Aina ya uongozi wa Rais Samia unafaa kwenye nchi au taifa lenye taasisi imara na huru lililojengwa katika msingi imara wa Kikatiba

Aina ya uongozi wa Rais Samia unafaa kwenye nchi au taifa lenye taasisi imara na huru lililojengwa katika msingi imara wa Kikatiba

Mimi ninachoamini, hata mtu kuwa katikati ya mfumo mbaya, lakini anaweza kusimama mwenyewe kwa misingi yake akajitenga na huo mfumo mbovu akafanya mambo yake na jamii ya watanzania anayoiongoza ikamuelewa.

Chukulia mfano wa Magufuli, ulizuka mtindo wa kuita serikali ya Magufuli na CCM ya Magufuli, hii ilikuwa na maana kwamba, CCM na serikali vyote vilikuwa vinaendeshwa kwa mtazamo na maono ya Magufuli, hapa ndipo unapoita udhaifu wa sheria na Katiba kwenye andiko lako.

Utaona wazi kwamba, kumbe huo udhaifu wa sheria na Katiba unaweza kutumia na kiongozi aliyepo madarakani either positively au negatively, zile sheria ziko pale kwenye maandishi lakini mtekelezaji ndie anaebeba huo mzigo wa udhaifu wake, hasa ukizingatia anaweza kuugeuza huo udhaifu ukaonekana na manufaa kwa jamii anayoiongoza.

Sasa turudi kwa Samia, naona umeamua kutupia lawama zako zote kwa wasaidizi wake, kwamba wao ndio chanzo cha makosa anayofanya Samia.

Na makosa hayo ni mengi, kuanzia zile teuzi zake, anateua leo anatengua kesho ambapo hiyo tabia imekuwa ikijirudia mara kwa mara toka alipoapishwa. Sasa kwa hali ya kawaida alitakiwa aone kama hawa wasaidizi wangu wananipotosha nakosea kila wakati, ni bora nifanye mambo yangu kwa mtazamo na maamuzi yangu.

Nchi yetu na Katiba tuliyonayo inampa hayo mamlaka na nguvu za kufanya hivyo kama tulivyoona kwa mtangulizi wake (Magufuli). Tujiulize kwa nini asifanye hivyo?

Hapo utapata jibu moja kwamba Samia either ni mvivu asietaka kufuatilia mambo kwa karibu, au anapuuzwa na wasaidizi wake.

Kuhusu kupuuzwa na wasaidizi wake, kuna zile tetesi zilizoenea wakati wa kifo cha Magufuli, kwamba alikuwa akifichwa taarifa za msingi za kifo cha Magufuli na kuna mambo yaliyokuwa yakiendelea chini chini ili kumuondoa kwenye nafasi yake ya VP awekwe mwingine.

Hapa utapata picha kwamba, kama hawa waliokuwa wakimficha hizo taarifa bado wamemzunguka mpaka leo, basi tutegemee mabaya zaidi mbeleni, angetakiwa kuwaondoa hawa wote mapema alipoapishwa aweke watu wake afanye nao kazi.

Hilo la uvivu naliacha kila mmoja afikirie kwa namna yake, hasa akizingatia kule Samia alipotokea, tabia za watu wa kule, na mengineyo.
 
"Bora amalizie maika yake ya urithi"



Nilimsikia dereva akinyonga usukani akilalamikia kupanda kwa mafuta.
 
Watanzania hatujui tunataka nini, kwa hali hii hata akiletwa aliyewahi kuwa best president USA basi usishangae jamaa zetu wakamuita kilaza hana uwezo na kejeli zote.....kuna hatari watu hawa hata wote tukachagua yule ambaye ni chaguo lao wakaja kusema naye ni kilaza hatufai...
Hakika ndivyo atakavyokuwa...!

Kwani tangu lini unga wa sembe safi ukatoa ugali safi kama maji unayotumia kuchanganyia huo unga motoni game hang any ikan a na tope...?

Ndivyo ilivyo, hata tukipata Rais mwema na msafi wa viwango vyote akipewa nchi hii chini ya mfumo wa utawala wa kisheria na kikatiba huu tulionao, lazima atakuwa mchafu na asiyefaa tu ndani ya muda mfupi....!!!

Hujaelewa tu tuna maana gani kusema hivyo?

Tunahitaji KATIBA MPYA YA WANANCHI ili kuchuja na kuondoa tope lote lililopo ndani ya hii ya 1977...
 
Mimi ninachoamini, hata mtu kuwa katikati ya mfumo mbaya, lakini anaweza kusimama mwenyewe kwa misingi yake akajitenga na huo mfumo mbovu akafanya mambo yake na jamii ya watanzania anayoiongoza ikamuelewa.

Chukulia mfano wa Magufuli, ulizuka mtindo wa kuita serikali ya Magufuli na CCM ya Magufuli, hii ilikuwa na maana kwamba, CCM na serikali vyote vilikuwa vinaendeshwa kwa mtazamo na maono ya Magufuli, hapa ndipo unapoita udhaifu wa sheria na Katiba kwenye andiko lako.

Utaona wazi kwamba, kumbe huo udhaifu wa sheria na Katiba unaweza kutumia na kiongozi aliyepo madarakani either positively au negatively, zile sheria ziko pale kwenye maandishi lakini mtekelezaji ndie anaebeba huo mzigo wa udhaifu wake, hasa ukizingatia anaweza kuugeuza huo udhaifu ukaonekana na manufaa kwa jamii anayoiongoza.

Sasa turudi kwa Samia, naona umeamua kutupia lawama zako zote kwa wasaidizi wake, kwamba wao ndio chanzo cha makosa anayofanya Samia.

Na makosa hayo ni mengi, kuanzia zile teuzi zake, anateua leo anatengua kesho ambapo hiyo tabia imekuwa ikijirudia mara kwa mara toka alipoapishwa. Sasa kwa hali ya kawaida alitakiwa aone kama hawa wasaidizi wangu wananipotosha nakosea kila wakati, ni bora nifanye mambo yangu kwa mtazamo na maamuzi yangu.

Nchi yetu na Katiba tuliyonayo inampa hayo mamlaka na nguvu za kufanya hivyo kama tulivyoona kwa mtangulizi wake (Magufuli). Tujiulize kwa nini asifanye hivyo?

Hapo utapata jibu moja kwamba Samia either ni mvivu asietaka kufuatilia mambo kwa karibu, au anapuuzwa na wasaidizi wake.

Kuhusu kupuuzwa na wasaidizi wake, kuna zile tetesi zilizoenea wakati wa kifo cha Magufuli, kwamba alikuwa akifichwa taarifa za msingi za kifo cha Magufuli na kuna mambo yaliyokuwa yakiendelea chini chini ili kumuondoa kwenye nafasi yake ya VP awekwe mwingine.

Hapa utapata picha kwamba, kama hawa waliokuwa wakimficha hizo taarifa bado wamemzunguka mpaka leo, basi tutegemee mabaya zaidi mbeleni, angetakiwa kuwaondoa hawa wote mapema alipoapishwa aweke watu wake afanye nao kazi.

Hilo la uvivu naliacha kila mmoja afikirie kwa namna yake, hasa akizingatia kule Samia alipotokea, tabia za watu wa kule, na mengineyo.

1. Ndivyo ilivyo, kama hawa waliokuwa wa Magufuli ndio wataendelea kumzunguka, basi tutegemee the worst...

2. Kwamba aweza kutumia udhaifu wa kisheria na kikatiba kufanya mambo mazuri kwa kutumia busara na hekima yake?

HAPANA, si rahisi na pengine haiwezekani kabisa...!!

Kwa sababu, kiasili binadamu ni mtu avutwaye na tamaa ya kupenda madaraka na kutawala wengine na huweza kuvuka mipaka na akatumia nguvu zake za kimamlaka kutaka kulazimisha anaowatawala wamwabudu...

3. Hivyo, ili kumwokoa asiingie kwenye maangamizi yake mwenyewe na kuwaangamiza wengine, ni lazima awekewe mipaka mikali ya kisheria ili aweze kuongozà wanadamu wenzake kwa haki bila kuwaonea akijua kuwa akivuka mipaka hiyo, adhabu yake inakuwa inamtazama...!!

3. Akili na hekima yake pekee haiwezi kuwa msaada wake. Binadamu kamwe hawezi kutumia udhaifu wa sheria na kikatiba kuleta uchanya katika jamii...

The bitter truth ni kwamba, binadamu hawezi kujiongoza kwa kutumia akili na maarifa yake mwenyewe. Lazima amtegemee Mungu...

Walipo wawili au watu na wakakubaliana pamoja kwa wema, basi Mungu yuko katikati yao. Yaani makubaliano hayo yana baraka za Mungu mwenyewe...

Katiba ni sheria mama ya nchi. Katiba ni mapatano na makubaliano ya watanzania wote ya jinsi wanavyotaka kujitawala na kuendesha mambo ya nchi yao kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiuchumi. Mungu atakuwa ndani ya makubaliano hayo...!!
 
Back
Top Bottom