Aishi na risasi 3 mwilini kwa miaka 11 baada Muhimbili na Bugando kutomfanyia upasuaji

Aishi na risasi 3 mwilini kwa miaka 11 baada Muhimbili na Bugando kutomfanyia upasuaji

Kauli ya Muhimbili, MOI

Alipoulizwa kutaka kufahamu kama Makasi alipokelewa, Msemaji wa MNH, Aminiel Aligaesha alisema taarifa za mgonjwa huyo hazionekani.

“Nimeangalia kwenye mfumo sijaona kama alitibiwa hapa Muhimbili, nadhani alipofikishwa hapa alielekezwa kwenda MOI,” alisema Aligaesha

Ofisa Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi naye alisema taarifa za mgonjwa huyo hazioni ingawa suala hilo halizuii mgonjwa kutibiwa.
Seriously?

Kwa hio ametunga kwamba alienda ila hakwenda? Hii inaingia akilini kweli?
 
Kauli ya Muhimbili, MOI

Alipoulizwa kutaka kufahamu kama Makasi alipokelewa, Msemaji wa MNH, Aminiel Aligaesha alisema taarifa za mgonjwa huyo hazionekani.

“Nimeangalia kwenye mfumo sijaona kama alitibiwa hapa Muhimbili, nadhani alipofikishwa hapa alielekezwa kwenda MOI,” alisema Aligaesha

Ofisa Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi naye alisema taarifa za mgonjwa huyo hazioni ingawa suala hilo halizuii mgonjwa kutibiwa.[emoji2827]
 
Em ngoja kwanza..
Ni risasi hizi hizi ambazo Wakina Taylor wanazitoaga na visu afu wanamwagia Whiskey au Hanson's choice ???
Wewe ulidhani zipi?

Na zile za maigizo ya cinema na movie za kivita sio zenyewe maana zile hazina madhara, uwe unachukua muda wako kuangalia behind the scenes za movies utajifunza kitu, kwenye movies wanafanya kitu kinaitwa make-up kinafanya na make-up designers au make-up artist
 
View attachment 2404685
Julai 6 mwaka 2011 ni siku ambayo hatoisahaulika kwa Kulwa Makasi (32) baada ya kupigwa risasi tatu, moja kichwani, mgongoni na kwenye paja la kulia anazoishi nazo kwa miaka 11 sasa.

Mkazi huyo wa Shibula jijini Mwanza kwa sasa anatembea kwa kiti maalum kutokana na ulemavu alioupata baada ya kupigwa risasi na askari polisi wakati wa operesheni ya kuwaondoa wamachinga katikati ya mji mwaka huo. Kwa ulemavu alionao, familia yake sasa inatunzwa na mkewe, Salome Peter.

Siku ya tukio, polisi kwa kushirikiana na mgambo walikuwa wanawaondoa wamachinga katika Mtaa wa Makoroboi na Kulwa anasema alitoka nyumbani kwake Mtaa wa Mabatini kwenda kwenye biashara zake ndipo alikuta watu wakikimbizana.

“Nilipofika Makoroboi nilikuta taharuki ya Jeshi la Polisi, mgambo na wamachinga. Nikauliza kuna nini, wakaniambia wamesema tusifanye biashara eneo hili, nikasikia sauti ya askari akisema wenye mizigo eneo hili waje waitoe,” anakumbuka Makasi.

Baada ya kusikia kauli ya askari huyo, akiwa na wenzake watatu, anasema waliingia stoo na ndani ya dakika tatu walisikia mabomu ya machozi yakipigwa nje.

“Tulitaharuki, tukaamua kutoka na tukaona watu wanakimbia, nasi tukakimbia kuelekea lilipokuwa Soko Kuu la Mwanza. Tukiwa tunakimbia tulisikia askari akitoa amri kwamba ‘piga risasi.’ Zikanipiga tatu,” anasema.

Kutokana na kutokwa damu nyingi, anasema alipoteza fahamu na alipozinduka alijikuta katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) cha Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando alikokaa kwa mwezi mzima lakini hakufanyiwa upasuaji wa kuondoa risasi hizo kutokana na ubovu wa mashine hivyo akapewa rufaa ya kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako alikaa kwa mwaka mmoja bila kufanyiwa upasuaji, sababu ikiwa ni hitilafu za mashine.

“Vipimo vya Muhimbili walisema matibabu yangu kwa wakati huo hayakuwepo nchini hivyo nilihitajika kusafirishwa kwenda India kufanyiwa upasuaji huo,” anasema Makasi.

Matumaini yaligonga mwamba baada ya familia yake kushindwa kumudu gharama za usafiri na matibabu ambazo hazikumbuki kutokana na kupoteza karatasi yenye taarifa hizo.

“Baada ya kukaa muda mrefu hospitalini bila matibabu madaktari walishauri nirudishwe nyumbani,” anasema.

Kutokana na risasi zilizo mwilini mwake, Makasi anasema kuna wakati humsababishia hasira jambo linalomfanya aonekane mwenye tabia tofauti kwenye familia na kipindi cha baridi anahisi maumivu na vichomi jambo linalomkosesha usingizi.

Huku akibubujikwa machozi, Salome, mke wa Makasi anasema hakutarajia mume wake angekuwa mlemavu.

“Wakati mwingine nakata tamaa kwa sababu mambo yameniwia magumu mno, nawaomba mtusaidie. Naamini akiondolewa risasi mwilini anaweza kurejea kwenye utimamu wa afya ili tusaidiane kulea hii familia,” anasema.

Kauli ya Muhimbili, MOI

Alipoulizwa kutaka kufahamu kama Makasi alipokelewa, Msemaji wa MNH, Aminiel Aligaesha alisema taarifa za mgonjwa huyo hazionekani.

“Nimeangalia kwenye mfumo sijaona kama alitibiwa hapa Muhimbili, nadhani alipofikishwa hapa alielekezwa kwenda MOI,” alisema Aligaesha

Ofisa Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi naye alisema taarifa za mgonjwa huyo hazioni ingawa suala hilo halizuii mgonjwa kutibiwa.

MWANANCHI
1.) Yaani taarifa hazionekani na mtu amekaa hapo mwaka mmoja?

2.) Ni mashine gani hiyo iliyoharibika na hadi leo haijatengenezwa?
 
Hivi risasi za plastic kama zinazotumika kweny mamuvi hamna jaman...
 
Watumie mitandao ya kijamii kuomba msaada.
Maana hii ni taarifa tu, ni vizuri kama wangeambatanisha na mawasiliano yao watu huenda wakachangia chochote.
 
Ushauri,arudi tena MOI,tutakuwa nyuma yake kumpambania,maana sidhani kwa uongozi wa sasa pale Muhimbili wanaweza kumuacha bila ya kumpatia matibabu,na swala la gharama,iwekwe wazi tu taarifa za matibabu yake,hawezi kukosa wasamaria wema kumchangia...
 
Em ngoja kwanza..
Ni risasi hizi hizi ambazo Wakina Taylor wanazitoaga na visu afu wanamwagia Whiskey au Hanson's choice ???
Inategemea zipo sehemu gani mwilini.
Kaka ndugu yangu anayo mbavuni toka 1998 imefika kwenye uti wa mgongo (spinal column/spinal cord) sasa ikitolewa ata pooza anakuwa kilema hatosimama wala kutembea.
Risasi ikikaa vibaya kwenye fuvu la kichwa (skull) ukiitoa pressure kwenye ubongo inaweza kusababisha ubongo uvuje na mtu anakufa au anapata ulemavu wa kudumu.

Note: Mimi siyo daktari haya ni maoni yangu tu kama mtu wa kawaida.
 
Sidhani kama maelezo aliyoyatoa yana ukweli kitaalamu, eti mashine za hospital 2 kubwa nchini zilikosa umeme hivyo kushindwa kuzitoa hizo risasi! Ninavyofahamu risasi (hasa hizi za shot guns) zina kawaida ya ku lodge mwilini na Maamuzi ya kuzitoa mara nyingi yanategemea na sehemu zilipo Mfano km zipo karibu na mfumo wa fahamu au karibu na mshipa mkubwa wa damu kitendo cha kuzitoa linaweza kuwa na madhala makubwa ikiwemo kifo au ulemavu mkubwa kuliko kuziacha! Rahisi ni zile zinazokwama kwenye misuli maana Kadri muda unavyoenda ndivyo zinapanda juu mwishowe unaweza zitoa kwa urahisi.
 
Kwani Kikwete bado yuko hai maana hii ilikuwa awamu yake!!!
 
UNYAMA HUU.
RAIS AWAMU YA SITA HAPENDI NA WALA HATAKI MAMBO YA NAMNA HII,NADHANI SOON ATASAIDIKA,KATIKA AWAMU HII YA SITA, AMBAYO NI AWAMU YENYE MUNGU NDANI YAKE.
Linapokuja swala la siasa, Mungu muweke mbali.
 
View attachment 2404685
Julai 6 mwaka 2011 ni siku ambayo hatoisahaulika kwa Kulwa Makasi (32) baada ya kupigwa risasi tatu, moja kichwani, mgongoni na kwenye paja la kulia anazoishi nazo kwa miaka 11 sasa.

Mkazi huyo wa Shibula jijini Mwanza kwa sasa anatembea kwa kiti maalum kutokana na ulemavu alioupata baada ya kupigwa risasi na askari polisi wakati wa operesheni ya kuwaondoa wamachinga katikati ya mji mwaka huo. Kwa ulemavu alionao, familia yake sasa inatunzwa na mkewe, Salome Peter.

Siku ya tukio, polisi kwa kushirikiana na mgambo walikuwa wanawaondoa wamachinga katika Mtaa wa Makoroboi na Kulwa anasema alitoka nyumbani kwake Mtaa wa Mabatini kwenda kwenye biashara zake ndipo alikuta watu wakikimbizana.

“Nilipofika Makoroboi nilikuta taharuki ya Jeshi la Polisi, mgambo na wamachinga. Nikauliza kuna nini, wakaniambia wamesema tusifanye biashara eneo hili, nikasikia sauti ya askari akisema wenye mizigo eneo hili waje waitoe,” anakumbuka Makasi.

Baada ya kusikia kauli ya askari huyo, akiwa na wenzake watatu, anasema waliingia stoo na ndani ya dakika tatu walisikia mabomu ya machozi yakipigwa nje.

“Tulitaharuki, tukaamua kutoka na tukaona watu wanakimbia, nasi tukakimbia kuelekea lilipokuwa Soko Kuu la Mwanza. Tukiwa tunakimbia tulisikia askari akitoa amri kwamba ‘piga risasi.’ Zikanipiga tatu,” anasema.

Kutokana na kutokwa damu nyingi, anasema alipoteza fahamu na alipozinduka alijikuta katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) cha Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando alikokaa kwa mwezi mzima lakini hakufanyiwa upasuaji wa kuondoa risasi hizo kutokana na ubovu wa mashine hivyo akapewa rufaa ya kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako alikaa kwa mwaka mmoja bila kufanyiwa upasuaji, sababu ikiwa ni hitilafu za mashine.

“Vipimo vya Muhimbili walisema matibabu yangu kwa wakati huo hayakuwepo nchini hivyo nilihitajika kusafirishwa kwenda India kufanyiwa upasuaji huo,” anasema Makasi.

Matumaini yaligonga mwamba baada ya familia yake kushindwa kumudu gharama za usafiri na matibabu ambazo hazikumbuki kutokana na kupoteza karatasi yenye taarifa hizo.

“Baada ya kukaa muda mrefu hospitalini bila matibabu madaktari walishauri nirudishwe nyumbani,” anasema.

Kutokana na risasi zilizo mwilini mwake, Makasi anasema kuna wakati humsababishia hasira jambo linalomfanya aonekane mwenye tabia tofauti kwenye familia na kipindi cha baridi anahisi maumivu na vichomi jambo linalomkosesha usingizi.

Huku akibubujikwa machozi, Salome, mke wa Makasi anasema hakutarajia mume wake angekuwa mlemavu.

“Wakati mwingine nakata tamaa kwa sababu mambo yameniwia magumu mno, nawaomba mtusaidie. Naamini akiondolewa risasi mwilini anaweza kurejea kwenye utimamu wa afya ili tusaidiane kulea hii familia,” anasema.

Kauli ya Muhimbili, MOI

Alipoulizwa kutaka kufahamu kama Makasi alipokelewa, Msemaji wa MNH, Aminiel Aligaesha alisema taarifa za mgonjwa huyo hazionekani.

“Nimeangalia kwenye mfumo sijaona kama alitibiwa hapa Muhimbili, nadhani alipofikishwa hapa alielekezwa kwenda MOI,” alisema Aligaesha

Ofisa Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi naye alisema taarifa za mgonjwa huyo hazioni ingawa suala hilo halizuii mgonjwa kutibiwa.

MWANANCHI
Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu itamsaidia kupata matibabu mungu atakuponya usikate tamaa
 
Back
Top Bottom