesa huu ni unyanyasaji
Kaka Vitus, unataka kusema kuwa unaweza kumpatia mpita njia pesa zako bila kufikiria atazirudishaje? Huo ni utaratibu tu wa Bank na Financial Bodies zenye kusaidia WAJASI.

Nawashukuru kwa kupata uzoefu wa kupata mkopo kupitia bank. Ngoja kwanza niendelee na vicoba hadi pale nitakapopata nguvu mpya, ari mpya na kasi mpya. Subira yavuta heri.
 
mkopo wa nyumba au mali isiyohamishika unazingatua zaidi thamani ya mali husika.

huwezi jenga nyumba ya milioni 3,thamani ya kiwanja(eneo) milioni 5,ukapewa mkopo wa milioni 10,una nyumba ya thamanj angarau 50mln basi mkopo wa 30 milion utapata.kumbuka hiyo ni dhamana lazima izingatie rejesho kamili la mkopo na gharama zake kwanza,ndipo afisa mkopo husika atatoa greenlight ya mkopo kupitishwa.
Mikopo inahitaji nidhamu sana, kuna jirani yangu amechukua mkopo ameweka dhamana nyumba ila sasa kakimbilia kula bata Tangaaaa!!!!
 
maaana yangu ni waangalie madharti tu mkuu,mbona kwenye simu online siku hiz kuna vimikopo na app zipo kibao unaanza kopa anzia kias kidogo hvyo hvyo hadi unapanda kwa kujidhamini mwenyewe tu,kwann bank wao wanashindwa?
Hiyo mikopo ya sijuwi M PESA na nduguze nayo wana ku test na viela kidooogo. Usipolipa wanakeketa kwenye salio na maokoto yoyote yatakayoingia kwenye App. Hata hivyo, wanavyo vigezo lukuki kuidhinisha mtonyo kukufikia na siyo kirahisi kama unavyofikiri. Wanafuatilia mazoea yako na line unayoitumia, intensity ya transaction unazofanya mara kwa mara n.k.

Ndugu yangu,
Kwa turn over ya mil 150; nakusihi uushinde moyo wako na endelea tu na biashara huku ukiomba heri. Anza kuweka milioni moja kila mwezi na ndani ya mwaka utakuwa umefikia malengo yako.
 
Kaka Vitus, unataka kusema kuwa unaweza kumpatia mpita njia pesa zako bila kufikiria atazirudishaje? Huo ni utaratibu tu wa Bank na Financial Bodies zenye kusaidia WAJASI.

Nawashukuru kwa kupata uzoefu wa kupata mkopo kupitia bank. Ngoja kwanza niendelee na vicoba hadi pale nitakapopata nguvu mpya, ari mpya na kasi mpya. Subira yavuta heri.
😄😄
 
Back
Top Bottom