Aishi Manula anapewa sifa asizostahili! Hawezi kuifikisha popote Simba na Taifa Stars

Aishi Manula anapewa sifa asizostahili! Hawezi kuifikisha popote Simba na Taifa Stars

Ni tofauti kabisa na alivyokuwa AZAM FC,kipindi kile alikuwa TZ one alionyesha uwezo mkubwa wa kudaka lakini sasa hivi naona anaporomoka hana tofauti na Dida.Nimeangalia mechi ya jana dhidi ya Al-Ahly kwa kweli inasikitisha,umefika wakati sasa wa vilabu kuanza kutrain vijana wadogo kwa ajili ya kureplace nafasi za wakongwe!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwangu mimi Juma Kaseja atabaki kuwa Tanzania One mpaka siku ntakayoridhika na kiwango cha kipa mwingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anakula vizuri, analipwa vizuri. Ule moyo wa kuridhika na kuanza kunenepa na jitihada ndogo kwenye mazoezi ndo huwa zinawashusha viwango hawa jamaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umesema kweli mkuu!! Wachezaji wa kitanzania ni wepesi sana kuridhika hebu angalia mchezaji km kichuya ivi karibuni amekuwa mchezaji wa kawaida na hta sijui hao waarabu wa misri wameona nn kwake mpaka wamemsajili.....halafu nimeskia wengine wakisema eti sie tunafungwa kwa sababu hatuandai wachezaji tokea wapo wadogo nikawaambia waangalie wachezaji wa as vita wengi wao hawajakulia kwenye academy wamekulia kwenye mazingira mabovu tena zaidi ya wachezaji wetu lakini hebu angalia perfomance yao uwanjani? Mi nadhani kitu kinachotautisha ni kwa kiasi wachezaji wetu wana kiu dhidi ya mafanikio ukilinganisha na wa as vita? Km ulifuatilia game ya simba na as vita uliona jinsi jamaa walivyokuwa na commitment uwanjani tofauti na wachezaji wa simba ambao walikuwa hawana concetration kbsa yaan km walilazimishwa kicheza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna hata goli moja kati ya kumi yaliyotokana na makosa ya manula, tena alituokoa sana na Vita ilikua tunapigwa nane. Tatizo la wabongo wanapenda sana kutafuta mtu wa kumpa lawama. Simba ina tatizo kubwa haiwezi kujilinda. Wale waarabu walikua wanafungu sio kupiga mpira golini. Mtu aniambie ni goli la ngapi manula angeweza kuokoa? Badala ya kuwalaumu maprofeshino wenu ambao hawana msaada wowote mnamlaumu mtoto wa mjomba wenu. Pmbv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna hata goli moja kati ya kumi yaliyotokana na makosa ya manula, tena alituokoa sana na Vita ilikua tunapigwa nane. Tatizo la wabongo wanapenda sana kutafuta mtu wa kumpa lawama. Simba ina tatizo kubwa haiwezi kujilinda. Wale waarabu walikua wanafungu sio kupiga mpira golini. Mtu aniambie ni goli la ngapi manula angeweza kuokoa? Badala ya kuwalaumu maprofeshino wenu ambao hawana msaada wowote mnamlaumu mtoto wa mjomba wenu. Pmbv

Sent using Jamii Forums mobile app


Umesema kweli ndugu, sijui kwa nini hatuwezi kukubali kuzidiwa!!!!
 
Mkuu AROON

Uko sahihi kwa hoja yako hii...Manula uwezo wake kwa sasa umepungua mno....Taifa Stars inabidi atafutwe kipa mwingine...Simba waendelee naye au wamtumie Beno ambaye atakwenda huko baada ya Yanga kumshitukia
Benno hatumtaki Bora kipa WA Simba B
 
Hila zile goli za Al ahly sikuona kosa la manila, mabeki ndio wana matatizo hawakabi
 
Huu ni kweli mchungu, Manula amekuwa akisemwa ni 'Tanzania one' na maneno kibao, lakini ukweli ni kipa wa kawaida sana na kwa kuwa ni wa kawaida naomba niseme timu ya Taifa na Simba hazitafikia kilele cha mafanikio.

Ili timu ifikie kilele cha mafanikio inahitaji kuwa na kipa aliyekamilika wataalamu wanaita A GOOD STOPPER,

Kuna kipindi kipa anatakiwa aibebe timu, hasa kwenye mazingira magumu, hii ndio sifa ya STOPPER,

Kwa kipindi cha nyuma Smba waliwahi kufikia angalau mafanikio ya juu, kwa kuwa na STOPPER kama JUMA KASEJA

Naomba niseme sioni Smba ikitusua mbali zaidi kwa kuendelea kuwa na makipa wa kiwango cha Manula. Hata timu yetu ya Taifa haitafika popote kwa kuendelea kuwa na makipa wakiwango cha Manula

Hebu angalia mtu kama Kakolanya au Jma Kaseja wa enzi zake au yule Dida( Deo Munishi) wa Yanga, kuna kipindi waliziokoa timu zao, zilipokuwa kwenye mazingira magumu

Sikatai Manula ni golikipa mzuri ila sio Stopper wakuifikisha kwenye kilele cha mafanikio Smba na timu ya Taifa,
Tulishaandika humu kitambo sana
 
Back
Top Bottom