Mad Max
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 26,961
- 77,890
Wakuu.
Kwa wapenzi wa pikipiki kwa matumizi binafsi, unapendelea aina ipi? Au umewahi kumiliki aina ipi? Yepi mazuri na mabaya ya iyo aina? Ulinunua wapi na bei vipi?
Baadhi ya aina ambazo mimi nimekutana nazo na kua na experience nazo kidogo ni hizi chache:
Sport Bikes
Nazipenda muonekano wako, very aggressive na unavyoendesha unalala. Nilikua nayo CBR600RR ni nzuri lakini sishauri kwa mtu anaetaka first bike.
Chagua yenye cc ndogo mfano Yamaha R15 (usimix na R1), KTM RC390
Ukiweka na Akaprovic exhaust lazima mtaani wakuwekee kikao.
Ubaya wake ukiangusha mara moja tu ayo maplastic (fairings) yanapasuka, hapo kuyapata msala inabidi uagize or ndio uanze kuyaunga unga kama simtank lililotoboka.
Sport bikes nyingi tunauziana used hapa, kuna wahindi town wanaagiza nje na pia kama unaweza kufuata Zanzibar jambo jema.
Bei ni kuanzia Mil 3.5 used hadi 20+ kutegemeana na brand, engine size, mwaka nk.
Mfano hii nimeikuta inauzwa Mil 10. Sio mbaya ila pia ni bei ghali kama hauna mapenzi na pikipiki.
TVS hawa hawa wanaotengeneza izi pikipiki wana chuma kizuri sana kinaitea Apache RR-310, sema wanakibania kutuletea Tanzania.
Nadhani kwa bei zao elekezi, tungefanikiwa kuendesha Sport bikes kwa chini ya Mil 6 mpyaa.
Naked Bikes
Hizi ni pacha wa sport bikes, ila zimekua zimeondolewa ayo maplastic ya pembeni.
Mfano, KTM RC390 naked wake ni KTM Duke 390.
Honda yeye ana CB150R ni tamu sana hii chuma.
Yamaha anakuaga na MT series nk.
Hizi tofauti na Sports bike, zenyewe unaendesha ukiwa wima kabisa. So, maumivu ya mgongo kwa safari ndefu hauwezi yasikia sana.
Hizi unaweza kununua Mpya, mfano TVS RTR 160 na 180 4V zilikua zinauzwa Mil 3.5 hapa hapa Tanzania, kama zinepanda sahivi zitakua Mil 4.5 hivi.
Kwa muonekano sio haba, na ni nzuri pia ukichukulia zinatoka kwa reputable brand.
King Lion nae hayupo nyuma, ana vyuma vyake unaweza pata uka enjoy kipyaaa kabisa au used, kwa chini ya Mil 3.5 hivi.
Sema ujinga wa baadhi ya brands mfano iyo juu, unakuta ni kaunga unga kanunua kutoka China yeye kaziita King Lion, ukiitani spare ndio utazijua rangi zote.
Dirt Bikes
Hivi vinakuaga na cc ndogo na ni kwaajili ya off-road na michezo ya ajabu ajabu.
KTM kateka sana soko hapa kwa Enduro, SX na SX-F series. Hizi wengi wanazitumia kama second bike kwaajili ya off-road na kucheza na matope.
Yamaha na Honda pia wana dirty zao, imara na nzuri sana
Hizi sio common kununua kwaajili ya trip ya mjini au kazini utaonekana wa ajabu labda mishe zako ziwe pori kwa pori. Pia sio common kipiga trip ndefu.
Used ni chini ya Mil 5 kwa brand za KTM na Yamaha ila kuna brand za kichina izo sina uzoefu.
Scooters
Hizi Scoter ni ndogo na slow, ni kwa misele ya mjini na siku hizi wakina mama wapambanaji wanazipigania sana.
Kama mishe zako Kariakoo au mji uliojazana sana unaweza pambania haka. Mali safi sana.
Kwa wenyeji wa Zanzibar mashahidi kule ni moja ya usafiri maarufu sana unaotumiwa na wanaume kwa wanamama.
Nazo zipo za bei ndogo kuanzia Mil 2 na kwenda juu hadi 8 na zaidi.
Kama unapenda au una miliki pikipiki za matairi mawili au manne unaweza share experience.
Edit 1:
Standard Bikes
Hizi ni kundi la pikipiki za kawaida ambazo uwa tunapishana nazo kila siku, na zinatumiwa sana na maafisa usafirishaji (bodaboda).
Unaweza kuzichanganya na naked bikes au na cáfe racer ila izi nyingi zinakua na cc ndogo 150 kushuka.
Unavoendesha unakua umekaa wima, tofauti na sports ambazo unalala, na wengi wanashauri ziwe beginner bike.
Mfano kwa Tanzania, Boxer BM-150, TVS, Kibao cha Mbuzi, Haojue, San LG nk.
Hizi pikipiki zilivyoshoot bei hakuna anaelewa. Zamani zilikua 1.6 hadi 1.8 millions, ila sahivi mpya nyingi ni Mil 2.5 hadi Mil 3.
Used zipo za kuanzia Laki 7 kuendelea, ila lazima zitakua na changamoto.
Touring/ Sport Touring Bikes.
Kama jina linavyosema, haya ni mapikipiki kwaajili ya masafa, na wote wawili wewe na abiria wako mkikaa mnakua comfortable tofauti na pikipiki zingine, kwahiyo mnaweza ata kusafiri distance kubwa.
Nyingi zinakuaga na cc kubwa, fairings, tank kubwa za mafuta, vioo kwa mbele kupunguza madhara ya upepo na uzito wake unafika hadi kg 250 kuendelea.
Kwa wapenzi wa pikipiki kwa matumizi binafsi, unapendelea aina ipi? Au umewahi kumiliki aina ipi? Yepi mazuri na mabaya ya iyo aina? Ulinunua wapi na bei vipi?
Baadhi ya aina ambazo mimi nimekutana nazo na kua na experience nazo kidogo ni hizi chache:
Sport Bikes
Nazipenda muonekano wako, very aggressive na unavyoendesha unalala. Nilikua nayo CBR600RR ni nzuri lakini sishauri kwa mtu anaetaka first bike.
Chagua yenye cc ndogo mfano Yamaha R15 (usimix na R1), KTM RC390
Ukiweka na Akaprovic exhaust lazima mtaani wakuwekee kikao.
Ubaya wake ukiangusha mara moja tu ayo maplastic (fairings) yanapasuka, hapo kuyapata msala inabidi uagize or ndio uanze kuyaunga unga kama simtank lililotoboka.
Sport bikes nyingi tunauziana used hapa, kuna wahindi town wanaagiza nje na pia kama unaweza kufuata Zanzibar jambo jema.
Bei ni kuanzia Mil 3.5 used hadi 20+ kutegemeana na brand, engine size, mwaka nk.
Mfano hii nimeikuta inauzwa Mil 10. Sio mbaya ila pia ni bei ghali kama hauna mapenzi na pikipiki.
TVS hawa hawa wanaotengeneza izi pikipiki wana chuma kizuri sana kinaitea Apache RR-310, sema wanakibania kutuletea Tanzania.
Nadhani kwa bei zao elekezi, tungefanikiwa kuendesha Sport bikes kwa chini ya Mil 6 mpyaa.
Naked Bikes
Hizi ni pacha wa sport bikes, ila zimekua zimeondolewa ayo maplastic ya pembeni.
Mfano, KTM RC390 naked wake ni KTM Duke 390.
Honda yeye ana CB150R ni tamu sana hii chuma.
Yamaha anakuaga na MT series nk.
Hizi tofauti na Sports bike, zenyewe unaendesha ukiwa wima kabisa. So, maumivu ya mgongo kwa safari ndefu hauwezi yasikia sana.
Hizi unaweza kununua Mpya, mfano TVS RTR 160 na 180 4V zilikua zinauzwa Mil 3.5 hapa hapa Tanzania, kama zinepanda sahivi zitakua Mil 4.5 hivi.
Kwa muonekano sio haba, na ni nzuri pia ukichukulia zinatoka kwa reputable brand.
King Lion nae hayupo nyuma, ana vyuma vyake unaweza pata uka enjoy kipyaaa kabisa au used, kwa chini ya Mil 3.5 hivi.
Sema ujinga wa baadhi ya brands mfano iyo juu, unakuta ni kaunga unga kanunua kutoka China yeye kaziita King Lion, ukiitani spare ndio utazijua rangi zote.
Dirt Bikes
Hivi vinakuaga na cc ndogo na ni kwaajili ya off-road na michezo ya ajabu ajabu.
KTM kateka sana soko hapa kwa Enduro, SX na SX-F series. Hizi wengi wanazitumia kama second bike kwaajili ya off-road na kucheza na matope.
Yamaha na Honda pia wana dirty zao, imara na nzuri sana
Hizi sio common kununua kwaajili ya trip ya mjini au kazini utaonekana wa ajabu labda mishe zako ziwe pori kwa pori. Pia sio common kipiga trip ndefu.
Used ni chini ya Mil 5 kwa brand za KTM na Yamaha ila kuna brand za kichina izo sina uzoefu.
Scooters
Hizi Scoter ni ndogo na slow, ni kwa misele ya mjini na siku hizi wakina mama wapambanaji wanazipigania sana.
Kama mishe zako Kariakoo au mji uliojazana sana unaweza pambania haka. Mali safi sana.
Kwa wenyeji wa Zanzibar mashahidi kule ni moja ya usafiri maarufu sana unaotumiwa na wanaume kwa wanamama.
Nazo zipo za bei ndogo kuanzia Mil 2 na kwenda juu hadi 8 na zaidi.
Kama unapenda au una miliki pikipiki za matairi mawili au manne unaweza share experience.
Edit 1:
Standard Bikes
Hizi ni kundi la pikipiki za kawaida ambazo uwa tunapishana nazo kila siku, na zinatumiwa sana na maafisa usafirishaji (bodaboda).
Unaweza kuzichanganya na naked bikes au na cáfe racer ila izi nyingi zinakua na cc ndogo 150 kushuka.
Unavoendesha unakua umekaa wima, tofauti na sports ambazo unalala, na wengi wanashauri ziwe beginner bike.
Mfano kwa Tanzania, Boxer BM-150, TVS, Kibao cha Mbuzi, Haojue, San LG nk.
Hizi pikipiki zilivyoshoot bei hakuna anaelewa. Zamani zilikua 1.6 hadi 1.8 millions, ila sahivi mpya nyingi ni Mil 2.5 hadi Mil 3.
Used zipo za kuanzia Laki 7 kuendelea, ila lazima zitakua na changamoto.
Touring/ Sport Touring Bikes.
Kama jina linavyosema, haya ni mapikipiki kwaajili ya masafa, na wote wawili wewe na abiria wako mkikaa mnakua comfortable tofauti na pikipiki zingine, kwahiyo mnaweza ata kusafiri distance kubwa.
Nyingi zinakuaga na cc kubwa, fairings, tank kubwa za mafuta, vioo kwa mbele kupunguza madhara ya upepo na uzito wake unafika hadi kg 250 kuendelea.