Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Askari wa usalama barabArani ndo wanaosababisha ajali kwa uzembe wao, hawakagui gari, wanachofanya, wanasimamisha gari,wanachukua chao, generally siwapendi police, hasa wa usalama barabarani
 
Sio tu kufutiwa leseni bali kufutiwa forever. Maisha yao yote wasiendeshe gari ya abiria wala ya mizigo, labda gari binafsi, bajaj, bodaboda na iwe baada ya miaka angalau mi5 ya kutumikia adhabu ya kutokuendesha chombo chochote cha moto. Hapo watatia adabu.

Eneo lingine la kuangalia ni kupiga marufuku pome aina ya viroba. Vimeathriri sana madereva na vimechangia sana ajali vikisaidiana na simu za mikononi.
 
Kwa hiyo wakifutiwa leaeni majeruhi walio poteza viungo watapona na walio fariki watafutuka??
Ninge muelewa angesema kuanzia sasa maaskari wanao wapa madereva leseni kwa hongo, na wakaguzi wa magari wanaopokea hongo na kuruhusu mwendo kasi na magari mabovu kupakia abiria watafutwa kazi nakufungwa jela. Kamanda Mpinga amekuwa mno mwanasiasa kuliko askari.
Akiambiwa vijana wake ni wala rushwa huwa ana watetea wakati sisi ndio tuko nao na tunajua matendo yao. Naona sasa hata kama ni uhome boy, IGP Mangu afumbe macho afanye marekebisho kikosi cha usalama barabarani. Mauaji ya ajali Tanzania yamezidi ya boko haramu na malaria.

Unadhani ataweza?Kama anataka kweli kupunguza ajali za barabarani aanze na kuondoa RUSHWA polisi.

1.Rushwa ipo kwenye kuchukua hizo leseni kubwa kwani tunaona hata UTINGO anaendesha basi na hata Shule ya udereva hajaenda.Ukiingia ndani zaidi hata ALAMA za BARABARANI hazijui,kwanza aondoe RUSHWA.

2.Awalazimishe waajiri au Owners wa mabasi waajiri madereva walioenda shule ya udereva viginevyo tutamalizika...........
 
hatua muafaka kabisa

Halafu

hata hivyo hatua hizi hazitoshi.
1. wapelekwe mahakamani na wahukumiwe kama wauwaji
2.wamiliki nao wachukuliwe hatua hizo hizo kwa kupakia abiria katika magari mabovu
3.fidia kwa wafiwa itolewe ya kutosha kulingana na sheria za nchi

Umejishtukia au ulisahau kusign out ili kutumia ID nyingine?
 
Askari wa usalama barabArani ndo wanaosababisha ajali kwa uzembe wao, hawakagui gari, wanachofanya, wanasimamisha gari,wanachukua chao, generally siwapendi police, hasa wa usalama barabarani

Kwa hiyo lile lori lililoparamia basi Mafinga kule Iringa na likauwa zaidi ya 40 ni trafic police walisababisha? Askari wa Usalama barabarani haiwezekani wawe kila eneo la nchi kudhibiti ajali.

Hivi unajua tabia za madereva zilivyo? Wakigundua mbele kuana askari wote wataendesha kwa mwendo wa kondoo ila wakishavuka tu eneo lenye askari upuuzi ni uleule. Zaidi ya 90% ya ajali ni uzembe wa madereva, mengine visingizio tu.
 
Eneo lingine la kuangalia ni kupiga marufuku pome aina ya viroba. Vimeathriri sana madereva na vimechangia sana ajali vikisaidiana na simu za mikononi.

Kwani pombe aina ya viroba ndo ina kilevi tuu? Wakinywa pombe nyingine ruksa?
 
Binafsi sioni kitu kipya hapo, sio kwamba sithamini juhudi za serikali kupambana na ajali, tatizo langu ni hizo hatua sio za kudumu na hazina lengo la dhati la kupunguza au kuzuia ajali.

Ikumbukwe palikua na sheria ya mabasi ya kutokusafiri usiku, sijui iliishia wapi japo kila ajali ikitokea utasikia kuanzia sasa mabasi hayaruhusiwi kusafiri usiku.

Ikaja suala la speed governor, watu wakapiga hela zao leo hii hata ukiulizia ule mradi ulikua na lengo gani na uliishia wapi hakuna atakaekupa majibu ya kueleweka.

Karibuni likaja suala la abiria kufunga mikanda wawapo safarini, mwanzoni pakawa na ukaguzi mkali sana mabasi yakawekewa mikanda, lakini licha ya askari wa barabarani kujaa kila eneo mnaposafiri na kuingia kwenye mabasi kwa ukaguzi, sijawahi kuona hatua zikichukuliwa kwa kosa la kutokufunga mkanda abiria, na mengine hayana kabisa kama sio mikanda kuwepo lakini mibovu na haifungi.

Kwa ufupi, hizi juhudi na matamko zinakua ni kama za muda mfupi na za kisiasa zaidi.
 
Kwani pombe aina ya viroba ndo ina kilevi tuu? Wakinywa pombe nyingine ruksa?

Viroba are so portable and cheap compared to other kinds of alcoholic drinks. Matumizi ya hovyo ya viroba miongoni mwa madereva wakiwa barabarani yako wazi wala haina haja ya ku-debate.
 
''Kutokana na ajali za barabarani ambazo watalawa kama vile wameshindwa kusimamia au kuchukua hatua za dharura kunusuru maisha ya watu ambayo yanapotea kila siku; Ningekuwa kiongozi ningesema haya yafuatayo:

''Sitaki kusikia ajali zinatokea, hivyo basi kamanda wa usalaama barabani wa eneo usika (eneo la ajali), mkuu wa wilaya wa eneo n.k , barua zao ziko tayari kufukuzwa kazi kama hayo yatatokea katika eneo lao ikiambatana na kutunga sheria ya kufungwa kwa miaka 3 jela kushindwa kuweka mikakati ya kuzuia ajali''

MATOKEO:Wakuu hao wataweka mitakati ya kudhibiti ajari, hutasikia ajari za hovyo ovyo.

2.Kama wauzaji wa madawa ya kuleya wamewekewa sheria kali,kwa nini madereva na wamiliki wa kampuni ya usafirishaji yasiwekewe sheria kali.

Mfano🙁a)ikithibitika ni uzembe wa dereva;Dereva akisababisha ajari atalipa fidia ya sh TZS 10 billion Na kifungo cha maisha jela
(b) Wamiliki wa mabasi hayo pia watalipa fidia ya TZS 10 billion na kufungiwa kufanya shughuli za usafirishaji kwa miaka isiopungua 5

3.Serikali kufuta vyuo vya mitaani ambavyo havina sifa za kufundisha udereva.

Je kama haya yakisimamiwa kutakuwa na ajari barabari

e
WADAU TUJADILI

nimekuelewa na nina ku support, hata mimi ningekuwa kiongozi ningefanya hivyohivyo hawa ngedere tukiwachekea watatuteketeza
 
Wamechelewa! Hii pamoja na kumrudisha darasani dereva ni dawa tosha
 
Ajali nyingi za barabarani zinasababishwa na uzembe wa madereva. Nidhamu ya kuendesha gari na usalama wa barabarani kwa dereva wa kitanzania ni hafifu mno. Waulize hao vijana wanaoendesha gari wamepitia VETA ipi, hawawezi kukupa jibu lililonyooka kwani wamefundishana wenyewe kwa wenyewe.

Barabara zetu kuu zintumiwa na madereva mbali mbali kutoka nchi za jirani. Takwimu zinaonyesha ajali nyingi ni za madereva wa kitanzania wasiotaka kusomea udereva.

Na wewe unayesoma hapa sasa hivi, jiulize leseni yako uliipataje?
 
Mimi niulize tu,ni nani ameshaona Lorrys & buses vituoni zikiwa zimeenda kukaguliwa katika ile wiki ya 'nenda kwa usalama'?Na cha kustaajabu yote wayakuta yanazo sticker.~~~~Solution ni kulivunja geshi la porish.
 
Mbona ubovu wa barabara hamzungumzii jamani?
Hapa naona kila mtu anatoa hitimisho kua madereva ndo chanzo cha ajali!!
Mmesahau miundombinu yetu iliyochoka? Barabara mbovu sana kwenye baadhi ya sehemu hapa nchini, kuna sehem hakuna alama za barabarani km vile limit za speed za magari mfano 50 km/h
Utakuta dereva kaweka 80km/h ghafla anapigwa tochi na police anasimama na kutoa hongo kisha anendelea na safari wakati hata hilo eneo hakuna alama yoyote inayozuia dereva kuendesha 80km/h
 
Katika ajali zinazoendelea kutokea hapa nchini serikali inabidi ikae chini na kujitafakari ni wapi ni wamekosea na hau ni maagano gani ambayo waliingia hapo hawali na miungu ya mababu zetu na kushidwa kuyatekeleza ahadi walizo ingia la sivyo tutaendelea kupoteza nguvu kazi kwa taifa hili kila kukicha

Kama wameona wameshidwa ni bora jamii ikaambiwa ukweli ili wachukue jukumu la kuzikataa ili zisiendelee kuleta maafa katika taifa

Kiwira tena hiyo........ mungu tunusuru katika wakati huu mgumu

Mungu ibariki tanzania...
 

Attachments

  • 1429266614641.jpg
    1429266614641.jpg
    39 KB · Views: 651
  • 1429266633904.jpg
    1429266633904.jpg
    39.4 KB · Views: 574
Taifa inabidi liingie katika maombi mazito, hii sio hali ya kawaida.......Mungu tunusuru na haya majanga.
Mungu awatie nguvu wote wanaopoteza wapendwa wao katika hizo ajali.
 
Inshue ni miundombinu na elimu juu ya matumizi sahihi ya barabara.
 
Taifa inabidi liingie katika maombi mazito, hii sio hali ya kawaida.......Mungu tunusuru na haya majanga.
Mungu awatie nguvu wote wanaopoteza wapendwa wao katika hizo ajali.

Maombi hayawezi kuzuia ajali. Muhimu ni kufanya yafuatayo:

1. Kutengeneza barabara za maana. Siyo vichochoro ccm wanatutapeli eti ni barabara. Barabara gani imejaa matuta, nyembamba ka njia ya waenda kwa miguu? Huu utakuwa ni uchizi

2. Vyombo vya usafiri vya maana
Magari yakiwemo mabasi, vipanya, magari binafsi na milori, huwa vinaingizwa nchini katika kiwango cha mwisho ambapo hakitakiwi kutumika katika nchi kilikoanzia kutumika. Mataifa tajiri hutumia njia hii ku dispose of machine chakavu. Tanzania ndiyo huwa tunanunua. Hata kama uwezo wetu uko chini, lakini tumezidi kunua scraper. Zingine hazitengenezeki, kwa nini zisiue watu?

3. Madreva wasio na uwezo
Hili siyo katika kusababisha ajali tu, bali pia kusababisha usumbufu barabarani. Jams nyingi zinasababishwa na madreva waso na ujuzi.

4. Tabia ya kibongo bongo ya kutojali maisha au mali ya wengine
Kutojali ni shida sana. Mtu anaamua kuharibu au kumdhuru mtu kutokana na kutojali. Hii ni mifumo ya kifamilia zaidi iliyoharibika. Watu katika families nyingi za kibongo hawawafundishi watoto au members wengine kujaliana. Ubinafsi wa kipu.uzi. Fikiria mtu anaovateki kwenye kona ambako pamoja na kuwepo alama za barabarani na yeye kuona hali halisi, bado anaovertake.

Kwa hayo yote, hakuna utachomuomba Mungu akakusikiliza. Ataona kama wewe ni mzembe flani na wala hujui unachokiomba. Sioni cha kuomba, tufanye kazi tupate pesa, tujenge barabara za juu na ardhini na tuweze kununua magari mapya. Njia nyingine ni za kubahatishaaaa
 
Usihofu, ajali zitapungua baada ya uchaguzi.
 
Back
Top Bottom