Ajali iliyoua wanafunzi Mtwara, Haice ilikuwa na watu 30. Haice inaruhusiwa kubeba abiria wangapi?

Ajali iliyoua wanafunzi Mtwara, Haice ilikuwa na watu 30. Haice inaruhusiwa kubeba abiria wangapi?

Mkuu speed sio tatizo mama,hawa politicians na watendaji wasikufanye na wewe uwe unapenda majibu rahisi, tatizo letu barabara zetu ni mbovu, magari mengi yapo unroadworthy, overloading, law enforces wengi wana cancer ya rushwa, miaka ya 80s buses hasa route ya Dar to Iringa yalikuwa yanatumia 10hrs kwa sababu barabara zilikua Safi, na matengenezo Safi,nakumbuka bus za railways zilikuwa zikifika mikumi lazima ziende garage zikaangaliwe,utaratibu huu ulikua ni standard na zile za kwenda mbeya na kyela lazima zikaguliwe tena pale Iringa workshop, nini kiliua hili shirika na standard hizi ni debate for another day, Speed SIO tatizo pekee otherwise wasingetuwekea speed ya 200 kwenye magari
Upo vizuri sana mkuu.
 
Tanzania kuna law enforcement, kila mwezi wanapokea salary lakini bado ajali zipo, magari mabovu yanatembea na dereva wasiokua na vigezo wanazidi kuongeza.
Kuna umuhimu gani kua na traffic police kama hivo vyote vinaongezeka?
Traffic police abakizwe na jukumu la kuongoza magari, Tanroad inapaswa mbadilike hizi barabara za kupishana kwa mstari mweupe katikati mnaita “Highway” wanaotengeneza magari huko Japana hawajui hilo,
Wekeni njia za wakwenda wakwenda, wakurudi wakurudi “double road”
Tuache kuingiza magari chakavu Tanzania, mpaka leo unaingiza gari inatumia CD au Tape recorder mnaita mpya, hizi ni chuma chakavu

Barabarani watafute mzabuni waeke camera amabazo zitakua na kazi ya kucheki speed na kuandika cheti hapo hapo na kutumiwa mmiliki wa gari.

Narudia tena kama ajali bado zipo traafic mbaki kuongoza magari na sio kuvizia makosa

Wananchi wenyewe wengi wana simu zenye camera zinazoweza kurekodi madereva wanaofanya uhuni barabarani na kuhatarisha maisha ya watu. Ukirekodi unasambaza kwenye social media, unasambaza whatsapp, unaibandika hapa JF, unasambaza kila mahali mtandaoni. Zitawafikia tuu wanaohusika penda wasipende. Teknolojia tukiitumia vizuri itaweza kutatua matatizo mengi sana kwenye jamii.
 
kwani daladala mjini dar inauwezo wa kupakia watu wangapi? 30 tu. mbona wanajaza 50
 
Back
Top Bottom