AJABU: Vyombo vya Habari Tanzania na Watanzania tunavyofuatilia uchaguzi Kenya, tuna maslahi gani haswa?

AJABU: Vyombo vya Habari Tanzania na Watanzania tunavyofuatilia uchaguzi Kenya, tuna maslahi gani haswa?

mavumbi

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2013
Posts
596
Reaction score
328
Wana JF nisaidieni.

Asubuhi mchana usiku taarifa za maendeleo ya Uchaguzi Kenya katika vyombo vya habari hapa Tz hadi kushangaza. Labda niko nyuma ya wengine lakini najiuliza ni lipi hasa la kutufanya tushabikie na kushobokea uchaguzi wa wenzetu kwa kiasi hicho?

Ingelikuwa Marekani ama Uingereza ama China naam maana hawa Wababe wana maslahi kwetu! Misaada, Rushwa, Ulinzi nk.

Kwa uchambuzi wa haraka huenda hii ni dalili ya mnyonge unayetamani hayo ya mwenzako yangeonekena kwako! Ume ya miss mno.. unafurahia na kuburudika anavyofanya mwenzio na mwishowe unashusha pumzi ya nguvu baada ya matokeo ya mwisho na kusema Aaaah! Kweli walichuana.

Sioni labda Wajaluo ama Wamasai walioko Tanzania wenye ndugu zao Kenya ndio wakafaidika vipi

Hebu tuache ushamba na tuache upuuzi huo!
 
Wana JF nisaidieni.

Asubuhi mchana usiku taarifa za maendeleo ya Uchaguzi Kenya katika vyombo vya habari hapa Tz hadi kushangaza. Labda niko nyuma ya wengine lakini najiuliza ni lipi hasa la kutufanya tushabikie na kushobokea uchaguzi wa wenzetu kwa kiasi hicho?
Wewe kama unaona ni ushamba na upuuzi endelea na ujenzi wa taifa, pengine huna elimu ya uraia vya kutosha. Chaguzi zote zinafuatiliwa na watu, hata serikali yetu inafuatilia nani atashinda kwasababu ya sera za chama chake na msimamo wake binafsi, kila siku unasikia nchi Sasa imefunguka Ina maana Kuna mtu alikuwa na sera ya kufunga nchi, Kuna mtu sera sake hazikuwa rafiki kwa diplomasia ya kimataifa.

Amekuja mwingine kwenye chama hicho hicho ana msimamo tofauti na Sasa anafungua alipofunga mwenzake. Hata hivyo Kuna mengi ya kujifunza uhuru wa tume na wa vyombo vya habari, na hakuna matumizi ya nguvu na vitisho kutoka vyombo vya dola.

Mwisho tusipangiane Cha kufuatilia wewe kama unapenda maigizo endelea nayo.
 
Kenya ni jirani yako na hapa ni Africa utakua mpuuzi kupuuzia yanayoendelea kwa jirani yako ambayo yanaweza kukuathiri mambo ya kinda vibaya. Kumbuka pia tuko na kenya ndani ya EAC.

Kuna ya kujifunza kutokana na uchaguzi unavyo endeshwa kwa jirani yako. Kuna wanaotaka kutuaminisha kwamba hapa kwetu mambo yako poa na kama wewe hawataki tujue kinacho endelea huko.
 
Umeandika kama mtu mjivuni asiye na utashi, anayependa kudogosha jirani zake na asiye na haja ya kuwajua jirani zake.

Kwani Watanzania wakitamani mazuri ya jirani zao Kenya kuna ubaya gani?

Wakenya huwa wanafanya mambo yanayokuja kutokea Tanzania. Walianza kuruhusu vyama vingi, hilo likafuatia Tanzania. Walianza kufungua uchumi wao, hilo likatokea Tanzania.

Sasa wameuana katika chaguzi, wamepata katiba mpya, wamepata uraia pacha, wamepata wagombea binafsi, wamefanya chaguzi zenye uwazi zaidi.

Kwa Mtanzania mwenye kujitambua, na kutaka kujifunza kutoka Kenya ili apate mazuri yaliyotokea Kenya, bila kupitia mabaya waliyopitia, ni muhimu sana kufuatilia chaguzi za Kenya na hata maisha yao kwa ujumla. Pengine kuliko Marekani, Uingereza na China, nchi ambazo ziko mbali nasi.

Kuna watu wanafanya biashara Kenya na habari za maendeleo ya uchaguzi zina impact kwenye biashara zao.

Kuna watu wanaangalia hali ya usalama inayoweza kubadilika dakika yoyote na kusababisha wakimbizi wengi wa Kenya kuja Tanzania.

Kuna watu wana hoteli zao na apartments Tanzania zimejaa Wakenya waliotaka kuondoka Kenya kipindi cha uchaguzi.

Ukijiona wewe huna interest na uchaguzi wa Kenya, inawezekana wewe ndiye mwenye tatizo la kutokuwa mtashi kuhusu mazingira yako.
 
Wana JF nisaidieni.

Asubuhi mchana usiku taarifa za maendeleo ya Uchaguzi Kenya katika vyombo vya habari hapa Tz hadi kushangaza. Labda niko nyuma ya wengine lakini najiuliza ni lipi hasa la kutufanya tushabikie na kushobokea uchaguzi wa wenzetu kwa kiasi hicho?

Ingelikuwa Marekani ama Uingereza ama China naam maana hawa Wababe wana maslahi kwetu! Misaada, Rushwa, Ulinzi nk.

Kwa uchambuzi wa haraka huenda hii ni dalili ya mnyonge unayetamani hayo ya mwenzako yangeonekena kwako! Ume ya miss mno.. unafurahia na kuburudika anavyofanya mwenzio na mwishowe unashusha pumzi ya nguvu baada ya matokeo ya mwisho na kusema Aaaah! Kweli walichuana.

Sioni labda Wajaluo ama Wamasai walioko Tz wenye ndugu zao Kenya ndio wakafaidika vipi

Hebu tuache ushamba na tuache upuuzi huo!
Halafu yalivyo manafiki na mas£ng£ uchaguzi WA 2020 umefanyika hapa mania ya watu wameuawa Bara na Zanzibar wengine wamepotezwa , kupigwa na kubambikiziwa kesi + uvunjifu WA taratibu za uchaguzi kama kuwaxuia waangalizi toka vyama pinzani , kujaza Kura feki Kwa lazima kwenye vituo vya uchaguzi , wagombea kutekwa na kunyang'anywa fomu zao na wengine wengi majina Yao kukatwa kihuni na kuzuia kurudisga fomu za kugombea ,.

Halafu yakakaa kimya Tu , k£ng£ kabisa hizi, Tanzania Hamna vyombo vya habari kuna vijiwe vya machawa na wachumia tumbo basi
 
Wewe kama unaona ni ushamba na upuuzi endelea na ujenzi wa taifa, pengine huna elimu ya uraia vya kutosha. Chaguzi zote zinafuatiliwa na watu, hata serikali yetu inafuatilia nani atashinda kwasababu ya sera za chama chake na msimamo wake binafsi, kila siku unasikia nchi Sasa imefunguka Ina maana Kuna mtu alikuwa na sera ya kufunga nchi, Kuna mtu sera sake hazikuwa rafiki kwa diplomasia ya kimataifa.

Amekuja mwingine kwenye chama hicho hicho ana msimamo tofauti na Sasa anafungua alipofunga mwenzake. Hata hivyo Kuna mengi ya kujifunza uhuru wa tume na wa vyombo vya habari, na hakuna matumizi ya nguvu na vitisho kutoka vyombo vya dola.

Mwisho tusipangiane Cha kufuatilia wewe kama unapenda maigizo endelea nayo.
Umedadavua vema sana kumjibu kilaza huyo!
 
mbona dw kuna makala maalumu wanachambua uchaguzi hata bbc napo wanafuatilia ww kinakuuma nn uchaguzi kufutiliwa kama unakereka jiue uende kaburini kule ndo hamna kufuatiliana
 
Loh!
Naona wote mnatoka povu kwa kutaka kutetea unyonge wenu.

Miaka 60 ya Uhuru, bado mnatolea macho siasa za jirani ambaye mnadai mnajifunza toka kwake! Vyama vingiTanzania tumeanza jana? Kufungua uchumi tumeanza leo?

Acheni uchovu wenu, ni ushamba tu kushangilia mafanikio ya mwenzio - wakati unao uwezo wa kubadili maisha yako nyumbani kwako.

Poleni sana!
 
Kaka hiyo ni ya maslahi yake wewe - na kwenu mna kipindi kama hicho? Kwa lugha ya Kijerumani? 000 Zero!
 
Wewe... nyie ya kwenu mliyasema? Uchaguzi wenu 2020 ulikuwa uchafu mtupu hamkuinua midomo yenu kuongea lolote lile~ Shobo nyingi kwa ya wenzenu kuhusu haki na demokrasia wakati uozo mnao hapa NA MNASHANGILIA --IBILISI WAKUBWA
 
Umeandika kama mtu mjivuni asiye na utashi, anayependa kudogosha jirani zake na asiye na haja ya kuwajua jirani zake.

Kwani Watanzania wakitamani mazuri ya jirani zao Kenya kuna ubaya gani...
Uungwana huanzia nyumbani usiwe mwoga wa kufikiri mzembe wewe! rekebisha ya kwako nyumbani kwako kwanza sio kushobokea mambo ya jirani yako!
 
Soma kitabu la yericko nyerere ujasusi wa kidola na kiuchumi yote yameongelewa mle
 
Wana JF nisaidieni.

Asubuhi mchana usiku taarifa za maendeleo ya Uchaguzi Kenya katika vyombo vya habari hapa Tz hadi kushangaza. Labda niko nyuma ya wengine lakini najiuliza ni lipi hasa la kutufanya tushabikie na kushobokea uchaguzi wa wenzetu kwa kiasi hicho...
Maslahi ni mengi na makubwa,wanakatiba mpya nzuri ,Wana tume huru ya uchaguzi ,Wanaahakama huru,Wana bunge huru , wenzetu na siye hatuna chochote🤔.Bila kusahau Wana democrasia Bora EAC na Afrika🏃
 
Back
Top Bottom