Air Tanzania yadai uhaba wa Injini umesababisha Ndege kukaa muda mrefu Karakana Malaysia

Kwa kifupi nimemaanisha kuwa kinachotokea kwenye hizi ndege ni matokeo ya planning na uendeshaji mbovu wa serikali na shirika lakini siyo tatizo kutoka kwenye Boeing per se. Air Tanzania ina ndege za kampuni tofuati tofauti lakini kila siku kunawa na sababu za kijinga za kuhalalisha ndege inaposhindwa kufanya kazi.
 
Inawezekana ila Engine za Boieng zipo kwenye shida kidogo naona mashirika mengi wanalalamika..
 
Inawezekana ila Engine za Boieng zipo kwenye shida kidogo naona mashirika mengi wanalalamika..
Boeing wameingia kwenye lawama mbali mbali hasa kuhusu usalama wa baadhi ya ndege ila tukurudi nyuma. ni shirika lililokuwa na linaaminika. Hivyo basi hata walipokuwa wanaagiza hizi dreamliners wasingeweza ku-forecast kuwa kutakuja kuwa na matatizo.
 
CEO ATCL tunaomba kujua kuwa kuna ndege ngapi zinaruka na ndege ngapi zipo kwenye maintenance ndani ya nchi na nje ya nchi. Ushauri wa bure achieve ngazi kabla mambo kuwa mabaya zaidi. Story zimezidi.
 
Boeing wameingia kwenye lawama mbali mbali hasa kuhusu usalama wa baadhi ya ndege ila tukurudi nyuma. ni shirika lililokuwa na linaaminika. Hivyo basi hata walipokuwa wanaagiza hizi dreamliners wasingeweza ku-forecast kuwa kutakuja kuwa na matatizo.
Kwa hiyo ununuzi wa ndege ni bora ya Gari yaani unanunua ndge haijapita hata miaka kumi hakuna Warant yeyote ikiharibika ni kama umenunuq simu Mtaa Kongo acheni utani na fedha ndugu zangu...
 
Ndiyo maana ya ku-employ consultants expert

Huku Bongo Kuna wakati naona Viongozi wa Kisiasa wanataka mawazo yao ndiyo yawe final hata Kwa maeneo ambayo hawana uzoefu napo

Tungepata mtaalamu mshauri kwenye hilo eneo la anga, huenda tungefanya vizuri sana na Faida ingeonekana kwenye Shirika letu la ndege

Upande wa customer service ya ndani ya ndege walau wanajitahidi pamoja na kutangaza Korosho zetu za Mtwara
 
Mmiliki alikuwa Mzungu wa Netherlands na hiyo ya pili mmiliki alikuwa huyo Rostam Aziz
Thats the point, hawa wahindi wakiajiriwa na mhindi mwenzao (rostam) au mzungu they are perfect waajiri wewe mpenda rushwa utalia kilio cha mbwa koko, wanawatumikia wazungu vizuri wapate opportunity za kwenda kuishi ulaya kwa visa nzuri,
 
Ndio uende chato sasa ukapige hivyo viboko km utarudi salama
 
ET-Addis nadhani wanafanya wana faclities za kutosha kwa wide body zote..
Hakuna ndege ya mtumba, C & D check inaweza kufanyika kokote benye maintenance and overhaul facilities ( MRO), East africa hakuna such facility
 
Mnachanganya desa mno, Boeing hatengenezi engine, Dreamliner inatumia engine za kampuni mbili tu Royce Royce na General Electric basi...ni uqmuzi wa Shirika husika kuchagua kampuni waitakayo...
Inawezekana ila Engine za Boieng zipo kwenye shida kidogo naona mashirika mengi wanalalamika..dess
 
ATCL inawaponza siasa, Hiyo C check huwa haizidi wiki 3, Kusema wamekosa injini za kufunga wakati zingine zikiendelea na matengenezo ni uongo usio na maana kwa kizazi hiki, kama ndege ipo C check ina maana wanaangalia mifumo zaidi ya injini pekee. Pia hamna mahali ukipeleka ndege yenye injini mbovu wanakufungia injini mpya ukaendelee na kazi zako eti wakimaliza kurekebisha zako urudishe hizo walizokufungia, ni bora wangesema injini hazifai tumekosa zingine. Tatizo ATCL mnatoa taarifa mlizotakiwa kuzitoa mwaka 1962 katika zama hizi za utandawazi kila kitu kinajulikana.
 
Thats the point, hawa wahindi wakiajiriwa na mhindi mwenzao (rostam) au mzungu they are perfect waajiri wewe mpenda rushwa utalia kilio cha mbwa koko, wanawatumikia wazungu vizuri wapate opportunity za kwenda kuishi ulaya kwa visa nzuri,
Huenda ikawa sababu ilikuwa Kila Ijumaa CEO wetu alikuwa akifanya presentation Kwa njia ya mtandao kuhusu progress na mauzo.

Nimegundua hata sisi Wabongo tukiajiriwa Kwa kupimwa KPIs huwa tuna perform sana

Japo kusiwe na urasimu kwenye vitendea kazi πŸ™Œ
 
Mkuu, idea za magufuli zilikuwa sawq, ndege zimilikiwe na serikali atcl wakodishwe na makampuni binafsi nayo yakodi wakihitaji, tangu aondoke hili la kukodishwa kwa wahitaji wengine limekufa kibudu,
 
M
Delivery ya Boeing 787-8 yenye codename 5H-TCJ ilikuwa October 25, 2019. 2020 haikuruka shauli ya zuio la COVID 19 na kutokuwa na vibali kwa vigezo China.
Kama kuruka imefanya miruko kadhaa kwenda China ikipokezana Boeing 787-8 5H-TCG na hata hivyo ikazuiliwa China kwa sababu zisizotajwa lakini baadaye ikahamishiwa Malaysia kimya kimya. Kama kigezo cha kufanya Maintanance ni miruko 1000 ilitimia? Kama haikutimia na tayari iliishafanyiwa C-check nchini, huko Malaysia inafanyiwa matengenezo gani Ili mwezi wa sita ianze tena kazi wakati huo huo tukitegemea Boeing nyingine 787-8 5H-TCR mwishoni mwa mwezi huu? Mkuu huoni kama kuna janja janja inachezwa hapa na Boeing dhidi yetu?
Maana yake tunaponunua ndege za Boeing ni lazima tununua injini mbili zaidi za akiba zitakazotumika wakati wa matengenezo. Swali la msingi ni kweli hizo ndege tulinunua mpya au refurbished ? Je ni zetu kweli? Sisi ni wamiliki wa body tu wakati injini ni mali ya Boeing? Au tumekodisha? πŸ€”
 
Ndege hata isiporuka, muda wa checking ukifika itafanyiwa. Nadhani kwenye maelezo wamesema ni miruko 1000 au kigezo kingine ambacho nadhani ndicho wametumia.
 
Mkuu hii ndege, ina engene bora kabisa, ila kuna sehemu nimesoma engene ilikutwa na kutu na makandokando kibao, pia kuna sehemu eng matindi anasema hili tatizo nilakutoka kiwandani, inawezekana tunachezewa mchezo mchafu tunauziwa bodi jipya engene kukuu, ipo haja ya kuachana na majina makubwa kama boeng,
 
Ndege hata isiporuka, muda wa checking ukifika itafanyiwa. Nadhani kwenye maelezo wamesema ni miruko 1000 au kigezo kingine ambacho nadhani ndicho wametumia.
Hiyo miruko 1000 ilitimia?
 
Naku
Nakubaliana nawe kuwa kuna mahali tunachezewa. Ukifuatilia kwa makini Production list na Deliveries za Boeing kuna ujanja unatumika wa Boeing kushikilia soko dhidi ya mpinzani wake Airbus. Tunapaswa kufungua akili vinginevyo tutaendelea kula hasara.
Kumbuka, ile ndege ya mizigo walizua dosari kwenye matenki ya mafuta ya ndege aina ya Boeing 767 na tulilazimika kuingia gharama zaidi.
 
Ndege walizinunua Malaysia? Hapa ndio msemo wa nafuu ni gharama unapochukua mkondo wake. Kupenda vya bei nafuu kunaigharimu zaidi Serikali wala sio shirika, ninavyoelewa, hizo ndege zimenunuliwa na Serikali. Ndege hata miaka 5 haina, inahitaji matengenezo makubwa kiasi cha kuhitaji mtambo mbadala? Je kulikuwa na waranti wakati wa manunuzi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…