#COVID19 Aina mpya, hatari zaidi, ya Kirusi cha Corona yagunduliwa Afrika Kusini

#COVID19 Aina mpya, hatari zaidi, ya Kirusi cha Corona yagunduliwa Afrika Kusini

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Mamlaka nchini Afrika Kusini zimeripoti kuwepo kwa aina mpya ya Virusi vya Corona, B.1.1.529, ambavyo ni tofauti na aina zingine za virusi vinavyofahamika.

Mkuu wa Kitengo cha Magonjwa ya Mlipuko nchini Afrika Kusini, Prof. Tulio de Oliveira amesema kuwa kirusi hicho kipya kina zaidi ya mabadiliko (mutation) 50 kwa ujumla na mabadiliko mengine 30 katika muundo wa protini ambayo ndio shabaha kuu ya chanjo na njia ya virusi hivyo kuingia katika seli zetu za mwili.

Baadhi ya mataifa duniani yamekwishaanza kuchukua tahadhari dhidi ya Kirusi hiki kipya, ikiwamo Uingereza ambayo imetangaza kuweka zuio la muda la kusafiri kwa mataifa sita ya Afrika Kusini, Namibia, Zimbabwe, Botswana, Lesotho na Eswatini, huku wasafiri wanaofika wakilazimika kukaa karantini.

Waziri wa Afya wa Uingereza, Sajid Javid amesema kuwa wasiwasi wa kirusi hiki unatokana na idadi kubwa ya mabadiliko (mutation), ikitajwa kuwa mara mbili ya kirusi cha Delta pamoja na uwezekano wa chanjo kushindwa kuhimili kirusi hiki, huku akionya kuwa uwezekano wa kutokea kwa maambukizi ni mkubwa kuliko aina zingine za virusi vya corona.

Mpaka sasa kuna jumla ya maambukizi 77 yaliyoripotiwa katika Jimbo la Gauteng pekee nchini Afrika Kusini, maambukizi 4 nchini Botswana na moja nchini Hong Kong, ambayo ni ya msafiri aliyetoka nchini Afrika Kusini.

Kuna wasiwasi kuwa kirusi hicho kinaweza kuwa kimesambaa zaidi, huku ikikadiriwa kuwa maambukizi yote yanayoripotiwa katika jimbo la Gauteng yanaweza kuwa ya aina hii mpya ya Kirusi, huku maambukizi yakikadiriwa kuwa yamesambaa katika majimbo mengine.

UPDATE: MATAIFA YACHUKUA HATUA KUKABILIANA NA AINA MPYA YA KIRUSI

Baada ya Afrika Kusini kuripoti aina mpya ya Kirusi cha Corona, Mataifa kadhaa yakiwemo Singapore, Ufaransa, Kenya na Japan yametangaza kuchukua hatua kukabiliana nacho

Ufaransa, Uholanzi na Japan zimetangaza kuzuia safari za ndege kutoka Afrika Kusini na Nchi jirani. Israel, Singapore na Italia zimeiweka Afrika Kusini, Botswana, Namibia, Zimbabwe, Lesotho na Eswatini kwenye orodha ya Nchi hatari

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema itachukua wiki kadhaa kuelewa madhara ya Kirusi hicho ambacho kwa sasa kinafahamika kama B.1.1.529
 
tulisha yasema haya kuwa haya majanga tutaendele kwenda nayo mpka walioyaleta warizike,

na huo ni mwanzo tu, kuna makubwa na yakutisha yanakuja mbelen ambayo yatageuza mitindo ya maisha ya wanadamu dunian.

hofu nying zitatanda huku kila mtu hajui wap atakapoponea, nasisitiza tena huu ni mwanzo tu, makubwa na yakutisha yanakuja na lazima yaje, ili hata wale wapumbav waliokuwa wakipinga kuwa hii dunia haimilikiwi na watu wachache waamini ukwel,

hamjachelewa ndugu zanguni huu ndyo wakat sahh wakuyapanga maisha yako sawa, na uzao wako sawa, maana yambeleni huyajui, maisha tunayoish leo, si yale watakayoish wazawa wa baadae.

dunia si sehem salama hata kidogo, huu ndyo wakat wa kama waafrika kuungana na kutokomeza hira zote za hao wakoloni wetu, huu si muda wakushadadia ujinga na upumbav...tuamke jamani
 
Ugonjwa unadhidi kuwa hatari,, ila hatuogopi tena. Liwalooo na liweee
 
tulisha yasema haya kuwa haya majanga tutaendele kwenda nayo mpka walioyaleta warizike,

na huo ni mwanzo tu, kuna makubwa na yakutisha yanakuja mbelen ambayo yatageuza mitindo ya maisha ya wanadamu dunian.

hofu nying zitatanda huku kila mtu hajui wap atakapoponea, nasisitiza tena huu ni mwanzo tu, makubwa na yakutisha yanakuja na lazima yaje, ili hata wale wapumbav waliokuwa wakipinga kuwa hii dunia haimilikiwi na watu wachache waamini ukwel,

hamjachelewa ndugu zanguni huu ndyo wakat sahh wakuyapanga maisha yako sawa, na uzao wako sawa, maana yambeleni huyajui, maisha tunayoish leo, si yale watakayoish wazawa wa baadae.

dunia si sehem salama hata kidogo, huu ndyo wakat wa kama waafrika kuungana na kutokomeza hira zote za hao wakoloni wetu, huu si muda wakushadadia ujinga na upumbav...tuamke jamani
HAPA HAKUNA NAMNA ZAIDI YA SISI WAAFRIKA KUUNGANA! Tatizo walafi wa madaraka wako tayari!!?
 
Katika classification za corona virus kuna virus of concern and virus of interest.

Virus of concern ni virus hatarishi zaidi kama ilivyokuwa delta virus na hiki cha sasa wataalam wanatoa taarifa kuna ni hatari zaidi ya delta.

Mbaya zaidi kimeanza kutokea kwa majirani zetu uko kusini mwa Africa na inawezekana hata hapa TZ kimeanza kusambaa na soon watu wataanza kuugua na kufa kwa wingi wakati tunaendelea na utamaduni wetu wa kuficha taarifa au kutoa taarifa fake.

Wakati nchi za mbali kama US UK European Union zikichukua hatua kali za kutokupokea wageni toka nchi za kusini mwa Africa TZ kupitia wizara husika ya Afya tuko kimya na si ajabu ATC inakwenda South Africa kubeba waathirika na kuleta TZ.

Wizara ya afya inabidi haraka sana mtoe tamko kuhusu tahadhali za hii corona virus mpya ili kupunguza madhara kwani nchi yetu waliopata chanjo ni wachache sana kama nchi nyingine za Africa
 
V
Katika classification za corona virus kuna virus of concern and virus of interest.

Virus of concern ni virus hatarishi zaidi kama ilivyokuwa delta virus na hiki cha sasa wataalam wanatoa taarifa kuna ni hatari zaidi ya delta.

Mbaya zaidi kimeanza kutokea kwa majirani zetu uko kusini mwa Africa na inawezekana hata hapa TZ kimeanza kusambaa na soon watu wataanza kuugua na kufa kwa wingi wakati tunaendelea na utamaduni wetu wa kuficha taarifa au kutoa taarifa fake.

Wakati nchi za mbali kama US UK European Union zikichukua hatua kali za kutokupokea wageni toka nchi za kusini mwa Africa TZ kupitia wizara husika ya Afya tuko kimya na si ajabu ATC inakwenda South Africa kubeba waathirika na kuleta TZ.

Wizara ya afya inabidi haraka sana mtoe tamko kuhusu tahadhali za hii corona virus mpya ili kupunguza madhara kwani nchi yetu waliopata chanjo ni wachache sana kama nchi nyingine za Africa
Vitisho tu yanakuja yanaenda...........huu ugonjwa wakuwatisha labda hao mabepari ila sio sie hizi habari marudio tu......tumeshazoea
 
tulisha yasema haya kuwa haya majanga tutaendele kwenda nayo mpka walioyaleta warizike,

na huo ni mwanzo tu, kuna makubwa na yakutisha yanakuja mbelen ambayo yatageuza mitindo ya maisha ya wanadamu dunian.

hofu nying zitatanda huku kila mtu hajui wap atakapoponea, nasisitiza tena huu ni mwanzo tu, makubwa na yakutisha yanakuja na lazima yaje, ili hata wale wapumbav waliokuwa wakipinga kuwa hii dunia haimilikiwi na watu wachache waamini ukwel,

hamjachelewa ndugu zanguni huu ndyo wakat sahh wakuyapanga maisha yako sawa, na uzao wako sawa, maana yambeleni huyajui, maisha tunayoish leo, si yale watakayoish wazawa wa baadae.

dunia si sehem salama hata kidogo, huu ndyo wakat wa kama waafrika kuungana na kutokomeza hira zote za hao wakoloni wetu, huu si muda wakushadadia ujinga na upumbav...tuamke jamani
Hutaeleweka na wengi, dunia imejaa programmed people ambao hata uwaambieje, bado tumaini lao litabakia kutegemea serikali, Yesu, Mungu, Mtume Mohd, Allah na deities wengineo.
Hawajishughulishi kutaka kujua taarifa, na watoa taarifa kama wewe siku zote hulaaniwa.
Hey people, emancipate your self from mental slavery, and no one can help you than yourself.
Aliimba Mvuta bange, Bob Marley

Huyo huyo mvuta bange aliimba "Babylon system is a vampire, sucking the blood of sufferers
 
Tusitishane watu tumepoteza wapendwa wengi tu kwa magonjwa mengine pia, hili halina maajabu ....hujitambui wewe na makondoo wenzio
Utafaninishaje magonjwa mengine na pandemic au haulewi pandermic ni nini
 
Utafaninishaje magonjwa mengine na pandemic au haulewi pandermic ni nini
Ishu ni kufa......nimeona magonjwa yanayoua haraka na idadi kubwa ya watu kuliko huo utopolo wenu wa corona....ishu kama ni pandemic hata kua likondoo nayo ni pandemic.......acheni kusambaza hofu na hayo mafua
 
tulisha yasema haya kuwa haya majanga tutaendele kwenda nayo mpka walioyaleta warizike,

na huo ni mwanzo tu, kuna makubwa na yakutisha yanakuja mbelen ambayo yatageuza mitindo ya maisha ya wanadamu dunian.

hofu nying zitatanda huku kila mtu hajui wap atakapoponea, nasisitiza tena huu ni mwanzo tu, makubwa na yakutisha yanakuja na lazima yaje, ili hata wale wapumbav waliokuwa wakipinga kuwa hii dunia haimilikiwi na watu wachache waamini ukwel,

hamjachelewa ndugu zanguni huu ndyo wakat sahh wakuyapanga maisha yako sawa, na uzao wako sawa, maana yambeleni huyajui, maisha tunayoish leo, si yale watakayoish wazawa wa baadae.

dunia si sehem salama hata kidogo, huu ndyo wakat wa kama waafrika kuungana na kutokomeza hira zote za hao wakoloni wetu, huu si muda wakushadadia ujinga na upumbav...tuamke jamani
Ninacho jiuliza mara kwa mara kwa nini Africa Kusini mara nyingi ndiko kunako zuka variant mpya za virus vya kovid-19 kuna nini huko, je,kuna maabara za siri za kibailojia za jeshi la magharibi zinazo jihusisha na ujinga huu, kwa nini mleta taarifa anazungumzia masuala ya chanjo, ni as if anaona chanjo hazichangamukiwi kwa wingi hivyo wana genetically manipulate virus ili wazalishe virus ambavyo na hatari zaidi walete taharuki ili solo LA chanjo liongezeke exponentially au wana ajenda za kutumaliza kiana baada ya kugunduwa kwamba waafrika hatuathiriki sana kwa virus vya Covid, wakabuni plan "B".

Kitu kingine cha kutilia shaka sana kinahusu Bill Gates ambaye miaka ya karibuni amewekeza sana nchini Afrika kusini na Dunia inajuwa misimamo yake hasi ie wa kishenzi kuhusu jinsi ya ku-deal na ongezeko la binadamu Duniani, pamoja mbinu zake na mamillionea wenzake ya jinsi ya kupunguza idadi ya watu Duniani mbinu zake zinajulikana, na katika hilo Bill Gates na wenzake wako dead serious na harakati zao za kupunguza idadi ya watu Duniani hasa ambao wana wachukulia kwamba hawachangii chochote cha maana katika kuendeleza ustawi na maendeleo ya sayansi na teknolijia ili kusaidia binadamu wenzao Duniani - watu kama hao kwa Bill Gates anawachukulia kama ni expendable. Vile vile Billionea wa kampuni kubwa ya uuzaji products kwa njia ya mtandao (Amazon) nae kawekeza kwa wingi nchini Afrika - swali ni: kwa nini???

Viongozi wa mataifa ya kiafrika wa form task force ya ku-probe kinacho endelea kwenye maabara zinazo kuwa funded na Bill Gates na wenzake pamoja na zile zanazo kuwa funded na US Intel agencies.
 
Back
Top Bottom